Prof Kabudi: Kati ya pesa na heshima ya nchi yetu, tutasimamia heshima. Tuko tayari kuwasikiliza na kujadiliana kwa heshima

Prof Kabudi: Kati ya pesa na heshima ya nchi yetu, tutasimamia heshima. Tuko tayari kuwasikiliza na kujadiliana kwa heshima

Kabudi ni Prof anaedhani kila mhadhara ni kueleza theory za hustoria.. you talking to the world alafu unatumia lugha ya ubabe na iliyokosa diplomasia?
Sishangai maana bado ni mbunge wa viti maalum
Ameshinda ubunge tena bila kupingwa
 
- Media zilitangaza bure kuhusu Corona

- Dawa za kupuliza zilikuwa msaada na baadaye Magufuli alizipiga marufuku tena kwa maneno makali kabisa akisema Corona ni futa hivyo unapopulizia dawa unaua kunguni!

*Nilichogundua na wewe unabahatisha na hauna majibu hivyo bado serikali inatakiwa itujibu pesa zimekwenda wapi?
 
Alipiga marufuku zikiwa zimesha nununuliwa tayari

-Media zilitangaza bure kuhusu Corona
-Dawa za kupuliza zilikuwa msaada na baadaye Magufuli alizipiga marufuku tena kwa maneno makali kabisa akisema Corona ni futa hivyo unapopulizia dawa unaua kunguni!

*Nilichogundua na wewe unabahatisha na hauna majibu hivyo bado serikali inatakiwa itujibu pesa zimekwenda wapi?
 
Yaan mpk muda huu najiuliza kuwa huyu kabudi hiyo elimu ya profesa mbona kama haitendei haki mweupe kichwani
Bunge la ulaya linauliza vigezo gani vilitumika kuipatia Tanzania hela wakati wao walisema corona free country nilitegemea majibu yake yangeanzia hapo alichokuja kujibu La Haula yaan kama ingekuwa swali la essay hata mtoto wa form four angejibu vizuri
Sitoaacha kusema elimu sio kuelimika bali ni kupata kazi ili uendeshe maisha yako
Yaan kama maprofesa wenyewe ndio dizaini ya kina Kabudi tumekwisha nina mashaka na uprofesa wake labda tumpe profesa wa jalalani mwenyewe alishasema ametoka jalalani naanza kuamini
 
Walitii masharti ya kutumia fedha hizo kama vile kupima watu korona kila siku na kutangaza matokeo kama alivyokuwa analalamika yule rais wa EU?
Safari hii Kalamaganda Kabugi amebugi vibaya sana maana anaenda kuozea jera
 
Kwani uongo hawakuchota mali zetu na kupeleka kwao?

Kama walibeba hadi kichwa cha Mkwawa, sembuse madini?

Wamebeba hadi masalia ya mijusi halafu nyie mpo mnakata mauno kuwasifia.

Wana husika sana katika underdevelopment of Africa hao vikaragosi wenu.
Kwani Wazungu walitawala nchi zote za Afrika?
 
Huyu kibudu sijui kama ni mzima!! Mtu uliyeokotwa kwenye mavumbi tangu lini ukawa na heshima? Mtu kila siku unaambiwa mpumbavu halafu unakenua meno, bado una heshima wewe?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Prof Kabudi ambaye ni waziri wa mambo ya nje amesema Tanzania haiwezi kuyumbishwa na vitisho vya kunyimwa misaada.

Kabudi amesisitiza kuwa Tanzania ni nchi huru inayoheshimu utu wa mtu na kamwe haitayumbishwa na nchi yoyote kwa vitisho vya kukatiwa misaada.

Kuhusu uchaguzi Prof Kabudi amesema ulikuwa huru na wa haki na dunia nzima imeshangaa maana hatukutumia posta kama wale wengine lakini uchaguzi wetu umefanyika kwa amani kabisa.

Source ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
=========

Prof. Kabudi: Nayasema haya kwa sababu kizazi cha sasa wanadhani hii nchi ndogo, sisi ndio nchi pekee hatujawahi kushindwa vita, hakuna mahali majeshi yetu yalipokwenda yakashindwa vita. Si Zimbabwe, Msumbiji, Comoro, Seychelles, si Uganda na hivi karibuni sio DRC Congo.

Nawahamasisha pia na vyombo vyetu vya habari tujue nini cha kuiambia dunia na watanzania, uchaguzi huu katika bara la Afrika umekuwa tulivu, wa amani.

There is nobody in the world has ever conducted a perfect election, give me one country! There is no country in the world which has conducted a perfect election. Perfect election is only conducted in heaven.

Mataifa yote yanafanya uchaguzi ambao ni huru, haki na wawazi na sisi wa utulivu na amani. Lazima tuiambie dunia hivyo na Taifa hili, nimesema na narudia, halijawahi kupigishwa magoti.

Na si jambo la kukumbusha kila wakati, sipendi, haina maana tunataka kufanya hivyo. Tulivunja uhusiano wa kibalozi na Uingereza mwaka 65 mpaka 72 na Mwalimu hakuvunja tu balozi na Uingereza, aliwarudishia msaada wao wote wa paundi milioni 5 na wakati ule zilikuwa nyingi, aliwarudishia.

Sisi leo watu wakisema vikwazo tu, tunaanza tetemeka nini? Hivi mngekuwa wakati wa Mwalimu! Hivi Tanzania ya 65 ni Tanzania ya leo? Lakini aliona kati ya heshima ya Tanzania na kudhalilishwa, aliwaambia waingireza, tumeshindwa kuelewana katika haya, basi. Ingawa tulibaki kuwa wanachama wa commonwealth.

Wajerumani mwaka 64 walipoanza kumpa masharti mwalimu baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ujerumani mashariki iko Zanzibar, Ujerumani Maghiribi iko Tanzania bara, tukawaambia hapana, hamuwezi kuanza kunipa masharti. Suala la kufunga ubalozi wa Ujerumani Mashariki Zanzibar, si la kuamua mimi, tupeni muda.

Walipomletea kejeli alilihutubia Taifa, aliwafukuza wataalam wote wa kijerumani na aliwarudishia hela yao dochmark milioni 35, sisi leo watu wachache tu wakikaa kuzungumza, ooh tutafanya hivi! tayari watu kwenye mitandao.

Kati ya pesa na heshima ya nchi yetu, tutasimamia heshima ya nchi yetu. Kati ya misaada na utu wetu, tutasimamia utu wetu. Hatutakubali kutoheshimiwa na utu wetu kudharauliwa kwa sababu ya misaada na pesa lakini tutashirikiana na mataifa yote duniani ambayo, moja yatatuheshimu sisi ni Taifa huru na yanatuheshimu sisi ni binadamu tulio sawa na wanadamu wengine wote na tuko tayari kuwasikiliza na kujadiliana kwa heshima yale ambayo wanadhani yamepungua kwetu na yale ambayo tunadhani yamepungua kwao, tuko tayari. We are ready for constructive engagement with those that respect we are sovereign state but who also respect that we are equal and as humans we have our dignity on those matters of principal, we will not compromise.

However we are ready to work with all nations in the world who share our values, sovereignity, equality of nation, human dignity and respect of all human kind and we will never, never allow anyone to use aid or assistance to undermine our sovereignity, NEVER.

That did not happen during the time of Mwalimu, it will never happen now and this is why I distributed this booklet to all staff from mwalimu Nyerere.
Heshima kuu kwa Profesa.
Profesa katika Azimio la Arusha iliamuliwa kuwa nguzo kuu za uchumi ziwe chini ya umma na Mwalimu akataifisha mabenki,makampuni,viwanda na hata mashamaba makubwa,what happened?
Mwalimu alivunja uhusiano na Uingereza baada ya I an Simith kufanya unilaterald declarartion na Mwalimu alikuja kutembelea Uingereza 1975,kwa nini Malkia au Waziri Mkuu hakuwa wa kwanza kuja kwetu?
Mwaka 1978/79 tulipigana vita na Uganda na tukashinda,je Profesa pangekuwa na fursa ya kujadiliana bado ungependelea vita kwa kuwa hatujawahi kushindwa?
Profesa,ikiwa nchi yetu ilikuwa na uchumi sawa na Thailand na baadhi ya nchi nyingine za Asia kusini na leo wametupita mara nyingi katika uchumi huoni kuwa misimamo yetu na maamuzi yetu tuliyowahi kufanya yamechangia katika hili?
Profesa,mwekezaji mkubwa toka nje ya Tanzania ni Kenya,kwa nini?
Nimeusilikiliza mjadala wote,walikuwa wanajdilaina wao kwa wao na sidhani kama hata walikuwa na hisia ya kuw atunafuatilia (ili waongeze mbwembwe kama wabunge wetu wanvyocharuka wakiona TV camera),hakuna mahali ambapo wametufokea,wameulizana kuhusu pesa za walip kodi wao,KWA NINI TUNATESEKA?
 
Prof Kabudi ambaye ni waziri wa mambo ya nje amesema Tanzania haiwezi kuyumbishwa na vitisho vya kunyimwa misaada.

Kabudi amesisitiza kuwa Tanzania ni nchi huru inayoheshimu utu wa mtu na kamwe haitayumbishwa na nchi yoyote kwa vitisho vya kukatiwa misaada.

Kuhusu uchaguzi Prof Kabudi amesema ulikuwa huru na wa haki na dunia nzima imeshangaa maana hatukutumia posta kama wale wengine lakini uchaguzi wetu umefanyika kwa amani kabisa.

Source ITV habari

Maendeleo hayana vyama!
=========

Prof. Kabudi: Nayasema haya kwa sababu kizazi cha sasa wanadhani hii nchi ndogo, sisi ndio nchi pekee hatujawahi kushindwa vita, hakuna mahali majeshi yetu yalipokwenda yakashindwa vita. Si Zimbabwe, Msumbiji, Comoro, Seychelles, si Uganda na hivi karibuni sio DRC Congo.

Nawahamasisha pia na vyombo vyetu vya habari tujue nini cha kuiambia dunia na watanzania, uchaguzi huu katika bara la Afrika umekuwa tulivu, wa amani.

There is nobody in the world has ever conducted a perfect election, give me one country! There is no country in the world which has conducted a perfect election. Perfect election is only conducted in heaven.

Mataifa yote yanafanya uchaguzi ambao ni huru, haki na wawazi na sisi wa utulivu na amani. Lazima tuiambie dunia hivyo na Taifa hili, nimesema na narudia, halijawahi kupigishwa magoti.

Na si jambo la kukumbusha kila wakati, sipendi, haina maana tunataka kufanya hivyo. Tulivunja uhusiano wa kibalozi na Uingereza mwaka 65 mpaka 72 na Mwalimu hakuvunja tu balozi na Uingereza, aliwarudishia msaada wao wote wa paundi milioni 5 na wakati ule zilikuwa nyingi, aliwarudishia.

Sisi leo watu wakisema vikwazo tu, tunaanza tetemeka nini? Hivi mngekuwa wakati wa Mwalimu! Hivi Tanzania ya 65 ni Tanzania ya leo? Lakini aliona kati ya heshima ya Tanzania na kudhalilishwa, aliwaambia waingireza, tumeshindwa kuelewana katika haya, basi. Ingawa tulibaki kuwa wanachama wa commonwealth.

Wajerumani mwaka 64 walipoanza kumpa masharti mwalimu baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ujerumani mashariki iko Zanzibar, Ujerumani Maghiribi iko Tanzania bara, tukawaambia hapana, hamuwezi kuanza kunipa masharti. Suala la kufunga ubalozi wa Ujerumani Mashariki Zanzibar, si la kuamua mimi, tupeni muda.

Walipomletea kejeli alilihutubia Taifa, aliwafukuza wataalam wote wa kijerumani na aliwarudishia hela yao dochmark milioni 35, sisi leo watu wachache tu wakikaa kuzungumza, ooh tutafanya hivi! tayari watu kwenye mitandao.

Kati ya pesa na heshima ya nchi yetu, tutasimamia heshima ya nchi yetu. Kati ya misaada na utu wetu, tutasimamia utu wetu. Hatutakubali kutoheshimiwa na utu wetu kudharauliwa kwa sababu ya misaada na pesa lakini tutashirikiana na mataifa yote duniani ambayo, moja yatatuheshimu sisi ni Taifa huru na yanatuheshimu sisi ni binadamu tulio sawa na wanadamu wengine wote na tuko tayari kuwasikiliza na kujadiliana kwa heshima yale ambayo wanadhani yamepungua kwetu na yale ambayo tunadhani yamepungua kwao, tuko tayari. We are ready for constructive engagement with those that respect we are sovereign state but who also respect that we are equal and as humans we have our dignity on those matters of principal, we will not compromise.

However we are ready to work with all nations in the world who share our values, sovereignity, equality of nation, human dignity and respect of all human kind and we will never, never allow anyone to use aid or assistance to undermine our sovereignity, NEVER.

That did not happen during the time of Mwalimu, it will never happen now and this is why I distributed this booklet to all staff from mwalimu Nyerere.
Professor wa jalalani.
 
Mtu akishakuwa mwalimu Kwa muda mrefu anakuwa theoretical sana, Hawa ma Prof perfomance zao sipo chini hawaujui uhalisilia ndo mana Mkwere aliachana nao wendelee kula vumbi la chaki
 
Back
Top Bottom