KERO PSSSF fanyeni malipo acheni urasimu

KERO PSSSF fanyeni malipo acheni urasimu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Rigidity

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2024
Posts
391
Reaction score
482
Habari ya muda huu wanajukwaa.

Nimelazimika kuandika hapa jukwaani kuhusu taasisi tajwa hapo juu. Tangia mwezi oktoba nilijaza fomu za kuomba fao. Nilijibiwa kama taarifa zimepokelewa na mwajiri na pia ofisi za PSSSF

Isitoshe nimewapigia simu wakasema watalipa mwezi September. Hawajalipwa bado. Mara wanasema mhasibu hajapeleka vocha mara subiri mwezi December.

Mzee Abdu Razak Badru simamia haki za watu. Waambie wahasibu wako waache urasimu.

Ninajaribu kujiuliza maswali yafuatayo mara baada ya kuwapigia simu hawa wasumbufu

1: Eti wanasema mhasibu alitoka ofisini akasahau kupeleka vocha benki. Je hiyo ni ofisi au ni duka la mtu? Akisahau leo kesho hapeleki?

2: Wanasema eti wanafanya malipo mwisho wa mwezi. Hapo ndio nimestaajabu. Mwisho wa mwezi kwani huo ni mshahara? Kwanini unakaa na taarifa za mtu kwa muda mrefu kisha ukimaliza unatoa visingizio visivyona mbele wala nyuma?

3: Au mnachukua hela za wateja mfanyie mizunguko yenu kisha ndio mnawaingizia. Mhasibu achunguzwe. Kunajambo hapo.

Ninachoweza kuwaambia PSSSF nikwamba LIPENI HELA ZA WATU KWANI NI NGUVU NA JASHO LA WATANZANIA WENZENU.

Nawatakia utekelezaji mwema.
 
Hii tabia ni KERO kwa kweli..... Kuna ndugu yangu amejaza fao la uzazi toka October lakini mpaka leo hakuna malipo.

Ukienda OFISI zao kuuliza wanasema mara anayetakiwa kulipa yuko likizo mpaka arudi
Sasa unajiuliza mtu akitoka kazi zote zinasimama?

Mbona kwenye makato huwa hakuna excuse kama hizo?

Hii taasisi inahitaji kuchunguzwa.
 
Hii tabia ni KERO kwa kweli..... Kuna ndugu yangu amejaza fao la uzazi toka October lakini mpaka leo hakuna malipo
Ukienda OFISI zao kuuliza wanasema mara anayetakiwa kulipa Yuko likizo mpaka arudi
Sasa unajiuliza mtu akitoka kazi zote zinasimama?
Mbona kwenye makato Huwa hakuna excuse kama hizo?
Hii taasisi inahitaji kuchunguzwa
Hawajawahi kuwa likizo kwenye malipo. Kuna urasimu wa kiwango cha lami
 
Ila huyo mkurugenzi wa mfuko ni tatizo. Tena ni jipu. Kuanzia yupo HESLB ufanisi wake ni mdogo sana.

Rushwa ilitawala pale Sasa sijajua kama hata huko PSSSF wanataka rushwa ama kitu gani.

Ila serikali imfuatilie huyo mhasibu wa mfuko nae ni tatizo.
 
Hao wamesema tu watu wajaze fomu online lakini nadhani bora tu kwenda kujaa kwenye ofisi zao au sijui wanataka mpaka wanaotaka hela zao waende na mabango hapo ofisini na waandishi wa habari!

Kila anapopewa ofisi huyo mzee urasimu hauishi. Labda ndio bingwa wa urasimu!
 
Hii tabia ni KERO kwa kweli..... Kuna ndugu yangu amejaza fao la uzazi toka October lakini mpaka leo hakuna malipo
Ukienda OFISI zao kuuliza wanasema mara anayetakiwa kulipa Yuko likizo mpaka arudi
Sasa unajiuliza mtu akitoka kazi zote zinasimama?
Mbona kwenye makato Huwa hakuna excuse kama hizo?
Hii taasisi inahitaji kuchunguzwa
Sasa ukiwakuta ofisini wanavyojifanya wapo bize. Kumbe usanii tu hamna uwajibikaji wa asilimia mia
 
Sasa ukiwakuta ofisini wanavyojifanya wapo bize. Kumbe usanii tu hamna uwajibikaji wa asilimia mia
Unaweza ukasema wana ubinadamu kumbe ni unyama tu.

Unakaaje na hela za mtu aliyekamilisha taratibu?

Kuidai serikali hela zako ni bora ukakope mtu unasikilizwa na kukopeshwa haraka.

Nawaona hao kama kausha damu tu.
 
Hao wamesema tu watu wajaze fomu online lakini nadhani bora tu kwenda kujaa kwenye ofisi zao
Au sijui wanataka mpaka wanaotaka hela zao waende na mabango hapo ofisini na waandishi wa habari
Kila anapopewa ofisi huyo mzee urasimu hauishi. Labda ndio bingwa wa urasimu
Halafu wanajifanya wameboresha huduma
 
Wakikaa kwenye PC wanasikilizatu muziki.

Utakuta staff mwenzake anaingia ofisini kwa kuruka foleni ya watu lakini ndani wanachojadili ni majungu, story za staff wengine, wakati mwingine utakuta mtu yupo busy na simu katoka mitandao ya kijamii.

Muda wa kwenda kula ni masaa mawili saa nne Hadi saa 6 mchana
 
Halafu wanajifanya wameboresha huduma

Hakuna kitu ni heri muda wa kufanya kazi ofisi za serikali upunguzwe uwe masaa 5, saw 2 asbh hd saw 7 ili wawe huru kufanya mambo yao binafsi kuliko kuzuga zuga tu ofisini

Sasa zipo kada zingine hata ofisi hawaendi kama maafisa kilimo na maendeleo ya jamii wa kata, kwenda kazini Hadi siku apende yeye kwenda
 
Utakuta staff mwenzake anaingia ofisini kwa kuruka foleni ya watu lakini ndani wanacho jadili ni majingu, story za staff wengine
Wakati mwingine utakuta mtu yupo busy na simu ktk mitandao ya kijamii
Muda wa kwenda kula ni masaa mawili saa nne Hadi saa 6 mchana
Halafu wapo watu wameweka hela zao hapo miaka tele lakini hawajaliwi wakifika ofisini
Nadhani watakua wanataka rushwa
 
Hii tabia ni KERO kwa kweli..... Kuna ndugu yangu amejaza fao la uzazi toka October lakini mpaka leo hakuna malipo
Ukienda OFISI zao kuuliza wanasema mara anayetakiwa kulipa Yuko likizo mpaka arudi
Sasa unajiuliza mtu akitoka kazi zote zinasimama?
Mbona kwenye makato Huwa hakuna excuse kama hizo?
Hii taasisi inahitaji kuchunguzwa
Wanaona wivu kuwapa watu hela zao. Hao niwachawi
 
Back
Top Bottom