Profesa Janabi: Ogopa sana vitu vitamu vitamu

Profesa Janabi: Ogopa sana vitu vitamu vitamu

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa Mohamed Janabi amesema utumiaji wa sukari kupita kiasi haufai kwa afya ya mwanadamu.

“Ukinywa glass moja asubuhi machungwa matano, mchana matano na jioni matano maana yake kwa mwezi ni machungwa 450, unaharibu afya yako, ogopa zaidi vitu vitamu tamu, unavyozungumzia sukari sio sukari tu bali ni vitu vitamutamu. Pale Muhimbili tunao watoto wa miaka tisa wana kisukari.” amesema Profesa Janabi

Amasema hayo mkoani Mwanza wakati akiwasilisha mada katika mkutano wa Mafunzo wa 108 wa watayarishaji wa vipindi vya Elimu kwa Umma ulioandaliwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Washiriki wa mkutano huo ni watumishi kutoka taasisi mbalimbali za serikali.

Huyo Muheshmiwa ana hoja ila kuna kitu MUHIMU anakosa katika mafundisho yake.....
Mfano: Wote tunajua kuwa machungwa ni kati ya matunda mazuri na muhimu sana kuupatia mwili Vitamin C. Sasa kwa kauli yake alitakiwa apendekeze kuwa mtu asizidishe machungwa kadhaa kwa siku (kama anauwezo wa kuyapata kila siku)
hata hivyo watanzania walio wengi hata akila machungwa 10 kwa siku, Inaweza kuwa sio tatizo kwao kwani hawana uwezo wa kuyapata hivyo kila siku. Inaweza kuwa amekula hivyo mara tatu au pengine nne kwa mwezi kiasi ambacho ni cha kawaida kabisa....
Vyakula vyote ni muhimu kwa mwili ila vinatakiwa viliwe kwa Kiasi sasa yeye ajikite kueleza Kiasi kinachostahili kuliwa LAKINI PIA AZINGATIE KAZI WANAZOFANYA WATANZANIA.... sioni kama ni sawa kusema mtu ale milo miwili kwa siku........SIJUI kama huyu Muheshimiwa amewahi kulima (ambako ndipo ajira ya watanzania wengi ilipo kwani angejua kuwa, milo miwili haimfikishi mtu popote...) hapo sijataja wajenzi nk nk nk
 
Amewasemea wakaaji kwenye viyoyozi na viti vinazunguka, haya na sie wabeba zege, tofali, wakulima, wavuja jasho...tuke vitu gan?
 
Back
Top Bottom