Prof. Ali Mazrui mwalimu wangu wa masafa marefu

Prof. Ali Mazrui mwalimu wangu wa masafa marefu

Sheikh Mohamed na wewe unasikiliza mambo ya kikafir? Sikutegemea statement kama hiyo kutoka kwako Mzee wetu.
Dudus,
Bahati mbaya sana kwako.
Kwani ulikuwa na picha gani yangu?

Hapakuwa na haja ya kuwatukana watu wenye imani nyingine kwa kuwaita ''makafiri.''

Ungeweza kuaandika hayo yote kwa adabu na ungeeleweka.

Nilijaaliwa kipaji cha muziki toka udogo wangu.

Baba yangu alikuwa na collection kubwa sana ya muziki wa nyakati zake hadi Ball Room Dancing.

Athari za ukoloni wa Waingereza.

Nimezaliwa nimeikuta hiyo maktaba.

Najua kupiga guitar, key board na naweza kuimba ingawa ni miaka mingi sana imepita.

Lakini huwa nasikiliza muziki ninapokuwa na wakati.

Nimepata kuwashangaza wengi pale ninaponyanyua guitar au ninapokaa nyuma ya piano ingawa niko ''rusty.''

Hii picha nimepiga nyumbani kwa Dr. Harith Ghassany Mascut mwaka wa 2015 lakini hapa alikuwa anajua kuwa mimi najua kupiga piano.

Mara yake ya kwanza kushagaa ilikuwa 1999 hapa hapa nyumbani kwake nilipompigia, ''Crying in the Chapel,'' yeye na mkewe.

Ilikuwa ndiyo siku ya kwanza tunakutana.

1611400797033.png
 
Wazee wa takbir bana.
Wa kupuliza,
Unatoa hukumu haraka ukiwa unanihukumu kwa fikra zako utataabika.

Mimi ni huyo hapo chini nikiwa mwanafunzi Uingereza katika ujana wangu:

1611401120731.png


Hiyo picha hapo chini nilipiga nyumbani kwa Abdilatif Abdalla Humburg waka wa 2011, nilikuta mwanae ana guitar pale nyumbani.

Nilimfunza mwanae chords chache na nikapiga baadhi ya nyimbo ambazo bado nazikumbuka kama ''As Tears Go By,'' ya Rolling Stones.

Abdilatif alishangaa sana.

Ningependa kukufunza kitu.
Mimi si wa lugha hiyo ya ''bana'' na kejeli.

Kuwa na heshima andika kwa adabu tunaweza tukajadili mengi ambayo yatastawisha hii barza na tukafaidika sote, mimi, wewe na wengine.

Wanangu huangalia picha zangu za utotoni na wakaniuliza mengi kwa adabu kwa nia ya kutaka kunijua nami huwaeleza makuzi yangu.

1611401585639.png
 
The Boss,
Ahmed Rajab ni kaka kwangu, ndugu na rafiki.

Nimemtaja sehemu nyingi inabidi niingie Maktaba nianze kuchakura.

JF anaijua na angetaka angeshajiunga siku nyingi.
Mmmh, hapo sawa. Ahmed Rajab moto wa kuotea mbali. But not Mazrui, he is a nut, tungwita Farisayo.
 
Mmmh, hapo sawa. Ahmed Rajab moto wa kuotea mbali. But not Mazrui, he is a nut, tungwita Farisayo.

Mazrui was a nut? Nakushangaa sana wewe unaesema hivyo!!!!! Labda alikuwa na akili nyingi hata wazungu walimuheshimu.

Kwenye moja ya documentaries zake ‘The Africans: a triple heritage’ alieleza jinsi alivyokuwa promoted from lecturer to full professor bila ya kupitia zile hatua nyingine za chuo. Hata wenzake walishangaa.

Au unadhani akili nyingi wanazo wazungu tu?
 
Asante kwa bandiko

Hivi profesa Mazrui ana ujamaa na Ahmed Mazrui yule aliyetajwa kwenye kitabu cha Dr. Harith Gasanny cha 'Kwaheri ukoloni kwa heri uhuru'?

Mazrui wa katika kitabu hiko alikuwa akimiliki kampuni ya ujenzi ambayo John Okelo alikuwa kibarua katika kampuni hiyo.

Jecha, Mazrui ni kabila tu la waarabu kama vile ya huku bara. Mfano ukisema Mnyamwezi unajua anatoka Tabora.

Mazrui wa ‘Okello’ kama ninakumbuka vyema ni mzee wake Nassor Mazrui (iliwahi kuzungumziwa kwenye Zanzinet miaka kadhaa nyuma).

Nimejaribu kumtafuta yule aliyeandika ile makala sikufanikiwa.
 
MZEE KUMBE UMESOMESHWA NA WAKATOLIKI?

UNA KILA SABABU YA KUMSHUKURU NA KUMTUKUZA YESU KRISTO MWANA WA MUNGU ALIYE HAI KWA BARAKA ZAKE ZILIZOKUPATIA ELIMU

"Siku moja napita Kanti Bookshop duka la vitabu karibu na shule yangu St. Joseph's Convent nikakiona kitabu chake, "On Heroes and Uhuru Worship."
Huwa nawachukia sana watu kama Nyie. Watu wanajadili masuala wewe unawatoa kwenye mada! Bakia tu na kazi ya kulamba nayo za watawala huku tuache tunataka kujifunza. Tuache bhana
 
Back
Top Bottom