LEGE
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 5,122
- 9,209
- Thread starter
-
- #2,101
SEHEMU YA 34
kutoa ruhusa ya kumuua mtu ambaye
amekwenda kinyume na jumuiya na ndiyo
maana nataka nishike nafasi ya uenyekiti
ili kusitokee mkwamo wa aina yoyote .Kwa
hiyo Boaz nitafutie huyo mtu wa kuifanya
hiyo kazi yangu” akasema Jeremiah halafu
wakaendelea na maongezi mengine na
baadae Boaz akaondoka kwenda
kupumzika
“Mhh !! hili jambo linakoelekea
limeanza kunitisha.Hii ni kama filamu ya
usaliti.Dr Richard ametusaliti wenzake na
kutuuza kwa mwanae Marcelo,Ernest
Mkasa amewasaliti Alberto’s na sasa
Jeremiah na wenzake wanataka kufanya
usaliti mwingine kwa kwenda kinyume na
makubaliano ya kikao chao cha
pamoja.Sifahamu nini mwisho wa filamu
hii lakini huko tunakoelekea si kuzuri hata
kidogo.Watu
wamechanganyikiwa
hawafikiri sawasawa.Mimi nadhani suluhu
pekee hapa ni kumuua rais ambaye ndiye
anayeonekana kuwa kikwazo.Tukiendelea
kumuacha hai hatujui nini malengo
yake.I’m confused!! Akawaza Boaz.Kwa
upande wangu nadhani nisijiingize sana
katika mambo haya ya Alberto’s bali
nijikite katika kujihakikishia usalama wetu
mimi na wenzangu.Tuhakikishe kitabu
kinapatikana na papo hapo tuanze kubuni
mikakati ya kuifanya biashara yetu
iendelee endapo mambo hayatakuwa
mazuri.Tunatakiwa tujenge uwezo wa
kuendesha mambo yetu bila ya
kuwategemea sana Alberto’s.Hata hivyo
nina uhakika mkubwa Alberto’s
hawatakubali kushindwa na Ernest.Nina
imani huko makao makuu yao hivi sasa
watakuwa wanapanga mikakati mikubwa
namna ya kufanya” akawaza Boaz na
kukumbuka kuwa alihitaji kuongea na
Wilson Mukasha.Akachukua simu na
kuzitafuta namba za Mukasha akapiga
“Boaz !! akasema Mukasha kwa
mshangao
“Hallo Wilson”
“Hallo Boaz.Nimestuka kidogo
,sikutegemea kama ungenipigia mida hii”
akasema Mukasha.
“Usistuke Mukasha.Unafahamu mimi
huja na kuondoka kama mvua.Samahani
kwa kukupigia mida hii .Bado uko kazini?
“Hapana nimefika nyumbani muda
huu”
“Poleni sana kwa mambo yaliyotokea
na yanayoendelea kutokea”
“Ahsante Boaz.Ni kweli kuna upepo
mbaya unavuma sasa hivi na hali si nzuri
sana” akasema Mukasha
“Hicho ndicho hasa kilichonirudisha
nyumbani haraka.Kwa namna mambo
yanavyokwenda unadhani yanaweza
yakatulia hivi karibuni? Akauliza Boaz
“Hapana sina uhakika Boaz.Hii ni vita
ngumu.Ernest amejipanga sana kwa
mapambano.Ni wakati wa kuwa
waangalifu mno”
“Nalifahamu hilo Wilson na tayari
tumekwisha
anza
kuchukua
tahadhari.Wilson kilichonifanya nikupigie
usiku huu ni kutaka kufahamu jambo
moja”
“ Jambo gani Boaz?
kutoa ruhusa ya kumuua mtu ambaye
amekwenda kinyume na jumuiya na ndiyo
maana nataka nishike nafasi ya uenyekiti
ili kusitokee mkwamo wa aina yoyote .Kwa
hiyo Boaz nitafutie huyo mtu wa kuifanya
hiyo kazi yangu” akasema Jeremiah halafu
wakaendelea na maongezi mengine na
baadae Boaz akaondoka kwenda
kupumzika
“Mhh !! hili jambo linakoelekea
limeanza kunitisha.Hii ni kama filamu ya
usaliti.Dr Richard ametusaliti wenzake na
kutuuza kwa mwanae Marcelo,Ernest
Mkasa amewasaliti Alberto’s na sasa
Jeremiah na wenzake wanataka kufanya
usaliti mwingine kwa kwenda kinyume na
makubaliano ya kikao chao cha
pamoja.Sifahamu nini mwisho wa filamu
hii lakini huko tunakoelekea si kuzuri hata
kidogo.Watu
wamechanganyikiwa
hawafikiri sawasawa.Mimi nadhani suluhu
pekee hapa ni kumuua rais ambaye ndiye
anayeonekana kuwa kikwazo.Tukiendelea
kumuacha hai hatujui nini malengo
yake.I’m confused!! Akawaza Boaz.Kwa
upande wangu nadhani nisijiingize sana
katika mambo haya ya Alberto’s bali
nijikite katika kujihakikishia usalama wetu
mimi na wenzangu.Tuhakikishe kitabu
kinapatikana na papo hapo tuanze kubuni
mikakati ya kuifanya biashara yetu
iendelee endapo mambo hayatakuwa
mazuri.Tunatakiwa tujenge uwezo wa
kuendesha mambo yetu bila ya
kuwategemea sana Alberto’s.Hata hivyo
nina uhakika mkubwa Alberto’s
hawatakubali kushindwa na Ernest.Nina
imani huko makao makuu yao hivi sasa
watakuwa wanapanga mikakati mikubwa
namna ya kufanya” akawaza Boaz na
kukumbuka kuwa alihitaji kuongea na
Wilson Mukasha.Akachukua simu na
kuzitafuta namba za Mukasha akapiga
“Boaz !! akasema Mukasha kwa
mshangao
“Hallo Wilson”
“Hallo Boaz.Nimestuka kidogo
,sikutegemea kama ungenipigia mida hii”
akasema Mukasha.
“Usistuke Mukasha.Unafahamu mimi
huja na kuondoka kama mvua.Samahani
kwa kukupigia mida hii .Bado uko kazini?
“Hapana nimefika nyumbani muda
huu”
“Poleni sana kwa mambo yaliyotokea
na yanayoendelea kutokea”
“Ahsante Boaz.Ni kweli kuna upepo
mbaya unavuma sasa hivi na hali si nzuri
sana” akasema Mukasha
“Hicho ndicho hasa kilichonirudisha
nyumbani haraka.Kwa namna mambo
yanavyokwenda unadhani yanaweza
yakatulia hivi karibuni? Akauliza Boaz
“Hapana sina uhakika Boaz.Hii ni vita
ngumu.Ernest amejipanga sana kwa
mapambano.Ni wakati wa kuwa
waangalifu mno”
“Nalifahamu hilo Wilson na tayari
tumekwisha
anza
kuchukua
tahadhari.Wilson kilichonifanya nikupigie
usiku huu ni kutaka kufahamu jambo
moja”
“ Jambo gani Boaz?