Uchaguzi 2020 Profesa Lipumba: Wingi wa watu kwenye mikutano ya kampeni ya wagombea wengine wa Urais haunitishi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba amesema wingi wa watu kwenye mikutano ya kampeni ya wagombea wengine wa urais haumtishi.

Profesa Lipumba amesema hayo jana Iringa Mjini wakati akifanya mahojiano na waandishi wa habari kuhusu mwenendo wa kampeni mpaka sasa.

Profesa Lipumba amesema anachokifanya ni kwenda maeneo ya vijijini ambako ndio kuna changamoto kubwa za Wananchi na sio kukusanya watu kwenye malori na mabasi kuwapeleka kwenye mikutano kama vyama vingine.

"Kampeni mpaka hivi sasa zinaendelea vizuri na nimejikita zaidi kwenda vijijini maana ndiko ziliko kero za Watanzania, mimi siishii mijini kama wenzangu ambao wamekuwa wakikusanya watu kwenye malori na mabasi.

Chanzo: Mwananchi
 
Hata wa bwana T.Lissu.

Chadema hawatakuelewa kabisa kwa hili jambo.
 

Sijui akiingia kwenye blanketi yake usiku anajihesabu na kujitafakari kama anafanya kampeni au anazurura!!!
 
Iringa shikamooni

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
We mzee hata udiwani kwenu kaliua huwezi pata
 
Hahaha ukiisha bebwa na shetani (ccm) wananchi hawatakukubali kamwe.

Ndio ajifunze kuwa usaliti ni laana.
 
Chama kinamlipa masurufu wakati wa kuzunguka. Na ndio nia yake kubwa hiyo. Per diem inatosha... Angependa kampeni ziendelee mpaka mwishoni mwa mwaka ili per diem iwe kubwa zaidi. Wala hana mpango na Urais.
Sijui akiingia kwenye blanketi yake usiku anajihesabu na kujitafakari kama anafanya kampeni au anazurura!!!
 
Ubunge jimbo gani CUF itashinda? Hata kata moja sidhani kama watapata
Wanasiasa huwa wana malengo ya mbali nje ya uchaguzi mkuu pia.
Unajua hapa anajipima uhai wa chama na kutafuta wanachama wapya.
Tunaweza kumbeza lakini anaeneza sumu ya chama chake mioyoni mwa watu.
Anakopita hatakosa wanachama wapya hivyo ni njia mojawapo ya kujenga chama hatimaye atakuwa na madiwani na wabunge baadae kuliko kutokwenda kabisa

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…