Prof. Makubi afanya kikao cha kimkakati na Madaktari Bingwa/bobezi ndani ya MOI

Prof. Makubi afanya kikao cha kimkakati na Madaktari Bingwa/bobezi ndani ya MOI

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Makubi.jpg

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Prof. Abel Makubi, leo Julai 12, 2023 amefanya kikao na madaktari bingwa/Bobezi wa MOI ili kujadili kwa pamoja namna ya kuboresha huduma kwa wagonjwa, suala la huduma kwa wateja, uwajibikaji wenye matokeo , kuwa na mtazamo chanya pamoja na kuongeza na kuifanya Taasisi iweze kupata fedha za kutosha kununua vifaa na dawa ili kuondoa mahangaiko kwa Wananchi.

Kikao hiki ni muendelezo wa vikao baina ya Prof. Makubi na makundi mbalimbali ya watumishi wa MOI vyenye lengo la kupata maoni, ushauri na changamoto ili kuleta mageuzi makubwa katika Taasisi ya MOI ambayo sasa ina miaka 26 tangia kuanzishwa kwake.
252f4d6a-cfd0-4cfc-9e33-e1f28497dccb.jpg

2c8b69dd-8757-4b2e-9621-604ed28024b7.jpg

Prof. Makubi amewaomba ushirikiano wa dhati madaktari bingwa ili kuleta mageuzi makubwa katika utoaji huduma za kibingwa za Mifupa, Ubongo, Mgongo na mishipa ya fahamu hapa nchini.

“Niwaombe madaktari bingwa na wasomi wenzangu, kila mtu abadilike na kujielekeza kwenye muelekeo huu wa menejimenti unaolenga kuleta matokeo chanya, kuongeza uwajibikaji; sioni sababu ya kwanini tubaki hapa tulipo nashauri twende haraka tuboreshe huduma, mazingira ,vifaa na dawa viwepo vya kutosha; naamini uwezo huo tunao” Alisema Prof. Makubi

“Katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu tujipange kukamilisha ujenzi wa jengo jipya kisasa la kuona wagonjwa wa nje (OPD) ambalo litakuwa na vyumba vya kliniki vya kutosha na vyenye hadhi ya kimataifa ili wagonjwa wengi zaidi kutoka Tanzania na mataifa mengine wapate huduma” Alisema Prof. Makubi.
m.jpg

Kwa upande wao Madaktari bingwa wa MOI wamemuahidi Prof. Makubi kuongeza uwajibikaji, kufanya kazi kwa bidiii, kuwa na ‘Sense of ownership’ kwa taasisi ili kuboresha huduma kwa wagonjwa pamoja na kuifanya taasisi iweze kumudu gharama za mahitaji ya msingi ya kutolea huduma.
 
Mimi maoni yangu wawe waadilifu, nilikuwa na mgonjwa wangu hapo Muhimbili (sio MOI) alipofariki dawa zilizobaki hatukuziona!
 
View attachment 2685799
Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Prof. Abel Makubi, leo Julai 12, 2023 amefanya kikao na madaktari bingwa/Bobezi wa MOI ili kujadili kwa pamoja namna ya kuboresha huduma kwa wagonjwa, suala la huduma kwa wateja, uwajibikaji wenye matokeo , kuwa na mtazamo chanya pamoja na kuongeza na kuifanya Taasisi iweze kupata fedha za kutosha kununua vifaa na dawa ili kuondoa mahangaiko kwa Wananchi.

Kikao hiki ni muendelezo wa vikao baina ya Prof. Makubi na makundi mbalimbali ya watumishi wa MOI vyenye lengo la kupata maoni, ushauri na changamoto ili kuleta mageuzi makubwa katika Taasisi ya MOI ambayo sasa ina miaka 26 tangia kuanzishwa kwake.
View attachment 2685800
View attachment 2685801
Prof. Makubi amewaomba ushirikiano wa dhati madaktari bingwa ili kuleta mageuzi makubwa katika utoaji huduma za kibingwa za Mifupa, Ubongo, Mgongo na mishipa ya fahamu hapa nchini.

“Niwaombe madaktari bingwa na wasomi wenzangu, kila mtu abadilike na kujielekeza kwenye muelekeo huu wa menejimenti unaolenga kuleta matokeo chanya, kuongeza uwajibikaji; sioni sababu ya kwanini tubaki hapa tulipo nashauri twende haraka tuboreshe huduma, mazingira ,vifaa na dawa viwepo vya kutosha; naamini uwezo huo tunao” Alisema Prof. Makubi

“Katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu tujipange kukamilisha ujenzi wa jengo jipya kisasa la kuona wagonjwa wa nje (OPD) ambalo litakuwa na vyumba vya kliniki vya kutosha na vyenye hadhi ya kimataifa ili wagonjwa wengi zaidi kutoka Tanzania na mataifa mengine wapate huduma” Alisema Prof. Makubi.
View attachment 2685803
Kwa upande wao Madaktari bingwa wa MOI wamemuahidi Prof. Makubi kuongeza uwajibikaji, kufanya kazi kwa bidiii, kuwa na ‘Sense of ownership’ kwa taasisi ili kuboresha huduma kwa wagonjwa pamoja na kuifanya taasisi iweze kumudu gharama za mahitaji ya msingi ya kutolea huduma.
Hizi ni siasa katika taaluma! Taasisi inaongozwa na misingi yake pamoja na mission yake. Ni andiko, sio maneno mdomoni ya kupeana kwenye vikao.
Si ahadi kwamba sasa tutawajibika n.k. ni masuala ya utendaji, na asiyefokia viwango, asiyefuata miongozo ya utendaji, anatolewa, si suala la kubembelezana. Ndio maana taasisi nyingi Tz zinakosa ufanisi kwa kila jambo kuiga ccm wanavyoiendesha nchi.
 
Back
Top Bottom