Profesa Assad ashtakiwe kwa kukiuka maadili akiwa ofisini. Alimpeleka dereva kufanya kazi masjala isiyoendana na proffession yake

Majukumu hayo ni yaliyo ndani ya kada husika, nesi umfanye kuwa mwalimu eti kisa mkataba unasema na majukumu mengine utayopangiwa. Reasoning ya wapi hiyo bwana raslimali watu ?
 
Mkataba Wa kazi wa huyo dereva uliuona ? Hadi useme Kuna kipengele cha kupangiwa kazi yeyote? .. Tusigeneralize mikataba au mambo .. Tuongee kitu katika uhalisia unafanyaje kazi sio yako ..

Dereva aende masjala .. ?

Akiboronga huko masjala utatumia taratibu zipi za kumhoji au miongozo ipi ya taaluma yake ikiwa sio taaluma yake..


Au Hamtaki kuona mtu amekaa kaa tu mnamfanyisha kazi zisizo zake.. Mmeshindwa nini kuajiri mtu wa masjala hadi Dereva aende hapo huoni unabania kazi za watu au waliopo masjala hawatoshi?..


Bora awe anakuja anakosa gari ili mpate akili ya kutafuta gari.. Kwanza ni kosa la kiutawala kuleta watumishi wengi kuliko rasilimali zilizopo
 
Sahihi
 
Majukumu hayo ni yaliyo ndani ya kada husika, nesi umfanye kuwa mwalimu eti kisa mkataba unasema na majukumu mengine utayopangiwa. Reasoning ya wapi hiyo bwana raslimali watu ?
Na hao rasilimali watu waliohusika kwenye hilo waburuzwe mahakamani pamoja na Profesa Assad kwa kutotumia weledi wa fani zao na kuonea huyo dereva professional kumpeleka masjala walitaka akaendeshe mafaili? Yasiyo na usukani wala break?
 
Uko sahihi mia kwa mia
 
100% correct
 
Kwani dereva hakuwa na ujuzi wa kufanya kazi hapo.

Wapo wafanyakazi hawasaidiani kazi wakihitajika kwa wenzao?

Umechemsha jionee aibu.
What????? Unajua maana ya kuajiriwa kwa proffession yako?

Mfano yeye Assad ana leseni ya udereva huwa anaendesha gari zake

Kwa hiyo siku Raisi kaamka vibaya aseme kuanzia leo wewe sio CAG utakuwa kazi yako udereva kuendesha gari la bosi wa masjala wa ofisi ya CAG
 
Hiyo ina apply huko kwenu madrasa labda sio katika ulimwengu wa sasa unaoheshimu proffesionalism
 
Ok,mahakama ya kazi?
Tulia mawakili wanajipanga kukomesha huo ubwege liwe fundisho

Haki ya mtu haipotei ikiwemo ya huyo Dereva nyanyasika na Proffessor Assad

Yeye naye ni proffesional kwenye eneo lake la udereva kama ambavyo Proffessor Assad naye ni proffesional eneo lake

Tuliza kichwa ha tu empty kila kitu stay tuned
 
Nimeuliza Hivyo kwa sababu,kama ni issues ya kazi mahakama ya kazi.
 
Hiyo alifanya akiwa Muslim University of Morogoro, labda ashitakiwe kwa Sharia 🐒
Popote sio sahihi iwe public, private au religious sector

Tena Religious ndiko kubaya sana ni matumizi mabaya ya sadaka za waumini kama kazi ya udereva haipo hastahili kuwepo kazini kupunguzia mzigo waumini wakumgharimia wakati gari hana
 
Umewezaje kujua kuandika yote hayo bila kujua vitu vidogo tu. Kwamba hiyo haimaanishi kufanya kazi yoyote bali ni kwenye fani yako bila kuathiri utendaji. Kwa akili zako mhasibu anaweza kupangiwa upasuaji kwa sababu job description inasema na kazi zingine? Ficha undezi mkuu
 
Masijala ni sehemu nyeti sana kumpeleka dereva mule ni kupafungua na kukiuka mipaka ya masijala. Kwanza aliapa wapi kutunza siri za mule na je alikua na taaluma ya kutunza document za siri?
 
Masijala ni sehemu nyeti sana kumpeleka dereva mule ni kupafungua na kukiuka mipaka ya masijala. Kwanza aliapa wapi kutunza siri za mule na je alikua na taaluma ya kutunza document za siri?
Hakuna mahali pasipo na unyeti.
Huyo dereva kama ni mtumishi lazima amekula kiapo cha utii na kutunza Siri za serikali. Acheni kutukuza mambo.
Vipi mbunge ambaye sifa kujua kusoma tu anawezaje kutunga Sheria za nchi kwaajili ya Watanzania zaidi ya milioni 60?
Kamasijala cha ofisi moja tu kana unyeti gani zaidi ya Bunge ambalo linatunga Sheria za nchi?
Mngekuwa mna ufahamu mngeishinikiza serikali kuwa mbunge yeyote awe amesoma shahada ya Sheria au awe na shahada ya pili ya fani yoyote.
Kwanza hiyo kozi ya record management unajua imeanza lini hapa Tanzania?
Je, kabla ya hiyo kozi ya record masijala hapakuwa na watu?
 
Kama itakupendeza naomba CV ya Waziri wa Afya wa sasa
 
Dereva kama magari ya kuendesha hamna mnataka kusema akae tu angojee mshahara ?

Profesa yuko sawa tu, dereva kwenda masijala iko sawa, tena qualification zinaingiliana.

Ofisi fulani mhudumu aliwahi kuwa dereva, kulikuwa na upungufu naye akawa na leseni wakampa test akafaa akawa reallocated.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…