Prof. Shivji apinga sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema


Kwani mahakama kuu imesema kuwa hukumu yake ina-apply kwa wabunge tuu?
 

lol. Kwa hiyo wewe ukim defame NN basi mie nikamshtaki kwa sababu ni wajibu wangu kuhakikisha kuwa sheria za nchi zinatekelezwa?

A court of law is a court of justice and not an academy of law.

Neither is a court of law a place to test your legal theories.

Thus, to maintain an action before a court of law a litigant must assert interference with or deprivation of, or threat of interference with or deprivation of, his/her own right.

The fact that you have a right sue anyone does not mean that you have the legal reasons to do so.
 

Naona kama suala linaloleta mgogoro hapa siyo ratio decidendi (reason) ya hukumu bali orbiter dicta (said in passing) ya hukumu.
 
 

EMT, Richard,

..je, nitakuwa nimekosea nikidai kwamba mwaka 82, katika hukumu yake dhidi ya Mgonja, mahakama ya rufaa ilifanya makosa kwa kumpa haki mpiga kura yeyote yule, kupinga matokeo ya uchaguzi wowote, kwa sababu zozote zile??

Ndiyo maana kwenye kesi ya Lema Mahakama ya Rufaa imesema kuwa kesi ya Mgonja wa wrongly decided.

Labda mahakama ingeenda mbali zaidi na kueleza why the thought it was wrong decided.

May be tatizo ni kwamba hukumu ya Lema is not detailed. Waheshimiwa majaji kama vile walifanya summary tuu ya principles.

Kwa hiyo, inakuwa ngumu kujua how they analysed the issues and applied the relevant laws, japokuwa issues zilikuwa straightforward.

But it is good to have these sort of decisions. Kesi kama hizi zinaamsha wale waliolala.

Subiri bunge likianza kuna mbunge atatoa povu bungeni kuwa Mahakama ya Rufaa imeingilia mamlaka ya bunge ya kutunga sheria.
 
Vp kuhusu kipengele kilichotumika katika kufungua kesi husika?
Inawezekana kabisa kuna kipengele kinachompa mpiga kura haki ya kufungua kesi huku kikiambatanisha mazingira, lakini labda wapiga kura hao (walalamikaji) walikuja kufungua kesi wakitumia kipengele kingine (pacha), ambacho hakitoi wide ground kwa mpiga kura, mnaliongeleaje hili?
 
kwa uelewa wangu, Shivji anataka mpiga kura awe na haki ya kupinga mtokea ambacho ndo kilitokea kwa kesi ya Lema, lakini anasahau kuwa kurudishiwa ubunge kwa Lema hakikutokana na kama mpiga kura ana haki ya kupinga matokea au la, bali madai ya wapiga kura wale hayakuwa na athari yoyote kwenye matokeo ya uchaguzi.
 
Okay, no problem.

Lakini, je, unaona ingefaa zaidi kama mahakama ingekuwa more specific?

Not only specific but also in detail.

Kwanza tuna wabunge wa kuchaguliwa, kuteuliwa na wanaopita bila kupingwa. Je, hukumu yao una-apply kwa wabunge wote?

Nani atawashtaki wabunge wa kuteuliwa au wale wanaopita bila kuoingwa kama Waheshimiwa Mizengo Pinda na January Makamba?

As it stands, hukumu inaonyesha kama ina-apply both kwa wabunge na madiwani. Lakini ingekuwa more specific, the better.

Kuna suala la "election litigation is not a public interest litigation" Labda wangefafanua kidogo. Does this include all election litigation?

Lakini kama nilivyosema kwenye ile thread nyingine, tunaweza kusema kuwa there is an important public interest in clarifying the legitimacy of the ballot.

However, for electoral policy to be policed by what are, in effect private civil law actions brought at the expense of the litigant (plaintiff), cannot be acceptable.
 
hiyo statement uliyoiweka mwishoni, inabeba sababu ya kwa nini wafungua kesi wengi mahakamani huwa wanashindwa kesi hizo na kutakiwa kulipa gharama za kesi. Wengi huwa hawatazami legal reasons za kufawafanya washinde, wengi huwa wanajikita kwenye social reasons na kusahau kuwa only legal reasons will make them win any case.
 

Wangeweza kufungua chini ya Ibara 26(2) ya Katiba inayosema kuwa "Kila mtu ana haki, kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria, kuchukua hatua za kisheria kuhakikisha hifadhi ya Katiba na sheria za nchi."

Kwa mujibu wa Mahakama ya Rufaa "Article 26(2) of the Constitution..permits any person to bring a public interest litigation."

Lakini walalamikaji na hasa Mussa Mkanga labda aliona hakuna haja hiyo kwa sababu tayari alishashinda kesi nyingine kwa kutumia kifungu hicho hicho cha sheria ya uchaguzi (refer kesi ya Makongoro Nyerere).

Na kama Mkanga angeshinda kesi ya Lema, kuna uwezekano jamaa angefungua tena kesi kama in future angeshinda tena mgombea wa upinzani. Ila sasa kapigwa stop na Mahakama ya Rufaa.
 
naomba kuwa mmoja wa wanaaomshangaa shivji...hivi ni kweli sheria inaruhusu kufunguliana kesi? nimetukanwa mimi wewe umeumia hata ukaenda mahakamani? haki ya mungu tena haya filauni
 
Shivji kaamua kuchafua hewa kwa makusudi kabisa na hii ni dhambi ambayo itamrudia tu.
Hii ni 2012 awareness ya binadamu inazidi kuongezeka kila sekunde inayopita.
Tutarajie kuna madudu mengi kutoka kwa watu wenye majina kama Shivji.

Ni kweli awareness ni kubwa ndiyo maana watu wanaona wazi upuuzi uliomo kwenye sehemu ya hukumu ya kesi ya Lema. Kama huelewi tafsiri ya mbali zaidi ya anachokisema Shivji, katika masuala ya uchaguzi na mengine kwa ujumla ....nguvu ya umma kwanza, nguvu ya umma ni wananchi (wapiga kura) na si mgombea. Hoja ya Shivji na wengine iko wazi, tena nashangaa watu wa Chadema kupingana nayo wakati ipo upande wa kutetea haki za wengi (wapiga kura) dhidi ya wachache (wagombea).
 

Watu wa Chadema wametoka wapi? Si muijadili hiyo sheria tu bila kuweka siasa kama magwiji ya sheria hapa JF akina EMT walivyofanya?

Wengine kusoma na ku like inatosha!
 
Last edited by a moderator:

Mkuu msome vizuri Prof Shivji yeye anaelezea tafsiri za sheria wewe umejikita zaidi kwenye ushabiki wa kisiasa.
 
Naogopa kuongea pumba...sitachangia chochote
Ila naomba modes waiweke hii thread kuwa sticky...
 
Huyu nae BHAAANGE zake zinampeleka pabaya!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…