Prof. Kabudi: Rais amenituma kuwashukuru Watanzania kwa maombi, asema ameuona mkono wa Bwana

Prof. Kabudi: Rais amenituma kuwashukuru Watanzania kwa maombi, asema ameuona mkono wa Bwana

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
May 24, 2020
Dar es Salaam, Tanzania

Prof. Palamagamba Kabudi amesema ametumwa na Mh. Rais John Magufuli kuwashukuru waTanzania wote kwa maombi yao kipindi hiki cha janga la corona.



Prof. Palamagamba Kabudi akisoma ujumbe wa Rais unaosema alipoamua kutofunga nyumba za ibada wala kuifunga nchi kwa lockdown ni kuwa hakuyasema yeye kama binadamu (Mh.Rais) aliyeumbwa kwa nyama na damu bali alipata ujasiri na imani hiyo toka kwa Mungu. Kwani Mungu alimleta afanye kazi hiyo kama Musa alivyofanya kazi ya kuwavusha wana wa Israeli wavuke salama bahari ya Shamu kuwaepuka askari wa Farao.

Haikuwa uamuzi mdogo kwani kwa mujibu wa wataalamu idadi ya waTanzania zaidi ya 100,000 walitabiriwa lazima wafe kwa gonjwa la corona. Hivyo kutofunga Dar es Salaam wala Makanisa, Misikiti, Mahekalu na Masinagogi uamuzi huo ulikuwa mzito lakini Mungu ashukuriwe idadi ya vifo kutokana na corona ipo ndogo kabisa na vile ilivyotabiriwa kwa kweli ipo mbali sana na 100,000.

Mh. Rais anawaomba na kuwashukuru wa Tanzania walioomba Ijumaa, Jumamosi na Jumapili na waendelee kufanya hivyo kwa Mungu na kuliombea Taifa , anahitimisha Prof. Kabudi akiwakilisha Salaam za Mh. Rais kwa waTanzania.
 
Aibu Watanzania wengi akili zao bado zimeshikiliwa na wazungu. Sasa waliokufa ni wazungu wengi hasa USA, UK, Spain nk. Sasa leo hii wanabeza juhudi za taifa la Tanzania chini ya uongozi wa JPM.
 
Safi sana JPM rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Prof Kabudi wataendelea kuwa juu tu mtake msitake. Wivu unawasumbua wengi tu humu kwa sababu hawawezi kufanya yanayofanywa na mashupavu wa Tanzania.
 
May 24, 2020
Dar es Salaam, Tanzania

Prof. Palamagamba Kabudi amesema ametumwa na Mh. Rais John Magufuli kuwashukuru waTanzania wote kwa maombi yao kipindi hiki cha janga la corona.



Prof. Palamagamba Kabudi akisoma ujumbe wa Rais unaosema alipoamua kutofunga nyumba za ibada wala kuifunga nchi kwa lockdown ni kuwa hakuyasema yeye kama binadamu (Mh.Rais) aliyeumbwa kwa nyama na damu bali alipata ujasiri na imani hiyo toka kwa Mungu. Kwani Mungu alimleta afanye kazi hiyo kama Musa alivyofanya kazi ya kuwavusha wana wa Israeli wavuke salama bahari ya Shamu kuwaepuka askari wa Farao.

Haikuwa uamuzi mdogo kwani kwa mujibu wa wataalamu idadi ya waTanzania zaidi ya 100,000 walitabiriwa lazima wafe kwa gonjwa la corona. Hivyo kutofunga Dar es Salaam wala Makanisa, Misikiti, Mahekalu na Masinagogi uamuzi huo ulikuwa mzito lakini Mungu ashukuriwe idadi ya vifo kutokana na corona ipo ndogo kabisa na vile ilivyotabiriwa kwa kweli ipo mbali sana na 100,000.

Mh. Rais anawaomba na kuwashukuru wa Tanzania walioomba Ijumaa, Jumamosi na Jumapili na waendelee kufanya hivyo kwa Mungu na kuliombea Taifa , anahitimisha Prof. Kabudi akiwakilisha Salaam za Mh. Rais kwa waTanzania.

Prof bhana!.........mbali kabisa na 100,000 ndio wapi huko?

Hahahaaaa........ Natania tu bwashee!
 
Aibu Watanzania wengi akili zao bado zimeshikiliwa na wazungu. Sasa waliokufa ni wazungu wengi hasa USA, UK, Spain nk. Sasa leo hii wanabeza juhudi za taifa la Tanzania chini ya uongozi wa JPM.
Taabu ni kuwa katika nchi hii sasa tunachanganya sayansi na siasa. Kama unaelewa sayansi ya magonjwa haya huwezi kulinganisha nchi za ulaya na chi za Africa. Tunatofautiana sana katika mambo yanayopelekea maambukizi, hivyo hatuwezi kujigamba kuwa hatua tulizochukua ndio zimepunguza maambukizi! Acheni siasa, litazameni hili jambo kisayansi ili tuongelee na kusupport maamuzi yanayoonyesha kuwa maambukizi yamepungua, with evidence!
 
Taabu ni kuwa katika nchi hii sasa tunachanganya sayansi na siasa. Kama unaelewa sayansi ya magonjwa haya huwezi kulinganisha nchi za ulaya na chi za Africa. Tunatofautiana sana katika mambo yanayopelekea maambukizi, hivyo hatuwezi kujigamba kuwa hatua tulizochukua ndio zimepunguza maambukizi! Acheni siasa, litazameni hili jambo kisayansi ili tuongelee na kusupport maamuzi yanayoonyesha kuwa maambukizi yamepungua, with evidence!

Pengine unachukulia hili jambo kwa udogo/ukubwa hoja hapa ni Je, JPM alichukua hatua sahihi? Jibu ni ndiyo kwa sababu hatukuathirika ki-vile wengi walivyotegemea. Sasa hapo unaongelea sayansi ipi? Sayansi ipo kwenye dawa siyo jinsi unavyokabiliana na janga. Je Wazungu wamepata dawa? Hapana, sisi Tanzania tayari dawa ipo sasa unataka nini? Kuhusu maambukizi: Je, wapi kulikuwa na maambukizi mengi Tanzania au Ulaya?
 
Ila hii serekali kweli imedhamiria kwa dhati kumdhihaki Mungu.

serekali ime opt kwenye "herd immunity" option ambayo kwa hesabu za haraka haraka inaweza kuua Watanzania kati ya laki 5 hadi milioni 1 (idadi ambayo itakuwa approx 50% ya Waafrika wote watakaopoteza maisha potentially) endapo sisi wananchi wenyewe hatutachukua hatua za kujilinda na kuendekeza uzwazwa wa hawa kina zero brain (Bashite, etc).

lakini hapana shaka Mungu wetu mkuu atakuwa ameandaa moto ulao dhidi ya hawa watesi wanaonuka damu za Watanzania wengi wasio na hatia. Karma!

Watanzania tujilinde huku tukiendelea kuomba msaada wa Mungu. Killer corona is lurking out there big time!
 
Back
Top Bottom