DOKEZO Prof. Shukuru Manya, Naibu Waziri wa Madini yuko wapi na analipwa kwa kazi gani?

DOKEZO Prof. Shukuru Manya, Naibu Waziri wa Madini yuko wapi na analipwa kwa kazi gani?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Sasa wewe unamyanganya cheo Professor tena wa madini na miamba unakwenda kumkabidhi wizara, Mtu wa education Mwalimu wa digree ambaye ajui chochote kuhusu madini, kwanini tusiwe na maswali?
 

Attachments

  • 3A265213-649F-43EF-B956-1EEBAED63E71.jpeg
    3A265213-649F-43EF-B956-1EEBAED63E71.jpeg
    10.6 KB · Views: 4
Mimi sawa na upeo mdogo wa covcs, wewe unamjua huyu mleta nada ni nani, na anafanya Nini, au na wewe na wale watu wa makasiriko. Mwenye upeo mkubwa mleta mada hajui hata kama ni mbunge na bunge lipo live , yaani mwenye uelewa mkubwa hajui urai wa kawaida kuwa profesa si kamishina wa madini mpaka anaamini kuwa analipwa pasi na kufanya kazi yoyote, wewe mwenye uelewa mkubwa civics ni pamoja na kuwa current na mambo ya kitaifa na kimataifa.
Mleta mada kuna jambo alitaka watanzania walifahamu na mapungufu yaliyotokea huko Tume ya madini baada ya Professor kupanda cheo.
 
Hilo la kumuondoa Professor wa madini na miamba kwenye wizara ya madini na kumuweka Mwalimu kuwa Waziri wa madini hilo nalo nendeni MKALITIZAME
 
Ndugu watanzania, mtajwa hapo juu ni mtumishi wa Serikali ya Tanzania.

Hajulikani aliko, anachokifanya ndani ya Wizara ya Madini tangu ateuliwe na JPM hadi sasa.

Cha kushangaza na kusikitisha nafasi aliyokuwa nayo huko Tume ya Madini, awali ilikaimishwa mtu hadi leo imekaimishwa tena mtu asiye na CV ya hiyo kazi.

Matokeo yake Tume ya madini kila mtu anafanya lake tena bila uoga.

Huyu Professor mwambieni aliko asaidie watanzania walio maskini kwani alisomeshwa kwa kodi za watanzania, analipwa mshahara mkubwa kwa kodi zetu na yafanyi kazi yoyote.
Chuki binafsi. Manya si naibu waziri. Manya ni mbunge wa kuteuliwa tu kwa sasa.
 
Mbunge asiye na jimbo.Yupo pale UD anafundisha.
Mungu ampe nguvu.
Nia yao ilikuwa kumtetelekeza msomi na Mtanzania ambaye angeweza kumfanya serikali kupata Trilion of money kupitia sekta ya madini
 
Sasa wewe unamyanganya cheo Professor tena wa madini na miamba unakwenda kumkabidhi wizara, Mtu wa education Mwalimu wa digree ambaye ajui chochote kuhusu madini, kwanini tusiwe na maswali?

 
Si Dr kiruswa ndio naibu waziri wa madini
Ona vijana wa kitanzania walivyokata tamaa kwenye sekta ya madini wakati huo huo unaye professor wa madini unamtoa unamuweka Mwalimu kuisimamia,
 
Mleta uzi fuatilia huko Bungeni Prof Shukulu Manya amekuwa attached kwenye kamati ipi make mtu kulitumikia taifa siyo lazima kuwa kiongozi wa idara/wizara husika. Unaweza ukawa mtumishi wa kawaida tu na mchango wako ukawa wa muhimu.
 
Mungu ampe nguvu.
Nia yao ilikuwa kumtetelekeza msomi na Mtanzania ambaye angeweza kumfanya serikali kupata Trilion of money kupitia sekta ya madini
Kila Rais na taste zake.Manya hafai kwa mujibu wa plans za Samia.Huwezi jua .
 
Mleta uzi mwenyewe huna faida upo upo tu acha kuchukulia mambo personal sana yatakuumiza au ww ndo mpangaji mkuu wa kazi za serikali?
 
Mleta uzi mwenyewe huna faida upo upo tu acha kuchukulia mambo personal sana yatakuumiza au ww ndo mpangaji mkuu wa kazi za serikali?
Huko serikali Professor hawahitajiki unatishia watanzania? Uwe na hekima Ili tusikuvunjie heshima
 
Ndugu watanzania, mtajwa hapo juu ni mtumishi wa Serikali

Huyu Professor mwambieni aliko asaidie watanzania walio maskini kwani alisomeshwa kwa kodi za watanzania, analipwa mshahara mkubwa kwa kodi zetu na yafanyi kazi yoyote.
Anaitwa Profesa Shukrani Manya, huyu jamaa ni kichwa sana!.
P
 
Mleta mada kuna jambo alitaka watanzania walifahamu na mapungufu yaliyotokea huko Tume ya madini baada ya Professor kupanda cheo.
Vema, kama lengo lilikuwa ni Hilo. Tatizo ni namna alivyowasilisha , amewasilisha kwa namna ambayo siyo ya mtu anayetaka kujua jambo. Mleta mada yeye anajua prof yupo tu haendi ofisini, lakini ana kula mshahara mnono. Angeeleza tatizo la tume ya madini baadaya ya kukosekana kwa prof . Sasa huyu kwa uandishi huo angekuwa amesoma Sheria halafu akaenda law school, si tungeishia kulaumu walimu wa law school kwamba wanafelisha.
 
Back
Top Bottom