Pre GE2025 Pwani: Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura kufanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 13 hadi 19 Februari, 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji Rufaa (Mstaafu) Mbarouk Salim Mbarouk amefungua mkutano wa wadau mkoani Pwani leo Februari 01, 2025 ambapo ametangaza ratiba ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye mkoa huo ambao utafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 13 hadi 19 Februari, 2025.

Uboreshaji huo utafanyika sambamba na Mkoa wa Tanga kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri za Miji ya Handeni na Korogwe na Halmashauri za Wilaya ya Kilindi, Lushoto na Muheza.

Soma,Pia: Lindi: Viongozi, Wananchi wajiandikisha daftari la mpiga kura, wahamasisha wananchi kujitokeza

 
Naomba kuuliza wakuu kuijiandikisha kupata kitambulosho Cha kura mwisho lini maana Kwa huku kibaha sioni waandikishaji au ndio habari imeisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…