Putin asema Urusi ipo tayari kwa mazungumzo kuhusu Ukraine

Putin asema Urusi ipo tayari kwa mazungumzo kuhusu Ukraine

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
2,652
Reaction score
4,593
Putin pia amesema kuwa Urusi iko tayari kwa mazungumzo na maridhiano kuhusu Ukraine, lakini inahitaji upande wa pili uwe tayari pia. Aidha, alionyesha utayari wa kukutana "wakati wowote" na Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump, ambaye ameahidi kufanikisha mkataba wa amani wa Ukraine mara baada ya kuingia madarakani Januari.

Rais Putin pia, amekiri kasoro za vyombo vya usalama vya nchi yake kufuatia mauaji ya Jenerali Igor Kirillov jijini Moscow, yaliyodaiwa kufanywa na Ukraine.

Akizungumza katika mkutano wake wa mwisho wa mwaka, Putin amesisitiza haja ya kuboresha mfumo wa ulinzi ili kuepuka makosa makubwa kama hayo.

Putin amebainisha kuwa vikosi vya Urusi vinashikilia udhibiti mkubwa katika vita lakini hajui lini Urusi itarudisha eneo la Kursk lililovamiwa na Ukraine.

Kremlin hivi karibuni iliunga mkono ukosoaji wa Trump kwa Biden kuhusu kuiruhusu Kyiv kutumia makombora ya Marekani kushambulia Urusi, hatua inayoongeza mzozo wa karibu miaka mitatu.

Chanzo: DW Kiswahili
 
Tunataka amani na Dunia tulivu tumechoka na vita
 
Syria imeshamalizwa na marekani na jumuiya ya ulaya. Sasa bomba la gesi kubwa kutoka QATAR kwenda WEST EUROPE kujengwa kupitia syria. Ndo maana ULAYA na MAREKANI lazima wailinde ISRAEL maana wayahudi ni kiungo mchezeshaji mzuri kwao. Long live the JEWS.

GESI YA URUSI ILIKUWA INAMPA KIBURI SASA ITAKOSA SOKO. PUTIN AWE MPOLE TUUUU
 
Putin pia amesema kuwa Urusi iko tayari kwa mazungumzo na maridhiano kuhusu Ukraine, lakini inahitaji upande wa pili uwe tayari pia. Aidha, alionyesha utayari wa kukutana "wakati wowote" na Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump, ambaye ameahidi kufanikisha mkataba wa amani wa Ukraine mara baada ya kuingia madarakani Januari.

Rais Putin pia, amekiri kasoro za vyombo vya usalama vya nchi yake kufuatia mauaji ya Jenerali Igor Kirillov jijini Moscow, yaliyodaiwa kufanywa na Ukraine.

Akizungumza katika mkutano wake wa mwisho wa mwaka, Putin amesisitiza haja ya kuboresha mfumo wa ulinzi ili kuepuka makosa makubwa kama hayo.

Putin amebainisha kuwa vikosi vya Urusi vinashikilia udhibiti mkubwa katika vita lakini hajui lini Urusi itarudisha eneo la Kursk lililovamiwa na Ukraine.

Kremlin hivi karibuni iliunga mkono ukosoaji wa Trump kwa Biden kuhusu kuiruhusu Kyiv kutumia makombora ya Marekani kushambulia Urusi, hatua inayoongeza mzozo wa karibu miaka mitatu.

Chanzo: DW Kiswahili
Na ndio maana warusi washaona imekula kwao mazima apo gesi, itakayotoka Qatar 🇶🇦 . Italeta matokeo chanya sana kwa wazungu na kwa waqatari wenyewe na ndio maaana Urusi kashaona vita havina maana
 
Vita ni nzuri , inaleta heshima. Ukiona mbabe anaomba suluhu, jua yuko hoi.

Hapa Ukraine kama anapumzi anapaswa kuitumia vizuri ili aweze kumaliza raund 12. Ushindi wa mezani huwa haukai muda mrefu.
 
Back
Top Bottom