Punguzo la PAYE kwa asilimia 1 ni dhihaka kwa wafanyakazi!

Punguzo la PAYE kwa asilimia 1 ni dhihaka kwa wafanyakazi!

Kodi ni kwa ajili ya wanyonge tu? raisi, makamu wa raisi, waziri mkuu, mawaziri, wabunge na wakuu wa Mikoa na wilaya hawakatwi payee! Hii ni haki? kweli inauma sana sana jamani.:frusty:

Si kweli kwamba wafanyakazi ambao kwa kiasi kikubwa mna elimu kwamba mnaumia kwa kodi la sivyo mngechukua hatua kali inaonekana mmesoma ila tatizo upeo wa kiakili nyie wenyewe na viongozi wa TUCT.
 
Kama kwa mwaka wanapunguza 1% kwhyo mpaka bajeti ya 2018/2019 ndio itafikia single digit 9% endelea kufanya kazi tu kupata nafuu ya (1900 x 4=7600)

tanzania hapafai kuishi. Unaongozwa na mandondocha yani ni full kutabika!
 
kama kweli wamepunguza asilimia 1 wafanyakazi kwa pamoja kuna haja ya kuitoa serikali hii madarakani kwa kuinyima kura ccm

Wafanyakazi wa tz kama mazezeta ndio maana viongozi na wanasiasa huwafanya watakavyo
 
Wafanyakazi wa tz kama mazezeta ndio maana viongozi na wanasiasa huwafanya watakavyo



Umewahi kuona au kusikia kodi wanazokatwa wafanyakazi kwa nchi zilizoendelea?
 
Lakini bado mnaendelea kuiweka ccm madarakani. Nina hakika ccm ikiondoka chama cha upinzani kikijipanga vizuri kuhusu mapato ya kodi na kuziba wizi wa watumishi TRA kwa kuifumua na kuisuka upya pia kuindioa kabisa misamaha ya kodi ya kijinga na kuongeza wigo wa kodi kwa kuhangaika na wakwepa kodi hali ya mapato itakuwa nzuri sana. Hii itapelekea PAYE kupungua sana. Shame on you CCM.


Unataka waingie chadema wanufaishe kabila lao?
 
Umewahi kuona au kusikia kodi wanazokatwa wafanyakazi kwa nchi zilizoendelea?

Umewahi kuona au kusikia jinsi hizo kodi wanazokatwa wafanyakazi zinavyofanyiwa kazi kwa manufaa ya nchi zao?
 
hatari sana. kwa kifupi, mwenye mşhahara wa tshs 700,000 anamzidi kwa mbali sana mwenye mshahara wa tshs 750,000 kwa take home, kisa kodi!!!

Ndio maana yake mkuu, atakuwa group 4. Hivyo atalipa kodi ndogo.
 
...Kweli mkuu tuache
kulalamika. Hebu ona Ridhiwani alivotoka fasta baada ya kuanza
"biashara" mzee alipoingia ikulu. Angalia Chenge alivotoka baada ya
kutununulia RADA ya kutuangalizia ndege mbinguni. Na sasa kuna ESCROW -
hapo jamaa wasipotoka tutashangaa!

mawazo ya kimasikini
 
Mkuu
Naona unaleta siasa za kupinga kila kitu kilicho tofauti na Chama chako

Sie wengine sio wanachama wa chama chochote na tulimpigia kura Raisi Wetu , kwa maana alituahidi kupata maisha bora kwa kila Mtanzania

Nauliza ? Je ni kweli kumpunguzia mfanyakazia kodi ya sh 1900 kunamletea nafuu yoyote ili hali ,mfumuko wa bei haujadhibitiwa , Kodi za simu zimeongezeka.

Huyu huyu mfanyakazi atapoteza asilimia 18 ya mapato yake yote kwenye kila anachonunua kwa kupitia VAT

Kwa hiyo mtu mwenye Gloss ya 3,023,000/= anakatwa kodi ya 704,010/= sawa na 24% ya msharaha wote ,juu ya hapo 18% ya mapato ya huyu mtu analipa kodi kupitia VAT

kwa hiyo jumla ya mapato yanapokwa na serikali kwa mgongo wa kodi ni 42% ya mashahara wote


Mfanya kazi huyo analipa paye zaidi ya 8,400,000 , niambieni ni mfanayabiashara gania anayelipa kodi kama hii ?

Waziri amekiri mwenyewe kwamba PAYE na VAT ndio vinachagia 80% ya mapato yote , inamaaan mfanyakazia nchi hii ndie anayenyonwywa kugharimia serikali inayoponda mali ya Tanzania

Mkuu umesomeka vizuri tu.

Na mimi labda hujasoma post yangu ya mwanzo.

Hata mimi nimesema kuwa serikali haikumsaidia chochote mwananchi wa kawaida ktk hili.
Lkn kumbuka kwa serikali yenyewe hizi ni pesa nyingi mno.
Na hatuna budi kwenda hivo hivo tu!

Unless serikali iongeze kodi kwa hayo makampuni makubwa sisi wanyonge tutaendelea kuumia tu!

Hakuna njia nyingine.
 
Heshima mbele mkuu
Tupo pamoja

Mie nadhani serikali isingepunguza hii paye baadala yake ,hilo punguzo ambalo kwa upande wa serikali ni pesa nyingi kwa kuwa zinakuswanywa kutoka kwa wengi, hizi zingiweza kusaidia kupunguza vifo vya akina Mama na watoto wanopoteza maisha wakati wa kujifungua .Mbaya zaid hawa wakina mama wanapokufa wanaacha pengo kubwa sana nyuma yao

Hili punguzo alikufikiriwa vizuri ,limekaa kisiasa zaidi
 
tanzania hapafai kuishi. Unaongozwa na mandondocha yani ni full kutabika!

Kenyatta Sr aliwahi kumuambia Nyerere kwamba anaongoza MAITI! ni kweli kwamba watanzania wengi wana akili kama za maiti ndiyo maana kila mwaka huwachagua CCM ili wamalizie kazi ya kuwazika!
 
Umewahi kuona au kusikia kodi wanazokatwa wafanyakazi kwa nchi zilizoendelea?

hivi wewe pimbi kwanini unapenda kutuvurugia mijadala na kututafutia ban? kwani tanzania ni NCHI ILIYOENDELEA? na unajua wafanyakazi ktk nchi zilizoendelea wanalipwa mshahara sh ngapi? kwanini unafananisha vitu ambavyo havifanani?
 
Mkuu umesomeka vizuri tu.

Na mimi labda hujasoma post yangu ya mwanzo.

Hata mimi nimesema kuwa serikali haikumsaidia chochote mwananchi wa kawaida ktk hili.
Lkn kumbuka kwa serikali yenyewe hizi ni pesa nyingi mno.
Na hatuna budi kwenda hivo hivo tu!

Unless serikali iongeze kodi kwa hayo makampuni makubwa sisi wanyonge tutaendelea kuumia tu!

Hakuna njia nyingine.

sasa kwanini hawafanyi hivyo? wewe unataka tuendelee kuvumilia mpaka lini? kwanini humuambii haya katibu wako na kila siku unakutana naye hapo lumumba? ungependa watanzania waendelee kuteseka hadi Yesu atakaporudi?
 
Kenyatta Sr aliwahi kumuambia Nyerere kwamba anaongoza MAITI! ni kweli kwamba watanzania wengi wana akili kama za maiti ndiyo maana kila mwaka huwachagua CCM ili wamalizie kazi ya kuwazika!
Kwann hutumii kichwa kufikiri? Kwann umechangia ukurasa mzima peke yako?
 
Kwann hutumii kichwa kufikiri? Kwann umechangia ukurasa mzima peke yako?

usitishwe na kiasi cha michango yangu bali unapaswa kuzingatia theme ya yaliyomo...hilo ndilo suala la msingi. serikali yako imeonyesha udhaifu mkubwa sana wa kiuongozi.
 
Kweli hii ni dharau ina maana mkuu wa kaya alikuwa anatafuta umaarufu wa kupigiwa makofi ama wachumi wake hawakumshauri vizuri . Kama mshahara wa mfanyakazi ni 80000 na PAYE itakuawa 1200 kwa 15% na kama atakuwa amepunguza 1% hivyo atakuwa amepunguza tshs 12. Sasa swali linakuja kama angeogeza mshahara kweli angeongeza hicho kiasi cha pesa kwenye mshahara?
 
Kweli hii ni dharau ina maana mkuu wa kaya alikuwa anatafuta umaarufu wa kupigiwa makofi ama wachumi wake hawakumshauri vizuri . Kama mshahara wa mfanyakazi ni 80000 na PAYE itakuawa 1200 kwa 15% na kama atakuwa amepunguza 1% hivyo atakuwa amepunguza tshs 12. Sasa swali linakuja kama angeogeza mshahara kweli angeongeza hicho kiasi cha pesa kwenye mshahara?

mkuu, uongozi wa nchi hii ni majanga makubwa sana. ubovu wa uongozi unaifanya safari ya kuelekea 2015 ionekane kama safari ngumu ya Musa kuwatoa watu wake utumwani kutoka Misri kuelekea Kaanani--ni safari ndefu na yenye misukosuko kibao.
 
Back
Top Bottom