Profesa Shivji: Wasomi wanaogopa kukosoa Serikali ili wapate teuzi. Hawana msaada tena kwa jamii ya Watanzania

Lkn sisi Waafrika bhana, hata mwenye uchungu na nchi na Wananchi na anayejaribu kuwatetea bado ni Muhindi pia, wasomi weusi wote wizi tu, wanaibia na kuharibu hata nchi waliozaliwa!
 

Kuwa mwepesi wa kukimbilia kukosoa nako ni udhaifu. Mtu mwenye ueledi na uhodari huwa anashauri na kutoa mapendekezo.
 
Lkn sisi Waafrika bhana, hata mwenye uchungu na nchi na Wananchi na anayejaribu kuwatetea bado ni Muhindi pia, wasomi weusi wote wizi tu, wanaibia na kuharibu hata nchi waliozaliwa!
Sio Muhindi Prof Issa Shivji, ni Mtanzania kama mimi na wewe.

Utanzania sio Ubantu pekee.
 
Sio Muhindi Prof Issa Shivji ni Mtanzania kama mimi na wewe.

Najua lkn ana asili ya India, yani wazazi wake wote wawili walitokea Asia, hata ukimuangalia siyo Muafrika kwa muonekano atleast!
 
Najua lkn ana asili ya India, yani wazazi wake wote wawili walitokea Asia!
Hayati Karume alikuwa na Asili ya Nyasaland leo Malawi ina maana Bi Fatma Karume akijenga Hoja utasema Mmalawi anaupiga mwingi?

Samia Suluhu ana asili ya Mboka Kindu Maniema huko Kongo ya Mashariki

Akituhutubia kwa Kiswahili chake fasaha utasema kuna Mkongo anatuhutubia?

Acha ubaguzi ndugu.
 
Hayati Karume alikuwa na Asili ya Nyasaland leo Malawi ina maana Bi Fatma Karume akijenga Hoja utasema Mmalawi anaupiga mwingi?

Usinielewe vibaya, sijampinga Shivji, ila kuna ukweli ambao huwezi kuukwepa kwamba Shivji ana asili ya Asia, hata kwa muonekano tu, Malawi ni Afrika bado hivyo sidhani kama
inafanana!
 
Usinielewe vibaya, sijampinga Shivji, ila kuna ukweli ambao huwezi kuukwepa kwamba Shivji ana asili ya Asia, hata kwa muonekano tu, Malawi ni Afrika bado hivyo sidhani kama
inafanana!
Wote wewe mimi na Shivji tumezaliwa na Mama mmoja.
 
Sema huyu Mzee Ukomunisti wake ndio huwa unaboa.
 
Professor Shivji ameongea ukweli mtupu,
Shida ni kwamba hela za kule bungeni ni tamu sana, taamu mno!
 
Wasomi wapo kwa ajili ya matumbo yao tu. Hawana msaada wa kitaaluma kwa taifa letu tena. Hawakosoi kwa manufaa ya umma
Ni msomi yupi Tanzania anayepoteza muda wake maabara au Maktaba akihangaika na utayarishaji wa machapisho ya utafiti alioufanya.

Kaangalie, kote kwenye vyuo vyetu na taasisi maalum zenye wajibu wa kutafiti maswala mbalimbali yanayoweza kufumbua matatizo ya wakulima wetu, au huduma zetu za kiafya, ama usindikaji wa viwandani, ni machapisho mangapi yanayofanyika toka huko kwa mwaka nyakati hizi!

Lakini ukitafuta wataalam hawa wanavyohangaika na mikutano ya kisiasa ya CCM, huwezi kukosa kujua ni wapi panapowekewa uzito zaidi.
Lakini isingekuwa neno, kama uwepo wao huko kwenye hicho chama kungesaidiwa na utaalam wa watu hawa, ili kupitia huko nchi inufaike. Lakini wapi, wanapoingia huko inakuwa kama wamenyofolewa bongo zao kichwani.

Lakini tusiwalaumu wanazuoni pekee. Ni mfanya biashara yupi asiyejihusisha na siasa ili anufaishe biashara yake mwenyewe. Kwa hiyo lawama zote zinabebwa na huyo anayefanya mazingira ya watu hawa kutelekeza maeneo yao na kuingia huko kwenye siasa, kwa sababu ndiko kunakolipa zaidi.
 
Kila mkubwa yeyote akisimama jambo la kwanza ni kumsifia Rais. Why?. Wewe chapa kazi na kutokana na uchapa kazi yako Rais atakuona tu. Wengi ni wachumia tumbo.
 
Badala ya kutaja serikali kuwa imetoa huduma kutoka Kwenye makusanyo ya kodi za wananchi,

Badala yake wanamsifia kiongozi Mkuu utasema hiyo hela kaitoa mifukoni mwake ,

Na kwamba kama vile ni hisani badala ya wajibu .

Inashangaza mno!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…