Profesa Kabudi, nenda Madagascar ukatuletee miche ya Vanilla

Profesa Kabudi, nenda Madagascar ukatuletee miche ya Vanilla

Sehemu za moro vijijini inakubali
Kikubwa serikali iwekeze msisitizo na hamasa watu walime, watumie nguvu kama wanavyotumia kwenye mambo ya bongo fleva

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
Kweli serikali imelala kwenye biashara ya zao la vanilla. TADB na wizara ya kilimo wakatengeneze miradi na kutoa mikopo ya kutosha kwenye miradi ya vanilla.
Vanilla ni zaidi ya korosho, ufuta, kahawa na pamba. Vanilla ni utajiri.
 
Kweli serikali imelala kwenye biashara ya zao la vanilla. TADB na wizara ya kilimo wakatengeneze miradi na kutoa mikopo ya kutosha kwenye miradi ya vanilla.
Vanilla ni zaidi ya korosho, ufuta, kahawa na pamba. Vanilla ni utajiri.
Kama ndio utajiri kwanini hakuna msukumo wa serikali,shida ni nini?
 
Vanilla inalimwa maeneo mengi ya Tanzania hasa Kagera, Kilimanjaro na Morogoro. Hapa Tanzania wakulima wengi wanalima vanilla kama zao la ziada na wengi wanakuwa na miche michache ni nadra kukuta mkulima ana miche (pods) zaidi ya mia mbili. Bei ya vanilla kwa kilo haifiki laki moja kama mnavyotaka kutuaminisha, ni zao rahisi sana kulima kwasababu linaota sambamba na miti hasa kahawa, ugumu wake ni kwenye curing process hivyo kufanya wakulima wengi wauze ikiwa mbichi ambapo bei yake inakuwa ndogo kulinganisha na vanilla iliyokaushwa. Kwa hapa Tanzania kuna kiwanda cha ku process Vanilla kiko Moshi kinaitwa Natural extracts industries (NEI) na hao ndio wanunuzi pekee kwa sasa. Vanilla inayolimwa Kagera nyingi inauzwa nchini Uganda ambao pia ni wazalishaji wakubwa kwa hapa Afrika Mashariki.
 
Kama ndio utajiri kwanini hakuna msukumo wa serikali,shida ni nini?
Shida viongozi wetu serikalini na watanzania hatujui kuchangamkia fursa hasa makabila mengi tofauti na wachagga.
NB: Mimi siyo mchagga.
 
Kama ndio utajiri kwanini hakuna msukumo wa serikali,shida ni nini?
Kuna kamsukumo flani kalikuwepo miaka ya nyuma kwenye 2000 mpaka 2004 baada ya hapo hamna kitu. Sio siri Tanzania tuna rasilimali na mazao meengi yanayoweza kuunzwa nje na kuinua kipato cha wakulima, tatizo ni siasa
 
Kweli serikali imelala kwenye biashara ya zao la vanilla. TADB na wizara ya kilimo wakatengeneze miradi na kutoa mikopo ya kutosha kwenye miradi ya vanilla.
Vanilla ni zaidi ya korosho, ufuta, kahawa na pamba. Vanilla ni utajiri.
Nchi mkulima anapambana kivyake

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Vanilla inalimwa maeneo mengi ya Tanzania hasa Kagera, Kilimanjaro na Morogoro. Hapa Tanzania wakulima wengi wanalima vanilla kama zao la ziada na wengi wanakuwa na miche michache ni nadra kukuta mkulima ana miche (pods) zaidi ya mia mbili. Bei ya vanilla kwa kilo haifiki laki moja kama mnavyotaka kutuaminisha, ni zao rahisi sana kulima kwasababu linaota sambamba na miti hasa kahawa, ugumu wake ni kwenye curing process hivyo kufanya wakulima wengi wauze ikiwa mbichi ambapo bei yake inakuwa ndogo kulinganisha na vanilla iliyokaushwa. Kwa hapa Tanzania kuna kiwanda cha ku process Vanilla kiko Moshi kinaitwa Natural extracts industries (NEI) na hao ndio wanunuzi pekee kwa sasa. Vanilla inayolimwa Kagera nyingi inauzwa nchini Uganda ambao pia ni wazalishaji wakubwa kwa hapa Afrika Mashariki.
Kuna mkulima mmoja Bukoba aliniambia yeye anamuuzia bwana mmoja anayefanya kazi kiwanda cha sigara Dsm. Sasa sikuelewa hiyo vanilla inachanganywa kwenye sigara ama vipi.
 
Mche mmoja kiasi gani?
Heka moja inachukua miche mingapi kwa wastani?
Mche mmoja unazalisha kilo/gramu ngapi kwa msimu?
Miche inachukua muda gani mpaka ifikie kuvunwa?
Msaada tafadhali...
Mche mmoja wa mita mbili unauzwa kwa kati ya tshs 4,000 na tshs 6,000. Mche mmoja unachua miezi 9 au zaidi kuanza kuzaa na unatoa kati ya kilo 1 hadi tatu z ya vanilla mbichi ambayo ikikaushwa inaweza kuleta takribani nusu au robo tatu ya kilo. Vanilla inatoa matunda mfano wa maharage ndiyo ambayo huvunwa, mche wenyewe unaendelea kubaki na kukua ukiongezeka urefu. Miche yako ikiwa mirefu zaidi unaeza kuiuza kwa kukata kama unafanya prunning maana vanilla unapanda kipande cha mti wa vanilla yenyewe na sio mbegu.
 
Hujui kama Kuna watu wanalima vanilla hko kagera na bukoba tena Kuna wakati wakulima ikifika karibia
Na kuvuna wanalinda mashamba yao kwa ulinzi mkali sna....
Wewe labda ungeishauri serikali iwasisitize na kuweka nguvu kubwa watu walime zao Hilo
Kwani hata mbeya, tukuyu, moro vijijini zao Hilo likilimwa linakubali
Nna ushahidi kna mtu alienda kijiji cha rubale na alichkua miche ya vanilla na alienda kujaribu kupanda tukuyu mbeya na ilikubali, jamaa alikuwa na plan ya kufanya mradi huo huko mbeya ila bahati mbaya jamaa alikujaga kufariki
Tatizo watz siyo watu wa kufatilia mambo na kutekeleza
We washauri serikali ikazanie watu walime vanila
Maana Kuna maeneo mengi inakubali

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
@mrangi mkuu,tumetoka mbali mimi na wewe mkuu ujue! Kule kwetu tulipokuwa tunalima matikiti maji,kwa Faizafoxy,napo haya makitu yanakubalii!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mche mmoja wa mita mbili unauzwa kwa kati ya tshs 4,000 na tshs 6,000. Mche mmoja unachua miezi 9 au zaidi kuanza kuzaa na unatoa kati ya kilo 1 hadi tatu z ya vanilla mbichi ambayo ikikaushwa inaweza kuleta takribani nusu au robo tatu ya kilo. Vanilla inatoa matunda mfano wa maharage ndiyo ambayo huvunwa, mche wenyewe unaendelea kubaki na kukua ukiongezeka urefu. Miche yako ikiwa mirefu zaidi unaeza kuiuza kwa kukata kama unafanya prunning maana vanilla unapanda kipande cha mti wa vanilla yenyewe na sio mbegu.
Hekari moja miche mingapi?
Spacing yake inakuwaje?
Mkuu funguka zaidi, ndiyo elimu hii tunapeana.
 
Kuna mkulima mmoja Bukoba aliniambia yeye anamuuzia bwana mmoja anayefanya kazi kiwanda cha sigara Dsm. Sasa sikuelewa hiyo vanilla inachanganywa kwenye sigara ama vipi.
Sina hakika kama alikuambia ukweli watu wa sigara ni vigumu kununua vanilla ya shambani wakati wanaweza kupata ambayo tayari imefanyiwa curing na imekuwa extracted kupata vanilla concentrate.
 
Kama ndio utajiri kwanini hakuna msukumo wa serikali,shida ni nini?
Rejea maneno ya Rais Kwa wakazi wa bukoba 2016 baada ya tetemeko.


Serikali haina mpango wowote na mikoa yenye wasomi wengi maana wanapata challenge kubwa mfano ni kagera na KLM.

Ndo maana waliatibu mashirika Yote yaliyokuwa katika mikoa hio maana yalitaka kuizidi serikali.




Pia kagera ni mkoa wa mpakani . Ukiendelea Sana Una weza jitenga.
Ndo serikali inavyooamini.



We staajabu mkoa wa kagera Una watu million 3 ukiwa wa tatu baada ya dar na mwanza lakin haunaga mradi wowote hata stendi Tu wakazi Tu wenyew ndo wanajijengea.


Chuki hiz ndo zimesababisha Tz tuwe maskini Hadi leo
 
Vanilla inalimwa maeneo mengi ya Tanzania hasa Kagera, Kilimanjaro na Morogoro. Hapa Tanzania wakulima wengi wanalima vanilla kama zao la ziada na wengi wanakuwa na miche michache ni nadra kukuta mkulima ana miche (pods) zaidi ya mia mbili. Bei ya vanilla kwa kilo haifiki laki moja kama mnavyotaka kutuaminisha, ni zao rahisi sana kulima kwasababu linaota sambamba na miti hasa kahawa, ugumu wake ni kwenye curing process hivyo kufanya wakulima wengi wauze ikiwa mbichi ambapo bei yake inakuwa ndogo kulinganisha na vanilla iliyokaushwa. Kwa hapa Tanzania kuna kiwanda cha ku process Vanilla kiko Moshi kinaitwa Natural extracts industries (NEI) na hao ndio wanunuzi pekee kwa sasa. Vanilla inayolimwa Kagera nyingi inauzwa nchini Uganda ambao pia ni wazalishaji wakubwa kwa hapa Afrika Mashariki.
Unaona serikali yetu ilivyo ya ajabu na chuki zake.


Inashindwa nini kujenga kiwanda cha vanilla huko bukoba ili watu waache kuuza Uganda.


Pia Uganda kilo ni laki moja kama imekauka
 
Hekari moja miche mingapi?
Spacing yake inakuwaje?
Mkuu funguka zaidi, ndiyo elimu hii tunapeana.
Vanilla hailimwi peke yake kwasababu ni mmea pori unahitaji sana kivuli ndio maana vanilla inalimwa kwenye mashamba ya kahawa na migomba au mashamba ya kokoa au miembe. Ni mmea unaotambaa kama passion fruit kwa hiyo unahitaji support ya miti mingine yenye kivuli ili uweze kustawi vizuri. Huu mmeq hauchukui nafasi kubwa kwasababu unaota kuelekea juu hivyo spacing yako inategemea zao mama kama ni kahawa au mikokoa.
 
Back
Top Bottom