PSRS iendelee kuajiri au turudi kwa mashirika yaajiri tena kama ilivyokuwa awali?

PSRS iendelee kuajiri au turudi kwa mashirika yaajiri tena kama ilivyokuwa awali?

herikipaji

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2016
Posts
1,198
Reaction score
1,369
Leo mkuu wa nchi ambae ni Rais ameagiza na kuruhusu mashirika kuajiri watumishi wa umma moja kwa moja.

Hii ina maana sasa hayo mashirika mfano TRA, TANESCO na mengine yaliokuwa yatumia PSRS sasa yamepewa ruhusa kuajiri tena bila kupitia PSRS.

Maoni yangu hii haitokuwa vizuri.
Sababu mwanzoni kabla ya mfumo wa PSRS haya mashirika yalikuwa na fursa ya kuajiri lakini yalishindwa kuendesha mchakato wa ajira kwa taratibu yenye kufata misingi ya haki na maslahi ya taifa.

Kurekebisha ukaanzishwa mfumo wa sasa wa PSRS.

Mfumo huu wa kupitia PSRS wanaajiri upo kisheria, sasa hayo mashirika kuajiri tena ni kwa sheria ipi au wanafata maagizo ya mtu mmoja kama kawaida ya Tanzania?

Hivi nchi inaongozwa kwa kufata katiba na sheria au maagizo tu ya mtu?

Mfumo wa PSRS umekuwa msaada kwa wengi, wako ambao wamepata ajira bila kupitia njia za kujuana au kupeana rushwa, njia za ujanja ujanja, lakini wamepata na leo wako makazini.

Awali mashirika yalikuwa yanaajiri kukaonekana shirika moja linaweza kuwa na watu wa kabila fulani tu ngazi ya juu hadi chini, ubabaishaji, rushwa, kujuana na wengine wasio na mtu referee au wasotoa rushwa hata interview hawakuitwa kurekebisha hayo ukaekwa mfumo wa PSRS.

Sasa agizo la kuruhusu mashirika yaanze tena kuajiri anataka kuturudisha kule tulikotoka kwenye ubabaishaji, ajira za kujuana na mengine ya namna hiyo?

PSRS wana mapungufu hayo inatakiwa yafanyiwe kazi lakini si kurudisha ile corrupt system ya kuajiri kama anavyoagiza irudi.

Tumeona na hata dunia inafahamu hulka za Watanzania walio wengi, hawana uadilifu, majizi, wapenda rushwa hata hayo mashirika yamekua yanajiri pasipo kupitia PSRS mfano TANROAD lakini vijana wengi wameishia kulia kutokana na madudu yanayofanyika katika mchakato wa ajira kwa hayo mashirika.

Hayo mashirika yakiajiri hayatendi haki.
Yalikuwa yanaajiri hayakutenda haki, ukaletwa mfumo wa PSRS angalau umekuwa unaajiri kwa haki ukiachana na mapungufu madogo madogo yaliyopo.

Sasa kurudi kule Babylon kuajiri kupitia mashirika yaleyale tena inakuaje sasa yamebadilika?

Nini kimebadilika kwa hayo mashirika yalokua hayaajiri kwa haki na sasa yanaruhusiwa tena kuajiri?

Kama hilo agizo la rais likifanyika wengi watalia, wengi watakosa kupata hizo ajira wataishia kuajiriwa ndugu, wenye kutoa fedha kuhonga rushwa, ukabila.

Kimsingi bila kufahamu vema ni anaruhusu madudu yarudi tena mambo yakuwajaza watu uwanja wa taifa kupigania ajira ambazo washapewa wachache yatarudi tena, subirini muone.
 
Ila Kuna kitu naona watanzania wengi sio waelewa ndo maana hata mitihani tunafeli.

Nilivyomuelewa mm ni kwamba zile ajira za mda za haraka haraka..
Hizo ajira za haraka haraka ndio ajira za rushwa kwa 99% kwenye mashirika ya umma.
Hutasikia popote zikitangazwa, hakuna usaili, na watu utakuta wameajiriwa.

Kwanza ajira za haraka haraka zinapaswa kufutwa kabisa kama inawezekana, na kama zikiendelea inabidi ziwe chini ya PSRS
 
Ni kweli, alizungumzia ajira za muda mfupi. Na kweli haileti maana, ajira ya mwaka mmoja inachukua takribani miezi mpaka saba toka kutumwa maombi na watu kufanya saili na kutangazwa/kuitwa kazini.
Lakini itakuwa ni upenyo fulani ila wakija kuajiri za kuduma wale waliofanya za mda wapewe kipaumbele.

Nina hakika Kwa hili kwa vile hata uanagenzi na kujitolea kwa sasa kupata ni mpaka connection hali ni mbaya wasomi kibao.
 
Ila Kuna kitu naona watanzania wengi sio waelewa ndo maana hata mitihani tunafeli.

Nilivyomuelewa mm ni kwamba zile ajira za mda za haraka haraka..
Utumishi kweli wanatabia na kutumia mda mrefu sana ajira za mda mrefu hata hizo kwa mda mfupi.

Lakini nafikiri wana mazuri yao ambayo ni mengi kuliko mapungufu, hivyo wanatakiwa agizo hili liwe kuwataka warekebishe haya mapungufu walokua nayo sasa.

Maana hata hizo za mda mfupi kuajiri kwa kutumia mashirika utatumika mwanya ule ule wa ujanja ujanja.
 
Hizo ajira za haraka haraka ndio ajira za rushwa kwa 99% kwenye mashirika ya umma.
Hutasikia popote zikitangazwa, hakuna usaili, na watu utakuta wameajiriwa.

Kwanza ajira za haraka haraka zinapaswa kufutwa kabisa kama inawezekana, na kama zikiendelea inabidi ziwe chini ya PSRS
Asante sana ndugu kwa fikra hizi nzuri kwa maslahi ya taifa letu.

Nafikiri wahusika wako humu wazifanyie kazi.
 
Leo mkuu wa nchi ambae ni rais ameagiza na kuruhusu mashirika kuajiri watumishi wa uma moja kwa moja...
Nchi inarejea shimoni kwa speed ya 5G katika uongozi wa huyu mama

Mashirika yanapoendesha mchakato wa ajira haki na uwazi hakuna...kuna mashirika hayatangazi ajira na kuna mengine yakitangaza basi baada ya watu kuomba hawatoi mrejesho wa maombi
 
Nchi inarejea shimoni kwa speed ya 5G katika uongozi wa huyu mama

Mashirika yanapoendesha mchakato wa ajira haki na uwazi hakuna...kuna mashirika hayatangazi ajira na kuna mengine yakitangaza basi baada ya watu kuomba hawatoi mrejesho wa maombi
Nimefatilia mchakato wa TANROAD hawa walikua wanaendelea kuajiri wenyewe kipindi chote hiki, lakini hakuna uwazi kabisa, wanapeana tu hizo ajira na kuuza kwa watu wenye fedha.
 
Watoto wa walalahoi ndio msahau kupata kazi katika hizo taasisi. Utumishi sifahamu makando kando yao mengine ila kwenye suala la ajira wako fair sana.

Ni kupitia mfumo wao wa ajira nimeona vijana waliotokea familia za kawaida (akina sie watoto wa mama ntilie) wakipata kazi mashirika/vitengo nyeti Serikalini.

Rais Mama Samia Usijaribu kuua mende kwa nyundo, fikiria tena kuhusu kauli/maamuzi yako, elewa tatizo lilipo kisha tatua ila sio kwa kuondoa mfumo rasmi uliopo.

Kati ya Mashirika yaliyoongoza kwa vi Memo kabla ya mfumo wa ajira kuwepo ilikua ni TTCL na hapo TRA, ofisi nzima ilikua inaongozwa na familia.
 
Mimi waendelee tu, Ila tu nawaomba kitu kimoja kwao.

• Wawe time management, yaan watangaze kazi kwa wakati, kuita usaili mapema na baada ya Oral kuitwa kazini iwe ndani ya wiki 2 au 3.

• Nao waombe kibali Cha Ajira ili wapate watu wengi ambao itasaidia kufanyika kwa saili Kila Kanda.

Ni hayo yangu Ila ukweli PSRS wako vizuri, wanachapa kazi na waendelee kupewa hii dhamana.

Nawasihi sana wasijisahau kwenye kazi zao, mambo ya kusemwa vibaya na mkuu wa Nchi kama hivi leo sio Vizuri na inawashushia Ile heshima yao kama Taasisi inayoaminika, So watu wasiofuatilia harakati za utumishi basi watawaona mafedhuri wanatoa Ajira kwa kujuana/rushwa kumbe Wala siyo hvyo..

Sekretarieti ya Ajira
 
Watoto wa walalahoi ndio msahau kupata kazi katika hizo taasisi. Utumishi sifahamu makando kando yao mengine ila kwenye suala la ajira wako fair sana...
Hata mie nawafahamu wengi wamepata ajira watoto wa walalahoi kupitia PSRS.

Lakini kwa mashirik utakuta watu wamejazana humo kama mali ya ukoo vile, sasa ndio turudi huko kweli!
 
Back
Top Bottom