Q Chillah anahitaji msaada gani?

Q Chillah anahitaji msaada gani?

Q-Chillah bado ana nafasi kubwa kimuziki. Inabidi asome soko linataka nini kwasasa na aendane nalo.
Pia ashirikishe vijana wanaotamba kwasasa kama Asley, Baraka Da Prince, Dogo Janja n.k.
Ila asiwashirikishe Vijana wa WCB. Hao wameishatengwa na Media hawatomfikisha popote.
Ushauri wako haumtendei haki jamaa.Yaan asiwashirikishe DABRIYUSIBII?
 
Huyu mpuuzi hajui kama kuna mamia kwa makumi elfu ya watumishi wameachishwa kazi kwa vyeti feki...

Na hakuna walipo lialia...
 
Unajuwa tatizo lake? kwanza hataki kuacha mziki anachotafuta huruma afanye mziki. baya zaidi anataka afanikiwe bila kufanya kazi kwa bidii kidogo anadhani kafika. muziki ni kama league unamaliza mechi unawaza kushinda tena. Muziki sio sauti tu ni nidhamu na hard work pia good management yeye ni kuwa na nidhamu ya hali ya juu na kubwa zaidi aache kuimba kizungu katika muziki wake maana soko unataka la ndani kizungu hakina nafasi.

Mkuu nakubaliana na wewe kitu kimoja jamaa kinachomfelisha ni NIDHAMU hana...namaanisha kuanzia kwenye kufanya show mpaka kwa management zake zilizomsimamia...
Ni kweli Chilla ana kipaji..lakini kipaji bila nidhamu na hard working kazi bure...

Diamond alipofika pale mpaka leo ana nidhamu na kazi yake na management yake yote..Ukimsikliza vizuri maneno yake ni kama anataka attention ya Watanzania.
 
ndio mkuu maisha yamemfua
Ngoma yake SIFAI.....ni classic mpaka leo..na haijawahi chuja.

Hawa wasanii wa bongo nafkiri wengi vizizi..

Kipaji kinapoteaje kirahisi namna hii.

Waache ushirikina.
 
Q-Chillah, T.I.D ni wasanii wakali sana ila wamekosa nidhamu tu, hata ukiwa na management ila ukakosa nidhamu kufanikiwa itakuwa ngumu sana, huwezi niambia Ali na Diamond ni wakali kuliko Chillah and T.I.D? ila utofauti uliopo kati yao ni nidhamu tu. Hakuna mtu mwenye pesa atawekeza pesa zake na muda wake kwa mtu ambaye hana nidhamu. NIDHAMU NDIO ILIOWAANGUSHA WASANII HAWA
Mia jamaa.
 
Namsikiliza hapa,naona ni upuuzi tu..hawa wasanii wanafikiri wao ndo wanashida tu hapa tanzania..mwanaume analialia tu kama mtoto wa kike..life is not simple,na hii ni kwa wote
amechezea sana pesa huyo "" so acha maisha ya muadhibu kidogo Ili awe na adabu ""
 
Unajuwa tatizo lake? kwanza hataki kuacha mziki anachotafuta huruma afanye mziki. baya zaidi anataka afanikiwe bila kufanya kazi kwa bidii kidogo anadhani kafika. muziki ni kama league unamaliza mechi unawaza kushinda tena. Muziki sio sauti tu ni nidhamu na hard work pia good management yeye ni kuwa na nidhamu ya hali ya juu na kubwa zaidi aache kuimba kizungu katika muziki wake maana soko unataka la ndani kizungu hakina nafasi.
q chief na Tid Hawa Jamaa wote wanajua kuimba lakini tatizo kubwa ambalo wanalo ni life skills " hawana" yaani wanajikuta wana vimba wanayale maisha ya wahuni wa kizamani ..kwamba mimi ndio mtoto wa mjini utanieleza Nini " ? so tabia yao hiyo imepelekea kugombana mnooo na wadau wenye mziki ambao ndio wameshikilia soko la mziki "" so hawawezi kupata nafasi ya kutamba kwa sbabu waliogombana nao ndio wale wale ambao wameshikilia soko la muziki wenyew
 
Hiyo ni laaana ya QJs muhonda ...hakuna asiyejua kuwa QJS alimtoa katika Mazingira gani Q.chief ....lakini alichokuja kumlipa ni mateke " so waliosema kuwa karma is a bitch Hawa kukosea ...
apambane tu na hali Yake ''""
 
Jamaa alikosea maisha tuu
Watu kibao hawasikiki kimziki lakin maisha yanaenda wala wake zao hawaja kimbia.
Ukiona mwanamke anakimbia jua akiona mchizi hana hata mipango amebaki kulalamika tu
hahaha sasa huyo analalamika kukimbiwa na mwanamke wakati yeye mwenyew Malaya...khaaa
 
Huyu si ndiyo alimtungia wimbo baba yake mzazi kuwa anamfuatafuata baada ya kuona yeye AMEKUWA TAJIRI!!?
hahaaa.."" katika maisha hakuna kitu ambacho unapaswa kukiogopa kama uhai wa umri mrefu....maana unaweza ukamcheka mtu kwa kufikwa na jambo Fulani...kumbe na wewe " muda unakusubiri ili ukifika wakati muafaka na wewe ukutwe na yako " aiseee maisha haya...sasa hapo nadhani anatamani kufuta yale mashairi aisee...
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] hakuna kumsaidia bana akacheze tatu mzuka asituzingue. Au asimame barabarani aimbe...am sure hatakosa wakumchangia mia mia
Kwa kweli akisimama barabarani na kuimba mimi mwenyewe nitakuwa mchangiaji wake
 
Hii kiki ya leo clouds nimeiheshimu. Mtu anakuja kutangaza kuacha mziki, anabembelezwa, anakubali, kisha kwa coincidence tu eti alikuja na ngoma mpya, na mentor/manager wake anasema tayari wana mipango mingi.
Sasa hapo alikuja kutangaza kuacha mziki kweli?
Hahaha Kiki ya kishamba kweli hii
 
Back
Top Bottom