Profesa Tibaijuka: Trump kusitisha misaada ARVs zitaadimika Afrika. African Union iitishe kikao maalum kuweka mkakati

Hapo watu hawana budi kuelewa ya kwamba professor Tibaijuka anaiamsha serikali iwe proactive katika ketenga bajeti mapema ya dawa za ARV wasisubirie mpaka watu watakapo kuwa wanadondoka kama kuku wa mdondo ndio hatua zichukuliwe,maana akili za watu weusi ni reactive wanasubiria mpaka waone athari za moja kwa moja wakati itakuwa too late .
 
Siku 85 wakati US anafanya hizo auditing ni nyingi kwa mtu mmoja mmoja kujitegemea lakini kama nchi naamini itafanya jambo
 
Unaelekea unapenda ushoga
Waambie Watawala wako wawe na Mipango na Mikakati madhubuti ya kuimarisha chumi za nchi zao, waache kutegemea Misaada kutoka kwa mashoga. La sivyo wakubali vigezo na masharti ya Watoa Misaada ikiwamo na kuukubali Ushoga. Kukubali Misaada kutoka kwa mashoga ni sawa na kuukubali Ushoga. Katika muktadha huu, Je, ni nchi gani hasa ya Afrika ambayo inaweza kujinasibu kwamba haikubaliani na Ushoga ikiwa miaka yote kabisa nchi hizo zimekuwa zikipokea Misaada kutoka kwa hao Watu?
 
Sawa sawa
 
Aiseeeeee! USA ni kiboko. Trump amekohoa kidogo tu dunia yote imeskia sauti yake. Wale ambao mmekuwa mnaitukana USA huku mkimeza ARV's za msaada kutoka USA mjitahidi muwe na shukrani. Ni imani yangu mheshimiwa Trump atarudisha moyo nyuma na kuendelea KUTUFIKIA.
 
Dunia tunayoishi ina mambo Kweli Kweli

Vijana badala ya kusikitika Wao ndio kwanza wanampongeza Rais Trump Kwa kuzuia dawa za kufubaza virus Vya ukimwi zisiletwe Kwa msaada

Nimeshangaa sana 🐼
Daah tumefikia huku😔😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…