Puuzeni taarifa ya Nipashe, hakuna uchotaji fedha BoT

Ndugu yetu Dr Mwigulu Nchemba, kama hakuna cash outflows BOT, je hiz pesa za kuendesha timu unazipata wapi ndugu yetu?
 
Kuna alikojibu? Umeangalia lile kanusho lake jingine hili hapa chini?

 
Ninatarajia Hao Nipashe wakanushe habari yao ya uongo baada ya wizara kuwaonesha ukweli. Tofauti na hapo ni kujilisha upepo.
 
Anatuona wajinga.

Ana uzi wake ule ameuandika Ijumaa halafu akaingia mitini.

Uzi wake aliukimbia na member mwingine alikuja na ushahidi wa kile ulichosema tukipuuze ila bado ukaingia mitini kwenye thread yako na yake.

Leo ameibuka tena na hizi story tena.

Mimi namuachia swali tu moja hivi ile report aliomba Samia siku anasomewa ripoti ya kwanza ya CAG tangu Magufuli afariki .

Samia aliomba taarifa za miamala iliyofanyika BoT kuanzia January 2021 hadi March 2021 tena kwa msisitizo maana yake kulikuwa na kitu kisicho cha kawaida na alikuwa na "tip"

Hiyo report tunaipata wapi au ndio ilipotelea hewani kama utani wa Nape?

Cc OKW BOBAN SUNZU
 
Acha maneno matupu ya siasa. Nchi ipo kwenye crisis kubwa ya kifedha na hakuna lolote la msingi unalofanya kulisaidia Taifa.

Kunq shida kubwa sana kwenye uchumi wetu hadi kusababisha uhaba mkubwa wa fedha za kigeni hasa dola

Hili limesababisha shida kubwa sana kwenye uchumi wetu na badala mje na njia mbadala za maana katika kufanya maamuzi sahihi mmekalia siasa na kujaza matumbo yetu tu!
 
Lakini tushukuru tu hata haya mambo tunasikia..
Wanaweza wakaamua kuchota, vyombo vya habari vyote vikapigwa spanner.

Na hakuna anayejali.
 
Niffah.....big up sana ukweli lazima usemwe...kunywa togwa chupa moja kwa mama mkude nitakuja kulipa maana umeupiga mwingi.
 
HHu
Njaa itakuuwa brother yani hauna tofauti na Lukas Mwashambwa, acheni kujipendekeza kwa watawala
 
You know, from a psychological point of view. Kichwa cha habari kimebeba uhalisia mzima wa kinachoendelea.

The fact kwamba kichwa kimetumia neno "Puuzeni" au kwa kiingereza "Ignore" neno ambalo mara zote hutumika subjectively. Badala ya kukanusha objectively ni kitu cha kustaajabisha kwa wenye akili na wadadisi makini wa mambo. Sababu siku zote binadamu subconsciously hupuuzia kitu anachojua ni kweli.

Wenye akili wamenielewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…