Priyanka Chopra: Star mkubwa Indiana Hollywood afunguka kuhusu ndoa yake

Priyanka Chopra: Star mkubwa Indiana Hollywood afunguka kuhusu ndoa yake

Fumbokhan

Member
Joined
Jan 16, 2021
Posts
6
Reaction score
23
Priyanka Chopra(38) amesema yeye na mumewe Nick Jonas(28) bado hawana mtoto sababu yupo busy sana na kazi kutokana na mikataba aliyosaini hivyo inakuwa ngumu kwake kubeba mimba kwasasa lakini muda sahihi ukifika atabeba mimba kwakuwa yeye na Nick wana lengo la kuanzisha familia.

Priyanka amesema ndoa yao iliyofungwa 2018 ni muhimu sana kwao lakini bado kila mmoja anamhimiza mwenzie kufanya kazi kwa bidii. Ameongeza kuwa sababu wote mara nyingi wapo busy na kazi lakini ni lazima kila baada ya wiki mbili au tatu mmoja wapo amfuate mwenzie alipo wakaonane hata kama ni nje ya nchi kikazi lazima wakaonane kisha kila mmoja anaendelea na majukumu yake.

Priyanka aliwahi kusema kuwa sababu iliyomfanya amuone Nick kuwa ndiye mwanaume sahihi katika maisha yake ni kujivunia mafanikio aliyonayo huku akizidi kumpa moyo asonge mbele kwa bidii ya kazi afanikiwe zaidi.

Priyanka amesema wanaume aliowahi kuwa nao kabla walikuwa hawajiamini na hawakufurahia mafanikio yake sababu ya kuwa mwanamke na yeye hakutaka kubweteka hata wazazi wake walimlea na kumsomesha kwa bidii awe huru hata kipesa badala ya kutegemea mwanaume.

Nick na Priyanka wote kila mmoja ni milionea.

IMG_0869.jpg
 
.... huyo mumewe ni mhindi mwenzie au ni race gani? Ila Priyanka kwisha habari yake; sura ya kizee iko wazi usoni.
 
Penzi lao limeshikwa na upendo wa dhati ndio maana wako pamoja. Hayo unayotaka kuibua hapa hayana hoja ka kuna upendo wa kweli.
Probably, but huyo Nick ni mhuni na huyo Chopra pia alitaka kujiweka Hollywood na kuishi Marekani ( wahindi wanapenda sana kuishi Marekani ).

Wakati ndoa yao inafungwa, wahindi walikuwa wanamponda sana Chopra kwamba why kaolewa na mtu wa nje wakati wahindi wapo ( Ukichukulia alikuwa Miss World )

Baadaye, wakashangaa media za US zikaanza kumponda Chopra kuwa yeye ndio kalazimisha Nick ( ambaye ni mdogo kiumri ) amwoe ili aweze kupenya Hollywood.

Kutoka kuona kama Mzungu ndio kapata faida mpaka, Ikabidi wahindi tena waanze kumtetea mtu wao.

Wazungu hawana shobo kabisa na hawa viumbe.
 
Kama tu ndoa ya kanye west vs Kardashian inavunjika basi nimeamini ndoa zinazoanza na mahaba makubwa mwisho wake huwa ni machozi
 
Back
Top Bottom