Professor wamchongo [emoji3]Kumbe povu lote la lipumba shida hakuna fungu la tume huru [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Revenue expenditure over Capital expenditure....deterioration of an economy..Lakini hata mimi naunga mkono kuwa hii bajeti nadhani ni ya ovyo kwa maana serikali yetu kutenga trilioni moja na kichele kwa ajili ya maendeleo AF trilioni 13 kwa matumizi ya kawaida hilo jambo linatia wasiwasi sana
Huyu jamaa hajawahi badili haya maneno tangu aingie siasaniWaziri wa fedha amechemka. Maana hata takwimu alizotoa hazilandani na kilichomo kwenye bajeti.
Na hii bajeti haikufanyiwa utafiti
Profesa Lipumba: Bajeti ya Serikali mbovu kuwahi kutokea.
===
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameikosoa bajeti ya Serikali akisema ni mbovu kuwahi kutokea tangu apate uzoefu wa kuzichambua bajeti zinazowasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Kutokana na kasoro alizodai kuwemo katika bajeti hiyo, Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa uchumi, ameishauri Serikali kujenga utamaduni wa kufanya utafiti wa kina wa sera za kodi ili kutengeneza mipango ya kukuza maendeleo na kuongeza ajira kwa vijana na kutokomeza umaskini.
Ameyasema hayo leo Juni 19 jijini hapa wakati akiichambua bajeti ya Serikali iliyosomwa bungeni Juni 14, akifafanua kuwa bajeti hiyo imeshindwa kuakisi malengo ya Rais Samia Suluhu Hassan likiwemo la kuanzisha Tume huru ya uchaguzi.
"Hotuba hiyo ilikuwa mbovu mbovu kuwahi kutokea kwa Waziri wa Wizara ya fedha tangu kupata uzoefu wangu wa kupitia na kuzichambua bajeti zote," amesema.
Ametoa mfano wa taarifa za Wizara ya Mifugo akisema hazioani na kitabu cha hali ya uchumi.
“Ukirejea kwenye kitabu cha uchumi wa taifa hazipo, napata wasiwasi. Naomba kabla ya kwenda kusoma bajeti ni vizuri zipitiwe na wataalamu kuhakikiwa tarakimu kabla ya kwenda kusomwa zifanane na zile zilizopo kwenye kitabu cha hali ya ukuaji uchumi wa taifa," amesema.
Kuhusu mfumuko wa bei amesema Watanzania wanalalamika kuongezeka kwa gharama za maisha. Kila kitu hasa vyakula na nishati vimepanda bei, lakini taarifa ya Serikali inaeleza kuwa bei zimeongezeka kwa asilimia 4 tu jambo ambalo alilodai kuwa si kweli.
"Vitu ulivyonunua kwa Sh100,000 Mei 2021, watu kwa sasa wanatumia Sh104,000 tu Mei 2022. inashangaza kuona takwimu za Serikali gharama za maisha nchini zimeongezeka kwa kasi ya chini kuliko gharama za maisha Marekani na nchi za Ulaya," amesema.
Kuhusu elimu bila malipo, Profesa Lipumba amesema katika bajeti hiyo Serikali imetangaza kufuta ada za kidato cha tano na sitana kujigamba kuwa sasa Tanzania ina elimu bure toka darasa la kwanza hadi kidato cha sita. lakini ukweli ni kwamba ada ni sehemu ndogo chini ya asilimia 10 kwa kidato cha tano na sita za gharama ambazo mzazi ana wajibika kulipa ili mwanae aenendelee na masomo.
Kuhusu sera za kodi, alisema Waziri huyo amefanya makosa kuunganisha vitambulisho vya taifa na ulipaji wa kodi hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali haijakamilisha zoezi la kuwapatia vitambulisho vya taifa watanzania wote baada ya zaidi ya miaka kumi toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kuanzishwa.
"Ni muhimu Serikali ikajikita kuharakisha Wananchi kupata vitambulisho vyao, lakini wakiendelea kuongelea suala hilo wanaweza kusababisha watu wasijisajili wakijua kufanya hivyo watatozwa kodi," amesema.
CREDIT: Mwananchi
Ndiye mpinzani anayetegemewa kuchambua bajeti tangu 1996Kasema vizuri ila kisiasa hapo ategemee mambo mawili kulamba asali ili atulie au kinyume chake ,kikubwa atulie .
Au Yoweri Museveni wa UgandaMuulize rais ,(Mwinyi senior) baada ya Nyerere
Hiyo point uliyowekea rangi ni ya muhimu sana kwani itafanya watu wasitafute tena hivyo vitambulisho vya NIDA kukwepa kodi. Ni sera ambayo imetolewa bila umakini wowote. Swala la vitambulisho vya uraia lisiunganishwe na kodi, ama sivyo watu hawatavitafuta. Lina unintended consequences nyingi kuliko faidaKuhusu sera za kodi, alisema Waziri huyo amefanya makosa kuunganisha vitambulisho vya taifa na ulipaji wa kodi hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali haijakamilisha zoezi la kuwapatia vitambulisho vya taifa watanzania wote baada ya zaidi ya miaka kumi toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kuanzishwa.
Sikumakinika kwenye hili, tume imeanzisha na imeshatimiza miaka 10? Wabongo wanaostahili kupata National ID ni wangapi? Wangapi wameshapatiwa?
Kazi kubwa na ya msingi ya hiyo NIDA ni nini?
Mimi ni mmoja wa wasio na hiyo ID.
Kiswahili rahisi kueleweka CCM na serikali yao wangesema tu kuwa, KODI YA KICHWA imerudishwa baada ya kuondolewa miaka zaidi ya 22 iliyopita ili watu tujadili na tujue tunakokwenda...Mtu mwenye Phd ya uchumi huwezi kupendekeza viga'amuzi kulipiwa tozo. Au kila mtanzamia akifikisha umri wa miaka kumi na nane alipe kodi. Ina maana ukiwa mtu mzima tu kodi.
Kusema kuwa national ID watu hawatavitafuta, ni kujidanganya tu...Hiyo point uliyowekea rangi ni ya muhimu sana kwani itafanya watu wasitafute tena hivyo vitambulisho vya NIDA kukwepa kodi. Ni sera ambayo imetolewa bila umakini wowote. Swala la vitambulisho vya uraia lisiunganishwe na kodi, ama sivyo watu hawatavitafuta. Lina unintended consequences nyingi kuliko faida
Mfano mmoja mzuri ni kuwa serikali ya Trump ilitaka kutumia Sensa ya mwaka 2020 kuweka kipengele ambacho kinataka mtu aeleze kama ni raia au si raia. Kifungu hicho kilipingwa vikali kwa sababu kingesababisha watu wasiokuwa raia wasijitokeze kuhesabiwa kwa kuogopa kunyanyaswa na serikali. Sensa inataka kujua widadi ya watu halisi wanaoishi nchini siyo kujua uraia wao; kikafutwa.
Tumia akili, soda ilikuwa inauzwa sh 500, sasa inauzwa 600, imepanda kwa aslimia 20. Nauli ilikuwa 400 sasa 500, imepanda kwa asolimia 25. Imflation kwa mwaka ni asilimia 20-25. Huo ni mfano tu, sasa mwigulu anasema inflation ni asilimia 4 amepata wapi. Usichoelewa ni nini hapo. Kifupi ukitaka kuweka watu wako kwenye uongozi haya ndio matokeo yake.Kwa hiyo hicho kilichoandikwa hapo ndio uchambuzi wa Professor Mbobezi na nguli wa uchumi!? Au mmepunguza alichosema? Maana sioni Hizo takwimu (facts and figures) alizotoa hapo!
Kweli unezaliwa juz na humjui proof vxrHuyu Lipumba amewahi kuleta impact gani kwenye uchumi wetu.
Toka nakua namuona yupo CUF anakimbizana na polisi.
Sasa huo ubobevu aliupata wapi?
Ni ngumu sana kumuamini mwanasiasa kama LipumbaWaziri wa fedha amechemka. Maana hata takwimu alizotoa hazilandani na kilichomo kwenye bajeti.
Na hii bajeti haikufanyiwa utafiti
Profesa Lipumba: Bajeti ya Serikali mbovu kuwahi kutokea.
===
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameikosoa bajeti ya Serikali akisema ni mbovu kuwahi kutokea tangu apate uzoefu wa kuzichambua bajeti zinazowasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Kutokana na kasoro alizodai kuwemo katika bajeti hiyo, Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa uchumi, ameishauri Serikali kujenga utamaduni wa kufanya utafiti wa kina wa sera za kodi ili kutengeneza mipango ya kukuza maendeleo na kuongeza ajira kwa vijana na kutokomeza umaskini.
Ameyasema hayo leo Juni 19 jijini hapa wakati akiichambua bajeti ya Serikali iliyosomwa bungeni Juni 14, akifafanua kuwa bajeti hiyo imeshindwa kuakisi malengo ya Rais Samia Suluhu Hassan likiwemo la kuanzisha Tume huru ya uchaguzi.
"Hotuba hiyo ilikuwa mbovu mbovu kuwahi kutokea kwa Waziri wa Wizara ya fedha tangu kupata uzoefu wangu wa kupitia na kuzichambua bajeti zote," amesema.
Ametoa mfano wa taarifa za Wizara ya Mifugo akisema hazioani na kitabu cha hali ya uchumi.
“Ukirejea kwenye kitabu cha uchumi wa taifa hazipo, napata wasiwasi. Naomba kabla ya kwenda kusoma bajeti ni vizuri zipitiwe na wataalamu kuhakikiwa tarakimu kabla ya kwenda kusomwa zifanane na zile zilizopo kwenye kitabu cha hali ya ukuaji uchumi wa taifa," amesema.
Kuhusu mfumuko wa bei amesema Watanzania wanalalamika kuongezeka kwa gharama za maisha. Kila kitu hasa vyakula na nishati vimepanda bei, lakini taarifa ya Serikali inaeleza kuwa bei zimeongezeka kwa asilimia 4 tu jambo ambalo alilodai kuwa si kweli.
"Vitu ulivyonunua kwa Sh100,000 Mei 2021, watu kwa sasa wanatumia Sh104,000 tu Mei 2022. inashangaza kuona takwimu za Serikali gharama za maisha nchini zimeongezeka kwa kasi ya chini kuliko gharama za maisha Marekani na nchi za Ulaya," amesema.
Kuhusu elimu bila malipo, Profesa Lipumba amesema katika bajeti hiyo Serikali imetangaza kufuta ada za kidato cha tano na sitana kujigamba kuwa sasa Tanzania ina elimu bure toka darasa la kwanza hadi kidato cha sita. lakini ukweli ni kwamba ada ni sehemu ndogo chini ya asilimia 10 kwa kidato cha tano na sita za gharama ambazo mzazi ana wajibika kulipa ili mwanae aenendelee na masomo.
Kuhusu sera za kodi, alisema Waziri huyo amefanya makosa kuunganisha vitambulisho vya taifa na ulipaji wa kodi hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali haijakamilisha zoezi la kuwapatia vitambulisho vya taifa watanzania wote baada ya zaidi ya miaka kumi toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kuanzishwa.
"Ni muhimu Serikali ikajikita kuharakisha Wananchi kupata vitambulisho vyao, lakini wakiendelea kuongelea suala hilo wanaweza kusababisha watu wasijisajili wakijua kufanya hivyo watatozwa kodi," amesema.
CREDIT: Mwananchi
Anamjua. Pale anamwambia boss wake kwamba kibarua wake ni chengaMwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Mhe. Ibrahim Lipumba amesema Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Mchemba amefanya makosa ya kimkakati kuunganisha vitambulisho vya Taifa na ulipaji kodi huku akieleza itaathiri motisha ya wananchi kujisajili kupata vitambulisho hivyo..
Chanzo: DarMpya Blog.
Yaani na Wewe Baba yangu Mzee Lipumba ninavyokuheshimu kwa kuwa na IQ kubwa hukumjua tu huyo ni typical Nut?
BAJETI YA KIHUNI HII UONGO MWINGI KULIKO UKWELI ETI TUNABANA MATUMIZI HUWEZI KUBANA MATUMIZI KWA NCHI YENYE VIONGOZI WASIO WAZALENDO KWA NCHI NA WANANCHIWaziri wa fedha amechemka. Maana hata takwimu alizotoa hazilandani na kilichomo kwenye bajeti.
Na hii bajeti haikufanyiwa utafiti
Profesa Lipumba: Bajeti ya Serikali mbovu kuwahi kutokea.
=========
Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ameikosoa bajeti ya Serikali akisema ni mbovu kuwahi kutokea tangu apate uzoefu wa kuzichambua bajeti zinazowasilishwa katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Kutokana na kasoro alizodai kuwemo katika bajeti hiyo, Profesa Lipumba ambaye ni mtaalamu wa uchumi, ameishauri Serikali kujenga utamaduni wa kufanya utafiti wa kina wa sera za kodi ili kutengeneza mipango ya kukuza maendeleo na kuongeza ajira kwa vijana na kutokomeza umaskini.
Ameyasema hayo leo Juni 19 jijini hapa wakati akiichambua bajeti ya Serikali iliyosomwa bungeni Juni 14, akifafanua kuwa bajeti hiyo imeshindwa kuakisi malengo ya Rais Samia Suluhu Hassan likiwemo la kuanzisha Tume huru ya uchaguzi.
"Hotuba hiyo ilikuwa mbovu mbovu kuwahi kutokea kwa Waziri wa Wizara ya fedha tangu kupata uzoefu wangu wa kupitia na kuzichambua bajeti zote," amesema.
Ametoa mfano wa taarifa za Wizara ya Mifugo akisema hazioani na kitabu cha hali ya uchumi.
“Ukirejea kwenye kitabu cha uchumi wa taifa hazipo, napata wasiwasi. Naomba kabla ya kwenda kusoma bajeti ni vizuri zipitiwe na wataalamu kuhakikiwa tarakimu kabla ya kwenda kusomwa zifanane na zile zilizopo kwenye kitabu cha hali ya ukuaji uchumi wa taifa," amesema.
Kuhusu mfumuko wa bei amesema Watanzania wanalalamika kuongezeka kwa gharama za maisha. Kila kitu hasa vyakula na nishati vimepanda bei, lakini taarifa ya Serikali inaeleza kuwa bei zimeongezeka kwa asilimia 4 tu jambo ambalo alilodai kuwa si kweli.
"Vitu ulivyonunua kwa Sh100,000 Mei 2021, watu kwa sasa wanatumia Sh104,000 tu Mei 2022. inashangaza kuona takwimu za Serikali gharama za maisha nchini zimeongezeka kwa kasi ya chini kuliko gharama za maisha Marekani na nchi za Ulaya," amesema.
Kuhusu elimu bila malipo, Profesa Lipumba amesema katika bajeti hiyo Serikali imetangaza kufuta ada za kidato cha tano na sitana kujigamba kuwa sasa Tanzania ina elimu bure toka darasa la kwanza hadi kidato cha sita. lakini ukweli ni kwamba ada ni sehemu ndogo chini ya asilimia 10 kwa kidato cha tano na sita za gharama ambazo mzazi ana wajibika kulipa ili mwanae aenendelee na masomo.
Kuhusu sera za kodi, alisema Waziri huyo amefanya makosa kuunganisha vitambulisho vya taifa na ulipaji wa kodi hasa katika kipindi hiki ambacho Serikali haijakamilisha zoezi la kuwapatia vitambulisho vya taifa watanzania wote baada ya zaidi ya miaka kumi toka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida) kuanzishwa.
"Ni muhimu Serikali ikajikita kuharakisha Wananchi kupata vitambulisho vyao, lakini wakiendelea kuongelea suala hilo wanaweza kusababisha watu wasijisajili wakijua kufanya hivyo watatozwa kodi," amesema.
CREDIT: Mwananchi