TANZIA President Bingu wa Mutharika of Malawi is dead!

Tb Joshua alitoa utabiri tarehe na mwezi gani? R.I.P RAIS
 
Kuweni na subira kabla ya kutoa RIP zenu. Wenyewe wanadai bado yuko hai, ila yuko ICU akiwa kwenye "critical condition". Saa moja jioni kwa saa za Malawi (sawa na saa mbili usiku kwa saa za hapa Tanzania) amehamishiwa Afrika ya Kusini kwa matibabu zaidi.

Incapacitated Mutharika taken to South Africa hospital | Malawi news, Malawi - NyasaTimes breaking online news source from Malawi

Inawezekana anaishi kwa msaada wa mashine na madaktari wa hapo wameshindwa, maana yuko unconscious tangu saa tatu asubuhi. Hapa ndipo tunapoona umuhimu wa kuwa na huduma bora za afya within the country, maana hata hawa wakubwa wetu wakishikwa ghafla angalau wanaweza kupewa huduma kabla ya kufikiria kuwapeleka nje ya nchi na hivyo kuokoa maisha yao. Magonjwa huwa hayabishi hodi, ni muhimu sana kuwa na huduma za afya ambazo ni bora ndani ya nchi. Kuita ambulance ya ndege na kupanga logistics zote hata kama ni kwenda Nairobi tu lazima masaa kadhaa yakatike ambayo inaongeza risk kwa mgonjwa kupoteza uhai.
 
Na bado wa magigoni katabiriwa ngojea tuone hatamaliza miaka 5
 
Huyo Rais alivyokuwa Mbaya, alitesa hadi rais wa sasa wa Zambia na Unajua alifanya kazi World Bank; labda walimwekea sumu mkewe alikufa sasa akawa anapikiwa na watumishi wake...

mbona alioa tena? alimuoa "former" minister wake ambaye waalipishana miaka kama 30 hivi.
wadau walikuwa wanasema mheshimiwa alikuwa anafanya mikakati ya kumrithisha mdogo wake
hiyo nafasi ya urais. rip bingu wa mutharika
 
Mmmh, ukisoma hapa ni kama vile anasema mwili unapelekwa south africa kwa ajili ya postmortem na maandalizi ya mazishi. Ila kama kweli amefariki basi T.B. Joshua wa Nigeria atapata maujiko ile mbaya. Maana ni juzi tu karudia kusisitiza kwamba kuna raisi mzee wa Africa atafariki. Hapo watu wanaweza kujikuta wanamwamini mtu badala ya Mungu.
 
Tb Joshua alitoa utabiri tarehe na mwezi gani? R.I.P RAIS

Alitoa mwezi uliopita ila sikumbuki exact date. Pia alirudia Jumapili ya juzi tarehe 1/4 akasema, "it is too close".

Wengi waliposikia utabiri huo walihisi umemlenga Mugabe ambaye wanasema ana saratani na kwamba alishapewa prognosis yake kwamba anaweza kuvuta kwa miaka 5 tu na si zaidi ya hapo. Hisia hiyo pia ilitokana na kauli za TB Joshua kwamba atakayekufa atakuwa ni Rais wa umri mkubwa na atakufa kwa ugonjwa na si kwa kitu kingine.

Kwa sasa Bob Mugabe yuko mashariki ya mbali japo anasema ameenda kusaka shule ya mwanae, Bona Mugabe. Tetesi za mtaa wa pili zinasema kwamba ameenda kujiangalia afya yake,

Ajabu ni kwamba media houses za Malawi nazo zilikuwa zimeanza kuhisi kuwa huenda ni Mutharika ndo anaweza kuvuta. Baada ya rumor kuwa kali sana Mutharika mwenyewe alisema kama wiki mbili zilizopita kwamba atakayekufa si yeye, kama kuna wa-Malawi wanategemea kwamba atakufa basi watasubiri sana maana yeye (Mutharika) ana afya njema, yu bukheri na wala si mzee!
 
mbona alioa tena? alimuoa "former" minister wake ambaye waalipishana miaka kama 30 hivi.
wadau walikuwa wanasema mheshimiwa alikuwa anafanya mikakati ya kumrithisha mdogo wake
hiyo nafasi ya urais. rip bingu wa mutharika
Mama Chimombo pole kwa kufiwa na Mzee.
 
Joshua alikuwa anamlenga Mugabe na siyo Mutharika.
 
LILONGWE (Malawi Democrat)- Malawi President Bingu wa Mutharika has died after doctors at Kamuzu Central Hospital failed to resuscitate him.

Natizama aljazeera wanasema he is in critical condition.
 
Joshua alikuwa anamlenga Mugabe na siyo Mutharika.
Kwa bahati mbaya hakutaja jina la rais atakayekufa,kwa hiyo hakuna anayeweza kuconfirm kwamba alikuwa anamlenga mgabe au mwingine. Lakini kwa kuwa jumapili tu amesistiza kwamba mfaji yupo karibu sana kuondoka na leo ndiyo amekufa huyu basi bila shaka huyu ndiye aliyelengwa. Kama kweli Joshua alikuwa anaona katika maono yatokanayo na Mungu basi ni dhahiri hata Joshua mwenyewe alikuwa hajui ni yupi wa kufa, zaidi ya kuelekezwa na Mungu kwamba kuna mtu atakufa. But hofu yangu ni kuwa isijekuwa Joshua anafanya kazi kwa nguvu za ibilisi. Maana sidhani kama katika utabiri, Mungu atamfunulia mtu hili, ili afanye nalo nini? Na lina fundisho gani katika imani? Napata mashaka katika hilo.
 

Nasikia pia kuna mgogoro mkubwa ndani ya chama chake cha DPP. Hii migogoro ndani ya vyama sio tuu Tanzania. Hata Bingu nae alikimbia chama chake cha zamani cha UDF na kuanzisha DPP. Huyu makamu wa rais nae alikimbia DPP na kuanzisha chama chake baada ya kaka yake na Bingu, Peter Muathirika, kutangazwa rasmi kuwa mgombea urais mwaka 2014. Waafrika tunapenda madaraka ile mbaya
 
Utabiri wa tb joshua watimia,alisema ndani ya miezi miwili kuna rais barani africa atakufa watu wakagues mugabe.

Utabiri wa hivyo mbona rahisi ndugu? Angesema jina, mahali, siku, saa na dakika ya kufa mtu hapo ningestuka, lakini hii general statement sidhani! After all nani anajua afya bwana mkubwa ilikuwaje na kama huyu supposedly nabii alipata fununu kuwa afya ya bwana bingu ni mgogoro!
 
Mkuu huyo Bingu mwenyewe aliondoka na Urais kutoka kwenye Chama chake cha zamani ni kwenda nao kwenye Chama chake kipya! Huyo mama sasa ataukwaa Urais. Kumbe katiba yao kama ya TZ manake hapa napo Rais akivuta basi makamo anapata ulaji!
 
Duh! Yule mchungaji na Nabii T.B. Joshua wa Nigeria sasa namuaminia!
Yani wewe na wenzako kadhaa kwaajili ya miujiza "mnaaminia'' inaonekana mtaangamia kwa kukosa maarifa... cheki maandiko hapa yanasema nini ndugu zangu.
 
Haya mambo ya kutegemea ndugu hayafai. Sijui hali ya Peter Mutharika ipoje sasa. Bingu akifa Peter atakuwa na misiba miwili! Kufiwa na kaka yake na kufiwa na ndoto za kuwa Rais!
 
Hizi si tetesi tena, ni kweli kafariki dunia. Hapa ndipo utajua kwamba T.B. Joshua tabiri zake huwa za kweli. Wazimbabwe walidhani ni Mugabe, wao wakakataa kuwa hawakumtaja Mugabe. Majuzi kasema kifo chake kimekaribia zaidi.

Prophet TB Joshua Says

TB Joshua ni noma aisee. Prophecy fulfilled. Huyu jamaa ana kipaji/upako.
 
hizi habari hata mie zimenipa mashaka sana na ndio maana nimeweka tetesi tu maana sijui ukweli uko wapi, baadhi ya media zinadai jamaa amesha-rest in peace, nyingine zinadai yuko ICU, nani mkweli hapa
 
Hata Kabila walisema wanampeleka Zimbabwe kwa matibabu kumbe ilikuwa danganya toto Mzee alikuwa mbele za haki siku nyiingi.

Nadhani wanawaandaa wananchi kisaikojia na kupata nafasi ya kuandaa mazishi ya kitaifa tu hao hakuna cha South Africa wala nini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…