Prof. Tibaijuka: Utaratibu wa Mgombea Binafsi utaimarisha vyama vya siasa nchini

Prof. Tibaijuka: Utaratibu wa Mgombea Binafsi utaimarisha vyama vya siasa nchini

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Muleba Kusini na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, amesema kuzuiwa kwa mgombea binafsi nchini kumeifanya Tanzania kuwa na demokrasia ya udikteta wa vyama.

Ameyasema hayo leo Septemba 14, 2024 alipokuwa akitoa mada ya ushiriki wa wanawake katika siasa katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Demokrasia, iliyoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na kufanyika Chuo Kikuu cha cha Dar es Salaam.

"Kwa nchi hii kuna tatizo. Katiba yetu inasema kama unataka kugombea ni lazima ujiunge na chama na hilo ni kwa kila mtu, kwa hiyo hapa tuna demokrasia ya vyama lakini ni udikteta wa vyama. Ni kwa nini mgombea huru asiruhusiwe?" amehoji.

Profesa Tibaijuka aliyekuwa akitoa mada kuhusu ushiriki wa wanawake katika siasa, amesema hicho ni kikwazo kwa kundi hilo. "Hili ni tatizo ambalo Rais Samia kama ataweza afanye marekebisho ili aruhusu wagombea huru. Itasaidia wanawake na wanaume na Watanzania kuboresha ongozi wa siasa," amesema.

Amesema hofu iliyopo miongoni mwa vyama vya siasa ni kusambaratika, endapo mgombea binafsi ataruhusiwa, jambo alilosema si sahihi.

"Mbona Marekani havijapotea? Unaweza ukawa Democratic au Republican na unaweza kuwa huru. Hivyo ndivyo unavyoweza kuimarisha vyama, " amesema na kuongeza: "Hapa unyanyasaji wa viongozi watarajiwa unatokana na kuwanyima uhuru wagombea binafsi. Unajua wananchi wanapopiga kura, wananchi hawapigii chama, wanampigia mtu. Kwa hiyo vyama vimewafunga watu wenye mawazo tofauti, kwamba wakae kweye msimamo wa chama"
 
Kwel kabsa maana wanasiasa wanaona ndo wanazo haki za kuishi tu na kufurahia nchi na Mali zake hadi kufanya mauaji ya makusudi
 
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Muleba Kusini na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, amesema kuzuiwa kwa mgombea binafsi nchini kumeifanya Tanzania kuwa na demokrasia ya udikteta wa vyama.

Ameyasema hayo leo Septemba 14, 2024 alipokuwa akitoa mada ya ushiriki wa wanawake katika siasa katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Demokrasia, iliyoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na kufanyika Chuo Kikuu cha cha Dar es Salaam.

"Kwa nchi hii kuna tatizo. Katiba yetu inasema kama unataka kugombea ni lazima ujiunge na chama na hilo ni kwa kila mtu, kwa hiyo hapa tuna demokrasia ya vyama lakini ni udikteta wa vyama. Ni kwa nini mgombea huru asiruhusiwe?" amehoji.

Profesa Tibaijuka aliyekuwa akitoa mada kuhusu ushiriki wa wanawake katika siasa, amesema hicho ni kikwazo kwa kundi hilo. "Hili ni tatizo ambalo Rais Samia kama ataweza afanye marekebisho ili aruhusu wagombea huru. Itasaidia wanawake na wanaume na Watanzania kuboresha ongozi wa siasa," amesema.

Amesema hofu iliyopo miongoni mwa vyama vya siasa ni kusambaratika, endapo mgombea binafsi ataruhusiwa, jambo alilosema si sahihi.

"Mbona Marekani havijapotea? Unaweza ukawa Democratic au Republican na unaweza kuwa huru. Hivyo ndivyo unavyoweza kuimarisha vyama, " amesema na kuongeza: "Hapa unyanyasaji wa viongozi watarajiwa unatokana na kuwanyima uhuru wagombea binafsi. Unajua wananchi wanapopiga kura, wananchi hawapigii chama, wanampigia mtu. Kwa hiyo vyama vimewafunga watu wenye mawazo tofauti, kwamba wakae kweye msimamo wa chama"
Tusidanganyane Tanzania suala la mgombea binafsi Bado haiwezekani na huu umri Bado hatujaufikia.

Tunapotaka kuiga mambo kwanza ni muhimu tuhakikishe tunafanana Hali za kiuchumi, kijamii na kisiasa na hao watu tunaotaka kuwaiga.

Suala la uwepo wa chama ni muhimu sana kwasababu hatuwezi kumpa nchi au jimbo mtu mmoja ni lazima mtu aungane na wenzake wajiwekee MIKAKATI na kanuni zao pamoja na sera ili Huyo mtu akipata uongozi awajibike kwanza kwenye kikundi chake yani awe na watu Ambao watasimamia misingi yake.

Kwani chama maana yake Nini? Hivi inawezekana kweli ukazunguka nchi nzima kuomba kura peke Yako bila watu wa kukuunga mkono na kukusindikiza? Yani inawezekana vipi wewe uwe mwenyewe peke Yako bila jamaa, ndugu, na marafiki?

Mimi binafsi sioni haja ya kuwa na mgombea binafsi: Hivi mtu kama utashindwa kuweka usawa na upatanishi kwenye kikundi Cha watu laki Moja utawezaje kuongoza watu milioni zaidi ya 60? Ikiwa utashindwa kukubalika, kuheshimika, kushawishi, na kuwa na nguvu ya kuongoza kikundi kidogo au chama je utawezaje kuongoza na kushawishi watu wa nchi nzima?

Hoja za mgombea binafsi naona zinalenga kuzalisha mafisadi na wavunja katiba.

USHAURI: UKIONA CHAMA CHAKO KINAKUCHANGANYA NA HUWEZI AU HUNA NGUVU YA KUJENGA USHAWISHI NA USAWA BASI NI VEMA UKAHAMA HICHO CHAMA KISHA HAMIA CHAMA KIKINGINE AU UNDA CHAMA KINGINE NA WATU WENZAKO AMBAO MTAENDA SAWA.
 
Alipokuwa ccm walikuwa mstari wa mbele kupinga, saa hizi katoka yuko benchi anajiongelesha.

Hii nchi ujinga ni mwingi sana. Hawa maprofesa jinsi wanavyoongea wakiwa ccm na serekalini inawaangalia unashindwa kumlaumu Mungu au wao

Juzi nilikwenda kwenye graduation mahali nikamuona profesa Mkumbo kakaa mbele asee nimekaa saa nzima namuangalia roho ikaniuma sana.
 
Hili swala liliwahi ongelewa bungeni miaka ya nyuma na yeye akiwa mbunge ila walilipinga vikali
 
Alipokuwa ccm walikuwa mstari wa mbele kupinga, saa hizi katoka yuko benchi anajiongelesha.

Hii nchi ujinga ni mwingi sana. Hawa maprofesa jinsi wanavyoongea wakiwa ccm na serekalini inawaangalia unashindwa kumlaumu Mungu au wao

Juzi nilikwenda kwenye graduation mahali nikamuona profesa Mkumbo kakaa mbele asee nimekaa saa nzima namuangalia roho ikaniuma sana.
🤣
 
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Muleba Kusini na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, amesema kuzuiwa kwa mgombea binafsi nchini kumeifanya Tanzania kuwa na demokrasia ya udikteta wa vyama.

Ameyasema hayo leo Septemba 14, 2024 alipokuwa akitoa mada ya ushiriki wa wanawake katika siasa katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Demokrasia, iliyoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na kufanyika Chuo Kikuu cha cha Dar es Salaam.

"Kwa nchi hii kuna tatizo. Katiba yetu inasema kama unataka kugombea ni lazima ujiunge na chama na hilo ni kwa kila mtu, kwa hiyo hapa tuna demokrasia ya vyama lakini ni udikteta wa vyama. Ni kwa nini mgombea huru asiruhusiwe?" amehoji.

Profesa Tibaijuka aliyekuwa akitoa mada kuhusu ushiriki wa wanawake katika siasa, amesema hicho ni kikwazo kwa kundi hilo. "Hili ni tatizo ambalo Rais Samia kama ataweza afanye marekebisho ili aruhusu wagombea huru. Itasaidia wanawake na wanaume na Watanzania kuboresha ongozi wa siasa," amesema.

Amesema hofu iliyopo miongoni mwa vyama vya siasa ni kusambaratika, endapo mgombea binafsi ataruhusiwa, jambo alilosema si sahihi.

"Mbona Marekani havijapotea? Unaweza ukawa Democratic au Republican na unaweza kuwa huru. Hivyo ndivyo unavyoweza kuimarisha vyama, " amesema na kuongeza: "Hapa unyanyasaji wa viongozi watarajiwa unatokana na kuwanyima uhuru wagombea binafsi. Unajua wananchi wanapopiga kura, wananchi hawapigii chama, wanampigia mtu. Kwa hiyo vyama vimewafunga watu wenye mawazo tofauti, kwamba wakae kweye msimamo wa chama"
Anna, siwezi kukusikiliza mana umehudumu katika mfumo kandamizi , ulikaa kimya na leo endelea kukaa kimya!
 
Nimemsikiliza Prof. Anna Tibaijuka katika moja ya uwasilishi wake katika kuadhimisha siku ya demokrasia duniani.

Prof. Tibaijuka ametolea ufafanuzi wa kina kwa nini kuna haja ya kuwa na mgombea binafsi. Anna anasema, "kutokuwa na mgombea binafsi ni udikteta wa vyama". Kwamba mtu ana uwezo kugombea na kushinda lakini katiba inamlazimisha kuwa chini ya chama cha siasa. Kisa eti umekatwa jina na Kamati Kuu. Demsheeti.

Prof anafafanua kisomi na kusema. "mfumo wa kisovieti tulioridhi kimsingi si maana ya demokrasia maana inabana watu wengine wasitumikie wananchi". Prof. Tiba anatolea mfano Marekani ambako kuna wagombea binafsi lakini vyama vya Republican na Democrats havijawahi kufa. Kwamba ni woga wa bure tu na usioakisi maana hasa ya demokrasia.

Kwa Republican na Democrats hujawahi kusikia neno Kamati Kuu au Halmashauri Kuu. USA wanampigia mtu kura na siyo chama. Kwa maoni yangu ushauri huu wa Prof. Anna Tibaijuka uchukuliwe kwa uzito mkubwa na Rais Samia Suluhu Hassan anayejipambanua kama mwana demokrasia.
 
Nimemsikiliza Prof. Anna Tibaijuka katika moja ya uwasilishi wake katika kuadhimisha siku ya demokrasia duniani.

Prof. Tibaijuka ametolea ufafanuzi wa kina kwa nini kuna haja ya kuwa na mgombea binafsi. Anna anasema, "kutokuwa na mgombea binafsi ni udikteta wa vyama". Kwamba mtu ana uwezo kugombea na kushinda lakini katiba inamlazimisha kuwa chini ya chama cha siasa. Kisa eti umekatwa jina na Kamati Kuu. Demsheeti.

Prof anafafanua kisomi na kusema. "mfumo wa kisovieti tulioridhi kimsingi si maana ya demokrasia maana inabana watu wengine wasitumikie wananchi". Prof. Tiba anatolea mfano Marekani ambako kuna wagombea binafsi lakini vyama vya Republican na Democrats havijawahi kufa. Kwamba ni woga wa bure tu na usioakisi maana hasa ya demokrasia.

Kwa Republican na Democrats hujawahi kusikia neno Kamati Kuu au Halmashauri Kuu. USA wanampigia mtu kura na siyo chama. Kwa maoni yangu ushauri huu wa Prof. Anna Tibaijuka uchukuliwe kwa uzito mkubwa na Rais Samia Suluhu Hassan anayejipambanua kama mwana demokrasia.
Naunga mkono hoja.
P
 
Nipo pamoja na Prof. Anna Tibaijuka kwa hoja hii.
 
FB_IMG_17267740492724978.jpg
 
Tusidanganyane Tanzania suala la mgombea binafsi Bado haiwezekani na huu umri Bado hatujaufikia.

Tunapotaka kuiga mambo kwanza ni muhimu tuhakikishe tunafanana Hali za kiuchumi, kijamii na kisiasa na hao watu tunaotaka kuwaiga.

Suala la uwepo wa chama ni muhimu sana kwasababu hatuwezi kumpa nchi au jimbo mtu mmoja ni lazima mtu aungane na wenzake wajiwekee MIKAKATI na kanuni zao pamoja na sera ili Huyo mtu akipata uongozi awajibike kwanza kwenye kikundi chake yani awe na watu Ambao watasimamia misingi yake.

Kwani chama maana yake Nini? Hivi inawezekana kweli ukazunguka nchi nzima kuomba kura peke Yako bila watu wa kukuunga mkono na kukusindikiza? Yani inawezekana vipi wewe uwe mwenyewe peke Yako bila jamaa, ndugu, na marafiki?

Mimi binafsi sioni haja ya kuwa na mgombea binafsi: Hivi mtu kama utashindwa kuweka usawa na upatanishi kwenye kikundi Cha watu laki Moja utawezaje kuongoza watu milioni zaidi ya 60? Ikiwa utashindwa kukubalika, kuheshimika, kushawishi, na kuwa na nguvu ya kuongoza kikundi kidogo au chama je utawezaje kuongoza na kushawishi watu wa nchi nzima?

Hoja za mgombea binafsi naona zinalenga kuzalisha mafisadi na wavunja katiba.

USHAURI: UKIONA CHAMA CHAKO KINAKUCHANGANYA NA HUWEZI AU HUNA NGUVU YA KUJENGA USHAWISHI NA USAWA BASI NI VEMA UKAHAMA HICHO CHAMA KISHA HAMIA CHAMA KIKINGINE AU UNDA CHAMA KINGINE NA WATU WENZAKO AMBAO MTAENDA SAWA.
Pumba tupu!
 
Back
Top Bottom