TANZIA Profesa Augustine Massawe, Daktari bingwa wa Magonjwa ya Watoto afariki dunia

TANZIA Profesa Augustine Massawe, Daktari bingwa wa Magonjwa ya Watoto afariki dunia

Nilipokuwa Moshi Sec. Form one,Dr. Massawe alikuwa form three.(1966)
Katika dormitory( tulikuwa boarding school),Massawe alikuwa kitanda cha pembeni yangu.
Shikamoo yako mkuu,dah mi nilidhani jamii forum tulio humu wengi ni sie vijana na watoto wa shule,kumbe kuna wazee ambao ni lika sawa la baba zetu......Uwe unatupa hekima na busara pale unapoona watoto wanaichafua jamii forum
 
Nilipokuwa Moshi Sec. Form one,Dr. Massawe alikuwa form three.(1966)
Katika dormitory( tulikuwa boarding school),Massawe alikuwa kitanda cha pembeni yangu.
Unaweza kukumbuka kama ilikuwa Hanang, Kibo, Shengena au mawenzi?
 
Lord have mercy on us, huyu dr. nlikua namskia tu. Mungu amrehemu.
 
Lala salama baba. Tunakushukuru sana wa huduma Mungu aliyokuwa amekujalia

Uliitumia vyema karama Mungu aliyoiweka ndani yako

Mwendo umemaliza 💔💔💔

---
Daktari Bingwa wa Watoto Dr Augustine Massawe wa Furaha Medical amefariki Dunia leo Jijini Dar es Salaam. Taarifa kutoka kwa familia ni kwamba Dkt. Massawe amefariki asubuhi hii katika hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa siku kadhaa kwa matibabu.

Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano kwa umma Muhimbili, Aminiel Aligaesha amethibitisha kutokea kwa kifo hicho, “Amefariki saa mbili na nusu asubuhi leo.

Mtoto mkubwa wa marehemu Dk Furaha Augustine amesema baba yake alikuwa anasumbuliwa na tatizo la upumuaji.

“Baba amefariki asubuhi ya leo alikuwa anaumwa na alilazwa Muhimbili kwa zaidi ya wiki na leo saa tatu asubuhi Mungu akamchukua,” amesema Dk Furaha ambaye ni daktari wa magonjwa ya kina mama na uzazi.

Pole sana Rafiki wangu john Kwa kuondokewa na baba yako Mungu ampumzishe kwema
 
RIP doctor. dr. massawe Mwenyezi Mungu Akuweke mahali pema ameen.
always My Top List doctors.
1. Massawe Rip
2. Dr. Ekenywa Rip
3. Dr Kundi
 
Yule Daktari Bingwa wa watoto Prof Massawe amefariki Dunia leo asubuhi.
Mwenye Furaha Medical

RIP MPENDWA SANA PROF MASSAWE

Huyu nakumbuka mtoto anaugua ukifika kwanza anakutuliza mzazi, anakuuliza, anacheza na mtoto anampima, halafu hakuandikii tu dawa, anakueleza kwanza tatizo nini, unawezaje kuzuia, anakupa dawa unaondoka na amani hata kama ulikuja saa sita mchana yeye akaingia saa mbili usiku. RIP Dr wa kweli.
 
Mtoto mkubwa wa marehemu Dk Furaha Augustine amesema baba yake alikuwa anasumbuliwa na tatizo la upumuaji.
Naanza kuogopa kama Muhimblili wameshindwa kuokoa maisha yake basi tujiweke tayari na corona. Upumuaji itakuwa ni corona
 
Back
Top Bottom