Uchaguzi 2020Prof. Lipumba: Wananchi wa hapa Somanga nasikia mnachomewa moto nyavu zenu na mnanyanyaswa sana, sasa nichagueni Oktoba 28 nimalize huu unyanyasaji
WANANCHI WA HAPA SOMANGA NASIKIA MNACHOMEWA MOTO NYAVU ZENU NA MNANYANYASWA SANA SASA NICHAGUENI OKTOBA 28,NIWE RAIS NISIMAMIE HAKI ZA BINADAMU"PROF.LIPUMBA"
KILWA- SOMANGA
Uvunjifu na ukiukwaji wa Haki za binadamu ni tatizo kubwa nchini Tanzania.
Hakuna chombo huru chenye nguvu cha kusimamia haki za binadamu.
Tume ya haki za binadamu haina nguvu za kuweza kupambana na wavunjaji wa haki za binadamu. Wengi wa hawa ni watendaji wakuu wa serikali ambao wanalindwa na mfumo uliopo.
Mkinichagua kuwa Rais wa nchi hii nitasimamia ipasavyo haki za Binadamu.