Profesa Janabi’s Diet: Njia rahisi ya Kupungua na ukaona matokeo ndani ya mwezi mmoja tu

Profesa Janabi’s Diet: Njia rahisi ya Kupungua na ukaona matokeo ndani ya mwezi mmoja tu

Kibongo bongo, ni ngumuu sanaaa
Imagine unamwambia mtanzania asile ugali, asile chapati, viazi au mihogo[emoji16][emoji16][emoji16]. Jaman embu muwe serious na maisha ya watu.

Haya maisha ukizidi ku complicate ndio yanazidi kukuchanganya!.
 
Imagine unamwambia mtanzania asile ugali, asile chapati, viazi au mihogo[emoji16][emoji16][emoji16]. Jaman embu muwe serious na maisha ya watu.

Haya maisha ukizidi ku complicate ndio yanazidi kukuchanganya!.
Yaani nimecheka ' kuweni serious na maisha ya watu.....'

Swala la diet kila mtu ana ujuzi wake wa kuelezea

Nimeshuhudia mtu aliyekuwa anakula healthy maisha yake yote hajawahi kuvuta sigara wala kunywa pombe, wanga kwake ilikuwa mwiko alitumia pesa nyingi kula chakula natural vitamin protein etc kwa wingi... Aliugua kidogo tu yaliyofuata alilia sana akauliza 'why ??
Aligundulika ana matatizo ya moyo kibaya zaidi aligundulika ana cancer alipewa muda wa miezi mitatu kuishi (bahati mbaya sikuwahi kuzungumza naye tena lakini niliambiwa alifariki)

Mwili tusiulazimishe kuadjust tuuuu ilimradi wamesema
Wahindi na Waarabu idadi ingepungua maana ndugu zetu hawa wanga ndio chakula chao kikuu
* Kila mtu na metabolism yake....zoezi ndio jibu
Huu ni mtazamo wangu
Tutaweza acha maandazi na vitumbua kweli??
 
Yaani nimecheka ' kuweni serious na maisha ya watu.....'

Swala la diet kila mtu ana ujuzi wake wa kuelezea

Nimeshuhudia mtu aliyekuwa anakula healthy maisha yake yote hajawahi kuvuta sigara wala kunywa pombe, wanga kwake ilikuwa mwiko alitumia pesa nyingi kula chakula natural vitamin protein etc kwa wingi... Aliugua kidogo tu yaliyofuata alilia sana akauliza 'why ??
Aligundulika ana matatizo ya moyo kibaya zaidi aligundulika ana cancer alipewa muda wa miezi mitatu kuishi (bahati mbaya sikuwahi kuzungumza naye tena lakini niliambiwa alifariki)

Mwili tusiulazimishe kuadjust tuuuu ilimradi wamesema
Wahindi na Waarabu idadi ingepungua maana ndugu zetu hawa wanga ndio chakula chao kikuu
* Kila mtu na metabolism yake....zoezi ndio jibu
Huu ni mtazamo wangu
Tutaweza acha maandazi na vitumbua kweli??
Kumbuka enzi hizo kijijini, mzunguko ulikuwaje!!!

Ni mara ngapi unakutana nachakula tofauti na ugali??? Labda ukale mabibo na korosho, lakini wazee walitoboa bila taabu mpaka 90yrs.

Siku hizi vijana kwa watu wazima tunang'ang'ana kula kwa draft lakini waapi, mara huyu kaamka anaumwa kichwa, mwingine korodani ya kulia imevimba, mwingine nyonga haina vilainishi, unakaza wee kupiga tizi mara paap, unatanua hipsi kama.....

Halafu kuja wajinga wameacha tu maisha yaendelee kama yanavyotaka[emoji1787][emoji1787], na yenyewe yamewaacha wafanye mambo yao[emoji16][emoji16].
 
Profesa Janabi’s Diet leo Katika Kipindi cha Clouds 360 Tarehe 25,April. Mkurugenzi wa Jakaya Kikwete Heart Institute.
Ametoa njia rahisi ya Kupungua na ukaona matokeo ndani ya Mwezi mmoja tu.
Kasema
1. Achana na Vyakula vyote vya ngano, Acha chapati, Mandazi,Mikate, Keki nk
2. Achana na vyakula vyote vya nafaka hata Ugali wa dona achana nao.
3. Acha juisi Hata za Kutengeneza Nyumbani Yaani juisi nachuro

Akaulizwa wewe unakula nini? Mfano kwa siku moja tueleze?
Professor akajibu

“Asubuhi amepiga kahawa akaenda kazini” Mchana ikifika anakula “Mboga za majani na samaki wa kuchoma”.
.
Bado amewaacha watangazaji Mdomo wazi wanamuuliza Umefanya hivyo kwa miaka mingapi?

Jibu lake: Professor janabi amewaambia watangazaji kwamba yeye binafsi hajanywa juisi ya matunda na vinywaji vyovyote vya baridi karibia miaka 10 sasa. Na amesema ni hatari sana unywaji wa juisi za matunda hata yakutengeneza nyumbani. Unamimina sukari ya Fructose nyingi kwa mkao mmoja. Pili hajala mkate na vyakuala vya ngano kwa miaka 3 sasa.

--------------------------------------------------------------------------------------------------
PART 2

Prof Janabi umesema kitu ambacho nimekuwa nikiwaimbia kwaya hapa kila siku na wengi wamekuwa “Wakicharuka sana na Kurusha Matusi”

Aonya Wanywaji wa juisi za Matunda kama Machungwa Maembe kwa kigezo ni NACHURO hawajaweka SUKARI ni Hatari kwa afya.

Mimi binafsi nikinywa juisi na soda nikapiga na wanga aisee nanenepa kwa kasi sana. Kuna kipindi mwili ulitaka kuniponyoka nikafanya tafiti kwa kina “Aina kuu tatu za Sukari duniani zinazopatikana kwenye vyakula asilia”
.
Nikagundua kwamba:
1. Unapokamua juisi ya matunda kama maembe machungwa unatengeneza Syrup ya sukari kama vile Juisi ya kiwandani.
2. Jinsi mwili unavyo chakata Sukari ya Juisi ya Embe nachuro na Juisi ya kiwandani ya embe mchakato (Biochemical pathways) kimwili ni uleule.
3. Duniani kuna aina Tatu za sukari Glukosi inapatikana kwenye Wanga na hata matunda pia, Sukari nyingine inaitwa Fructose ipo kwenye matunda asali, miwa na Tende na sukari nyingine ni Galactose ipo kwenye maziwa.
Sukari iliyo kwenye Tende,Miwa,Matunda huitwa Fructose hii ni Tamu zaidi ya mara mbili ya Glukosi. Ukiramba Fructose kijiko 1 utamu wake unalinganishwa na vijiko 2 vya Glukosi.
4. Sukari ni Sukari hakuna cha “Nachuro wala Kiwandani” Mchakato ni Uleule.
5. Sukari ya Matunda,Tende, Miwa, Unatakiwa Ule kwa kiwango kidogo. Kwa sababu mchakato wake ni kama Pombe Fructose hutumika na Kiungo kimoja tu mwilini INI. Na Unapozidisha Fructose INI huhifadhi sukari hio kama MAFUTA unapata Non Alcoholic Fatty Liver. Kuna wagonjwa wengi tu “Hawanywi Pombe wana Ini limetapakaa mafuta, Wengine Limedumaa mpaka wamepata kisukari “Hepatic insulin resistance” na Mwisho Linakufa kabisa “Liver cirrhosis Fructose induced”.
---------------------------------------------------------------------------------------------
PART 3

Professor Janabi’s Breakfast Lunch and Dinner Meal Plan Kwa siku Moja inakuwa hivi:
No Nafaka , No Ngano, No Sukari , No Juisi Nachuro ,No soda..! Zote hizo ni NO. Kinywaji baridi Chake ni MAJI.
.
1. Asubuhi : Amekunywa Kahawa (Coffee) glasi moja. Na salad ya Matunda Apple na Ndizi mbivu.

2. Lunch: Kipande cha samaki, Mboga za majani na salad hapo Pembeni.

3. DINNER (USIKU):Jioni Kuku, salad na Mboga za majani pia. .
Hajaanza Leo ameanza siku nyingi sana Kuishi hivyo Kwa mujibu wake.
.
Kwa Professor Anakula hivi? Je ina maana Profesa anajitesa?
1. Kwanza anaonekana kufurahia mfumo wake na anawashangaa ambao wana HOFIA kutoweza. Sky Eclat
2. Alianza Mfumo huu baada ya kuona Watu wengi wanavyo hangaika na magonjwa ya moyo huku wakiwa wana maisha mazuri na pesa. Sababu kubwa ni Kutokujua waleje ili kujikinga na magonjwa ya moyo.
3. Kutokana na Utafiti wake akaona Vyakula vya wanga na sukari ni adui namba moja akaacha kabisa na kwa miaka mingi anaishi na afya yake iko FITI. “Hataki na Yeye aje alazwe kitandani akizibuliwa Mishipa yake ya Moyo”.

Anauliza “Ipi gharama zaidi? Kuacha vyakula vya wanga upunguze uzito wako au Kuendelea kula upate unene uliokithiri magonjwa ya moyo tuje tukuzibue kwa milioni 8” ?.

View attachment 1083213

View attachment 1082897
Kwa uelewa wa kawaida tu brain cells zinatumia only glucose as fuel, hazitumii kingine chochote zaidi ya glucose ktk ufanyaji kazi wake.

Protein ni molecule kubwa na fatty acid zinabound na protein (albumin) hivyo haziwezi kupita kwenye blood brain barrier (BBB).

Sasa kama watu wataepuka vyakula vyenye glucose ndani yake tutegemee ubongo utafanyaje kazi?
 
Atakufa tuuu tena kizembe kweli. Ana udhaifu wake hiyo.
Wamuulize habari ya pombe na wanawake !!!
 
Daaah maisha ayo ndio naishi mimi wakuuu na mwalimu wa izo diet kwangu mm ni de boaz mkumbo na nainjoi kwa kwel na sisikiii njaa ovyo asbui supu tuu mchana kabich na usiku nyama choma na salad no kitambi na uzito na nafunga sana.
 
Kwa msosi huo, kwa kijana mambo yetu itakuwaje sasa? au kwa the oldies tu?
Unapiga safi tena unakuwa mwepesi zaidi kwa mfano mm ni kijana wa miaka 24 mwaka jana nilikuw na uzito wa kg 93 nikafanya iyo diet na nipo poa now nina kg 70 na nina muenekano mzuri tu
 
Chakula ni suala MTAMBUKA, bibi yangu ana miaka 90+, diet yake ina wanga wa kutosha, hajawahi kulazwa hoi kitandani...
 
Unapiga safi tena unakuwa mwepesi zaidi kwa mfano mm ni kijana wa miaka 24 mwaka jana nilikuw na uzito wa kg 93 nikafanya iyo diet na nipo poa now nina kg 70 na nina muenekano mzuri tu
👏🏼👏🏼👏🏼
 
Hahaaaa.. ,kazi kweli kweli..

Hebu mniache nile kitu roho inapenda;

Unajibana kote huko halafu unakuja kuwa diagnosed with diabetes melitus (kisukari) na presha uliyoridhi kutoka kwa wajomba zako[emoji28][emoji28]
 
Ukiwasikiliza sana hawa wasomi mwisho wa siku either utachanganyikiwa zaidi au utajawa na hofu karibu ya kila kitu maishani mwako..

Yeye anadai anakula samaki wa kuchoma waka kuna tafiti kibao tu zilizofanyika zinaelezea hatari ya kupata kansa ya kwenye utumbo (colorectal cancer) kutokana na ulaji mwingi wa vyakula, na hasa nyama za kuchoma (including samaki)
 
Anachokizungumza Prof ni hypothesis kwenye eneo ambalo anajaribu kufanyia tafiti. Kula wanga mwingi au kutokula hakuwezi kukuongezea maisha ila kunaweza kukajenga au kubomoa afya yako.Maisha anatoa Mungu ila usimjaribu bwana Mungu wako, ukipata maarifa tumia kuzuia madhara kwenye mwili wako.
 
Mi nafikiri shida yetu kubwa ni sedentary lifestyle. Maisha ya daladala, bodaboda na bajaji.
 
Nimeacha kuamini hawa Ma prof.
Yaani kukataa nachoro juisi[emoji485] ndio hoja halafu unakula ndizi mbivu[emoji287] huku umekataa tende? Hautaki kula whole grain food? Atafanya utafiti mwingine muacheni
 
Mungu azidi kumbariki Daktari Janabi kwa kutupatia watz maarifa kwaajili ya maisha yetu !

Imeandikwa” watu wangu wanawngamia kwa kukosa maarifa”

Prof hakutaka kuwa mchoyo wa hizo habari njema!

Mwenye masikio na afahamu
 
Dah!!

Wale wa biriani la kwa Sele Bonge na Mariam ndo basi tena
 
Hata ufanyaje ukifika muda wako utarudi kwenye udongo tu.. Hivi nchi hii na uchumi huu utaishi bila ya kutafuna ugali au mikate.. Ashindwe
 
Back
Top Bottom