Prof. Mkenda: Wanafunzi watakaopata mimba hawataruhusiwa kurejea madarasani na Vichanga wao

Prof. Mkenda: Wanafunzi watakaopata mimba hawataruhusiwa kurejea madarasani na Vichanga wao

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Waziri wa Elimu Profesa Mkenda amesema wanafunzi wa kike watakaopata mimba hawataruhusiwa kuingia darasani na watoto (vichanga) vyao baada ya kujifungua.

Mkenda amesema Watoto wana haki zao ambazo ni lazima ziheshimiwe hivyo watakaojifungua itawapasa kunyonyesha kwanza watoto wao kabla hawajapokelewa tena shuleni.

Profesa Mkenda amesema hana uhakika kama picha inayotrend mitandaoni ya mwanafunzi akiwa na kichanga chake darasani imepigwa Tanzania, ameahidi kufuatilia.

Mungu wa mbinguni awabariki nyote!

1122.jpg
 
Huku mtaan kama mnafanya kazi na mdada mwenye kichanga! Kuna mda anakwambia maziwa yanauma kujaa ngoja nkanyonyeshe cha! Sipati picha dent yupo class na ticha mnoko atampa swaga gan!
Labda mda wa break kuna watu(m(wa)zazi/m(wa)lezi wa mwanafunzi) watakuwa wanawapeleka watoto shule wawanyonyeshe alaf break ikiisha wanawarudisha nyumban
 
Niliona msumbiji, wadada wanaopata mimba wanaruhusiwa kuendelea na masomo yao.isipokuwa wanabadilishiwa tu muda wa kwenda shuleni.

Wanafunzi wa kawaida wanaingia shuleni ahsubuhi na kumaliza saa 8 mchana, halafu wadada waliopata mimba na wengine kujifungua wao wanaingia shule baada saa 8.

Kwa maana asubuhi yote watakuwa wamewahudumia watoto kikamilifu, utaratibu huo ni mzur hata kama watasoma kwa Massa 3 kwa siku kwa siku za kawaida.

Kwa muda zaidi wanaweza soma hata siku za jmos na wakati wa likizo wengine wakifunga wao wanaendelea ile gap watakuwa wame-i cover ya kumaliza masomo ya darasa wanalosomea, hivyo hawawezi kukutana na wanafunzi wengine wa kawaida.
 
Haya mambo mengine ni kama kutazama movie ya kusikitisha, huko madarasani sijui patakuwa na picha gani mbele ya safari tuendako, harufu ya maziwa itakuwa ndio perfume ya wanafunzi.
Kurudi shule sioni tatizo ila wangetengenezewa utaratibu wao maalum maana pia watanyanyapaliwa na wenzao.
Unajua kufanya kosa hakumaanishi ni mwisho wa maisha, kuna mdada alipata ujauzito tukiwa kidato cha nne. Hakufanya hata mtihani. Baadae kumbe alirudi shule, akaendelea. Leo hii ni daktari wa watoto mzuri sana na amefanikiwa sana na kubadili maisha ya nyumbani kwao.
Some people just need a second chance to make it right.
 
Kurudi shule sioni tatizo ila wangetengenezewa utaratibu wao maalum maana pia watanyanyapaliwa na wenzao.
Unajua kufanya kosa hakumaanishi ni mwisho wa maisha, kuna mdada alipata ujauzito tukiwa kidato cha nne. Hakufanya hata mtihani. Baadae kumbe alirudi shule, akaendelea. Leo hii ni daktari wa watoto mzuri sana na amefanikiwa sana na kubadili maisha ya nyumbani kwao.
Some people just need a second chance to make it right.
Sahihi kbsa kbsa
 
Niliona msumbiji,wadada wanaopata mimba wanaruhusiwa kuendelea na masomo yao.isipokuwa wanabadilishiwa tu muda wa kwenda shuleni.

Wanafunzi wa kawaida wanaingia shuleni ahsubuhi na kumaliza saa 8 mchana, halafu wadada waliopata mimba na wengine kujifungua wao wanaingia shule baada saa 8.

Kwa maana asubuhi yote watakuwa wamewahudumia watoto kikamilifu, utaratibu huo ni mzur hata kama watasoma kwa Massa 3 kwa siku kwa siku za kawaida.

Kwa muda zaidi wanaweza soma hata siku za jmos na wakati wa likizo wengine wakifunga wao wanaendelea ile gap watakuwa wame-i cover ya kumaliza masomo ya darasa wanalosomea, hivyo hawawezi kukutana na wanafunzi wengine wa kawaida.
Aiseh hili wazo nimelikubali ila liandaliwe fungu la part time kwa walimu watakaokuwa wanawafundisha kwa kuwalipa posho ya muda wa ziada. Kila shule itawatafuta walipo kwa haraka na watafundishwa vizuri likely kuliko wale wa muda wa kawaida.

Tena kwakuwa tuna Upungufu wa madarasa na hata wale watoro wanaohitaji kurudia mitihani ya darasa la saba na waliofeli na kusitishiwa matokeo wote wangeweza kuingia shuleni kwa utaratibu huu ili tusiwaathiri hawa walio kwenye mfumo rasmi

Sasa wale walioleta hili wazo watoe na hizo posho muda ni huu

Wazo zuri sana hili
 
Mambo mazuri ya kuiga kutoka dunia ya kwanza kama (invasion of technology) hatuyaigi...ila ya hovyo kama haya ndio fasta tunayaiga
O-Level nimesoma private school!

Ingawaje kwa sasa inaonekana ni shule ya kawaida sana lakini wakati ule ilikuwa ni shule ambayo majority of middle class wangependa kusoma!!

Ada tuliyokuwa tunalipa pale ni zaidi ya mara 10 ya ada ya shule za serikali! Ukichanganya na michango hii na ile, basi ilikuwa taabu tupu!!

Darasani kwetu tulikuwa tunasoma na msichana ambae alihamia pale akiwa Form III. Kwavile nilikuwa karibu nae, baadae nikagundua hapo kabla alikuwa anasoma shule ya serikali lakini akatimuliwa baada ya kupata ujauzito!

Kwavile home kwao kulikuwa na visenti kidogo vya kubadili mboga, ndipo akahamishiwa Private School!!

Now assume huyo binti angekuwa ni mtoto wa maskini...

Je, hiyo private school angeinusa au ingekuwa ndo mwisho wake wa kupata elimu?!

Ukiyatafakari hayo ndipo utagundua ni wewe kutoka Dunia ya Tatu ndie unahitaji zaidi mtoto akipata ujauzito aruhusiwe kuendelea kuliko huyo wa Dunia ya Kwanza mwenye MULTIPLE OPTION!

My classmate hakuhitaji serikali iruhusu mwenye ujauzito aendelee ili nae aweze kuendelea na shule!

Inawezekana hata wewe huhitaji serikali iruhusu mtoto wako aendelee na shule akipata ujauzito but am certain majority ya ndugu zako wanahitaji ruhusa hii ya serikali ili watoto wao waweze kuendelea na masomo inapotokea wamepata ujauzito kwa sababu bila hivyo hawataweza ku-afford gharama za private schools!!

Ingewaje imeshakuwa proved beyond reasonable doubt kwamba jamii IMESHINDWA kudhibiti ngono za utotoni, njia pekee ya kuwasaidia hao ambao nyinyi wenyewe mmeshindwa kuwadhibiti ni kuwaruhusu waendelee na shule!

That being said, hiyo misimamo yenu isiyo na msingi inamuathiri zaidi mtoto wa maskini kuliko mtoto wa mwenye nacho!! Hakuna mtoto wa mwenye nacho ambae atashindwa kuendelea na elimu eti kisa kapata ujauzito!!

Hapa anatetewa mtoto wa maskini ambae hana alternative na wala msilete unafiki wa kwamba kwanini aanze ngono wakati ni mwanafunzi! Nasema msilete huo unafiki kwa sababu am certain hata huko makwenu majority walianza ngono wakiwa bado wanafunzi, but just by chance, or by means of good lucky wakabahatika kutopata ujauzito!!

They did nothing kutopata mimba... IT'S JUST LUCKY!
 
Wadau swali la kizushi.

Mimi kama ndio mwalimu wa hawa wazazi nikichagua pisi 1 niile kuna kesi hapo si ntakuwa nakula mtu mzima mwenzangu.
 
Haya mambo mengine ni kama kutazama movie ya kusikitisha, huko madarasani sijui patakuwa na picha gani mbele ya safari tuendako, harufu ya maziwa itakuwa ndio perfume ya wanafunzi.

Hahah!

Kwa hiyo mkuu unashikilia msimamo wa JPM kwamba mtoto wa kike akishapata ujauzito, shule ndio bye bye!
 
Wadau swali la kizushi.

Mimi kama ndio mwalimu wa hawa wazazi nikichagua pisi 1 niile kuna kesi hapo si ntakuwa nakula mtu mzima mwenzangu.
Tunakufunga kwa kutembea na mwanafunzi, ila kabla ujaingia gerezani tunakupeleka uswahilini unachambwa na akina mama wa kiswahili kwa kumchafulia mtoto maziwa
 
Waziri wa Elimu Profesa Mkenda amesema wanafunzi wa kike watakaopata mimba hawataruhusiwa kuingia darasani na watoto (vichanga) vyao baada ya kujifungua.

Mkenda amesema Watoto wana haki zao ambazo ni lazima ziheshimiwe hivyo watakaojifungua itawapasa kunyonyesha kwanza watoto wao kabla hawajapokelewa tena shuleni.

Profesa Mkenda amesema hana uhakika kama picha inayotrend mitandaoni ya mwanafunzi akiwa na kichanga chake darasani imepigwa Tanzania, ameahidi kufuatilia.

Chanzo: ITV habari

Mungu wa mbinguni awabariki nyote!

5A462ED3-94DE-4D8C-B18A-C069952646B2.jpeg
 
Haya mambo mengine ni kama kutazama movie ya kusikitisha, huko madarasani sijui patakuwa na picha gani mbele ya safari tuendako, harufu ya maziwa itakuwa ndio perfume ya wanafunzi.
Magufuli alisema tutamkumbuka sana, hivi mwanafunzi aliyezaa akirudi darasani atawafundisha nini wenzake? Jinsi ya kupanua mapaja wakati wa ngono? Au anawapa funzogani wenzake?!
 
Back
Top Bottom