Profesa Ndalichako aagiza uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwachukulia hatua viongozi wa serikali ya wanafunzi

Profesa Ndalichako aagiza uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuwachukulia hatua viongozi wa serikali ya wanafunzi

Hawa nao si wawape tu hiyo mikopo!

Wanaendesha mashangingi ya bei mbaya na kujitanua kwenye viyoyozi wanakula machips tu!

Shangingi moja la hapo Ikulu likiuzwa linawalipia ada wanafunzi hamsini na zaidi!

Mmeyaatamia hayo mashangingi humo mna biashara gani nayo?

Halafu si tunasikia kwamba makusanyo yamepanda na mafisadi yote yamedhibitiwa hivyo mapesa yapo mengi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
DARUSO ni nguvu ya Mlimani. Jifunze umma ni nini?

DARUSO ni kikundi flani kinachoamini kuwa ndio kila kitu katika maamuzi ya wanachuo.

Wanaomba msaada kwa force. Kama pesa za baba yao. Sasa subirini mziki wake.
Hivi dola na nguvu ya uma nani mwenye power, usicheze na nguvu ya umma wewe umma ukiamua hakuna wa kuutuliza si polisi wala jeshi labda uuwe wote ,eti akuna wa kushindana na serikali,sema watanzania ni waoga tu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
USSR, Wanasaidiwaje wkt huo ni mkopo? Unajua lakini hawa viongozi wako unaowaona ni wazalendo walisomeshwa bure yaani bure kabisa na baba wa Taifa na wala hawakudaiwa hata sh. 1? Unafiki ni noma sana.
 
Serikali na wote wanaohusika (Bodi ya Mikopo)inapaswa iwaangalie wanafunzi wote ambao hawajapewa mikopo baada ya kuingia nao kwenye mkataba. Maisha chuo bila hela ni magumu mno. Kwa viongozi wa wanafunzi UDSM (DARUSO) mnastahili mtengue maneno yenu ya kuiamrisha serikali, Muige mfano wa SUA (SUASO) Walivyo andika barua yao kwa ustaarabu na hekima na yali ya juu, msiendeshwe na hasira kama haki ya kwenu mtapewa ila mkileta ubabe mtaisoma namba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wameleta shida kubwa sana hawa wazee (wabunge na watumishi wa wizarani) waliopitisha utaratibu wa kutoa mikopo kwa kubagua wakati wao walipata mikopo 100% kwa wote waliopata udahili bila kujali kipato cha mzazi au kozi ya mwanafunzi.
 
peno hasegawa,
Unamuonea bure fikiria kwa utulivu utajua tatizo liko wapi? Kuhusu mitaala ya Elimu ubadilishaji wake sio rahisi hivyo mkuu ni mchakato wa miaka kama 20+ fikiria tu kuhusu kuandaa wakufunzi na miundombinu mingine?
 
Kingjr2, Mkuu kuna uhuni mwingi unafanyika huko, nina wadogo zangu wawili huwezi amini wamepata mkopo na wako mwaka wa pili ajabu boom la first quarter hawakupata na walisaini tangu mwaka jana and this is another academic year.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We msomi wa wapi unatumia sera ndogo namna hii kuelezea suala la elimu? Unataka vyuo viwe vichache? Umesahau sera ya elimu imasema nini? Equality na equity inasemaje? Ni haki ya kila Mtanzania kupata elimu,na serikali yake ina haki ya kumwandalia mazingira mazuri ya kuapply elimu yake katika jamii husika na nchi yake.

Tuzingatie hoja muhimu kwakuwa kuongea pasipo kufikili kumetufikisha mahala pabaya pa kulaumu bila sababu badala yakutafuta ufumbuzi. Chikwuemeka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kasigazi kalungi,

It makes senses. Kuwasadia wengi kupata ufundi , kujifunza biashara, sana sana kilimo cha kisasa( irrigation, tractors, mbegu, udongo, dawa, masoko). Wakipata sehemu wapewe hizo facilities kimkopo wakifuna wanalipa. Tuna uwezo mkubwa kuwasaidia kwenye maeneo hayo. Tukiamua na wakiamua
 
Back
Top Bottom