Prof Jay: Operation rudisha shavu imeanza

Yesu amejitukuza kwenye maisha ya kaka Jay
Tuna mengi ya kujifunza toka kwenye msimu mgumu aliopitia
Na kwa wale wagonjwa wengine ambao waliugua na mwisho kufariki, vipi Tuseme Yesu hakutaka kujitukuza kwao? au Aliwapotezea? Au aliwadharau?

Kupona kwa prof jay Kwanza ni uwepo wa msaada wa kifedha uliopatikana kupitia Serikali yake na michango ya watu binafsi, maana Kwa maradhi yake kama kapuku kutoboa ni ngumu

Na mwisho kabisa ni bahati yake tu kuwa hai hadi muda huu, hayo mambo ya Yesu hivi au Yesu vile mbona wapo wanaofia Makanisani wakila maombi usiku kucha
 
Ni maradhi gani anayo Mkuu?
 


Kwetu kuishi ni Kristo kufa ni faida.

Wafilipi 1:21-27
Kwangu, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida zaidi.

Lakini, kama kwa kuishi nitaweza kufanya kazi yenye faida zaidi, basi, sijui nichague lipi!

Nakabiliwa na haya mawili yaliyo sawa. Natamani kuyaacha maisha haya nikakae pamoja na Kristo, jambo ambalo ni bora zaidi; lakini ni jambo la maana zaidi kwenu kama nikiendelea kuishi.
Nina hakika ya jambo hili, na hivyo najua kwamba nitaendelea kuishi pamoja nanyi nyote, ili nipate kuongeza maendeleo yenu na furaha katika imani.

Basi, nitakapokuwa nanyi tena mtakuwa na sababu ya kuona fahari juu yangu katika kuungana na Kristo Yesu.
Basi, jambo muhimu ni kwamba mwenendo wenu uambatane na matakwa ya Injili ya Kristo, ili kama nikiweza kuja kwenu au nisipoweza, nipate walau kusikia kwamba mnasimama imara mkiwa na lengo moja, na kwamba mnapigana vita kwa pamoja na mnayo nia moja kwa ajili ya imani ya Injili.
 
Ni maradhi gani anayo Mkuu?
Kwa taarifa ambazo sio rasmi, wanadai ni maradhi ya Figo mkuu, ni maradhi ambayo matibabu yake ni gharama sana ndugu yangu na ukiangalia muda ambao amejiuguza sio poa

Sasa inawezekana ilikuwa ishafikia hatua mbaya ndomana kakaa ICU almost nusu mwaka kabla ya kuondolewa na kuendelea na matibabu ya wodini Kwa mwaka mzima

tuwe wakweli tu Hapo kama mgonjwa ni kapuku na hana msaada wa kutoka kwenye familia yake au serikalini kama Kwa prof basi kuna Asilimia kubwa sana we ndio bye bye tu ndugu yangu
 
Astaghfilullah... yaani mchango wangu ndio umeenda kununua kiti moto?.. halafu nakaribishwa nikale?... sawa tu bwana Profesa, umeshinda wewe!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…