Wewe dada vipi.. Ni wapi nimeandika namchukia huyo mtoto?? Hivi nimchukie mtoto ambae sijui kama ana miaka hata miwili ili nipate nini??
Soma nilichoandika in general... Nimeongelea mitandao ya kijamii jinsi inavyotuaribia vijana wetu haijalishi nani kamfollow nani... Ni wapi nimesema watu wamfollow huyo Snura kwenye post yangu?? Nimesema ni aibu kwa mtoto mdogo kama huyo kupata followers zaidi ya laki tano wakati hana chochote anachokifanya.. It's a mess to have a country like that... Yaani unakuta account za matusi na kupigana vijembe zina followers laki 2 mpaka laki 5.. Hiyo ndiyo concern yangu.. Na kwenye post yangu nilishauri kama TCRA au Serikali inaweza kufungia hii mitandao au hata kulimit ni bora wafanye hivyo.. Kuna wakati mpaka video za ngono na picha za faragha zilikuwa zinatumwa kwenye hiyo mitandao kuchafuana tu angalau cyber crime pamoja na madhaifu yake imeweza kupunguza ilo tatizo..
Alafu ngoja nikwambie pia, NMB na hao wengine ambao wanamtumia huyo mtoto kwa matangazo ni kutokana na ujinga wetu wenyewe, NMB si wajinga waone huyo mtoto ana followers laki 5 wakaacha kumtumia.. Bad lucky ni kwamba hao followers laki 5 unaweza kukuta wote ni ambao kichwani hawako sawa kwahiyo hata kile wanachokilenga NMB hawakipati..
Subiri nikwambie kitu dada, Diamond ana followers million 2, wakati ana sign deal la Vodacom aliomba mashabiki wake wote wafollow Instagram Account ya Vodacom Tanzania, Akasema kama Mashabiki wake laki 1 wataifollow account ya Vodacom basi yule wa laki moja atampatia zawadi, by that time Vodacom ilikuwa na followers around 89k lakini mpaka leo Vodacom ina followers 96k pekee... Yaani ni sawa na kusema mtu mwenye influence ya followers million 2 amekusaidia kuongeza followers wasiozidi hata 10k... Alafu unajua hao NMB Tanzania anaowapromote huyo mtoto wana followers wangapi?? Wanao 6,637 mpaka dakika hii naandika... Sasa kwa mifano hiyo ndio ujue mashabiki wa hawa watu ni watu flani wasio na akili sawasawa bali wanatafuta umbeya na ujinga tu huko kwenye mitandao.. Ila simaanisha followers wao wote but majority ndio hao ambao hawana akili sawasawa... Ndio maana hata ile Ongea Daile ilishindwa..