Prof. Janabi: Kitu hatari zaidi ni sukari na wanga. Ataka watu kula wakihisi njaa kwani mwili hauendeshwi na ratiba ya chakula

watanzania ni watu wanao weza kutembea na ungonjwa mpaka anazeeka bila kujitibu, akipata malaria inamuua haraka kwasbb inakuta mwili umeshakua dhaifu mda mrefu, watanzania tungekua na utamaduni wa kucheki afya zetu na kutibu ma hospitali yangekua na foreni kama ya mpira wa simba na Yanga. Ila tunauchuna tu ndo maana tunakufa mapema.
 


mkuu hiyoo comment inahusiana na kupima?
 
Watanzania asilimia 99 hawapati breakfast bali wanakunywa maji yenye sukari au unga wenye sukari na ngano
 
Mwili unaendeshwa kwa mazoea ukiendekeza kula milo mitatu utakuomba chakula kila unapo fika mda, tumezoea kula sana wa Tanzania hata masikini anakula na anamafuta mwili ya ziada.
Pavlov aliielezea vizuri kwa kutumia mfano wa Mbwa, kuwa ikiwa Mbwa umemzoesha kabla ya chakula lazima ugonge kengele na muda ni ule ule, basi muda huo ukifika usipogonga kengele hatakula
 
Idadi ya wagonjwa wachache umeipata wapi?
 
Na hospital nyingi huongezea watu magonjwa ya figo sababu ya kuwapa dawa bila kuwapima sahihi
 
Mzee baba hapo kwenye red sijakupata.

IPO HIVI,

Ukila wanga/Complex Sugar(mahindi, viazi, mihogo etc) mwili unaibadilisha kua glucose/Simple Sugar na unautumia kupata nguvu,

Ukisindilia sana mwili kwa kutumia INI unakusaidia kuhifadhi huo wanga/glucose kupeleka katika mfumo wa glycogen ikilazimika mafuta wakati mwingne.

Kwanini hubadilishwa???
huwezi ukahifadhi katika mfumo wa glucose, maana itayeyuka itarudi kwenye damu nakujaa/zidi matokeo yake ni KISUKARI sasa, ndio maana Katika kupima Sukari mwilini wanasema Blood glucose/sugar level, yaani kiwango cha sukari kwenye damu,

Pindi mwili ukiishiwa nguvu/mfano umechelewa kula au hujala, ile glycogen inatolewa kule ilikohifadhiwa kwa kutumia hormone ya glucagon kuileta kwenye mfumo wa glucose ambao ndio unatumiwa na mwili kupata nguvu.

Kwa nini mtu anazidi kunenepa? Kwa kula wanga,

Sbb ni kwamba kila siku anakula wanga iliyozidi kiasi kinachohitajika, matokeo yake inaendelea kuhifadhiwa/jaa kama glycogen kwenye misuli na mafuta sehemu zenye cells za mafuta.

Haya tuconnect Dots..... sasa...,
Unapozungumzia wanga unazungumzia Sukari/sugar na ukizungumzia sukari unazungumzia glucose na ukizungumzia glucose unazungumzia Nguvu.

Glucose iliyozidi ni Glycogen/Mafuta, mafuta yaliyozidi ndio huo ubonge na madhara yake anayozungumzia prof.

Ushawahi jiuliza kwa nini wachezaji wanapewa glucose uwanjani sio Dona???
 
Pavlov aliielezea vizuri kwa kutumia mfano wa Mbwa, kuwa ikiwa Mbwa umemzoesha kabla ya chakula lazima ugonge kengele na muda ni ule ule, basi muda huo ukifika usipogonga kengele hatakula
Kama unakumbuka pavlova conditioning theory kwa 70% utakua mualimu wa degree mkuu, unafundisha wapi au umesha acha ualimu kama mpyayungu Village
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…