Profesa Nonga: Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport

Profesa Nonga: Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport

Kama aliomba kibali Wizarani na hakupata majibu, kwa nini aliingiza mzigo? Mzigo ungekuwa na hitilafu bado tungewalaumu Wizara kwa kutodhibiti uingizaji bidhaa holela. Namsikitikia mkulima huyu. Ila kama alifuata taratibu akadai haki/fidia mbele ya sheria.
Hii ndiyo hoja ya msingi! Huyo mwekezaji kama kweli anavyodai mkurugenzi wa DVS kwamba ameona barua baada ya vifaranga kufika Dar basi ni mpuuzi kama wapuuzi wengine! Serikali imefuata matakwa ya sheria!
 
Na hayo ndiyo maswali wanayoyapenda,je kuna sheria yoyote halali inayokataza kununua mifugo au breed zingine nje ya nchi?
Sheria ya katazo haipo ila kuna sheria na miongozo ya kuingiza mifugo na mazao yake kutoka nje! Sasa wafanyabiashara wetu wakubwa wamezoea njia za mkato ili wapige faida kubwa!
 
View attachment 2466380
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo,Herzon Nonga akionesha Vifaranga vya kuku wa mayai vilivyozuiwa kuingia nchini,kutokuwa na vibali na cheti cha afya katika kago ya mizigo ya uwanja wa ndege wa Juliasi Nyerere,jijini Dar es Salaam jana.


Kukamatwa kwa vifaranga vilivyokuwa vikiingizwa nchini kumeibua masuala ya uwajibikaji na kutofuata sheria miongoni mwa viongozi wa Serikali na wadau wa sekta ya ufugaji wa kuku.

Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.

Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.

Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.

Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.

“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.

“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.

Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.

“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.

Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.

“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.

Chanzo: Mwananchi
Kwenye bidhaa zinazoingia nchini kukamilisha taratibu siyo option bali ni prerequisite.

Baada ya vifaranga kufa huyo Importer asubiri kupandishwa kizimbani kujibu tuhuma za kuhujumu uchumi. Mambo yako wazi tusipepese macho.
 
Kwenye bidhaa zinazoingia nchini kukamilisha taratibu siyo option bali ni prerequisite.

Baada ya vifaranga kufa huyo Importer asubiri kupandishwa kizimbani kujibu tuhuma za kuhujumu uchumi. Mambo yako wazi tusipepese macho.
Una kiwango gani Cha elimu
 
Kwenye bidhaa zinazoingia nchini kukamilisha taratibu siyo option bali ni prerequisite.

Baada ya vifaranga kufa huyo Importer asubiri kupandishwa kizimbani kujibu tuhuma za kuhujumu uchumi. Mambo yako wazi tusipepese macho.
Uko sahihi mkuu! Naona hapa kuna ndezi zinatetea ujinga! Huyo mwekezaji amechemka!
 
Daah inamaana kulikuwa hakuna namna nyingine ya kusolve na hao walioleta hao vifaranga? Wenye mamlaka wanashindwa hata kutafakari vizuri kweli? Nikweli kabisa inawezekana waliowaleta walikosea kufuata utaratibu na sheria lakini nadhani kulikuwa na namna bora ya kusolve hili
Kwa hiyo unashauli tusifate sheria ila mambo yakiharibika turekebishe mbele kwa mbele?
 
Hasara haziwezi kuisha iwapo asilimia themanini katika taasisi hiyo ni wabovu na wapenda rushwa.
Nchi inaendeshwa kwa taratibu. Kama aliingiza vifaranga hivyo bila kibali acha avune alichokipanda.
 
Team walamba asali wamekaa kimya , kipindi cha magu kuchomwa wale vifaranga sidhani ata kama buku wanafika waliimba kila nyimbo za kumkashifu jpm ,hili la vifaranga zaidi ya elfu sitini imewabidi walamba asali wafunike makalio yao na kuacha mbupu zinaning'ia kwa aibu.
Ndio uelewe nchi hii ni ngumu sana.
 
Ingekua ni enzi ya mpendwa wetu Magufuli, angeambiwa yeye ndiye kaamuru hao vifaranga wakamatwe.ila kwa sababu hii ni awamu ya malaika basi hatusikii kelele za akina Mbowe wala Lisu.
Tulishajua kwamba nchi hii hakuna upinzani, wote ni wasaka tonge tu. Tulishaamua ni CCM tu itawale hata miaka mia ijayo.
 
Team walamba asali wamekaa kimya , kipindi cha magu kuchomwa wale vifaranga sidhani ata kama buku wanafika waliimba kila nyimbo za kumkashifu jpm ,hili la vifaranga zaidi ya elfu sitini imewabidi walamba asali wafunike makalio yao na kuacha mbupu zinaning'ia kwa aibu.
Watendaji wa wizara wa kipindi cha JPM waliochoma vifaranga ndo wale wale walioshindwa kutoa vibali vya awo vifaranga, hakuna jipya apo....mwendo ni uleule bora hata tutokapo kuliko tuendako.
 
Kipi bora, Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport, au Vifaranga 3,000 vilivyo chomwa moto mpaka wa Tanzania na Kenya huko Namanga?
 
Nini tofauti ya yule Dikteta aliyevichoma moto vifaranga kutoka Kenya kule kwenye mpaka wa Namanga na huyu mama mipasho aliyeviua kwa njaa vifaranga kutoka ubeligiji hapo uwanja wa ndege wa DAR?

Chama cha Mambuzi ni kile kile.
 
Back
Top Bottom