Prof. Lipumba aikataa Kamati ya Prof. Mukandala. Asema hakuna mjumbe aliyesema mchakato wa Katiba usubiri hadi mwaka 2025

Prof. Lipumba aikataa Kamati ya Prof. Mukandala. Asema hakuna mjumbe aliyesema mchakato wa Katiba usubiri hadi mwaka 2025

Huyu ni miongoni mwa Wajumbe walioteuliwa na Rais chini ya Rwekaza Mukandala, Anaitwa Haruna Lipumba ambaye ni Mwenyekiti wa CUF.

Jionee mwenyewe


"Mimi nilikuwa mjumbe kwenye mkutano uliofanyika Dodoma na hakuna mjumbe hata mmoja aliyesema mchakato wa katiba usubiri hadi mwaka 2025. Baraza la Uongozi linapinga pendekezo la kikosi kazi juu ya suala hili la katiba mpya kusubiri 2025"
mjumbe kachomoa betri
 
Wache hizi delaying tactics, hazisaidi kitu. Anzisheni mchakato wa katiba mpya muda na mazingira si rafiki kwenu.
 
Huyu ni miongoni mwa Wajumbe walioteuliwa na Rais chini ya Rwekaza Mukandala, Anaitwa Haruna Lipumba ambaye ni Mwenyekiti wa CUF.

Jionee mwenyewe


"Mimi nilikuwa mjumbe kwenye mkutano uliofanyika Dodoma na hakuna mjumbe hata mmoja aliyesema mchakato wa katiba usubiri hadi mwaka 2025. Baraza la Uongozi linapinga pendekezo la kikosi kazi juu ya suala hili la katiba mpya kusubiri 2025"
Dar es Salaam. Chama cha Wananchi (CUF) kimemteua Hamad Masoud Hamad kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, akichukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Haroub Mohamed Shamis.

Masoud ameteuliwa kushika wadhifa huo, akitokea Chama cha ACT Wazalendo alikokuwa akilalamika kuchezewa rafu katika uchaguzi aliogombea nafasi ya Mwenyekiti, ambapo Juma Haji Duni ndiye aliyechaguliwa kushika nafasi hiyo.

Baraza hilo pia limewateua Kona Vuai Haji na Juma Shaaban Nkumbi kuwa wajumbe wa baraza kuu huku nafasi nyingine zilizo wazi zikipangwa kujazwa katika kikao kijacho cha baraza kuu.

Kauli hiyo imetolewa leo Machi 28 jijini hapa na Mwenyekiti wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba wakati wa kutangaza maazimio ya ajenda 14 zilizotokana na mkutano wa baraza hilo, ikiwamo mabadiliko ya uongozi, hali ya ngumu ya maisha, vita vya Urusi na Ukraine na hali ya kisiasa.

“Baraza Kuu limemshukuru Haroub Mohamed Shamis kwa kazi kubwa aliyofanya kama Katibu Mkuu katika kipindi kigumu baada ya kifo cha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama, hayati Khalifa Suleiman Khalifa na kukiwezesha chama hicho kushiriki kikamilifu katika uchaguzi Mkuu wa 2020,” amesema Lipumba.

Azimio lingine la baraza hilo ni pampoja na kuweka kando masharti ya Ibara ya 116 kifungu kidogo cha 6 yaliyopo kwenye Katiba ya chama hicho ya mwaka 1992 Toleo la 2019, yanayozuia mwanachama mpya kugombea nafasi ya uongozi hadi atakapokuwa ametimiza miezi sita.

Baraza hilo pia limeondoa kikwazo hicho ili kuhakikisha wanachama wanaorejea ndani ya chama hicho kushiriki katika ujenzi wa chama hicho huku likitangaza kuanza kwa uchaguzi wa ndani kati ya Mei 14 mwaka huu hadi Oktoba 2023.
 
Lipumba hajawahi kuwa Professor hata siku moja cheo cha juu alichowahi fikia ni Associate Proffesa yaani msaidizi wa Profesa yeye na Huyo anaitwa Proffesa Assad hawajawahi fikia ngapi ya uprofessor wote waliishia kuwa wasaidizi wa maprofesa ila mitaani watu wanawaita ma Proffesa sijui kwa nini wakati vyeo vya juu waliyowahi fikia ni Associate Professor.

Hivi Dr Musukuma nae ni associate Professor au bado hajafikia.Bado sijaona tofauti Professor Lipumba na Associate Professor Musukuma.
 
Huyu ni miongoni mwa Wajumbe walioteuliwa na Rais chini ya Rwekaza Mukandala, Anaitwa Haruna Lipumba ambaye ni Mwenyekiti wa CUF.

Jionee mwenyewe


"Mimi nilikuwa mjumbe kwenye mkutano uliofanyika Dodoma na hakuna mjumbe hata mmoja aliyesema mchakato wa katiba usubiri hadi mwaka 2025. Baraza la Uongozi linapinga pendekezo la kikosi kazi juu ya suala hili la katiba mpya kusubiri 2025"
Kumbe Akina Mkandala walienda kutunga ya kwao?
 
Back
Top Bottom