Prof. Lipumba: Bajeti iliyosomwa ni mbovu haijawahi kutokea tangu tupate uhuru. Takwimu nyingi haziko sahihi

Prof. Lipumba: Bajeti iliyosomwa ni mbovu haijawahi kutokea tangu tupate uhuru. Takwimu nyingi haziko sahihi

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Waziri wa fedha amechemka. Maana hata takwimu alizotoa hazilandani na kilichomo kwenye bajeti.

Na hii bajeti haikufanyiwa utafiti

Profesa Lipumba: Bajeti ya Serikali mbovu kuwahi kutokea.

=========

Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameikosoa bajeti ya Serikali akisema ni mbovu kuwahi kutokea tangu apate uzoefu wa kuzichambua bajeti zinazowasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.

Kutokana na kasoro alizodai kuwemo katika bajeti hiyo, Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa uchumi, ameishauri Serikali kujenga utamaduni wa kufanya utafiti wa kina wa sera za kodi ili kutengeneza mipango ya kukuza maendeleo na kuongeza ajira kwa vijana na kutokomeza umaskini.

Ameyasema hayo leo Juni 19 jijini hapa wakati akiichambua bajeti ya Serikali iliyosomwa bungeni Juni 14, akifafanua kuwa bajeti hiyo imeshindwa kuakisi malengo ya Rais Samia Suluhu Hassan likiwemo la kuanzisha Tume huru ya uchaguzi.

"Hotuba hiyo ilikuwa mbovu mbovu kuwahi kutokea kwa Waziri wa Wizara ya fedha tangu kupata uzoefu wangu wa kupitia na kuzichambua bajeti zote," amesema.

Ametoa mfano wa taarifa za Wizara ya Mifugo akisema hazioani na kitabu cha hali ya uchumi.

“Ukirejea kwenye kitabu cha uchumi wa taifa hazipo, napata wasiwasi. Naomba kabla ya kwenda kusoma bajeti ni vizuri zipitiwe na wataalamu kuhakikiwa tarakimu kabla ya kwenda kusomwa zifanane na zile zilizopo kwenye kitabu cha hali ya ukuaji uchumi wa taifa," amesema.

Kuhusu mfumuko wa bei amesema Watanzania wanalalamika kuongezeka kwa gharama za maisha. Kila kitu hasa vyakula na nishati vimepanda bei, lakini taarifa ya Serikali inaeleza kuwa bei zimeongezeka kwa asilimia 4 tu jambo ambalo alilodai kuwa si kweli.

"Vitu ulivyonunua kwa Sh100,000 Mei 2021, watu kwa sasa wanatumia Sh104,000 tu Mei 2022. inashangaza kuona takwimu za Serikali gharama za maisha nchini zimeongezeka kwa kasi ya chini kuliko gharama za maisha Marekani na nchi za Ulaya," amesema.

Kuhusu elimu bila malipo, Profesa Lipumba amesema katika bajeti hiyo Serikali imetangaza kufuta ada za kidato cha tano na sitana kujigamba kuwa sasa Tanzania ina elimu bure toka darasa la kwanza hadi kidato cha sita. lakini ukweli ni kwamba ada ni sehemu ndogo chini ya asilimia 10 kwa kidato cha tano na sita za gharama ambazo mzazi ana wajibika kulipa ili mwanae aenendelee na masomo.

Kuhusu sera za kodi, alisema Waziri huyo amefanya makosa kuunganisha vitambulisho vya taifa na ulipaji wa kodi hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali haijakamilisha zoezi la kuwapatia vitambulisho vya taifa watanzania wote baada ya zaidi ya miaka kumi toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kuanzishwa.

"Ni muhimu Serikali ikajikita kuharakisha Wananchi kupata vitambulisho vyao, lakini wakiendelea kuongelea suala hilo wanaweza kusababisha watu wasijisajili wakijua kufanya hivyo watatozwa kodi," amesema.


CREDIT: Mwananchi
 
Waziri wa fedha amechemka. Maana hata takwimu alizotoa hazilandani na kilichomo kwenye bajeti.
Na hii bajeti haikufakyiwa utafiti
Profesa Lipumba: Bajeti ya Serikali mbovu kuwahi kutokea Profesa Lipumba: Bajeti ya Serikali mbovu kuwahi kutokea
Kwani Lipumba hajalamba asali?

Lipumba amelambishwa asali kiduchu kwenye kijiko, Anataka asali full galon la litre 5 na sio kupimiwa kama kijiko

Mpeni asali professor kama Zito kabwe

Mpeni asali atulie

Lakini professor nae atulie si alilamba asali mwaka 2015 wakati wa uchaguzi akaikacha ukawa na Mwenzake Dr Slaa, Watosheke sasa Waache vijana nao walambe asali
 
Kumbe povu lote la lipumba shida hakuna fungu la tume huru 😂😂😂😂
Kuhusu sera za kodi, alisema Waziri huyo amefanya makosa kuunganisha vitambulisho vya taifa na ulipaji wa kodi hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali haijakamilisha zoezi la kuwapatia vitambulisho vya taifa watanzania wote baada ya zaidi ya miaka kumi toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kuanzishwa.

Sikumakinika kwenye hili, tume imeanzisha na imeshatimiza miaka 10? Wabongo wanaostahili kupata National ID ni wangapi? Wangapi wameshapatiwa?

Kazi kubwa na ya msingi ya hiyo NIDA ni nini?

Mimi ni mmoja wa wasio na hiyo ID.
 
Wafipa wanasemaje
Wanasema [emoji116][emoji116]
FVC_WPnX0AAEHnv.jpg
 
Mwigulu anaandaa bajeti ili kumfurahisha bosi wake bila kuihusianisha na mipango, matokeo yake ndio haya ametengeneza bomu asilojua alitegue vipi.

Matokeo yake kila akitolea ufafanuzi wa jambo anazidi kuongeza maswali badala ya kutamaliza.
 
Bila shaka ni zile za kuweka mzigo mezani, halafu Maprofesa wenye njaa wanapitisha machapisho yako kiulaini.
Mtu mwenye Phd ya uchumi huwezi kupendekeza viga'amuzi kulipiwa tozo. Au kila mtanzamia akifikisha umri wa miaka kumi na nane alipe kodi. Ina maana ukiwa mtu mzima tu kodi.
 
Waziri wa fedha amechemka. Maana hata takwimu alizotoa hazilandani na kilichomo kwenye bajeti.

Na hii bajeti haikufakyiwa utafiti
Profesa Lipumba: Bajeti ya Serikali mbovu kuwahi kutokea.
===
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameikosoa bajeti ya Serikali akisema ni mbovu kuwahi kutokea tangu apate uzoefu wa kuzichambua bajeti zinazowasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.

Kutokana na kasoro alizodai kuwemo katika bajeti hiyo, Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa uchumi, ameishauri Serikali kujenga utamaduni wa kufanya utafiti wa kina wa sera za kodi ili kutengeneza mipango ya kukuza maendeleo na kuongeza ajira kwa vijana na kutokomeza umaskini.

Ameyasema hayo leo Juni 19 jijini hapa wakati akiichambua bajeti ya Serikali iliyosomwa bungeni Juni 14, akifafanua kuwa bajeti hiyo imeshindwa kuakisi malengo ya Rais Samia Suluhu Hassan likiwemo la kuanzisha Tume huru ya uchaguzi.

"Hotuba hiyo ilikuwa mbovu mbovu kuwahi kutokea kwa Waziri wa Wizara ya fedha tangu kupata uzoefu wangu wa kupitia na kuzichambua bajeti zote," amesema.

Ametoa mfano wa taarifa za Wizara ya Mifugo akisema hazioani na kitabu cha hali ya uchumi.

“Ukirejea kwenye kitabu cha uchumi wa taifa hazipo, napata wasiwasi. Naomba kabla ya kwenda kusoma bajeti ni vizuri zipitiwe na wataalamu kuhakikiwa tarakimu kabla ya kwenda kusomwa zifanane na zile zilizopo kwenye kitabu cha hali ya ukuaji uchumi wa taifa," amesema.

Kuhusu mfumuko wa bei amesema Watanzania wanalalamika kuongezeka kwa gharama za maisha. Kila kitu hasa vyakula na nishati vimepanda bei, lakini taarifa ya Serikali inaeleza kuwa bei zimeongezeka kwa asilimia 4 tu jambo ambalo alilodai kuwa si kweli.

"Vitu ulivyonunua kwa Sh100,000 Mei 2021, watu kwa sasa wanatumia Sh104,000 tu Mei 2022. inashangaza kuona takwimu za Serikali gharama za maisha nchini zimeongezeka kwa kasi ya chini kuliko gharama za maisha Marekani na nchi za Ulaya," amesema.

Kuhusu elimu bila malipo, Profesa Lipumba amesema katika bajeti hiyo Serikali imetangaza kufuta ada za kidato cha tano na sitana kujigamba kuwa sasa Tanzania ina elimu bure toka darasa la kwanza hadi kidato cha sita. lakini ukweli ni kwamba ada ni sehemu ndogo chini ya asilimia 10 kwa kidato cha tano na sita za gharama ambazo mzazi ana wajibika kulipa ili mwanae aenendelee na masomo.

Kuhusu sera za kodi, alisema Waziri huyo amefanya makosa kuunganisha vitambulisho vya taifa na ulipaji wa kodi hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali haijakamilisha zoezi la kuwapatia vitambulisho vya taifa watanzania wote baada ya zaidi ya miaka kumi toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kuanzishwa.

"Ni muhimu Serikali ikajikita kuharakisha Wananchi kupata vitambulisho vyao, lakini wakiendelea kuongelea suala hilo wanaweza kusababisha watu wasijisajili wakijua kufanya hivyo watatozwa kodi," amesema.


CREDIT: Mwananchi
Profesa Ibrahim Lipumba ni profesa wa uchumi anaetumia elimu yake, kulichumia tumbo lake.
 
Huyu Lipumba amewahi kuleta impact gani kwenye uchumi wetu.
Toka nakua namuona yupo CUF anakimbizana na polisi.
Sasa huo ubobevu aliupata wapi?
 
Kuhusu mfumuko wa bei amesema

"Vitu ulivyonunua kwa Sh100,000 Mei 2021, watu kwa sasa wanatumia Sh104,000 tu Mei 2022. inashangaza kuona takwimu za Serikali gharama za maisha nchini zimeongezeka kwa kasi ya chini kuliko gharama za maisha Marekani na nchi za Ulaya," amesema.
Hapa Profesa kachemka
Bei may zilikuwa chini Juni ziko juu na watu wananunua.

Inflation Haina shida kama.uwezo.wa watu kununua upo

Mei mosi Raisi alitangaza ongezeko la mishahara na marupurupu alitegemea bei zibaki palepale?
 
Hapa Profesa kachemka
Bei may zilikuwa chini Juni ziko juu na watu wananunua.

Inflation Haina shida kama.uwezo.wa watu kununua upo

Mei mosi Raisi alitangaza ongezeko la mishahara na marupurupu alitegemea bei zibaki palepale?
Punguza porojo. Bei za vitu zilipanda kabla hata mishahara kutangazwa kupandishwa au vita ya Ukraine kuanza. Baada ya vita kuanza ndipo Samia akaibuka kusingizia vitu vimepanda baada ya vita kuanza.
 
Punguza porojo. Bei za vitu zilipanda kabla hata mishahara kutangazwa kupandishwa au vita ya Ukraine kuanza. Baada ya vita kuanza ndipo Samia akaibuka kusingizia vitu vimepanda baada ya vita kuanza.
Ukitangaza tu publically mishahara kupanda Kesho wafanya biashara wanapandisha bei
 
Bei zilipanda kabla ya mishahara kutangazwa na kabla ya vita ya Ukraine. Baadae Samia akaibuka kuja kusingizia vita ya Ukraine. Anatuona WaTz wajinga tusiojua kitu.
Lipumba kalinganisha may na June hayo yako ya Ukraine vita ya Ukraine iliyoanza February baki nayo mwenyewe
 
Back
Top Bottom