Profesa Nonga: Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport

Profesa Nonga: Vifaranga 62,730 kutoka Ubelgiji vilivyokamatwa JNIA vyote vimefia Airport

Atakaye wajibika ni muagizaji sio aliyezuia.

Kwanza kuagiza bila kibali ni kosa tayari kwahiyo kama amekutuma kamwambie ameyakanyaga this time[emoji23]
Utawajibika Kwa mauwaji ya viumbe wasiokuwa na hatia. Kwani vifaranga vilishikiliwa na nani baada kukamatwa. Ni muingizaji au nyie. Shughuli pevu kwenu
 
Anae toa kibali ni DVS Mwenyewe ambae ndio alivizuia vifaranga hapo Airport. Kwa madai yake ni kwamba maombi ya vibali hayakumfikia.

By the way. Kuna kasumba ka watu kutojisumbua kuujua na kuufuata utaratibu. Na kuna kasumba ka watu kutoshirikisha ubongo katika kutatua changamoto ndo yanatufikisha hapa.

Wakati nasoma chuo kuna rafki yangu mchaga alikua ananambia nchi hii ina. mifumo miwili mfumo wa sheria na mfumo wa busara. Yaani kun wakati wafanya maamuzi wanatumia sheria na kunawakati sheria wanaweka pembeni wanatumia busara. Na ndivyo vinavyo tufikisha hapa




Sent from my CPH1819 using JamiiForums mobile app
Kwahiyo DVS alivizuia Kwa kukosa kibali. Je alijua ni viumbe hai au ni mawe. Kwanini hakuvipa huduma ya maji na chakula huku wakisubiri hatma ya vibali. Je hapo airport hao watu wanaozuia kuingia nchini bila vibali Huwa wanaachwa bila maji na chakula. Kuna Sheria za haki za binadamu na haki za wanyama ambazo zote zipo hai Tanzania.
 
View attachment 2466380
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo,Herzon Nonga akionesha Vifaranga vya kuku wa mayai vilivyozuiwa kuingia nchini,kutokuwa na vibali na cheti cha afya katika kago ya mizigo ya uwanja wa ndege wa Juliasi Nyerere,jijini Dar es Salaam jana.


Kukamatwa kwa vifaranga vilivyokuwa vikiingizwa nchini kumeibua masuala ya uwajibikaji na kutofuata sheria miongoni mwa viongozi wa Serikali na wadau wa sekta ya ufugaji wa kuku.

Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.

Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.

Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.

Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.

“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.

“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.

Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.

“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.

Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.

“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.

Chanzo: Mwananchi
Wapuuzi wengi wamejazana serikalini kiasi kwamba nchi nzima tunaonekana wapuuzi wapuuzi.

Hapo ni maagizo ya kukomoana na kukamiana.

Mungu atawamulika wajinga wote na wataenguliwa bila kujali nafasi zao
 
Huyo Mkurugenzi bwana Prof. Ni msemaji ws TRA?
 
Hujanielewa, namaanisha wawaishwe na pia wawe kwenye karantini.
Kweli kabisa hajakuelewa. Yaani wanakazania vibali tu wakati huduma za maji na chakula hawakuwapa. Wamefanya makosa makubwa sana Kwa kushindwa kuwapeleka kwenye karantini ambayo ndiyo ingetoa hitimisho ya vibali na magonjwa huku vikipatiwa huduma zote muhimu ambazo gharama angelipia muingizaji. Kuna watu wanasafirisha mbwa kwenda uingereza. Kufika kule mbwa waliwekwa karantini ya siku 14 kusubiri vipimo vya magonjwa na huku wakipatiwa huduma ya chakula na maji.
 
Bado huelewei kitu kwenye hizi taratibu.

Export permit ni kibali cha kule vilipotoka lakini kuingiza nchini kwetu lazima kuwe na import permit na cheti cha Afya.

Jaribu kutafakari vema haya mambo weka interest pembeni kwanza
Sasa hiyo Export Permit ilipokelewa na hao watu ?
 
Wewe ni Sukuma gang tu mnaongoza kwa Roho mbaya kupoteza uhai wa viumbe hamwoni shida bahati mbaya mlizaliwa Bara la giza mngezaliwa Ulaya au Marekani dunia ingejaa mateso ya kila namna.
Wafanyabiashara wa kipumbavu wanataka kutuingizia magonjwa ya mlipuko tukose kuku hapa nchini! Niko upande wa maafisa wa serikali!
 
Hakuna cha kufa hapo vimeshangia kwenye circle sasa hivi mnakula nyama zake🤣🤣🤣
 
Kweli kabisa hajakuelewa. Yaani wanakazania vibali tu wakati huduma za maji na chakula hawakuwapa. Wamefanya makosa makubwa sana Kwa kushindwa kuwapeleka kwenye karantini ambayo ndiyo ingetoa hitimisho ya vibali na magonjwa huku vikipatiwa huduma zote muhimu ambazo gharama angelipia muingizaji. Kuna watu wanasafirisha mbwa kwenda uingereza. Kufika kule mbwa waliwekwa karantini ya siku 14 kusubiri vipimo vya magonjwa na huku wakipatiwa huduma ya chakula na maji.

Unajitia ujuaji usio na maana.
Wapelekwe karantini kwa mujibu wa Sheria gani?
Hizi taratibu zilishaandika Kisheria sio kujisikia tu unafanya.

Humu mnakomenti kwa sababu mna bando, mkielimishwa mnakimbilia oooh mbona unatetea sasa kama tunajua taratibu kwanini tusiwambie nyie msiojua?
 
Mbona unatetea sana. Unaogopa nini. Mmefanya makosa Kwa kuwatesa viumbe wasio na hatia mpaka kupelekea vifo. Mnatakiwa muwajibike. Unajua viumbe hai vina uhuru wa kutokuwa na njaa au kiu. Sheria ya ustawi wa wanyama Tanzania inasema hivyo na nyie ndiyo wizara husika. Iweje mvunje Sheria mliyoianzisha wenyewe. Kuna mfugaji Moshi alichoma vifaranga, wizara ya mifugo ikasema itamchukulia hatua Kwa kukiuka Sheria ya ustawi wa wanyama, Haya Sasa na nyie jichukulie hatua Kwa kukiuka Sheria ya ustawi wa wanyama Tanzania.

Huna ujualo utasubiri uone kama kuna mtu atachukuliwa hatua zaidi ya aliyeagiza vifaranga.

Enzi za JPM vilichomwa moto kabisa, enzi hizi za Samia Serikali imekuwa na uungwana mwingi ndio maana muagizaji aliambiwa avirejeshe vilikotoka
 
Huna ujualo utasubiri uone kama kuna mtu atachukuliwa hatua zaidi ya aliyeagiza vifaranga.

Enzi za JPM vilichomwa moto kabisa, enzi hizi za Samia Serikali imekuwa na uungwana mwingi ndio maana muagizaji aliambiwa avirejeshe vilikotoka
Lakini majibu tutayapata tu yawe positive au negative.
 
Unajitia ujuaji usio na maana.
Wapelekwe karantini kwa mujibu wa Sheria gani?
Hizi taratibu zilishaandika Kisheria sio kujisikia tu unafanya.

Humu mnakomenti kwa sababu mna bando, mkielimishwa mnakimbilia oooh mbona unatetea sasa kama tunajua taratibu kwanini tusiwambie nyie msiojua?
Hujui lolote ni kelele tu na kulazimisha ueleweke. Hata Sheria ya mifugo kuingia nchini hujui. Weka Sheria hapa . Kama wewe ni afisa huko au muuza kuku mwenye wivu na wauza kuku wengine ni lazima muwajibike. Na lazima mama kaisha yapata kuwa mnataka kumuhurabia kupitia kichaka Cha Sheria badala ya kutumia busara
 
Wewe ni Sukuma gang tu mnaongoza kwa Roho mbaya kupoteza uhai wa viumbe hamwoni shida bahati mbaya mlizaliwa Bara la giza mngezaliwa Ulaya au Marekani dunia ingejaa mateso ya kila namna.
Chief sheria za nchi lazima zifuatwe!
 
View attachment 2466447
Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.
Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.
Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.
Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.
“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.
“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.
Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.
“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.
Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.
“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisemaJoto

View attachment 2466380
Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo,Herzon Nonga akionesha Vifaranga vya kuku wa mayai vilivyozuiwa kuingia nchini,kutokuwa na vibali na cheti cha afya katika kago ya mizigo ya uwanja wa ndege wa Juliasi Nyerere,jijini Dar es Salaam jana.


Kukamatwa kwa vifaranga vilivyokuwa vikiingizwa nchini kumeibua masuala ya uwajibikaji na kutofuata sheria miongoni mwa viongozi wa Serikali na wadau wa sekta ya ufugaji wa kuku.

Vifaranga vilivyozuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Desemba 22, 2022, ni mali ya Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliyopo Mkuranga mkoani Pwani.

Vifaranga hivyo vilivyofungwa kwenye maboksi 697 yenye thamani ya Sh200.262 milioni, vilikamatwa wakati wa ukaguzi walipokuwa wakiingizwa nchini kutoka Ubelgiji.

Mwananchi imebaini kuwa Kampuni ya Phoenix Farms Limited iliwasilisha barua ya maombi kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuomba kibali cha kuagiza vifaranga kutoka nchi hiyo ya Ulaya.

Pia, imethibitishwa kuwa waagizaji walikuwa wamepewa cheti cha mifugo na mamlaka ya Ubelgiji.

Baadhi ya wadau katika sekta hiyo wameishutumu wizara hiyo kwa kushindwa kutoa leseni za uagizaji bidhaa kutoka nje na kuchukua hatua za ziada kuwalinda wawekezaji wa ndani.

“Mamlaka zimeshughulikia suala hilo kwa njia isiyo ya haki. Walitakiwa kutoa kibali hicho kwa kuzingatia kwamba nchi haina uwezo wa kuzalisha kuku wa kukidhi mahitaji yake,” alisema mdau kwa sharti la kutotajwa jina.

“Vifaranga hivyo vingeweza kupelekwa kwenye shamba la kampuni hiyo na kuwekwa karantini humo. Vingegundulika kuwa na afya njema mwekezaji angeweza kuadhibiwa na vifaranga virudi kwake,” kiliongeza chanzo hicho.

Alipotafutwa, Ofisa Mkuu wa Phoenix Farms Limited, Irfan Mitha alikataa kutoa maoni yake kuhusu uhalali wa hati mbili zilizotajwa hapo juu.

“Niko busy leo; nipigie simu kesho, nitakuwa kwenye nafasi ya kutoa maoni yangu,” aliliambia gazeti hili.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo (DVS) katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Profesa Hezron Nonga alisema ombi la kibali cha kuagiza cha Desemba Mosi, 2022, halijafika ofisini kwake wala wizarani.

“Tuliona barua ya maombi ya vibali kutoka nje ya nchi, muda mfupi baada ya vifaranga kukamatwa JNIA. Kadhalika, cheti cha mifugo kilichoandikwa na Shirikisho la Ubelgiji la Usalama wa Mnyororo wa Chakula (FACFAS),” alisema Profesa Nonga.

Akitoa taarifa ya vifaranga hivyo, Profesa Nonga alisema vyote 62,730 vimekufa baada ya kutelekezwa kwenye uwanja wa ndege.

“Mwagizaji ana kesi nyingine ya kujibu mbele ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuwa mipango ya uteketezaji wa kuku inaendelea,” alisema.

Chanzo: Mwananchi
Wahusika wote wamefanya makosa makubwa sana! Wanafahamu joto Ulaya Sasa hivi ni nyuzi joto 0 mpaka 7 hivi. Hapo bongo ni nyuzi 32na zaidi. Joto lenyewe linatosha kuviua. Kwa kutambua hilo, wangeviachia kwa masharti na utaratibu maalum.
 
Asante mkuu kwa ushauri mzuri
Ushauri wa namna hii ndio ulioifikisha Nchi hii hapa ilipo kila mtu atakikufuata sheria kwa kutegemea njia za mkato na ndio maana kiongozi akifuata sheria tu anaonekana ni mtu mbaya/dikteta
 
Back
Top Bottom