Profesa Jay

Professor yupo juu!!! Acheni wivu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Mtakufa na wivu! Mbona mashairi yake yametulia, na jamaa anasauti bomba kabisa, tena kamiligado!!!


Nani amuonee wivu aisee. I'm not an artist trying to compete with him or something but nimekuwa nafuatilia huu muziki kwa zaidi ya miaka 15, I know whats good and whats not.

Tatizo wengi wetu tunapenda sifa kupitiliza. Tukiambiwa ukweli tunanuna.

Kasikilize wimbo wa Prof. J na Jide unaitwa Niamini alafu ufananishe na Kamiligado walau utaniamini.
 
Labda Mtu mzima Jay akanunue ama akakope Mashairi kutoka kwa Kijana Roma Mkatoliki...

Ile Pride waliyonayo wasanii wetu ndo inafanya wengi wao washindwe kununua mashairi kwa kujiona wao ndo wanajua zaidi. Hata wakiandikiwa husikii wakikubali kwamba imekuwa hivyo.
 
akiongea anabana pua mno..kama vile anaigiza sauti ya mtu mwingine..mwambie aongee kama yeye..na ajue umri ndio huo..umeshasonga aingie kwenye harakati sasa ya kutoa vijana wapya..na aache ubinafsi, toka aanze gemu hana history ya kuinua wasanii wadogo.
 

Ahsante kwa ushauri. Naamini watu wake wanasoma humu na ujumbe utamfikia. Live bila chenga
 
hayo ndo matatizo ya virus. prof J ni kirus wakuu.
 
Mtakufa na wivu! Mbona mashairi yake yametulia, na jamaa anasauti bomba kabisa, tena kamiligado!!!

Af huo wimbo mi sichoki kabisa kuusikiliza!? Upande wangu huo wimbo ni bora kuliko nyimbo zake zote za mapenzi alizowahi kuandika ukiacha ule wa 'Niamini' akiwa na HBC
 
prof uko juuuuuuuuuuuuuu,usisikilize hawa watu wa humu wivu tu umewajaa,kama wewe uko creative kushinda jay kwa nini usiingie studio tukakusikia?
 
Jay ndio anapotea kabisa ,nilishaanzisha thread kuhusu nyimbo yake mpya ya aliyoitoa mwaka huu "Kama ipo ..." Ila wadau wakamtetea sana.Ukweli ni kwamba Prof kwa sasa hana jipya na kwa wanaomfuatilia sana kwa kakaribu watakubaliana nami kuwa huyu jamaa kalewa sifa na amejisahau sana.Ila tumwombee asijeakaishia kuwa kama Mr. Nice. Yupo mwingine anayejisahau na kujiona yeye ni wa kimataifa zaidi AY,tatizo la AY anapata nafasi ya kufanya ft na wasanii wa nje ila anashindwa kutumia hiyo nafasi vyema.Ukisikiliza hizo nyimbo alizofanya ft kama vile anawaiga wao naye aonekane wa huko.Kwenye sanaa hakuna kitu cha msingi kama kuheshimu ID yako.Faly Ipupa amefanya ft na Olivia na amepata heshima coz ameweza kulinda ID yake (style) yake.
 

Mkuu nimetake note tangu mwanzo, nliposikia huo wimbo kama ipo sijui nlianza kupata wasiwasi lakini sasa nina uhakika mkubwa kaishiwa.
 
prof uko juuuuuuuuuuuuuu,usisikilize hawa watu wa humu wivu tu umewajaa,kama wewe uko creative kushinda jay kwa nini usiingie studio tukakusikia?

Sio lazima wote tuimbe. Ukifanya vizuri unasifiwa. Ukiboronga pia unaambiwa. Kama huo ni wivu. Najivunia 'kumuonea wivu' Prof. J
 
Af huo wimbo mi sichoki kabisa kuusikiliza!? Upande wangu huo wimbo ni bora kuliko nyimbo zake zote za mapenzi alizowahi kuandika ukiacha ule wa 'Niamini' akiwa na HBC

Tunapimaje mafanikio yetu? Kufanya kile ulichofanya jana ama zaidi ya kile cha jana? Kama anafanya wimbo wa mapenzi ambao kiwango chake kipo chini ya Niamini maana yake ni rahisi sana = KAISHIWA!
 
My opinion yeah, but the majority here agree. But then we can agree to disagree, no hard feelings!

Don't underestimate minority then..
all I can see here you're just trying to put him down .. Is not worth it ..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…