QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

daa saa sita lege?? kama vile tunasubiria mwaka mpya
ok poa sio mbaya
Mkuu hapo ni kweli tupu maana nje ya hapo nitakuwa naongopa .kuna shughuli namalizia hapa ndio niweke mwendelezo so haina shida hata asubuhi utaikuta mkuu utaisoma
 
Mkuu hapo ni kweli tupu maana nje ya hapo nitakuwa naongopa .kuna shughuli namalizia hapa ndio niweke mwendelezo so haina shida hata asubuhi utaikuta mkuu utaisoma
Mimi siondoki hapa mpaka nionane na Monica. You know what am sayn.,!
 
Mkuu hapo ni kweli tupu maana nje ya hapo nitakuwa naongopa .kuna shughuli namalizia hapa ndio niweke mwendelezo so haina shida hata asubuhi utaikuta mkuu utaisoma
Mkuu LEGE tumekesha kwa ajili yako ..........aminia wewe ndio main character.....
 
LEGE mkuu wangu saa sita na dk12 niko hapa nakusubiri mkuu jembe
 
LEGE mkuu uko kwenye comp yako?fanya mambo nakusubiria sana
 
Saa sita na .....nusu......usiku mkuuu LEGE.it is high time ........mkuuuu
 
SEHEMU YA 31



“Its just a joke Austin” akasema Job
huku akicheka
“Job nadhani tumeongea mengi na
ninahitaji kuondoka kwani natakiwa
kumuhoji Dr Marcelo usiku huu.Kuna
mambo ambayo nahitaji kuyafahamu toka
kwake.Kabla sijaondoka kuna jambo
nataka nikuombe”
“ Jambo gani Austin?
“ Kwa hali ya mambo inavyokwenda
nahitaji kuhamisha makazi yangu na vile
vile natakiwa kumlinda pia Marcelo na
Monica.Pale mahala ninapoishi kwa sasa
tayari pamekwisha julikana kwa kuwa
katika nyumba hii hakuna mtu yeyote
anayeishi unaonaje endapo nitaweka
makazi ya muda humu mimi na Marcelo?
Hii ni sehemu salama na inaweza kunifaa
sana”
“Hakuna tatizo lolote katika jambo
hili Austin.Hata mimi nilikuwa nafikiria
jambo kama hilo Karibu tuishi sote hapa.Ni
nyumba kubwa ina vyumba vya kutosha
na usalama ni mkubwa.Hata hivyo kuna
jambo nataka ulifahamu” akanyamaza
kidogo na kusema
“ Sintarejea tena katika maisha yangu
ya uwazimu.Nimechoka kuishi maisha
yale.Nimeteseka sana Austin na
ninashukuru kwa ujio wako ambao
umenipa nguvu ya kuweza kuweka nukta
katika maisha yale magumu.Sikuwahi
kufikiri eti mtu kama mimi siku moja
nitaweza kuokota chakula majalalani,laini
imenilazimu kufikia hali hiyo ili
kuwakimbia
wanaonitafuta
waniue.Mwanzoni hawakuamini na
walikuwa nawaona wakinifuata na
kunichunguza ili wapate uhakika kweli
nimekuwa kichaa .Walinifuatilia kwa
miaka miwili ndipo walipokata tamaa
wakiamini kuwa kweli nimekuwa
kichaa.Uchungu nilio nao siwezi kuuelezea
Austin” Job akasema kwa hisia kali huku
machozi yakimtoka
“It’s ok brother,they‘ll all pay”
akasema Austin
“Sure they must pay.Kikubwa
ninachokitaka kwa sana ni kufahamu aliko
mwanangu kwani mateso yote haya
ninayavumilia kwa ajili yake.”
“Nakuhakikishia Job kati kati ya
sinema hii utafahamu alipo mwanao”
akasema Austin na wote wakacheka
“By the way,umewezaje kujenga
nyumba kubwa namna hii Job? Umepata
wapi pesa? Akauliza Austin.Job
akatabasamu na kusema
“Niliwahi kushiriki katika operesheni
moja huko Darfur kumtafuta mtu aliyeitwa
Hussein Hafidh Abdullah.Huyu ni kiongozi
wa ukoo mmoja na alikuwa anatafutwa
kwa kuchochea watu wa ukoo wake
kuvamia na kuwachinja kikatili watu wa
ukoo mwingine.Hussen alikuwa ni mtu
tajiri sana na ilituchukua muda kufahamu
maficho yake.Tulivamia nyumba yake na
yakatokea mapambano makali baina yetu
na walinzi wake,kati kati ya mapambano
hayo
Hussein
akafanikiwa
kutoroka.Tulipoipekua nyumba yake
tulikuta kuna chumba kimejazwa fedha
.Hatukuacha hata senti moja.Tulikuwa
watu kumi na tano,tukagawana fedha zote
na ndizo ambazo nilizitumia kujenga
jumba hili kwa siri bila ya mke wangu
kujua.Amarachi
ndiye
aliyekuwa
akisimamia ujenzi wa jumba hili wakati
nikiwa Darful hadi lilipokamilika kwa hiyo
hakuna mtu wangu yeyote wa karibu
anayefahamu kuwa jumba hili ni langu
zaidi ya Amarachi.Hii ni siri yako Austin
hatakiwi mtu mwingine kufahamu kwani
tulichokifanya haikuwa sahihi” akasema
Job na wote wakacheka.Job akamtembeza
Austin sehemu mbali mbali za jumba lile
kisha wakaagana
“Usiku wa leo nitakuwa na kazi moja
tu ya kufanya usafi humu ndani na kuweka
mazingira safi kabla hamjahamia humu”
akasema Job ,Austin akaondoka
 
Mkuu LEGE saa sita usiku ndio inayoyoma hatutaki upate ban chonde chonde mkuu dahhhh njooo tu upumzike
 
SEHEMU YA 32



alipotoka kuonana na Austin,Boaz
alimrejesha Maria hotelini kisha
akakodisha gari la hotelini hapo na
kuondoka.Usiku huu alikuwa na miadi ya
kuonana na aliyekuwa waziri mkuu.
“Austin amepewa kazi gani na rais?
Amekataa kabisa kuniweka wazi ni kazi ipi
anaifanya .Ujio wa Austin Tanzania
unaweza kuwa na uhusiano na hiki
alichokifanya rais Ernest? Nimefikiria sana
kuhusu jambo hili kwani baada tu ya
Austin kuja Tanzania ndipo rais
alipobadilika ghafla.Sina hakika sana
kuhusu jambo hilo lakini linatakiwa
lifanyiwe uchunguzi .Natakiwa kufahamu
ni kazi gani ambayo Austin anaifanya hapa
Tanzania.Kuna mtu mmoja tu ambaye
ninaamini anaweza kunisaidia kupata
jibu.Wilson Mukasha.Huyu ni mtu wa
karibu mno na rais na nina uhakika lazima
atakuwa anafahamu kazi ambayo Austin
anaifanya hapa Tanzania.Nitaongea naye
baada ya kuonana na waziri mkuu”
akawaza Boaz akiwa njiani kuelekea katika
makazi ya waziri mkuu aliyevuliwa
madaraka
“Bado suala la Marcelo linaniumiza
kichwa changu mno.Amejificha wapi?
Anashirikiana na akina nani? hii ni vita
nyingine imeanzishwa ambayo lazima
niipigane ili kukipata kitabu pamoja na
Austin.Kitabu kile ni muhimu mno na
endapo hatutakipata mimi na wenzangu
tutakuwa katika hatari kubwa.Kwa
vyovyote
vile
lazima
kitabu
kipatikane.Kwa nini lakini Dr Richard
ametufanyia hivi? Kwa nini ametusaliti
kiasi hiki? Nilimuamini mno na hakuna
aliyetegemea kama siku moja angeweza
kutuuza kiasi hiki.Kwa hiki alichokifanya
ni fundisho kwangu kuwa sitakiwi
kumuamini
mtu
yeyote
tena.Unayemuamini leo huyo ndiye
atakaye kuangamiza kesho.Tulifanya kosa
kubwa kumuamini Dr Richard na kosa hilo
linakwenda kutugharimu. Akaendelea
kuwaza Boaz
Aliwasili katika makazi ya aliyekuwa
waziri mkuu na kupokewa kwa furaha na
mwenyeji wake mheshimiwa Jeremiah
“Karibu sana Boaz.Karibu tena
nyumbani”
akasema
Jeremiah
akimuongoza Boaz katika chumba cha
maongezi
“Ahsante sana Jeremiah”
“Hebu nipe siri yako Boaz,miaka
inazidi kusonga lakini huzeeki.Whats your
secret? Akauliza Jeremiah na wote
wakacheka
“Nitakueleza siku nyingine Jeremiah
mzizi ninaoutumia” akajibu Boaz
“Pole sana Jeremiah kwa hiki
kilichokutokea.Sote tumestuka sana kwa
mambo yanayoendelea.Nini kimemfanya
Ernest akabadilika ghafla namna hii?
“Ahsante sana Boaz.Kilichotokea
kimemstua kila mtu ni kitu ambacho
hakuna aliyekuwa amekitegemea.Ni jambo
lililotokea ghafla sana.Hatujui ni kitu gani
kilichomfanya Ernest akabadilika namna
hii.Hata hivyo tunaendelea kujipanga
kukabiliana naye” akasema Jeremiah
“Mpaka sasa kuna hatua zozote
mlizochukua? Makao makuu ya Alberto’s
wanasemaje?
“Hicho ndicho kilichonifanya nikuite
hapa Boaz.Toka limetokea jambo hili
hakuna chochote kilichofanyika zaidi ya
kukaa kikao ambacho hakikuwa na suluhu
yoyote ya maana ya kulikabili suala
hili.Hatujui Ernest anashirikiana na akina
nani ila tunachojua ni kwamba he’s not
alone.Kikao kiliamua kulipa muda suala
hili kwa ajili ya kufanya uchunguzi
kufahamu ni akina nani anashirikiana
nao.Kanuni za jumuiya zinaeleza wazi
kwamba yeyoye anayekwenda kinyume au
kukiuka masharti au kufanya usaliti
adhabu yake ni kuuawa lakini cha
kushangaza mwenyekiti wetu kwa
makusudi amezuia hilo lisifanyike eti kwa
lengo la kufanya uchunguzi kubaini watu
ambao Ernest anashirikiana nao.Huu ni
upuuzi mkubwa kwani hatuna uhakika
uchunguzi huo utachukua muda gani na
kipindi hicho uchunguzi unafanyika Ernest
atazidi kujiimarisha na kuitokomeza
kabisa Alberto’s hapa nchini.Mimi,makamu
wa rais na mke wa rais tumekutana na
kulijadili suala hilo kwa upana wake na
tukafanya maamuzi kwamba ili tuweze
kuiokoa jumuiya hapa Tanzania basi
 
SEHEMU YA 33




mwenyekiti Obi auawe haraka sana na
kisha ifanyike kampeni na mimi
nichaguliwe mwenyekiti wa muda na hapo
nitaidhinisha rais auawe mara moja.Baada
ya Ernest kuuawa makamu wa rais
atakaimu nafasi ya rais kwa muda na
katika kipindi hicho atakachokaimu
atatengua maamuzi yote aliyoyafanya
Ernest.Ataurudisha tena ule muswada
ukajadiliwe bungeni pia atanirejeshea
wadhifa wangu wa waziri mkuu na
atamrejesha mkuu wa majeshi.Hilo
likifanyika sote tutakuwa salama.Biashara
zenu zote zitafanyika kwa uhuru na amani
.Endapo hilo halitafanyika nakuhakikishia
Boaz kuwa hatutabaki salama.We’ll all go
down.Ernest amekwisha onyesha dhamira
ya wazi ya kuifuta Alberto’s katika uso wa
Tanzania.We have to act very
fast.Nimekuita hapa kukupa taarifa hiyo na
kukuomba msaada wako.Nafahamu wewe
unafahamiana na watu wengi hivyo
naomba unisaidie kumpata mtu
atakayefanya kazi ya kumuua mwenyekiti
Obi.I need someone very professional.Can
you help me with that? Akauliza
Jeremiah.Boaz aliyekuwa anasikiliza kwa
makini akasema
“Nimekuelewa Jeremiah na kwangu
mimi hilo si tatizo.Ninafahamu watu
wengi wenye ujuzi wa hali ya juu wa
kuifanya kazi yako kwa ufanisi.Lakini nina
swali moja nini kitatokea endapo Alberto
mkuu akifahamu juu ya njama hizi?
Ukumbuke pia kwamba Alberto mkuu ni
mtu mwenye nguvu kubwa na uwezo wa
kung’amua mambo nina wasi wasi hata
mpango huu wa kumuua mwenyekiti
wenu anaweza akalifahamu na sote
tukaingia katika matatizo makubwa.Kwa
upande Fulani nadhani mwenyekiti wenu
anatumia busara kwani ni wazi Ernest
kuna watu anashirikiana nao na hao ndio
wanaompa ujasiri na nguvu ya kufanya
hayo anayoyafanya.You have to be sure
about what you want to do Jeremiah”
akasema Boaz.Jeremiah hakuonyesha
kufurahishwa na maneno yale ya Boaz
akasema
“Nielewe vizuri Boaz hali imechafuka
.Kila kitu kimesimama na hatujui nini
mipango ya kesho ya Ernest.Biashara yenu
inafanyika na kufanikiwa kwa mwavuli wa
Alberto’s na kama Alberto’s hawapo basi
hata ninyi hamtaweza kufanya tena
biashara zenu.You are nothing without
us.Suala hili si langu peke yangu ni suala
letu sote.Alberto mkuu yuko Italia na sisi
tuko hapa Tanzania.Hii ni nchi yetu na
endapo tutashindwa kufanya mabadiliko
basi misaada itakatwa na tutawekewa
vikwazo vya kiuchumi.Taifa hili litazidi
kudidimia katika umasikini.We have to
fight for our nation.Hata Alberto
mwenyewe endapo atagundua na halafu
akaona faida za tulichokifanya ninaamini
atatupongeza kwani lengo lake kubwa ni
kuibadili dunia na katika Afrika Tanzania
ni nchi anayoipa umuhimu mkubwa
mno.So are you going to find me what I
asked or not? Akauliza Jeremiah.Boaz
akamtazama kwa muda kisha akasema
“I’ll find someone to do your job”
“Thank you.Unadhani kufikia lini
utakuwa umempata ?
“Nipe siku mbili”
“Good” akasema Jeremiah na ukimya
mfupi ukapita.Boaz akasema
“Jeremiah kuna jambo nimelifikiri
kwa haraka haraka na sina uhakika kama
linaweza kuwa na maana yoyote kwako”
“Nieleze Boaz.Kwa hali ya sasa kila
ushauri una maana kwangu”:
“Baada ya kuyasikia maelezo yako
nimegundua kuwa tatizo hapa ni rais
Ernest Mkasa.Kama hivyo kwa nini basi
isitafutwe namna ya kuweza kumuondoa
Ernest na kumaliza matatizo yote bila ya
kumgusa mwenyekiti Obi? Hii inaweza
kuwa njia muafaka kabisa ya kuepusha
mambo mengine yasitokee ndani ya
jumuiya”
Jeremiah akavua miwani akatoa
kitambaa na kufuta macho kisha akasema
“Boaz wazo lako ni zuri na la msingi
,lakini tatizo lililopo ni kwamba kwa
mujibu wa taratibu zetu mwenyekiti wa
jumuiya nchini ndiye mwenye uwezowa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…