Project funding sources


Hongera, nitafute kama utakuwa interested na mm tuongee zaidi nitakusaidia
 
Msanii pliz respond ASAP
Mkuu niwie radhi sana kwa kutokufikia kwa wakati.
Nilikuwa bize na hizi movements za kuwapatia watu ukuu wa nchi naona nijiondoe huko maana hakusomeki vizuri..

nimepata contacts zako mkuu wangu
 
Mkuu
watu wa Oxfarm wanatoa funds kwa projects kama yako. wameshafadhili na kuendeleza miradi kadhaa afrika hivyo usisite kuwatafuta.

mimi nina knowledge ya fairtrade ambapo kama ukitaka tuition na contacts usiogope kuwasiliana.

FairTrade ya namna gani mkuu #Msanii
 
FTO kirefu chake ni Fair Trade Organizatio ambayo kubwa inaratibu mtandao wa masoko ulimwenguni ambayo yanawaunganisha moja kwa moja marginalized producers, suppliers, vendors na chain kubwa ya collectors, suppliers na shops kwa mfumo wa biashara huria.

Kuna orodha ya bidhaa ambazo unapoziingiza soko la Ulaya na Marekani kwa mfumo wa Fair Trade zimeondolewa kodi. Ofcourse utalipia kodi nchini kwako lakini kodi hiyo haitakuumiza kulingana na faida utakayoipata.

Soko ni kubwa, wenye elimu hii nchini ni wachache na wamegoma kabisa kufanya advocacy ili wengi mlijue, wenzetu Kenya wamekuwa wanasafirisha bidhaa nyingi sana zenye uasili wa Tanzania kwa mfumo huu. Na hili linachangiwa na umangimeza wa Chember of Commerce, Members wa Tanzania waliopo COFTA (FTO ya Afrika) na sisi wenyewe kutofanya tafiti za masoko.

Soko hili la FairTrade ni tofauti na Trade Fair. Ukishakubaliwa kuwa mwanachama wa COFTA unaingia moja kwa moja FTO. Zamani FTO ilikuwa inaitwa IFAT yaani International Fair Trade Association. Kumbuka kuwa FTO ni mwanachama mahususi wa WTO World Trade Organization. Mimi nilihappen kuifahamu vyema hii biashara kwa kufanya kazi katika organization moja iliyokuwa member wa IFAT hapa nchini. Ndipo nilipogundua umangimeza wa Watanzania kuwabania wengine linapokuja suala la mafanikio ya kiuchumi.

Faida ya kuingia na kujiunga na soko hili, ukishakubalika uanachama unakuwa unapokea weekly/ monthly marketing updates kupitia email yako. Na hizi updates ni outstanding orders ambapo unachopaswa ni kutuma quotation na picture samples za products, sambamba na hilo mode of payments Sipo very fair kwani wanakutumia 50% ambayo annotate kuandaa order na change inabaki, kisha ukishatuma (shipping ni gharama yao) wanakumalizia 50%. Pamela na kuwa utakuwa unalipwa 100% ya order kumkbuka kila order utakayotuma wanamkata receiver token inayoingia kwenye mfumo walioutengeneza uitwao SHARED INTEREST na hilo ni hela yako utakayopewa kila baada ya muda fulani. membership fee yako ambayo utaweza kuilipa ndiyo gateway ya wewe kutumiwa air ticket, accomodation na any other expenses kwa kila shughuli utakayoshiriki ya FTO ulimwenguni.

Nilipenda miaka mingi kutoa elimu hii kwa Watanzania wenzangu lakini sikubahatika kuona anyone interested. Kuna mengi sana katika hii biashara kwani wazungu wameshazindua miaka mingi mtaala wa Fair Trade na faida zake ni kubwa kwa nchi zetu zinazoendelea. Watakuja kukukagua, kukuelimisha kujikagua, wanazingatia governing laws kama child labor, women rights n,k. Pia unaelimishwa namna ya kuthaminisha products zako, packaging na kadhalika just for free.

Maadamu tumeamua kuwa msingi wa maendeleo ni siasa basi tuchape siasa labda tuta export siasa some day na kukuza uchumi
 
Unapata ujuzi how to participate in Trade Fair.

TANTRADE wangelikuwa moderate wangesaidia exhibitors wengi wanaoshiriki sabasaba. Ila undundundu wetu unatulipa mabua
 
Mh, am so interested with all that Hv been posted here.
I am regretting why I did not read these posts earlier. They are so good. Natamàn nianze kulima mihoho leo ila ngoja nisubiri nipate kidogo vijicent.
But plz ningependa kufahamu mtaji unaohitajka kwa hekali moja. Naomben kuwasilisha.
 
..................hongereni wanaJF kwa ushirikiano mnaounesha kila mara inapohitajika kufanya hivyo. Mungu awabariki

Mkuu naombaunipe aob za hiyo ki.
nataka nifanya da same project
 
FURSA YA KIFEDHA KWA WAJASIRIAMALI WA KUKU NA MAHINDI

Je wewe ni mjasiriamali?

Je ungependa kukuza biashara yako?

Kama ni msindikaji wa chakula una kuku, mzalisha ji wa vifaranga, msindikaji wa nyama ya kuku, mzalishaji wa mbegu za mahindi, msindikaji wa mahindi, nk… Watoa huduma na bidhaa nyingine zinazohusiana na mahindi mnakaribishwa kutuma maombi YENU!

Kufuzu lazima kampuni yako ijiendeshe kifaida na shughuli za biashara yako lazima zihusiane na sekta ndogo ya kuku au mahindi.

Biashara yako lazima iwe katika mikoa ifutayo Dar es Salaam, Zanzibar, Kilimanjaro, Arusha, Dodoma, Manyara, Morogoro, Tanga, Iringa, Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Tabora, Mara, na Singida. Pia ilenge kuboresha uzalishaji kwa wakulima na wafugaji kuku maskini katika maeneo husika.

Tafadhali tembelea ofisi ya tawi la BRAC iliyo karibu nawe, tovuti yetu tanzania.brac.net au wasiliana nasi kwa kupiga simu namba +255 754413533 au barua pepe ifuatayo leadtzf@gmail.com KUTUMA MAOMBI au kufahamu juu ya mfuko wa uwekezaji wa mradi wa Kuwezesha Kimaisha kupitia Maendeleo ya Kilimo na Mifugo (LEAD).

Tarehe ya mwisho ya kutuma maombi awamu hii ni Oktoba 31, 2015!


Supported by/ Imedhaminiwa na UKaid
1113
 
Hi wajasiliamali wenzangu!
We are a company of business and management experts dealing with various consultancies such as project write ups, pcroject evaluations, business plans, company registrations, Taxation, tax returns, business names, business consultancies etc.

Any firm , NGO, company or individuals who need to write a proposals for funding etc, are highly invited to PM the author.

We are committed to finish your work within a given time frame in a professional way you can't imagine. Our price is negotiable. "Kazi Bora kwanza!" is our motto. Mteja wetu huwa analeta kazi nyingine na Wateja wengine, jaribu kutupa kazi hautajuta! PM the author for more details or phone us through our # +255 688 778 484 advance payment siyo lazima kazi kwanza!
 
We are the company dealing with technical issues to support other businesses, achieve their goals.

We prepare and offer the following services to Non Government Organizations (NGOs) and Companies: (1)Concept Paper (2) Project Proposals (3) Business Plans and businesses registration (4) Budgets (5) Annual Work Plan (6) Annual Accounts (7)Annual Report (8) Sourcing Donors / Funders for your Projects. (9) Project Design (10) Project Management (11) Project Monitoring and Evaluation (12) Capacity Building & Training to your organization etc. For no small or big business we can't serve. Please Contact us through, Bizsolutions Co.Ltd, 0688778484. Email:-bizsolutions@mail.com
 
Unapata ujuzi how to participate in Trade Fair.

TANTRADE wangelikuwa moderate wangesaidia exhibitors wengi wanaoshiriki sabasaba. Ila undundundu wetu unatulipa mabua

Mkuu....kama hutajali hebu funguka zaidi ni Biashara gani wanazodili nazo hao ndg km hutajali nakuPM mawasiliano yangu...ili nipate hii Elimu vzr
 
Msanii shida yangu mimi ipo kwenye hizo mambo za proposal write up for NGOs ,nipe maelezo kidogo ya Oxfam
 
Last edited by a moderator:

In case mmeniandikia na sijapata ruzuku,?
 
Mkuu....kama hutajali hebu funguka zaidi ni Biashara gani wanazodili nazo hao ndg km hutajali nakuPM mawasiliano yangu...ili nipate hii Elimu vzr
Mkuu, biashara zilizopo kwenye fairtrade markets zimeorodheshwa kwenye constitution ya Fair Trade Organization. Nakutajia kwa uchache, Kazi za mikono yaani craftworks (kingoni), Mazao kama ndizi, kahawa, chai, Zanzibar Spices.... orodha kamili sinayo hapa ila naamini ukianza kulifuatilia hili soko utajifunza mengi sana.

Msanii shida yangu mimi ipo kwenye hizo mambo za proposal write up for NGOs ,nipe maelezo kidogo ya Oxfam
Tuwasiliane mkuu wangu

Kiongozi, nimejaribu kukutafuta nakukosa. Naamini kama ukimaanisha kuisaidia sekta ya wazalishaji nchini basi ukipata some hints kutoka kwangu utaweza kwenda beyond levels na kufungua fursa nyingi kwa wabongo...

Watanzania tambueni kuwa, mnapoona wageni hasa wakenya wanakuja kununua bidhaa nchini tena huko mashambani, just mjue wanaziexport ulaya kwenye soko la uhakika ambalo vendor anapanga bei. Na hizo bidhaa zikienda huko zinaenda na chapa ya Kenya.

Nimenena kwa ufupi sana.
 
mrejesho vipi ulipoishia mkuu

Ni kwamba mavuno hayakua mazur mdau,kama unavyojua hali ya hewa ya mwaka huu iligubikwa na ukame,briefly nimepata hasara,mwaka huu nimeshindwa kulima kwa kua mfuko wangu hauruhusu na pia nilishikwa na harakat za masono,may be msimu wa 2016/2017 ntarud tena shamba,kama nitalima Kusini bas ni Ufuta na Mbaaz,na kama ntalima Songea ni Mahindi na Tangawizi,bado naamini Kilimo kitafikisha somewhere
 

Pole sna mkuu kwa changamoto zilizokukuta, kikubwa ni kupigania kile unachokiamini hata kama utapita kwenye mazingira magumu.
Hope utafanikiwa msimu ukiwadia nakutakia kila jema kwako.
 
Pole sna mkuu kwa changamoto zilizokukuta, kikubwa ni kupigania kile unachokiamini hata kama utapita kwenye mazingira magumu.
Hope utafanikiwa msimu ukiwadia nakutakia kila jema kwako.

Asante sana mdau
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…