Profesa Kitila Mkumbo: Serikali ipanue barabara ya Dar-Moro-Dodoma ili kupunguza ajali, magari ni mengi kwa sasa

Profesa Kitila Mkumbo: Serikali ipanue barabara ya Dar-Moro-Dodoma ili kupunguza ajali, magari ni mengi kwa sasa

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Serikali imeshauriwa kuboresha na kuipanua barabara ya Dar es Salaam-Morogoro hadi Dodoma ili kupunguza uwezekano wa ajali kutokea kutokana na wingi wa magari yanayotumia njia hiyo kwa sasa.

Ushauri huo umetolewa kutokana na wimbi la ajali mfululizo katika barabara hiyo, ikionekana kuwa wembamba wa barabara unaweza kuwa chanzo cha ajali nyingi.

Mbunge wa Ubungo, Profesa Kitila Mkumbo ameshauri hivyo wakati akiaga miili ya Profesa wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Honest Ngowi na aliyekuwa dereva wake, Innocent Mringo ambao walifariki kwa ajali Machi 28, 2022, Mlandizi Mkoani Pwani wakiwa njiani kwenda Morogoro.

"Mara zote lazima kifo kiwe na sababu, lakini takwimu zinaonyesha kuwa barabara hii ya Dar hadi Morogoro hadi Dodoma ni kweli ina magari mengi sana, ni vema Serikali ikawa na mradi wa kuipanua ili iendane na matumizi," alisema Profesa Mkumbo.

Miili ya wawili hao imeagwa Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Chanzo: MwanaHalisi
 
Sambamba na hilo, kukamilika kwa SGR Dar - Mwanza na Tabora - Kigoma na kuja kuendeshwa vema kutachangia kupunguza sana idadi ya malori katika barabara hizo. Ilimradi SGR haitaendeshwa kihasara hasara kama TRC na Tazara.
 
Kupanda Mlima kitonga tu siku hizi kwa wingi wa malori ni zaidi ya lisaa kwa gari ndogo.

Na Dar - Moro masaa manne na nusu kwa gari ndogo kwa wingi wa Traffic kusimamisha na kukagua malori ya mzigo, lori likisimamishwa na lianze tena safari lina sababisha msururu wa magari nyuma - je ya kisamamushwa ishirini ndani ya lisaa.

Kuwepo na check points na ukaguzi wa vituo tu.

Na ufahamu mwendo mkubwa pekee sio chanzo cha ajali.

Chanzo kinaweza kuwa , ubovu wa gari, udereva, watumiaji wengine wa bara bara, miiundo mbinu, mlongo longo wa magari bila sababu kufuata mstari, biashara barabarani , matrafic kuvizia magari badili ya kusaidia , kuna baadhi ya meneo angalau kwenda 80km per hr, mengine 100km per hr,mengine 50km per hr , mengine 30km per hr, sasa huku kwetu lori trekta gari zooote ni mwendo sawa - lazima ajali zitakuwepo.

Elimu ni muhimu na utekelezaji kwa uweledi hata traf8cc wakasomeshwe sio uwezo wao kutoza faini tu.
 
Yakisafirishwa kwa njia ya reli je wenye magari ya mizigo wakabebe nini?
Kama lengo ni kupunguza ama kuiondosha ajali ingelifaa wajikite kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa chanzo Cha tatizo barabara T1.
 
ubovu wa tera kukatika rock na kuua profesa wetu kunahusiana nn aseme standard gauge imalizwe haraka Sana sio kupanua barabara
 
Sambamba na hilo, kukamilika kwa SGR Dar - Mwanza na Tabora - Kigoma na kuja kuendeshwa vema kutachangia kupunguza sana idadi ya malori katika barabara hizo. Ilimradi SGR haitaendeshwa kihasara hasara kama TRC na Tazara.
Kuna unoko fulani unahitajika ili kuhakikisha reli zinaperform bila kuhujumiwa, vinginevyo sisi wenye malori tutapenda reli zisiwe na ufanisi ili sisi tuendelee na biashara zetu. Tatizo la ufinyu wa barabara litarudi pale pale.
 
Dar - Dom ina traffic kubwa kuliko Dar - Mbeya?
 
Ikiwezekana magari yanayoenda na yale yanayorudi yatumie barabara tofauti kabisa yaani iwe hakuna kupishana highway.

Overtaking inachangia % kubwa tu kwenye hizi ajali za barabara kuu.

Halafu malori mengi brake lights zake haziwaki so ukizubaa unalivaa au unalikwepa unamvaa unayekutana nae.
 
Ikiwezekana magari yanayoenda na yale yanayorudi yatumie barabara tofauti kabisa yaani iwe hakuna kupishana highway.

Overtaking inachangia % kubwa tu kwenye hizi ajali za barabara kuu.

Halafu malori mengi brake lights zake haziwaki so ukizubaa unalivaa au unalikwepa unamvaa unayekutana nae.
Ma kontena kwenda zambia na congo kwanini hawatumii reli ya Tazara kama sio upigaji tu .Hii ingepunguza sana malori lakini ndio hivyo wenye malori ni wanasiasa wa ccm.
 
Upanuzi ni muhimu sana, utasaidia kupunguza ajali.. Inatakiwa kuwa na barabara nne kila upande.

Lorries, magari makubwa, Tractors, slow cars, yakae kwenye first lane, yaingie kwenye middle lane ku-overtake slow car in their lane na kurudi kwenye lane yao.
 
Kabwe Katali,

Shida ni ukiritimba na huduma kuwa unreliable.

Hata hii SGR inaweza isiondoe malori barabarani kama usimamizi utakuwa mbovu.
 
Baada ya kifo cha Magufuli, ilivyopita mwaka niliona wananchi wakishangilia tajiri mmoja kuingiza malori zaidi ya elfu moja,
Mwingine Tanga aliingiza mabasi lukuki, wakashangilia,
Nikasema juhudi za Magu hawakuzifurahia watu za kuongeza njia kadhaa moro road, SGR na usafiri wa majini!
Mawazo ya Magu yangepunguza foleni, ajali na barabara zetu zingeishi muda mrefu!
Sasa hivi watu wanakufa, wanakuwa vilema kwa sababu ya uchu wa madaraka!
 
Sambamba na hilo, kukamilika kwa SGR Dar - Mwanza na Tabora - Kigoma na kuja kuendeshwa vema kutachangia kupunguza sana idadi ya malori katika barabara hizo. Ilimradi SGR haitaendeshwa kihasara hasara kama TRC na Tazara.
Nadhani bado hatujapunguza tatizo..kumbuka malori mengi yanaelekea tunduma kuliko barabara ya kati.

Uhitaji wa kupanua hii barabara bado mkubwa sana..kulingana na mahitaji ya sasa.


#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom