Prof. Lipumba atoa maelezo ya CAG kuhusu CUF chama cha wananchi

Prof. Lipumba atoa maelezo ya CAG kuhusu CUF chama cha wananchi

Nimejaribu luwaza maneno yale na luyalinganisha na uaomi wake wa uchumi, NAHISI KAMA HAVINA UHUSIANO
 
Mwenyekiti wa Cuf Prof Lipumba amesema sh 300m za ruzuku walizihamishia kwenye akaunti binafsi ya mwanachama mwaminifu Omari Muhina ili kuzilinda zisiibiwe pale benki.

Prof Lipumba amesema hayo alipozungumza na waandishi wa habari leo.

Source ITV habari
Professor anayeamini mwanachana ni mwaminifu kuliko benki!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahaa sasa nimemuelewa Prof. walipewa 380, hizo 80 zikanunulia magari, wakaamua kuhamisha mia tatu ili zisiibiwe.
 
Ni zaidi ya mpigaji kama maccm wenzake
Ahaa sasa nimemuelewa Prof. walipewa 380, hizo 80 zikanunulia magari, wakaamua kuhamisha mia tatu ili zisiibiwe.

In God we Trust
 
Hiyo si ni sawa na yaliyowakuta AVEVA na NYANGE KABURU viongozi wa Simba wa zamani

Pale walipohamisha fedha za Uhamisho wa OKWI.

AU Siasa na soka ni tofauti
 
Hizi fedha ndiyo zilisababisha Lipumba na Magdalena Sakaya wakawa wanalala kwenye ofisi ya chama usiku wakawa wanafanya mazoezi ya judo.
 
Najiuliza wazo la Vyama vya siasa kupewa fedha za "ruzuku" mwanzilishi wake duniani alikuwa nani?
Wanasiasa au vyama vyao na watawala au viongozi wa vyama tawala ni makundi yanayogombea na yale yanayoishi kwa jasho la walalahoi.
Ili kupunguza ugomvi, ukawekwa utaratibu wa kuwagawia kidogo wale wenye lengo la kuwaondoa wale walioshikilia mirija kwa wakati huo.
Hata hivyo, utaratibu huu umekubalika na umehalalishwa kisheria (kwa mtazamo wa fikra huru).
 
Maelezo mazuri, siasa ni mradi mzuri sana nchini Tanzania.
P

Ingekuwa CHADEMA chama kikuu cha Upinzani na tishio kwa chama tawala, story hii ingekuwa kubwa sana kwenye media zote. Thank God haya yote yamefanywa na Lipumba na chama kibaraka wa CCM, so it doesn't really matter.

Siku moja haya yote yatapatiwa hukumu yake stahiki.
 
Bado zipo mpaka leo? Acheni uzwazwa Lumumba FC hizo ni kodi zetu
Mwenyekiti wa Cuf Prof Lipumba amesema sh 300m za ruzuku walizihamishia kwenye akaunti binafsi ya mwanachama mwaminifu Omari Muhina ili kuzilinda zisiibiwe pale benki.

Prof Lipumba amesema hayo alipozungumza na waandishi wa habari leo.

Source ITV habari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tarehe 26 March 2020, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere aliwasilisha ripoti ya ukaguzi wake ya 2018/19 kwa Rais John Magufuli katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Jijini Dodoma.Pamoja na Mambo mengine CAG Charles Kichere alisema:

"Mheshimiwa Rais, nilibaini Chama cha Wananchi CUF kilipokea ruzuku toka Serikalini ya Kiasi cha Shilingi milioni 369.38 Lakini Chama hicho kilihamisha kiasi cha shilingi milioni 300 kutoka akaunti ya Chama kwenda akaunti binafsi ya mwanachama na kiasi cha shilingi milioni 69 kilitolewa kama fedha taslimu.

Hata hivyo nyaraka za matumizi ya fedha hizo hazikuwasilishwa kwangu kwa ajili ya ukaguzi."

Kauli hii ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali imeleta mtafaruku na sintofahamu kubwa kuhusu usimamizi wa fedha za Chama cha CUF.Ni vema tukaweka sawa kumbukumbu zetu kwamba tukio hili lilitokea Januari 2017. Wakati huo Chama chetu kilikuwa katika mgogoro wa uongozi na akaunti za Chama katika Benki ya NMB zilikuwa na tishio la kuzuwiwa.

Naomba nikumbushe kuwa tarehe 2 Desemba 2016,Tume ya Taifa ya Uchauzi ilitangaza uchaguzi mdogo wa Udiwani katika kata 22 za Tanzania Bara.Nikumbushe kuwa baadaye Time ilifanya masahihisho na kueleza kuwa ni kata 20 ndizo zitakazohusika na uchaguzi mdogo.Pia CUF iliamua kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo la Dimani,Zanzibar.

Hatimaye Chama kilisimamisha wagombea 14 kati ya kata 20 zilizotangazwa kurejesha uchaguzi.Upande wa Zanzibar CUF iliweka Mgombea Ubungo Jimbo la Diwani
Naomba nikumbushe kuwa wakati uchaguzi mdogo unatangazwa,Chama kilikuwa hakipewi ruzuku ya serikali.Kwa sababu tulitaka kushiriki uchaguzi na hatukuwa na fedha,mnamo tarehe 28 Desemba 2016 nilimuandikia Msajili wa vyama vya Siasa kuiomba Ofisi yake ikipatie Chama chetu fedha zitokanazo na ruzuku ya kila mwezi ya chama toka Serikalini ili kiweze kishiriki kikamilifu katika chaguzi ndogo zilizotangazwa kurejewa hapa nchini na kutekeleza Mpango Mkakati wa Ujenzi wa Chama chetu.

Msajili wa Vyama vya Siasa aliridhia Chama kipate sehemu ya ruzuku ili kishiriki katika uchaguzi na kutekeleza shughuli za Chama.Fedha hizo ziliwekwa kwenye akaunti ya Chama ya Benki ya NMB,tawi la Temeke.

Katika kipindi kulikuwa na tishio la aliyekuwa Katibu Mkuu kuzuia akaunti zetu zote za Chama upande wa Tanzania Bara zisifanye kazi.Katika hali hiyo Kamati ya Utendaji iliamua shilingi 300 tulizoomba kwa ajili ya kugharamia uchaguzi zihamishwe akaunti ya Benki.Mwanachama huyo ni Masoud Mhina Omari,aliyekuwa Naibu Katibu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama na sasa Naibu Mkurugenzi wa Mafunzo,Itifaki na Udhibiti.

Shilingi milioni 69 zilitolewa kama fedha taslimu kuanzia kugharamia shughuli za kampeni za uchaguzi zikiwemo ziara za viongozi kwenda kwenye kata zenye uchaguzi mdogo.

Fedha zote zilizowekwa kwenye akaunti ya Masoud Mhina Omari zilitumiwa na Chama katika masuala ya Uchaguzi na uendeshaji wa shughuli za chama.Wakaguzi wa CAG waliokuja kutukagua walipewa maelezo haya na nyaraka za matumizi ya Chama ya Mwaka2016/17.

Chama kinamshukuru Masoud Mhina Omari kwa Uaminifu wake.Hatua ya kuweka fedha kwenye akaunti yake ilitusaidia kukamilisha shughuli za chama kwani baadaye Benki ya NMB ilizuwia kutoa fedha kwenye akaunti zetu zote za Tanzania Bara.

Naomba nisisitize tukio hili la kuhamisha fedha kwenda akaunti ya Masoud Mhina Omari lilitokea Januari 2017 kwa sababu ya tishio la kuzuia kutoa fedha toka akaunti za Chama.

Mgogoro wa Chama umemalizika na taratibu za fedha zinazingatia kanuni za fedha za Chama.

Tunakubaliana na Ushauri wa CAG kuwa mifumo ya udhibiti wa fedha ndani ya chama iimarishwe kwa kufuata sheria na Katiba ya Chama .Hivi sasa Mhasibu anaandaa mfumo imara wa udhibiti wa fedha ndani ya chama.

Prof.Ibrahim Haruna Lipumba
Mwenyekiti waTaifa,27 March 2020.
lipumba ni mwizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yeye katuhumiwa hadharan kwenye media na yeye anajibu kwenye media

Ikija kwenye mahojiano na Takukuru na yeye atawajibu kwa documents

Hapo kwenye hoja ya CAG hakuna wizi aliotuhumu, kilichokiukw ni control z fedha kitu ambacho sio kosa la jinai ni kosa la kiutendaji tu, ndio sababu CAG kaishia ku report kuwa fedha zilihamishiwa kwenye acoount binafsi hakusema fedha zimeibiwa
Baada ya kuhamishiwa kwny Account binafsi walichofanya ni kuhakikisha kila matumizi yalipata authority and supporting documents hapo mchezo umekwisha, Lipumba mtoto wa Mjini
Nafuu angenyamaza kimya,asubili Takukuru wakati wanamhoji ndipo awajibu,sasa anajibu kwenye vyombo vya habari ,hana hata aibu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mbona wanatofatiana maelezo na idara ya habar ya CUF, niliona uzi humu ndani wakisema kipindi hicho hawausiki,chama kilikuwa chini ya maalimu seif, au nulielewa vibaya wadau?
Yalikuwa ni maoni ya wa Cdm, Cuf walikuwa hawajatoa tamko lolote rasmi.
 
Back
Top Bottom