Prof Shivji Ametumwa na Wazanzibari?

Prof Shivji Ametumwa na Wazanzibari?

Sijauliza Prof Shivji kazaliwa wapi, nielewe tafadhali! Remember, Wazanzibari hawaukatai Muungano bali wanakataa Makanisa, keep that in mind, ndio utanielewa namaanisha nini.

Professor Shivji kaongelea hilo la makanisa? wacha kubadili mada, Shivji leo kaongelea katiba za Zanzibar. Hata alipoulizwa kuhusu fujo za Zanzibar kajibu ki usomi kabisa bila kumuudhi aliouliza wala wanaosikiliza.
 
Jaribu kuwa unafuatilia habari sio unakurupuka tu kulalamika bila data wala facts za kutosha leo ni mara ya tatu Prof Shivji, kuongea mambo ya katiba ITV wiki moja kabla ya leo Prof Shivji, alisema kipindi kijacho taongea kuhusu katiba ya Zanzibar na Muungano kabla hata fujo za Zanzibar hazijatokea...wewe unadhani Prof Shivji, kaongea leo baada ya sakata la Zanzibar, tuambie katumwa na nani?

Mkuu nakushukuru kwa kunipa mwanga kwamba niendelee kufuatilia japokuwa umekwepa hoja yangu!
 
Professor Shivji kaongelea hilo la makanisa? wacha kubadili mada, Shivji leo kaongelea katiba za Zanzibar. Hata alipoulizwa kuhusu fujo za Zanzibar kajibu ki usomi kabisa bila kumuudhi aliouliza wala wanaosikiliza.

Of course hakuongelea mambo ya makanisa ila mimi nimeliweka ili kupanua hoja kulingana na wachangiaji walivyokuwa wanachangia, na hakuna popote niliposema kwamba ameongelea hilo!
 

"Acha kupotosha hoja! Tunachodai ni Zanzibar yetu iliyo huru, hatuutaki muungano. makanisa yamekuwepo mwanzo Zanzibar kuliko hata huko Bara, soma historia acha kupotosha"


Mkuu sijasema hayo maneno uliyoya-cite kayasema Shivji, rudia kusoma ili utofautishe maneno yangu na yale ya Shivji!
 
we acha tu...mzee wa watu ameelezea mambo vizuri kabisa lakini watu kumbe hata kusikiliza huwa wanakurupuka...!

Mimi naongelea point moja tu juu ya ushiriki wa Wazanzibari katika kuongeza mambo 11 ya Muungano, hayo mengine kweli kaelezea vizuri, nimemkubali!
 
Inawezekana kabisa kuna mambo tunachanganya hapa.
Yale yalikuwa ni mawazo binafsi ya Prof kuwa wazanzibari hawakuongea kabisa, kwake prof hiyo inamaana kuwa hawakuwa radhi kwa yaliyoongezwa katika katiba kuhusu muungano.
Lakini sote ni mashahidi hapa kuwa mambo mengi katika mabunge yetu hupitishwa kwa kupiga kura, sasa hawakuongea vipi? Anayejua hapa ni prof.
 
Mkuu sijasema hayo maneno uliyoya-cite kayasema Shivji, rudia kusoma ili utofautishe maneno yangu na yale ya Shivji!

Kama kweli Serikali ya Tanganyika ina nia njema na Zanzibar na kuamini juu ya misingi ya Muungano wenye maslahi ya pamoja na fursa sawa (win - win situation) na kwamba Zanzibar inafaidika na mfumo wa Muungano uliopo ! SUALA:

Je, Serikali ya Tanganyika iko tayari katika kufuata mfumo na utaratibu huo huo iliyouasisi kwa kuona Zanzibar ambayo ni mbia na mshirika wake - inafutika, na badala yake ii...ngie ndani ya Serikali ya Muungano kama vile ilivyo sasa Tanganyika ndani ya Serikali ya Muungano? Yaani tuwe na Serikali ya Tanganyika na ile ya Muungano badala ya kuwa na Serikali ya Zanzibar na ile ya Muungano.

Na kwamba Makao Makuu ya Serikali ya Muungano yawe Zanzibar?

Na kwamba Tanganyika ipate 4.5% katika mgao wa mambo ya Muungano kama inavyopata sasa Zanzibar?

Na kwamba Tanganyika kwa kipindi cha miaka 48 isiwe na: Polisi yake, usalama, usafiri wa anga, bandari, leseni za viwanda, ushirikiano wa kimataifa, utafiti, takwimu, ushuru wa bidhaa, kodi ya mapato, biashara za nje, simu, posta, elimu ya juu, mafuta na gesi asilia, uraia, uhamiaji, Mahakama ya rufaa, mambo ya nje, mikopo ya nje, sensa ya watu na baraza lake la mitihani - na kwamba yote haya yawe chini ya mamlaka ya Zanzibar? Kwann hamkubali tubadilishane kwa utaratibu huo muliouweka?
 
Kubali tu kuwa umechemka wewe...usipende kuanzisha thread za k.i jing.a
 
Kama kweli Serikali ya Tanganyika ina nia njema na Zanzibar na kuamini juu ya misingi ya Muungano wenye maslahi ya pamoja na fursa sawa (win - win situation) na kwamba Zanzibar inafaidika na mfumo wa Muungano uliopo ! SUALA:

Je, Serikali ya Tanganyika iko tayari katika kufuata mfumo na utaratibu huo huo iliyouasisi kwa kuona Zanzibar ambayo ni mbia na mshirika wake - inafutika, na badala yake ii...ngie ndani ya Serikali ya Muungano kama vile ilivyo sasa Tanganyika ndani ya Serikali ya Muungano? Yaani tuwe na Serikali ya Tanganyika na ile ya Muungano badala ya kuwa na Serikali ya Zanzibar na ile ya Muungano.

Na kwamba Makao Makuu ya Serikali ya Muungano yawe Zanzibar?

Na kwamba Tanganyika ipate 4.5% katika mgao wa mambo ya Muungano kama inavyopata sasa Zanzibar?

Na kwamba Tanganyika kwa kipindi cha miaka 48 isiwe na: Polisi yake, usalama, usafiri wa anga, bandari, leseni za viwanda, ushirikiano wa kimataifa, utafiti, takwimu, ushuru wa bidhaa, kodi ya mapato, biashara za nje, simu, posta, elimu ya juu, mafuta na gesi asilia, uraia, uhamiaji, Mahakama ya rufaa, mambo ya nje, mikopo ya nje, sensa ya watu na baraza lake la mitihani - na kwamba yote haya yawe chini ya mamlaka ya Zanzibar? Kwann hamkubali tubadilishane kwa utaratibu huo muliouweka?

Inaonekana hujauelewa muundo wa muungano kama alivyouchambua Prof leo kwenye lecture yake leo. Zanzibari kwa mfumo uliopo ndio wenye dola iliyokamilika, Wadanganyika tuliporwa dola yetu, sasa sijui unadai kipi hapa.
 

"Acha kupotosha hoja! Tunachodai ni Zanzibar yetu iliyo huru, hatuutaki muungano. makanisa yamekuwepo mwanzo Zanzibar kuliko hata huko Bara, soma historia acha kupotosha"

Mkuu
Kama yalikuwepo tangu mwanzo sasa mnayachoma kwa nini?.
 
Sasa wewe ulikuwa unataka aongope kama ilivyo kawaida ya Magamba.Profesa ni mwana zuoni aliyebobea atakiwi kuwa longolongo kama Dr Wenu wa Uchumi ambaye anailetea nchii hii Umasikini mpaka MSD inaishiwa ata dawa za Malaria.Shivji anakuambia kuwa ameongea na ata Abdu Jumbe juu ya katiba ya Zanzibar baada ya mapinduzi ya kina Okelo,So anajua mengi na alikuwepo toka ASP na TANU azijaungana na wakati huo alikuwa tayari Mwalimu Cho kikuu cha Dsm. Na anakumbuka ata jinsi CCM ilivyokuwa inaitwa Chai na Maharage na madereva wa Maroli pale Ubungo. sasa wewe unatakaje ndugu ulieanzisha huu uzi? Ebu tujuze mkuu
Unataka aongee kama Dr Benson Bana?
 
Mkuu
Kama yalikuwepo tangu mwanzo sasa mnayachoma kwa nini?.
Tangu lini mzanzibari akawa na akili kama hata marais wao ni lazima kwanza waridhiwe na CCM Bara na wao wanakubali tu! Eti mapinduzi daima, mapinduzi kuchoma makanisa badala ya kupambana na CCM Zanzibar iliyowafikisha hapo!
 
Huyu Prof ukimwangalia kwa makini kwenye Mhadhara wa Katiba katika ITV leo anaonekana kuwatetea Wazanzibari badala ya ku-balance mambo:
Anadai kwamba eti kuongeza mambo ya Muungano, Wazanzibari waliokuwa kwenye kuongeza mambo ya Muungano "
walikuwa hawaongei sana," na Karume alikuwa hajali! Sasa kama walikuwa hawasemi sana, mimi sioni tatizo, si wamekubaliana?
Hapa Prof Simwelewi kabisa, ni kama katumwa vile!

acha ujinga...hawaongei maana yake ni kuwa walikaa kimya wakati Karume na Mwalimu wanakiuka makubaliano ya awali ya muungano pasi na ridhaa ya wananchi wa nchi husika yaani Tanganyika na Zanzibar.

ni kitu gani usichoelewa hapo? hujui kiswahili au na wewe umetumwa na Chai Chapati Maharage?????
 
Huyu Prof ukimwangalia kwa makini kwenye Mhadhara wa Katiba katika ITV leo anaonekana kuwatetea Wazanzibari badala ya ku-balance mambo:
Anadai kwamba eti kuongeza mambo ya Muungano, Wazanzibari waliokuwa kwenye kuongeza mambo ya Muungano "
walikuwa hawaongei sana," na Karume alikuwa hajali! Sasa kama walikuwa hawasemi sana, mimi sioni tatizo, si wamekubaliana?
Hapa Prof Simwelewi kabisa, ni kama katumwa vile!
Hao tatizo sio muungano, tatizo lao ni udini tu. Hawapendi wakristu, wamejaaa complications kibao, wanasema dini yao hairuhusu kuua, sasa wale wanaolipua wezao kwa kujitoa mhanga ni akina nani?? si wao wenyewee?? kama maisha yamemshinda si ajinyongee mwenyewe pekeyake.
 
Inaonekana hujauelewa muundo wa muungano kama alivyouchambua Prof leo kwenye lecture yake leo. Zanzibari kwa mfumo uliopo ndio wenye dola iliyokamilika, Wadanganyika tuliporwa dola yetu, sasa sijui unadai kipi hapa.

Changamoto iliyotolewa hapa ni sawa na kuimbia US ikubali kuwa US dollar isiwe tena hela inayotumika katika mambo ya kifedha/ ubadilisho na mizania ya biashara duniani.

Nilivyofahamu ni kuwa mchangiaji anataka kubadilisha kibao..tutajisikiaje?

Anashauri Tanganyika iwe kama Zanzibar ilivyo leo katika Tanzania. Tanganyika iwe na serikali na bendera na Zanzibar ndio igeuke Tanzania.

Kaazi kweli kweli! Serikali ya Muungano na taasisi zake zihamie Zanzibar na Tanganyika/ serikali ya Tanganyika iwe inawakilishwa kupitia Tanzania iliyohamia Zanzibar.


Kwa mtaalamu wa kutengeneza filamu hii ni movie script nzuri.
 
Reasoning yako ni nzuri ila conclusion yako inaonysha kama reasoning umesaidiwa. Prof. Kawaeleza Watanzania historia ya muungano na maoni yake ya wakati muungano unaundwa kama mtafiti.
 
Mkuu mimi sijauliza mambo ya chai maharage, MSD, TANU, ASP, nk bali ni juu ya kuongezwa kwa Mambo ya Muungano! Prof anataka kujenga dhana kwamba wakati mambo hayo yanaongezwa eti Wazanzibari walikuwa "hawasemi" ndani ya Bunge la Muungano! Hapa kinachomaanishwa ni kuchallenge uhalali wa mambo 11 ya Muungano yaliyoongezwa, kwa uelewa wangu, ni kura ndizo zinazoamua na ndivyo ilivyokuwa kwamba Wazanzibari waliridhia. Kwa hiyo Prof asituzuge hapa, tunamheshimu sana.

Na siyo lazima azungumze kama utakavyo, wala hatoi mihadhara kwa lengo la kukuridhisha kila utakalo. Chukua linalokufaa, potezea lisilokufaa hutabadili lolote
 

"Acha kupotosha hoja! Tunachodai ni Zanzibar yetu iliyo huru, hatuutaki muungano. makanisa yamekuwepo mwanzo Zanzibar kuliko hata huko Bara, soma historia acha kupotosha"


kama mnadai zanzibar yenu je makanisa na uhuru wenu vinajumuika vipi au tuseme kuwa rais,makamu na viongozi wengine wa SIRIKALI ya mapinduzi ya zanzibar ni wakristu sasa mnaona wao ni kikwazo? Tupeni taarifa kama wamehamia ukristu. Maana asilimia 99% ya viongozi wenu ni waislam dini ambayo inawapa kiburi. Kama ni muungano pambaneni na serikali na sio imani za watu, nyie wenyewe kwa wenyewe mna matabaka na sintashangaa kugawanyika kwa pemba na unguja baada ya kuvunjika muungano
 
Back
Top Bottom