Prigozhin asema hataki tena kupigana Ukraine, anakuja Afrika

Prigozhin asema hataki tena kupigana Ukraine, anakuja Afrika

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Baada ya utata wa muda mrefu wa mahali alipo kiongozi wa kikundi cha askari wa kukodiwa cha Wagner leo ameonekana hadharani nchini Belarus alikohamishia shughuli zake baada ya jaribio la kutaka kuipindua serikali ya Urusi kuzimwa.

Katika video iliyomuonesha akisalimiana na askari wake aliwaambia askari hao kwamba wamepigana kishujaa sana nchini Ukraine na kwamba kwa sasa hawatapigana tena Ukraine bali wajitayarisha katika vita kama hivyo barani Afrika.

1689784919185.png
 
Unafikiri wanapigana bure?Wanalipwa.Na mara nyingi wanakuwa upande wa serikali inayotaka kubaki madarakani maisha yote. Wale marais wanaotaka kufia madarakani ndo wanawaita Wagner,wanawalipa pesa ndefu mno na wanawapa madini ya dhahabu, diamond na mengineyo bureee kabisa. Wapo Nchini Mali na Africa ya kati.
Waje tu mbona mgodi wa North Mara si tutawapa tu, wakurya kama wakurya.
 
Africa imegeuka soko zuri la askari wa kukodisha hasa kule Sahel (Mali) na Africa ya Kati.

Lini Africa itaweza kujisimamia yenyewe ?...
Inasikitisha sana,watu wanakodisha majeshi ili tu waendelee kukaa madarakani.Wale wanajeshi Mali wamenogewa na wala sidhani kama watarudisha madaraka kwa utawala wa kiraia tena.
 
Unafikiri wanapigana bure?Wanalipwa.Na mara nyingi wanakuwa upande wa serikali inayotaka kubaki madarakani maisha yote. Wale marais wanaotaka kufia madarakani ndo wanawaita Wagner,wanawalipa pesa ndefu mno na wanawapa madini ya dhahabu, diamond na mengineyo bureee kabisa. Wapo Nchini Mali na Africa ya kati.
Duuh,kumbe wajomba tayari wapo na wanakula mema kabisa
 
Eti ndipo useme Afrika tutakuja kuishi kwa amani 🙆🙆🙆😪😪
Uzuri wa Wagner hawana uzalendo na upande wowote na wala hawana huruma.Siku wanakuwa nawe na siku wanakusakama kama walivyofanya kwa Putin. Vile vile wakiingia kazini wanapigana kama majini.Mfumo wao huu ndio ulioipa ushindi Urusi kule Bakhmut na siku walipoondoka askari wa Ukraine walifurahi sana,
 
Baada ya utata wa muda mrefu wa mahali alipo kiongozi wa kikundi cha askari wa kukodiwa cha Wagner leo ameonekana hadharani nchini Belarus alikohamishia shughuli zake baada ya jaribio la kutaka kuipindua serikali ya Urusi kuzimwa.

Katika video iliyomuonesha akisalimiana na askari wake aliwaambia askari hao kwamba wamepigana kishujaa sana nchini Ukraine na kwamba kwa sasa hawatapigana tena Ukraine bali wajitayarisha katika vita kama hivyo barani Afrika.

View attachment 2693406
Nyinyi warusi wa Kigoma si mlisema Prigo anaenda Belarus ili awe karibu na Ukraine, nini kimebadilika ?
 
Nenda tu urusi baba huku kwetu hapana aisee huyu mwamba mziki wake sio wa kitoto
 
Unafikiri wanapigana bure?Wanalipwa.Na mara nyingi wanakuwa upande wa serikali inayotaka kubaki madarakani maisha yote. Wale marais wanaotaka kufia madarakani ndo wanawaita Wagner,wanawalipa pesa ndefu mno na wanawapa madini ya dhahabu, diamond na mengineyo bureee kabisa. Wapo Nchini Mali na Africa ya kati.
NAKAZIA,
kuna siku polisi WA Russia walifanya ukaguzi kwenye nyumba ya Wagner wakati alipotaka kumpindua Putin, wakakuta zaid ya Dollar M100+ na vipande vya Gold kama vyote

Wagner hafanyi kazi za njaa na ela anapokea kabla hajafanya kazi .
 
Back
Top Bottom