Putin asaidiwe kuikomboa dunia dhidi ya nchi chache za Magharibi

Putin asaidiwe kuikomboa dunia dhidi ya nchi chache za Magharibi

Hakuna ubishi kuwa nchi za Magharibi zimejengwa kwa rasilimali kutoka mataifa mengine na watumwa. Mahitaji yaliyosababisha nchi za magharibi kutafuta makoloni na watumwa hayajakwisha hata kidogo, ile kiu ya kuzitawala nchi nyingine bado wanayo, na iko siku moja (sio mbali) watatumia NATO kutupora kwa nguvu rasilimali zetu ikiwemo ardhi ya kilimo na makazi.

Waafrika na nchi zote zilizowahi kutawaliwa na magharibi hatuwezi kubaki neutral kwenye hili kwa kisingizio cha aina yoyote ile. Kukaa kimya ni sawa na kumuunga mkono mtesi wetu ambae baada ya Urusi kuanguka atatuvamia tena.

Kila mtu mwenye akili anakumbuka namna misaada kutoka nchi za Magharibi kwenda nchi maskini na Afrika ilivyopungua ghafla baada ya USSR (Soviet) ilivyoanguka na kupelekea kwisha kwa vita baridi.

Leo hii baada ya kuimarika kwa Urusi na China kiuchumi na kijeshi magharibi wanarudi tena kwetu na misaada mbuzi ili tuwaunge mkono dhidi ya Urusi na China.

Hapa ndipo akina Nyerere, Nkrumah, Mugabe, Gaddafi, nk tunapo wamis.

Sikiliza wanaume waliobaki wanavyowaza kishujaa.


Walipora nusu ya robo tu yaani walipora asilimia 10 tu ya mali kwa maendeleo yote uyaonayo ulaya, but still 90 ya mali bado ipo nyingi tu afrika na haijatumika, ni wajibu wetu tu sisi waafrika tuzitumie tuwe na maendeleo kuwazidi wao.
Mfano mali zilizopo wilaya moja tu nchini unaweza ukalipa deni la taifa na kufanya maendeleo makubwa, tatizo utayari ndo haupo.
 
Viongoz wa Africa ni wezi
Viongozi Africa ambao ni wezi wameingizwa madarakani na wanalindwa na Magharibi. Wezi wote wanatawala milele bila kukemewa na nchi za Magharibi kuhusu demokrasia. Viongozi ambao sio wezi hawadumu kwenye uongozi, watakufa au kulazimika kuondoka hata kabla ya muda wao kumalizika
 
Wabongo kwa kushabikia pande zinazipingana na kubishana ndiyo kipaji chao. Sijui hii tabia ilitokana na nini. Kula ugali kwa wingi? Tanzania nzima sasa hivi kuna vita kali kati ya vijana wa Urusi VS vijana wa nchi za Magharibi. Hata ugumu wa maisha watu wamesahau. Nchi inakwenda kombo lakini vijana wake wako busy kubishana Urusi vs Ukraine.
Kwa maono ya karibu utaona uhusiki lakini kiuhalisia vita inatugusa hata sisi Afrika
 
Shida ya nyinyi wafrika mnafikiri bado mnaishi kwenye zama za mawe na kuoneana huruma.
Kama wewe hauna uwezo wa kuchimba unafikiri nani akuchimbie na mgawane faida sawa? Ukumbuke Wazungu na Waarabu walitutawala unafikiri kwasasa ndiyo wanatupenda sana?
1. Mejaza viongozi wenye tamaa za mali na kujiangalia wenyewe
2. Mfumo wenu wa elimu mbovu unafuata mtaala wa kikoloni
3. Sheria na katiba zenu za mwaka 1960 ni mbovu na zimepitwa na wakati
4. Wananchi wenyewe hawajielewi wanawaona viongozi kama miungu watu. Baadala ya kuchagua viongozi bora na wenye kulikomboa taifa wao wanachagua chama.
Usilolijua siku zote dunia haipo sawa 100%.
Kasome
A. Kingdom na Chiefdom
Hapa kuna expansion of Kingdom. Kingdom moja inavamia weak kingdom, inaua na kunyang'anya ardhi. Hapa ni kabla ya ukoloni na hawa ni wafrika. Unategemea mtu aliyeleta dini na slave trade akuonee huruma
B. Capitalism na pamoja na Phase zake
C. Neo-Colonialism
Kaka hao viongozi wazuri wasio wezi kwa Mali za mataifa Yao tulikuwa nao kama vile Nyerere, Nkrumah, Lumumba, NEto, Mugabe, Gaddafi, Assad, Saddam, Haile Ras, nk lakini waliuawa na kuangamizwa. Nyerere alifungiwa na IMF, WB na Magharibi hadi ikabidi ang'atuke mwenyewe. Kaka hayuko salama hadi hapo tutakapo rejea kwenye dini zetu za asili. Hizi dini tulizonazo Sasa ni chanzo kikubwa Cha mateso yetu.
 
Kumbe ndiyo maana mkuu mpya wa JWTZ akachaguliwa? Sasa drones na Himars na Iskander tutazitoa wapi? Uturuki? Maana nasikia nchi nzima kuna mizinga 7 ya zamani na vifaru 14 tu nayo mikweche.
[emoji23][emoji23][emoji23] mkuu kweli?
 
Hakuna ubishi kuwa nchi za Magharibi zimejengwa kwa rasilimali kutoka mataifa mengine na watumwa. Mahitaji yaliyosababisha nchi za magharibi kutafuta makoloni na watumwa hayajakwisha hata kidogo, ile kiu ya kuzitawala nchi nyingine bado wanayo, na iko siku moja (sio mbali) watatumia NATO kutupora kwa nguvu rasilimali zetu ikiwemo ardhi ya kilimo na makazi.

Waafrika na nchi zote zilizowahi kutawaliwa na magharibi hatuwezi kubaki neutral kwenye hili kwa kisingizio cha aina yoyote ile. Kukaa kimya ni sawa na kumuunga mkono mtesi wetu ambae baada ya Urusi kuanguka atatuvamia tena.

Kila mtu mwenye akili anakumbuka namna misaada kutoka nchi za Magharibi kwenda nchi maskini na Afrika ilivyopungua ghafla baada ya USSR (Soviet) ilivyoanguka na kupelekea kwisha kwa vita baridi.

Leo hii baada ya kuimarika kwa Urusi na China kiuchumi na kijeshi magharibi wanarudi tena kwetu na misaada mbuzi ili tuwaunge mkono dhidi ya Urusi na China.

Hapa ndipo akina Nyerere, Nkrumah, Mugabe, Gaddafi, nk tunapo wamis.

Sikiliza wanaume waliobaki wanavyowaza kishujaa.

Tayari KAZI imeshaanza wameshaanza kujiuzulu

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom