Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

Prof. Kabudi aieleza Jumuiya ya Kimataifa kuwa Tanzania haijawahi kushindwa vita ya aina yoyote

Sio lugha ya mwungwana. Prof ametegwa na system akaingia kingi (kama makonda kugombea kigamboni).. Atatumbuliwa soon kuridhisha wafadhili.. Atakuwa mbuzi wa kafara.. Serikali iljshakosea,wanatafuta namna ya kutoka
 
ila watanzania wanajua kujitutumua ila kwa wakati wa nyerere ilikuwa inawezekana ila kwa sasa sijui......

🙄 🙄 🙄
 
Nchi za afrika elewa haziwezi kamwe kujiendesha bila misaada ya au mikopo ya nje
Kila nchi ina kopa wamarekani wanadaiwa na China mkuu. Hivyo kukopa siyo shida hata hao wanaokopesha wanafanya hivyo ili wapate faida bila kukopesha wanakufa kwa njaa pia. Maana yake tunategemea wote!
 
kabudi alitakiwa kuwa mtu wa kutafuta suluhu na sio jeuri hii. Ukimwona hata ongea yake unagundua kuwa huyu mrtu sio mwanadiplomasia kabisa!
 
Kila nchi ina kopa wamarekani wanadaiwa na China mkuu. Hivyo kukopa siyo shida hata hao wanaokopesha wanafanya hivyo ili wapate faida bila kukopesha wanakufa kwa njaa pia. Maana yake tunategemea wote!
Unajihesabu nawe ni mjuaji, kwa kurahisisha mambo kihivyo!

Na si ajabu ukawa unashikilia nafasi mhimu ndani ya serikali hii inayopotosha kila jambo mradi tu ionekane inajitutumua.

Haya, hata nyinyi mna jeshi, kama walivyo nalo wamarekani. Unataka tuwape uwanja mkapimane nguvu?

Inawezekana kabisa usielewe maana ya mfano huo niliokuwekea hapo; na hata kama umeelewa utakaza tu shingo mradi uonekane mjuaji.

Watu wa hovyo sana nyinyi.
 
Watakaoumia ni wanyonge!
18901234.jpg
 


WAZIRI WA MAMBO YA NJE TANZANIA PROFESA PALAMAGAMBA KABUDI AWAJIBU MABEBERU, HATUJAWAHI KUPIGISHWA MAGOTI, UCHAGUZI ULIKUWA HURU NA HAKI

Waziri wa Mambo ya Nje Prof. Palamagamba Kabudi aijibu EU - Umoja wa Ulaya kufuatia kikao cha bunge hilo la ulaya huko makao makuu ya EU kutishia uwezekano wa vikwazo kupitia Kamati yake Mambo ya Nje ya Bunge la Umoja wa Ulaya kujadili uwezekano wa kuibana Tanzania kwa vikwazo vya aina mbalimbali ikiwemo kusitisha msaada wa kuifadhili bajeti ya Maendeleo ya Tanzania.

Prof. Palamagamba Kabudi ameomba msaada wa vyombo vya habari nchini kuisaidia serikali ya Tanzania kwa kujitokeza na kuieleza Jumuiya ya Kimataifa ukweli wa mambo. Na kueleza Nyerere aliwahi kuwadindia Germany na United Kingdom na kukataa misaada na fedha zao. Prof. Palamagamba Kabudi anashangaa waTanzania kuanza kutetemeka ktk mitandao ya kijamaii kuhusu nchi yetu kuwekewa vikwazo.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema Tanzania haifuati sera za kidiplomasia za kujitenga kufanya kazi na Jumuiya za Kimataifa. Hivyo waziri Prof. Kabudi amesema Tanzania ipo tayari kukaa ktk meza moja na wadau wa kimataifa kuzungumzia mapungufu yaliyopo lakini si kwa kuburuzwa na mabeberu bila kuwa na facts mezani.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa watu wahuni wachache wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Ulaya EU hawawezi kuitisha na kuidhalilisha Tanzania na watambue Tanzania ni nchi huru.

Prof. Palamagamba Kabudi amesema maneno hayo mazito akiongea na Wafanyakazi wa Wizara hiyo muhimu ya Mambo ya Nje akatumia fursa hiyo kujibu uvumi kuwa Tanzania itanyimwa misaada na kuwakumbusha wafanyakazi hao kutembea vifua mbele kwani Tanzania siyo nchi ndogo kidiplomasia, kimsimamo, kiji-Geopolitiki na kiushawishi kimataifa.

.....................................................

EU Parliament Committee on Foreign Affairs discussion on Tanzania​

Tujikumbushe walioitwa "wahuni wachache" na Prof. Kabudi, tarehe 19 November 2020 jijini Brussels kwa dakika 45 mfululizo walisema nini kuhusu Tanzania ktk kikao cha Kamati ya Mambo ya Nje cha Bunge la Jumuiya ya EU
Tazama / sikiliza dakika 45 za mjadala ktk kamati hiyo:



That’s right, prof! We have to stand our ground; we aren’t anyone’s colony!
 
Kila nchi ina kopa wamarekani wanadaiwa na China mkuu. Hivyo kukopa siyo shida hata hao wanaokopesha wanafanya hivyo ili wapate faida bila kukopesha wanakufa kwa njaa pia. Maana yake tunategemea wote!
TUNAWEZA KUKATAA MISAADA TUKAKOPA HILI HALINA SHIDA KABISA LAKINI EMBU TATHMINI JINSI DENI LA TAIFA LINAVYOPAA AT ATIME NA MISAADA TUNAPATIWA SASA MISAADA ISITISHWE NA TUWE TUNAKOPA TU NCHI ITAUZWA NDUGU
 
Huyu jamaa alinifanya nihairishe kusomea PHD pamoja na kuchaguliwa kusomea kozi hiyo Mlimani.

Yaani ukimuangalia unaona kabisa anaongea aliyotumwa akaseme Prof mzima unalazimishwa kuongea pumba kwa ajili ya kulinda nafasi yako
Prof Kabudi anajitoa ufahamu! Mwl Nyerere alikuwa na ubavu wa kuwakemea na hata kuwazuia hao anaowaita mabeberu. Mwl hakusita hata mara moja kutembelea na kuhutubia Umoja wa Mataifa, nchi mmoja mmoja na kuwapiga makofi (kauli kantu) bila woga. Aliweza hayo, mmoja kwa kuwa alikuwa na msimamo thabiti, alikuwa na mikono safi, aliaminika lakini pia alikuwa na nguvu ya ushawishi kwa ncha mbili- kwa wale Magharibi na kwa wale wa Mashariki! Ile vita baridi ilikuwa platform nzuri sana kwa Mwalimu.

Kwa sasa hivi, Prof Kabudi hajitambui, na wala hana plan B. Ukweli nisingependa nchi yangu inampigia magoti nchi nyingine, lakini si vyema, nchi yangu ikatumia mabavu kupata watawala, kukamata watu, kuhodhi vyombo vyote vya habari (CCM wamenunua vituo vyote vya Television - naamini bei haikufika kununua Azam TV, wamezuia magazeti yote huru na kuruhusu magazeti na vituo vya propoganda tena visivyo na lugha ya kiustrabu). Kwangu hizi tabia pia kwa taifa letu ndio KUPIGIA MAGOTI- KUJIDHALILISHA! Prof Kabudi anatakiwa aelekeze huko sio vingine!
 
Jalala bwana

Propaganda full na mimacho kilo mia elfu nane

Sovereignity kwa jambazi na uaji?

Wanapoiba na kuua watu ndio soverignity inasemwa wanataka....

Nyerere alikua na sababu serious na za kweli,jalala sababu zake ni uuaji na ujambazi wa kura...

Anadai ana takwimu na data ku-prove their case....data feki walizozipika wapeleke ziaminiwe,tunataka data kutoka kwa independent investigator na sio vitakwimu vilivyopikwa na jalala mwenyewe

Nchi huru yenye ruksa ya kuiba na kuua watu wake...kama uhuru ndio huo,basi na ufe!

Jalala
Uhuru wa Tanzania ni kuwabambikia kesi kesi uonevu unyanyasaji uovu mateso manyanyaso kuubaka kuunajisi kuulawiti uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani, hii ndiyo Nchi huru
 
Prof Kabudi anajitoa ufahamu! Mwl Nyerere alikuwa na ubavu wa kuwakemea na hata kuwazuia hao anaowaita mabeberu. Mwl hakusita hata mara moja kutembelea na kuhutubia Umoja wa Mataifa, nchi mmoja mmoja na kuwapiga makofi (kauli kantu) bila woga. Aliweza hayo, mmoja kwa kuwa alikuwa na msimamo thabiti, alikuwa na mikono safi, aliaminika lakini pia alikuwa na nguvu ya ushawishi kwa ncha mbili- kwa wale Magharibi na kwa wale wa Mashariki! Ile vita baridi ilikuwa platform nzuri sana kwa Mwalimu.

Kwa sasa hivi, Prof Kabudi hajitambui, na wala hana plan B. Ukweli nisingependa nchi yangu inampigia magoti nchi nyingine, lakini si vyema, nchi yangu ikatumia mabavu kupata watawala, kukamata watu, kuhodhi vyombo vyote vya habari (CCM wamenunua vituo vyote vya Television - naamini bei haikufika kununua Azam TV, wamezuia magazeti yote huru na kuruhusu magazeti na vituo vya propoganda tena visivyo na lugha ya kiustrabu). Kwangu hizi tabia pia kwa taifa letu ndio KUPIGIA MAGOTI- KUJIDHALILISHA! Prof Kabudi anatakiwa aelekeze huko sio vingine!
Kabudi kichwani kasalia na darasa la nne tu, vile alivyovisomea vyote vimefutika kichwani hana kilichosalia kwenye Ubongo ndiyo maana kawa na mikwara ya kichaa cha dog
 
Aliyoainisha Mhe Palamagamba Kabudi ni sahihi kabisa kwa upande mmoja wa sarafu lkn kwa mwenye akili aweza kuchambua hotuba ktk maeneo kadhaa kama ifuatavyo:-

(i). Kuhusu Mwl Nyerere kurudisha fedha kwa Uingereza na Ujerumani miaka ya 60 ilikuwa sawa - sasa kwa miaka hii ya 2020 ni sahihi kurudisha fedha sababu ya kulalamikiwa juu ya uchaguzi kughubikwa na mauaji, kutesa, na kukamata wapinzani?
Sawa ameeleza kuwa duniani kote huwa hakuna uchaguzi huru wala haki kwa standards ya 100 lkn amejiuliza kwa nini katiba ilitungwa, amejiuliza kwa nini Sheria zilitungwa? - Ni kwamba viwe vipimo vyetu ktk utendaji wa kila siku;

(ii). Madai ya kero za uchaguzi (kabla, wakati na baada ya uchaguzi). Hivi tumefika hatua ya kubariki mauaji, unyanyaswaji na ukandamizaji wa kidemokrasia kiasi cha kutambia dunia! Mie nilidhani kwamba angeeleza umma kuwa mambo yaliyojitokeza kwenye uchaguzi yanaendelea kushughulikiwa na mamlaka za ndani na kuahidi kupata suluhu kwa njia za mazungumzo na makundi yanayovutana - sasa chukulia mfano fedha za misaada zizuiliwe - hivi tutakuwa ni ukoo wa binadamu gani?

(iii). Viongozi, ndio wenye maslahi makubwa ya kitaifa sasa wasitengene njia za kuikosesha nchi misaada sababu bado tunaihitaji dunia, bado tuna changamoto kwenye afya, elimu, maji, kilimo, usafiri na usafirishaji, huduma za kiuchumi nk nk - kama tunatofautiana nao tutofautiane kwa sababu zenye uzito kama kukataa ushoga, udini, ukabila au ukanda lkn sababyinayotufanya leo tukosane ni ya kitoto na tunatakiwa kuizuia.

Mhe Palamagamba Kabudi, liangalie taifa hili limejaa watu wenye uhitaji sasa maslahi ya kisiasa kwa kundi dogo si sawa - wanaoathiriwa na kuzuiliwa fedha ni CCM, CDM, ACT, CUF, NCCR na vyama vingine pamoja na wasiokuwa na chama - ninyi mmeapa kutumikia hawa hawa ambao mnataka kuwasitishia misaada - NOT Good at all!

Msakila M Kabende
Kigoma
kweli wameapa kutumikia watu lakini hawajaapa kudharauliwa na wazungu kwa ajili ya misaada, BORA KUFA UMESIMAMA KULIKO KUISHI UMEPIGA MAGOTI.
 
Huyu naye na mahistoria yake ya kale kama kasuku. Sijui amekariri?

Vita ya idi Amini inatuhusu nini sisi? Watu wanahitaji chakula, maisha bora na economic security.

Stori za Idi Amini za kazi gani sasa! Hili zee nalo kwa kukariri halijambo!

Halafu hiyo sovereignty ni kitu gani? Kuua watu na kufanya uharamia bila kuulizwa?

Huyo profesa uchwara hatambui kwamba Tanzania ina wajibu wa kuheshimu sheria za kimataifa?

Ukiua watu wako recklessly kwa kutumia jeshi ni uhalifu wa kivita na unatakiwa kushughulikiwa na taasisi za kimataifa ikiwemo kuwekewa vikwazo, kupelekwa ICC au hata kushughulikiwa kijeshi kama Libya na Gambia!

Hakuna sovereignty ya kuua watu na kuwafanyia uharamia wa kijeshi. You must be answerable!

Huyu nae ni profesa wa sheria? Anafundisha family law NO WONDER!
 
Kuwa na degree 1, 2 au 3 haiondoi ujinga kama una njaa, hawa maprofesa wa Tz wanadhihirisha hilo
Wanaojiita maprofesa Tanzania ni tofauti na maprofesa wengine Duniani, wengi wa maprofesa wa Tanzania ni wasomi feki walioiba mitihani kununua vyeti kusoma kiujanja janja tu mpaka wakamiliki vyeti, ndiyo maana Akili zao ni za hovyo hovyo zisizofanana hata na maprofesa wa Sudan kusini
 
Back
Top Bottom