Proved: Diamond Platnumz alipia Matangazo Youtube

Proved: Diamond Platnumz alipia Matangazo Youtube

Kwahiyo wewe unataka Diamond aendeleze uswahili kwakuwa sisi ni waswahili?
Acha hizo wewe na ujiamini maana kila kitu wewe unafanya comparison

Sent using Jamii Forums mobile app
Uswahili ni nini kwanza..?? yawezekana hujui hata maana ya neno hilo..

Kwani ww binafsi unamtaka nini mtu mpaka uanze kumpangia jinsi ya kuishi na jinsi ya kuendesha maswala yake yanampo mkate wa kila siku.

Wengi kama wewe uchambuzi wenu umejaa chuki na vinyongo kwa watu mnaowakosoa.

Na hiyo comparision nimeifanya wapi zaidi ya kukuonesha kuwa kuna mastaa kibao wanatumia "add" katika kutangaza biashara zao hususan Ytube.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwahiyo, komaa na maisha yako ww hao tyr wametoka kimaisha

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa unashindwa kuelewa kipi mkuu au uelewa mdogo.
Hii ni forum na anaeongelewa hapa ni staa haijalishi amefanikiwa kimaisha au la. ustaa wao ndiyo unatufanya tuwajadili, huwezi kuondoa stress zako za maisha kwa kuacha au kuwajadili mastaa
 
Kanunue na wewe weka kwa msanii yeyote unae mtaka,wewe tu na ela yako
 
Nafikiri umenielewa vibaya ndugu yangu; vile vile ninajuta kuwa sikukumbuka kuwa thread za namna hii huwa ni za timu. Maoni yangu yalikuwa ni hiyo observation kuwa ninaletewa video hiyo hata jambo ninalofanya halina uhusiano na muziki. Niliangalia video hiyo mara tatu, na vile vile niliangalia ya kiba mara tatu pia kwa vile zilikuwa zimeandikwa sana mtandaoni. Ukiangalia screenshots nilizoweka hapo, utagaundua kuwa mimi ninaangalia muziki wa aina mbalimbali sana, siko tied na timu yoyote; samahani sana kama post yangu hiyo imekuudhi!
Je kiba kulipia Instagram na vevo ngoma yake iangaliwa Mara Nyingi hukuliona.....next time kaa fanya utafiti kwa pande zote mbili ila hapa tunakuona kama shabiki unaejificha kwny kichaka cha msema ukwl usiye na team.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Gepu linazidi kupungua tu day after kutoka 1M view ASA iv ni laki 6 nahisi washaanza kuchanganyikiwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Washaishiwa pumzi haoo.. Kesho tunawa overlap

IMG_20170904_195857_624.jpg
 
Dai alianza chokochoko mwenyewe, huruma za wananchi zikamuokoa kiba. Hili n funzo kwake hatorudia tena,. Tatizo alijiona kuwa na bashite basi kila anachokifanya kitakua sawa. Watu hawapendaji ujinga et

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Diamomd uswahili ndio unamgharim. Akiachana na mambo ya kiswahili na mameneja wa uswahilini, bado hana mpinzani.

Huo wimbo unaousema ni wimbo wa kawaida sana, sema yeye kaupa headline na jamaa katumia hyo kama kupata public sympathy, baada ya Alkiba kutoa wimbo na kesho yake WCB kutoa wao, Alkiba kapata huruma ya watu kwamba anabaniwa na WCB.

Angetumia akili wala huo wimbo wa Alkiba usingefika popote, ungekua ushajifia kifo cha asili, au usingepata media attention kiasi hicho.

Bado naamini Diamond akiacha uswahili atanedelea vizuri, vinginevyo atapotea.
Mnataka afanye UZUNGU gani...!!? wekeni wazi basi....!

Mnamaanisha nini...ina maana Kiba ana Uzungu...!? wekeni wazi wadau...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona hiyo siyo nyimbo ya kwanza kwa yeye kufanya hivyo. Na hata amefanya mini sioni tatizo, ukisikia watu wanafanya promotion ndiyo hivyo kaka!! Hata wasanii wakubwa wanafanya hiyo kitu. Tatizo lako wewe ushamba unakusumbua ndugu. Nyimbo mpya ukitoka kufanyiwa promo ni lazima.

Akili zako unanikumbusha siku moja nilienda kufanya kazi kwa mteja wa kampuni ninayofanyia kazi, nafika pale yule mteja akawa anasema "kampuni yenu siku hizi imeshuka sana kwa namba ya wateja, naona munajitangaza sana na wakati zamani munilikuwa hamufanyi". Mimi nikamuuliza swali dogo tu "mama kwani sisi na kampuni kama tigo, ipo ni kampuni kubwa?", "tigo kampuni kubwa". Nikamuuliza tena "huoni kila ikitembea dakika tano unakuta mabango ya tigo?? Ukifungua radio mara kwa mara unakutangazo za tigo??". Mwisho mama akawa kimya tu.

Na wewe acha majungu ndugu yangu, kama akili yaki haielewi maana ya promotion ilo ni kosa lako na mwalimu wako wa darasani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaakili sana we Jamaa umemjibu vizuri sana.hawa watu wanaachwa na teknolojia ya dunia hata hapa jf hawaoni matangazo siku hizi?
 
Vijana wa kitanzania, jishughulisheni na maisha yenu jamani, mnajihusisha na Diamond anawasaidia nini maishani?
Maisha yapo na entertainment lazima iwepo, let them talk but honestly am diamond fan ila amekosea sana kutoa wimbo afta seduce me, zilipendwa ni mwimbo mzuri kuliko huo wa kiba but ye ndo kafanya hiyo attention iwepo, ila ndo burudani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata Mimi nilikua nacheki kwenye YouTube Hotuba flani ya Tundu Lisu nimeshangaa kuona upnext wananiletea hiyo ngoma ya Diamond, nataka niangalie kama naweza ku-block wasiniletee upuuzi huo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je kiba kulipia Instagram na vevo ngoma yake iangaliwa Mara Nyingi hukuliona.....next time kaa fanya utafiti kwa pande zote mbili ila hapa tunakuona kama shabiki unaejificha kwny kichaka cha msema ukwl usiye na team.


Sent using Jamii Forums mobile app

(1) Sijaletewa video za kiba mahali ambapo hapahusiki vinginevyo ningecomment. Ninapoangalia We are the World ya mwaka 1985, sitegemi kuletewa video ya Bongoflava au Taarabu ya mwaka 2017; inapotokea, hivyo mara moja sitashangaa ila ikiwa ni trend, ni lazima nitashangaa.
(2)Kwa vile sasa nimeeleweshwa kuwa Zilipendwa imelipiwa hapo youtube kusudi iwe juu ya video nyingine ili ipate views nyingi basi sitashangaa tena nikilitewea wakati ninaangalia video nyingine.
 
Hilo la video kuwa na matangazo kule utube ni jambo la kawaida sana na ni kwa video nyingi tu.
hapana kalipia tangazo la wimbo wake,ukifungua videos lets say za marekani sababu location yako you tube wanajua uko TZ yatapop matangazo ya TZ kama airtel voda unatakiwa usubiri sekunde tano kama hutaki kuliangalia au ukaamua kuendela kucheki sasa yeye for the first time kalipia kabisa mwenyewe nilishangaa sana
 
Diamomd uswahili ndio unamgharim. Akiachana na mambo ya kiswahili na mameneja wa uswahilini, bado hana mpinzani.

Huo wimbo unaousema ni wimbo wa kawaida sana, sema yeye kaupa headline na jamaa katumia hyo kama kupata public sympathy, baada ya Alkiba kutoa wimbo na kesho yake WCB kutoa wao, Alkiba kapata huruma ya watu kwamba anabaniwa na WCB.

Angetumia akili wala huo wimbo wa Alkiba usingefika popote, ungekua ushajifia kifo cha asili, au usingepata media attention kiasi hicho.

Bado naamini Diamond akiacha uswahili atanedelea vizuri, vinginevyo atapotea.
we ndo mswahili asil manake majungu kwa mwenye nacho usichokuwa nacho sidhani ni kama uzungu
 
mbona alivyoweka tangazo la dr mwaka hamkushangaa msaniii ni lazma kubadilika kulingana na mazingira ili kuwa sawa anagalau na kilichopo
 
Back
Top Bottom