Profesa Kabudi, nenda Madagascar ukatuletee miche ya Vanilla

Profesa Kabudi, nenda Madagascar ukatuletee miche ya Vanilla

Mkuu umetoa ushauri mzuri sana wa kitaalam, hongera sana ila naona hukumuelewa vizuri mpandisha uzi.
Mtu kama wewe ambae hauna taarifa za mambo mengi ya nchi yako kuhusu kilimo huna moral authority ya kumshambulia na kumkosoa Prof. Kabudi kama ulivyofanya hapa.

FYI, aina ya Vanilla inayolimwa Madagascar ipo kwa wingi tu inalimwa mkoani Kagera. Hakuna haja ya kwenda kufuata mbegu za vanilla nchi nyingine.
Na vanilla kabila hiyo ndiyo bora zaidi duniani, inalimwa kwa wingi pia nchi jirani ya Uganda kiasi kwamba wanunuzi wakubwa wa vanilla ya Kagera wanatoka Uganda. Labda mshauri waziri wa kilimo akafanye hamasa ya miradi mikubwa ya kulima vanilla kibiashara zaidi kule Kagera. Ukitaka vanilla tuber cuttings kwa ajili ya mbegu wewe sema tukuuzie.
Pia ungeshauri watanzania wasiuze vanilla pods mbichi bali wafanye vanilla cure and vanillin extraction process hapa hapa nchini na kuuza bei ya soko la dunia.
 
Mbona Kagera bado kuna baridi sana karibu mwaka mzima?
Yes, Pemba wanalima, Kilimanjaro pia kuna watu wameanza kulima japo huko nahofia baridi inaweza kusababisha mazao duni.
 
Mkuu sina jibu la kitaalamu hapo ila ninachojua ni kuwa inastawi zaidi ikiwa pamoja na mazao mengine hasa kahawa na migomba.
Ni kwa sababu za kupata kivuli hasa majani ya migomba na hiyo mikahawa maana inakuwa inaleta kivuli
 
@mrangi mkuu,tumetoka mbali mimi na wewe mkuu ujue! Kule kwetu tulipokuwa tunalima matikiti maji,kwa Faizafoxy,napo haya makitu yanakubalii!?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahaha mkuranga, mwakisabe, mainge dah kule nlikuwa navuna tikiti na tango kma Sina akili nzuri
Mpaka Kuna jamaa walikuwa wafanyakazi hku wengine benki, wengine voda etc walinifata nao wakalime dah umenikumbusha mbali sana
Sawa Sawa ushauri wako ntakufanyia kazi
Ila connection najaribu kutoa Kadri Nnavyo weza
Mzee
Kama connection ya iliki niliwapa watu wngi mpaka chimbo wengine walifanya wengine tatizo wanataka
Kuletewa kitu mpaka wao walipo hawataki kuumia
Na siku zote nasema hakuna jambo rahisi rahisi
Lbda kama Kuna pesa mahali unachota

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
Na hio Vanilla ikionekana itawatoa wakulima then inaletewa Saga kama la korosho.

Bravo.
CCM iliuwa kahawa Bukoba na Kilimanjaro CCM ni wahujum uchumi number moja Tanzania!
 
Mche mmoja kiasi gani?
Heka moja inachukua miche mingapi kwa wastani?
Mche mmoja unazalisha kilo/gramu ngapi kwa msimu?
Miche inachukua muda gani mpaka ifikie kuvunwa?
Msaada tafadhali...
Mkuuu ntakupa jibu hivi karibuni shaka hondoa
 
Back
Top Bottom