QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

Nawaaga Rasmi
Sitosoma tena Manyanyaso haya
Kaeni na Monica wenu
71a13807b68342ac12efbf9ee399cc44.jpg

Nataman kupata uthibitisho wa maneno hayo
 
Ebu njoon bas mmalizie hii story mbududa na lege tunaheshim kazi nzuri mliyoifanya hasa lege msiitia doa
 
Mimi nina tabia moja huwa naangalia kwanza kama mleta story kaimaliza story yake na kama hajaimaliza na watu walioanza kuisoma wanalalamika sana huwa siisomi nisije nikapata arosto ya bure,,
 
SEHEMU YA 14: SEASON 5

Baada ya kumpa Maria simu
azungumze na rais,Austin, Amarach
na Job ambaye tayari alikuwa na
nafuu kubwa wakasimama nje ya kile
chumba wakimtazama Maria kupitia
kioo kikubwa na waliweza kusikia
kila alichokiongea .Austin na Job wote
walifahamu vyema lugha ya kiarabu
hivyo waliweza kusikia kila kitu
alichokizungumza Maria.Mara tu
Maria alipomaliza kuzungumza na
mama yake simuni Amarachi akaingia
akaichukua simu na bila kumsemesha
chochote akatoka
“ Austin mimi sifahamu lugha ya
kiarabu .Mnaweza kuniambia ni kitu
gani ambacho Maria alikuwa
anazungumza ?akauliza Amarachi
“ Amarachi alikuwa
anazungumza na mama yake Yasmin
Esfahani na alimfahamisha kwamba
amekuja Tanzania kwa dhumuni la
kumtafuta na kumkomboa.Kingine
alichokiongea Maria ni kwamba
ameshikiliwa mahali na watu fulani
wanaomtesa na hadi sasa hawezi
kutembea.Mwisho akamshukuru
mama yake kwa kumsaidia na
akamuahidi kuonana naye kesho”
akasema Austin
“Hili jambo limenishangaza
sana.Nilimuuliza rais kuhusu Yasmin
na akanijibu kwamba hana taarifa
zake lakini usiku huu anampa Yasmin
simu azungumze na mwanae na
hakutaka hata kunitaarifu kama
anayezungumza na Maria ni Yasmin
mwanamke ambaye
tunamtafuta.Najiuliza kwa nini rais
ametuficha kuhusu hili jambo? Kwa
nini ametudanganya? Kuna nini
kinaendelea kati yake na Yasmin?
Akauliza Austin na mara simu yake
ikaita.Alikuwa ni rais.Akawatazama
wenzake kisha akaipokea
“ Hallow mzee”
“ Habari za usiku hu Austin.Vipi
maendeleo yako na wenzako? Rais
akauliza
“ Tunaendelea vyema mzee”
akajibu Austin
“ Nafurahi kusikia hivyo.Endapo
kutakuwa na tatizo lolote usisite
kunitaarifu muda wowote .Kuhusu
yule mwanamama uliyeniambia
kwamba anashikiliwa hapa Tanzania
bado nasubiri taarifa zake .Watu
niliowapa kazi ya kufuatilia habari
zake hawajanipa mrejesho.Nikipata
taarifa zozote nitakujulisha.” Akasema
rais na sura ya Austin ikaonyesha
mshangao mkubwa.
“ Sawa mzee
nimekuelewa”akajibu
“ Vipi kuhusu majibu ya kipimo?
Mpaka sasa bado kimya? Akauliza
rais
“ Mpaka sasa bado kimya
hatujapata jibu lolote.Tunategemea
kesho kupata majibu”
“ Ok good.Sasa Austin
ninamuhitaji Maria kesho nina
mazungumzo naye “
“ Unamtaka Maria? Austin
akauliza kwa mshangao
“Ndiyo Austin.Mbona
umestuka?
“ Lazima nistuke mzee kwani
bado tunahitaji kumfanyia mahojiano
zaidi kumfahamu yeye ni nani.”
“ Nalifahamu hilo Austin .Hata
mimi kuna mambo nataka
kuzungumza naye halafu
nitamrejesha kwenu.” Akasema rais
na kukawa kimya
“Are you there Austin? Akauliza
rais
“Yes I’m here “
“Umenielewa? Akauliza rais
lakini Austin hakujibu kitu
“ Umenielewa Austin? Akauliza
tena
“Ndiyo mzee”
“ Good.Nitamuhitaji ikulu kesho
saa nne asubuhi kwa kuwa sifahamu
ni wapi ulipo.Utamtuma Amarachi
amlete hapa ikulu .”
“ Sawa mzee tutafanya hivyo”
“ Vizuri sana.Nitawasiliana nawe
kesho au muda wowote nikipata
taarifa kuhusu yule mama
unayemuhitaji .Kabla sijasahau jioni
ya leo ulinipa taarifa kuhusu Evans
kumshambulia Mukasha.Nimefuatilia
na kugundua kwamba wawili hawa
wana matatizo yao binafsi ,wana
tofauti zao za muda mrefu kwa hiyo
usiumize kichwa kuhusu wao.”
Akasema rais wakaagana akakata
simu.
“ Picha inaanza kujengeka na
sasa na papo hapo taa nyekundu
inaaza kuwaka.Kuna kitu kinaendelea
hapa.Muda mfupi uliopita
tumemsikia Maria akizungumza na
mama yake kuwa wataonana kesho na
sasa hivi rais anapiga simu kuwa
anamtaka Maria kesho ikulu.Ni wazi
kwamba anataka kumkutanisha na
mama yake.What’s going on here?
Akauliza Austin.Kuna mambo kadhaa
hapa,kwanza rais ametundanganya
kwamba hamfahamu Yasmin wakati
anafahamu hadi mahala aliko.Pili
anafahamu kuwa Maria ni mtoto wa
Yasmin.Kama tayari anafahamu haya
yote ni wazi tayari anafahamu kuwa
Yasmin ni mfuasi wa IS na kama hilo
analifahamu kwa nini basi
anashirikiana naye? Katika
mazungumzo yake na mama yake
,Maria alimshukuru mama yake kwa
kumsaidia.Mnaipata picha iliyopo
hapo? Akauliza Austin
“Kuna picha inaonekana hapa.Ni
wazi rais ana lengo la kumkutanisha
Maria na mama yake.”akasema Job
“ Kwa nini anafanya hivi?
Akauliza Amarachi
“ Inabidi tuanze kutafuta jibu la
swali hili la Amarachi.Tunahitaji
kufahamu kuna nini kinachoendelea?
Tuko katika vita moja na rais lakini
mwenzetu anaanza kuonekana kuwa
na ndimi mbili na mwenendo wake
umeanza kunipa shaka.Kwa hili
lililotokea usiku huu linatufanya na
sisi tuongeze jicho la tatu tuone mbali
zaidi” akasema Austin.
“ Aliposema anamtaka Maria
ulimkubalia? Akauliza Job
“Ndiyo nilimkubalia lakini
siwezi kufanya hivyo.Siwezi katu
kumuachia Maria.Kwa kuwa tayari
nimemkubalia rais kwamba kesho
tutampeleka Maria ikulu basi
tunapaswa kuutumia muda huu tulio
nao hadi asubuhi kufahamu kile
kinachoendelea kati ya rais na
Yasmin.Kitu cha kwanza
tunachotakiwa kufanya ni kutafuta
mahala aliko Yasmin.Tutafute simu ile
ya rais ilipigwa kutokea wapi?
Tukifanikiwa kwa hilo basi tutakuwa
tumefanikiwa kumpata Yasmin.Job
andaa vifaa na sehemu ya kufanyia
kazi.Amarachi twende tena kwa Maria
nataka nijaribu kuzungumza naye
kama anaweza akakubali kunieleza
chochote” akasema Austin na bila
kupoteza muda wakaenda tena katika
chumba cha Maria
“ Hallo Maria” akasema Austin
kwa upole.Maria hakujibu kitu
“ Najua unaendelea vyema hasa
baada ya kuzungumza na mama
yako.” Kauli ile ikamstua Maria
akamtazama Austin usoni.
“ Nani kakwambia
nimezungumza na mama? Wewe
ulinipa simu nizungumze na mama au
rais? Akauliza Maria.
“ Sikiliza Maria kuna kamera za
siri ndani ya chumba hiki na chochote
kinachofanyika humu tunakitazama
katika luninga kubwa hapo nje kwa
hiyo tumefuatilia maongezi yako
yote.Binafsi ninao uwezo wa
kuzungumza lugha kadhaa kwa
ufasaha kabisa.Ukiacha kiswahili na
kiingereza ninaweza pia kuzungumza
kireno,kichina,kirusi,kijerumani na
kiarabu.Yote uliyoyazungumza na
mama yako nimeyasikia”
Sura ya Maria ikazidi
kubadilika.Austin akaendelea
“ Tayari tunafahamu kuwa
mama yako Yasmin Esfahani ni
mfuasi wa mtandao wa kigaidi wa IS
na hapa nchini alikuja kwa lengo la
kuutanua mtandao huo katika eneo la
afrika mashariki.Ninachohitaji toka
kwako nataka uniambie mipango
yako na mama yako kwani nimesikia
ukimshukuru mama yako na
kumuahidi kuwa mtaonana kesho”
akasema Austin
“ Austin sina sababu ya kukujibu
chochote sasa hivi kwani tayari mama
yangu yuko huru na kesho
ninakwenda kuungana naye.Yale
makubaliano yetu yamekwisha na
nina imani kama bado hujapewa
maelezo hadi sasa basi yanakuja
kuhusu kuniachia huru.Usipoteze
nguvu zako kuuliza maswali ambayo
huwezi kupata majibu yake.Elekeza
nguvu zako katika matibabu upone “
akasema Maria
“ Sikiliza Maria wewe bado uko
mikononi mwangu .Chochote kile
ambacho rais ameongea nanyi
anawadanganya .You are both going
to die” akasema Austin
“ Ni bora nife kuliko kukueleza
kitu chochote Austin.Kwa sasa baada
ya kufahamu kuwa mama yangu yuko
huru siogopi tena kifo.If you want to
kill me,go ahead lakini sijui
utamueleza nini mkuu wako wa nchi”
akasema Maria kwa kujiamini
sana.Austin akamtazama kwa
umakini mkubwa
“ She’s not going to tell me
anything.Tayari ameahidiwa
kuachiwa huru na rais” akawaza
Austin na kutoka mle chumbani.
 
SEHEMU YA 15: SEASON 5
Imetimu saa moja za asubuhi
,rais wa jamhuri ya muugano wa
Tanzania Ernest Mkasa alipomaliza
mazungumzo yake na Jenerali Lameck
Msuba mkuu wa majeshi ya ulinzi
.Mazungumzo hayo marefu
yaliyochukua takribani saa moja na
nusu yalihusu tukio kubwa
linalotarajiwa kutokea nchini siku
hii.baada ya kumaliza maongezi na
mkuu wa majeshi Ernest akawapigia
simu walinzi wake waliokuwa
wakilinda nyumba walimolala Tariq
na Yasmin kuuliza maendeleo na
akataarifiwa kwamba hakukuwa na
tatizo lolote.Kisha kata simu
akampigia Austin lakini simu yake
haikuwa ikipatikana.Akampigia Job
lakini naye simu yake haikuwa
ikipatikana.
“ Hawa vijana wana tatizo gani
leo wote wawili simu zao
hazipatikani? Akajiuliza rais na
kuanza kujiandaa kuelekea ofisini
kwake.
Saa mbili na nusu rais akaingia
ofisini kwake na kitu cha kwanza
kukifanya akamuita mzee Pantaleo
Mgela.Huyu ndiye anayefanya kazi
katika chumba cha kutunzia nyaraka
kuu za Taifa.Kwa zaidi ya miaka
thelathini mzee huyu amekuwa ikulu
akifanya kazi hii ya uangalizi wa
nyaraka hizi kuu za taifa na
kuhakikisha zinabaki kuwa katika hali
nzuri bila kupoteza ubora wake.
Mzee Pantaleo alifika haraka
katika ofisi ya rais wakasalimiana
pamoja na kuweka utani kidogo kama
walivyozoea na kasha rais akamueleza
kile alichomuitia pale ofisini kwake
asubuhi ile.
“Mzee Pantaleo sijafika ofisini
kwako kwa muda mrefu kidogo.Vipi
maendeleo ya huko? Akauliza rais
“ Maendeleo mazuri
mheshimiwa rais.Kila kitu kiko sawa
na hakuna tatizo lolote”
“ Nafurahi kusikia hivyo.Kuna
kitu nataka unisaidie.Niletee ile hati
ya muungano nahitaji kuipitia kuona
maendeleo yake.Nimeelekezwa kuna
teknolojia mpya ya kuweza kuhifadhi
nyaraka mbali mbali kwa miaka mingi
kwa ubora mkubwa.Niletee niangalie
ubora wake ili nione kama tunaweza
kuhitaji hiyo teknolojia mpya au
tuendelee na hii tuliyonayo sasa”
akasema rais
“ Sawa mheshimiwa rais.”
Akasema mzee Pantaleo na kuondoka
“ I don’t know if I’m doing the
right thing .Ninachokifanya ni kitu
hatari mno kwa taifa na endapo hili
litafahamika wananchi watanitafuna
nyama au ninaweza kuozea
gerezani.Hata mimi inaniuma na
sipendi kufanya hivi lakini kipi bora
kuitoa hati ya muungano au kuiacha
nchi iharibiwe na Alberto’s? Mimi
kwa upande wangu naona ni afadhali
nchi ikavunjika vipande kuliko
kuwaacha Alberto’s watekeleze
mipango yao miovu kwa nchi
yetu.Misuko suko mikubwa itatokea
lakini nitakabiliana nayo na kama siku
moja huko mbeleni itagundulika hiki
nilichokifanya naamini wapo
watakoniunga mkono kwani
ninafanya haya kwa ajili ya kuokoa
kizazi cha watoto wetu kisipotee”
akawaza Ernest
Mzee Pantaleo akarejea akiwa na
mkoba mdogo mweusi akaufungua na
kutoa ile hati ya muungano wa
Tanganyika na Zanzibar iliyokuwa na
jalada gumu jekundu.
“ Kuna yeyote aliyeona au
kuifahamu kuwa umeitoa hati hii?
Rais akauliza
“ Hakuna anayefahamu .Ni mimi
pekee”
“ Good.Asifahamu mtu
yeyote.Ngoja niipitie halafu baadae
nitakuita uje uichukue.” Akasema rais
na mzee Pantaleo akaondoka.
Kwa zaidi ya dakika tano rais
alikuwa ameinamisha kichwa
akitazama hati ile ya muungano
“ I have to do this” akasema Rais
“ Tayari nimekamilisha kila kitu
walichokihitaji.Ninaye Tariq na vile
vile Yasmin.Kilichobaki ni kitu kimoja
tu anachokitaka Yasmin ambacho ni
mwanae Maria” akawaza rais na
kuchukua simu akajaribu kupiga
namba za simu za Austin na Job lakini
simu zao hazikupatikana.
“ Kuna tatizo gani? Mbona simu
zao leo hazipatikani? Au
wameshambuliwa? Akajiuliza halafu
akachukua simu na kuzitafuta namba
fulani akapiga
“ Hallow mzee shikamoo”
ikasema sauti ya upande wa pili
“ Marahaba Bill.Nipe ripoti
mmefikia wapi kuhusu Mukasha?
“Mpaka sasa bado hatujapata
taarifa zozote za kuhusu Mukasha ila
bado tunaendelea kumsaka”
“ Vipi kuhusu Job? Mlifanikiwa
kufahamu mahala alipo?
“ Hapana mzee.Mpaka sasa bado
hatufahamu”
“ Sawa Bill.Msifanye chochote
kwa sasa hadi hapo nitakapowajulisha
.Ninakaribia kufahamu mahala aliko
ila ongezeni nguvu katika kumsaka
Mukasha” akasema rais na kukata
simu
“Nilikuwa na wasiwasi labda
yawezekana akina Bill walifahamu
aliko Job na wakawavamia lakini
hawajafanya hivyo.Kwa nini basi
wote wazime simu?Saa tano leo
natakiwa kumkabidhi Yasmin hati hii
lakini lazima nimpate Maria pia ili
nifanye mabadilishano na Yasmin.Jana
nilimueleza kwamba nitampa
mwanae endapo atanirejeshea hati ya
muungano.Lakini kitendo cha akina
Austin kuzima simu wote kwa pamoja
kimenifanya nianze kuwa na wasi
wasi” akawaza rais.
“ Sitakiwi kupoteza muda
kuwawaza hawa jamaa kwani ni watu
ambao ninawamudu na
ninachokisubiri kwako ni majibu ya
kile kipimo cha vinasaba .Nikipata
majibu hayo nitawafutilia mbali”
akawaza na kutazama saa yake
akainuka akaipakia hati ile ya
muungano katika mkoba na kutoka
akawaagiza walinzi wake kupunguza
magari katika msafara wake na kubaki
na magari matatu tu na kuwapa
maelekezo wanakoelekea
“Hii ndiyo safari ya mwisho ya
Tanzania.Endapo juhudi za kuipata
tena hati ya muungano zitagonga
mwamba ndio utakuwa mwisho wa
nchi inayoitwa Tanzania kwani
hakuna uhalali wa kuitwa Tanzania
bila kuwa na hati inayoonyesha kuwa
Tanganyikana Zanzibar
ziliungana.Kuna wazo nimelipata
.Natakiwa kumshughulikia mzee
Pantaleo.Endapo mambo yataharibika
huyu mzee atakuwa wa kwanza kutoa
siri.Nitawelekeza vijana wangu
wamshughulikie haraka sana kabla ya
mchana wa leo” akawaza rais
 
SEHEMU YA 16: SEASON 5

Saa nne za asubuhi ,Austine
akiwa na wenzake,Job,Amarachi na
Marcelo walikuwa wakijadili namna
kumpata Yasmin Esfahani.Walijitahidi
kwa kadiri walivyoweza usiku mzima
uliopita kutafuta mahala ambako
Yasmin alitumia simu ya rais
kuzungumza na mwanae Maria lakini
hawakufanikiwa.
“Jana tulifanya kila tuliloweza ili
kufahamu mahala aliko Yasmin
hatukufanikiwa.Kuna jambo moja tu
ambalo tunaweza kulifanya ili
kumpata yasmin.Nitampa simu Maria
ampigie rais na aombe kuzungumza
na mama yake.Hilo likifanikiwa
nitazungumza na Yasmin na
atatueleza kile kilichopo kati yake na
rais” akasema Austin
“ Maria atakuwa tayari kufanya
hivyo? Tayari amekwisha hakikishiwa
uhuru na rais sidhani kama
aataonyesha tena ushirikiano
kwetu.”Akasema Amarachi
“Tutamfanya akubali kufanya
tunavyotaka” akasema Austin na bila
kupoteza muda wakaenda wote
chumbani kwa Maria isipokuwa
Marcelo.
“Maria ule wakati wa mzaha
umekwisha na nimekuja kikazi zaidi
kwa hiyo nitakuomba utekeleze kila
kile nitakachokuamuru
ukifanye”akasema Austin na sura
yake haikuonyesha masihara hata
kidogo.Siku hii alikuwa na nafuu
kubwa.Akatoa simu mfukoni na
kuiweka mezani.
“Nataka umpigie simu rais na
umwambie kwamba unataka
kuzungumza na mama yako mara
moja.” Akasema Austin.Maria
akatabasamu na kusema
“ Austin nimekueleza toka jana
kwamba usipoteze muda wako
kuhusu mimi au mama
yangu.Nadhani umekwisha pigiwa
simu na rais akikutaka uniachie huru
kwa hiyo siwezi kufanya hicho
unachoniamuru nikifanye.”akasema
kwa dharau na kuinamisha kichwa
“Maria nilikueleza awali
kwamba sihitaji mzaha siku ya leo
kwa hiyo chukua simu hiyo na
umpigie rais.”
“ No ! I cant do that!! Akasema
Maria kwa ukali.Sura ya Austin
ikazidi kujikunja kwa hasira
akamgeukia Amarachi
“ Bring Boaz here”
Amarachi akatoka kwenda
kumelata Boaz
“ If you do anything to my father
I swear I’ll kill you all!! Akasema
Maria kwa hasira.Baada ya dakika
tatu Boaz akaletwa mle
chumbani.Kwa sekunde kadhaa
akatazamana na mwanae Maria na
wote machozi yakawatoka
“ Austin kwa nini umetufanyia
hivi ? Tumekukosea nini? akauliza
Boaz kwa uchungu baada ya
kumuona mwanae namna
alivyoumizwa.
“Sit !!! akaamuru Austin na Boaz
akaketi kitini.Akawatazama kwa
zamu na kusema
“ Kwa miaka kadhaa nimeishi
nanyi kwa upendo mkubwa kama
familia moja.Niliamini ninyi ni watu
wema na wenye upendo wa kweli
kwangu lakini Mungu amenionyesha
kuwa watu nilioamini ni wazuri
kwangu nimashetani waliovaa miili ya
wanadamu.”
“ Unatuita sisi mashertani? Bila
ya sisi ungekuwa kaburini hivi sasa
.Kwa haya yote tuliyokutendea
unadiriki kutuita sisi mashetani?
Akauliza Boaz
“ Shut up !! akafoka Austin.
“ You are the family of
devils.Siku chache zilizopita huyu
mwanao amenipiga risasi nne na
nusura ningepoteza maisha.Look at
her.Ukimtazama huwezi kudhani
kama amewahi hata kuigusa silaha
lakini ni mtu hatari sana.Ana uwezo
mkubwa wa kutumia silaha.Ni
Mungu tu ameninusuru na kifo kwa
sababu anajua kunakazi kubwa
ninaifanya.”akanyamaza akamtazama
Boaz na kusema
“ Wewe na mwanao mliniambia
kwamba mama yake Maria alifariki
dunia angali maria akiwa mdogo.kwa
nini mkanidanganya wakati mama
yake Maria yupo hai?
“ That’s not true.She’s dead”
“ No ! She’s not dead.She spoke
with your daughter last night.Muulize
mwanao kama ninasema uongo”
akasema Austin na sura ya Boaz
ikabadilika
“ Maria ! akaita
“Her name is not Maria.She’s
Shamim” akasema Austin na kuzidi
kumchanganya Boaz
“ Shamim? Akauliza Boaz
“Ndiyo.Hufahamu kama
mwanao ana majina zaidi ya moja?
“hapana sifahamu
chochote.Mimi nalifahamu jina moja
nililompatia mimi wakati alipozaliwa
la Maria hayo mengine siyafahamu.”
Akasema Boaz na kumgeukia Maria
“ Maria my love tell me what this
man is saying is not true”
Maria akainamisha kichwa
“Nijibu Maria kama ni kweli
anachokisema Austin.Ni kweli mama
yako yuko hai?
“It’s true dady” akasema Maria
“Oh my God !!! akasema Boaz
“Umefahamuje kama mama yako
yuko hai ? akauliza Boaz
“ Ukweli ni huu” akasema
Austin
“Yasmin Esfahani ambaye
uliwahi kuishi naye na mkajaliwa
kupata mtoto mmoja ambaye ni Maria
ni gaidi wa kimataifa toka kikundi cha
kigaidi cha IS.Alikuja hapa Tanzania
kwa lengo la kutanua mtandao wao
katika eneo la afrika mashariki na
kabla hajafanikisha lengo lake
akakamatwa na kufungwa mahala pa
siri kwa zaidi ya miaka kumi
sasa.Mwanao Maria alikuwa
anafahamu suala hili kwa muda mrefu
na hakukueleza.Tumefuatilia
mawasiliano yake ya barua pepe na
mtu mmoja anaitwa Bin Omar na
alimtaarifu kuwa anakuja Tanzania
kwa lengo la kumtafuta mama yake na
alitegemea kunitumia mimi ili
kumpata mama yake.Sina shaka
yoyote kuwa Maria naye ni mmoja wa
wafuasi wa IS lakini anayefanya
mamboyake kwa siri kubwa.Nadhani
mpaka hapo tayari umekwisha pata
picha halisi ya mwanao “ akasema
Austin.
Uso wa Boaz uliloa
jasho,akamtazama mwanae kwa
hasira na kusema
“Maria ni kweli hayo anayosema
Austin?
Maria hakujibu kitu akainamisha
kichwa.Austin akamgeukia Maria
“ Maria it’s time now to pick the
damn phone and call mr President!!
Akasema Austin.Bado Maria hakujibu
kitu.
“Job give me the gun” akasema
Austin na Job akampa bastora
“Boaz nilikuheshimu kama baba
yangu lakini pamoja na heshima hiyo
kubwa niliyokupa bado ukadiriki
kuwa na mahusiano ya kimapenzi na
mdogo wangu ambaye ni sawa na
mwanao,ukamuingiza katika biashara
ya dawa za kulevya na mwisho
akafungwa gerezani.Hilo limeniumiza
sana.It’s your time to pay.Kama
nilivyokueleza awali kwamba ukiingia
katika anga zangu mimi ni mkatili
kuliko hata Simba na leo nitakuondoa
uhai wako lakini ni jambo moja tu
litakalokuokoa .Ni pale mwanao
atakapochukua simu na kumpigia
rais.Asipofanya hivyo ninakifumua
kichwa chako” akasema Austin na
kuielekeza bastora kichwani kwa Boaz
“ Maria you have one minute to
decide either your father to die or call
president” akasema Austin
“Austin please don’t do that to
my father.Dont kill him” akasema
Maria huku machozi yakimtoka
“ Three !!! akahesabu Austin
“ Austin please don’t do that
“ Two..!! take the phone and call
president !!! akasema Austin lakini
Maria alionyesha wazi kuwa hayuko
tayari kufanya alichoamriwa na
Austin na mara ukasikika mlio wa
risasi.Kila mmoja akafumba macho
.Baada ya sekunde kadhaa Maria
akafumbua macho na kumuona baba
yake ameketi kitini huku akitetemeka
mwili.
“Hilo lilikuwa ni onyo kwamba
huwa sifanyi utani na ndiyo maana
nimepiga risasi pembeni.Kama
utaendelea na kiburi chako nitafanya
kweli”akasema Austin
“ok ! ok ! Nitampigia rais.”
Akasema Maria na Austin akawasha
simu akazitafuta namba za rais
akapiga na kumpa simu Maria
“ Hallow Austin.Habari yako?
Nimekutafuta toka asubuhi bila
mafanikio .Kuna tatizo lolote?
Akasema rais baada ya kupokea simu
“ Shikamoo mzee.Unaongea na
Maria hapa”
“ Oh ! Maria habari yako. Tayari
umefika ikulu?” akasema rais
“ Mheshimiwa rais naomba
nizungumze na mama yangu
tafadhali”
“Kabla ya kuzungumza na mama
yako nataka kwanza kufahamu je
tayari umeshafika ikulu?
“ Mheshimiwa rais bado sijafika
Ikulu”
“ Uko karibu na Austin? Nahitaji
kuzungumza naye”
“ hapana mzee siko naye
karibu.Niko peke yangu” akasema
Maria
“ Sawa Maria naomba unisubiri
baada ya dakika tano utazungumza na
mama yako.Naelekea mahala alipo ila
mwambie Austin nahitaji sana
kuzungumza naye” akasema rais
“ Austin nadhani ametoka
pamoja na wenzake na sijui
wameelekea wapi.Waliniachia simu
hapa kwa ajili ya mawasiliano na
mama” akasema Maria
“ Ok Maria nitakupigia baada ya
muda mfupi” akasema rais na kukata
simu
“ Good.Umefanya vizuri.Wakati
mwingine usitake
kunijaribu.Nikikuamuru kufanya
jambo Fulani ,lifanye bila kusita!!
Akasema Austin huku akimtazama
Boaz ambaye alikuwa amejisaidia haja
ndogo kwa woga uliompata baada ya
kukoswa na risasi
“ Take him away” akasema
Austin na Amarachi akamchukua
Boaz akamrejesha katika chumba
chake. Baada ya dakika tano kama
alivyoahidi rais akapiga simu.Monica
akaipokea na kuanza kuzungumza
kiarabu baada ya kufahamu
aliyekuwa anaongea ni mama yake.
“ Give me that phone” akasema
Austin na Maria akampa simu
“ hallo Yasmin” akasema Austin
kwa lugha ya kiarabu
“ wewe ni nani na unataka nini?
Kwa nini haujamuachia huru
mwanagu hadi sasa ? Akauliza
Yasmin kwa kiarabu
“ naomba unisikilize vizuri
Yasmin.Binti yako Shamin pamoja na
mumeo Boaz ,wote ninawashikilia
hapa na usalama wao utategemea
sana namna utakavyotii maelekezo
yangu”
“ Nini unahitaji? Akauliza
Yasmin
“ Kwanza nahitaji kufahamu
kuna kitu gani kinachoendelea kati
yako na rais?
“ rais ameniachia huru na
tumeweka makubalino kuwa siwezi
kuondoka bila ya mwanangu Shamin
na ndipo alipokupigia simu akakupa
maelekezo kuhusu kumuachia
Shamim.Leo saa nane mchana
ninaondoka kwa hiyo namuhitaji
mwanangu kabla ya muda huo bila
hivyo makubaliano yetu na rais
yatakuwa yamekufa” alasema Yasmin
“ Kwani mmekubaliana jambo
gani? Rais amefanya makubaliano
gani na mtu ambaye anafahamu kuwa
ni mfuasi wa IS? Akauliza Austin
“ Rais hajafanya makubaliano na
mimi wala IS bali amefanya
makubaliano na Alshabaab na moja
kati ya jambo walilokubaliana ni mimi
kuachiwa huru.Kwa hiyo sifahamu
wamekubaliana mambo gani ila mimi
na yeye tumekubaliana kuwa lazima
nimpate mwanangu kabla sijaondoka
leo”
“ Sikiliza Yasmin,mwanao
Shamim niko naye mimi na hataweza
kuachiwa hata kwa amri ya
rais.Hautamuona tena katika maisha
yako “
Shamim akasikika akivuta pumzi
ndefu kisha akasema
“ Ni vipi iwapo mimi na wewe
tutafanya makubaliano? Kuna kitu
cha thamani sana ambacho
nitakukabidhi ili unipe mwanangu”
“ Kitu gani hicho?
“ Kuna kitu kikubwa sana
nitakupatia lakini endapo utakuwa
tayari kwa mambo yafuatayo.Kwanza
utanikabidhi mwanangu Shamim na
pili utanisaidia niweze kupata hati
mpya ya kusafiria itakayoniwezesha
niende mbali kabisa mimi na
mwanangu.Ukinifanikishia hayo
nitakupa kitu hicho kikubwa kwa
ajiliya usalama wa nchi yenu.Uko
tayari kwa hilo” akauliza Yasmin, na
kukawa kimya.
“ hallo, uko tayari kwa hilo
nililokueleza? Akauliza Yasmin
“ Siwezi kufanya maamuzi hadi
hapo utakaponieleza ni kitu gani
hicho chenye thamani ambacho
unataka kunipatia”
“ Siwezi kukueleza sasa hivi ni
kitugani hadi hapo nitakapokuwa
nimekabidhiwa.Niambie kama uko
tayari ili nianze kuweka mipango ya
kukutana nawe”
“ Niko tayari ” akajibu Austin
“ Vizuri.Kaa tayari nitakupigia
simu muda wowote baadae nitakupa
maelekezo ila tafadhali naomba
mwanangu asiendelee kuteswa”
akasema Yasmin na kukata
simu.Austin na wenzake wakatoka
mle ndani wakarejea sebuleni.
“ Pole Austin it wasn’t easy”
akasema Amarachi
“ Thank you”akajibu Austin na
kuvua fulana yake kwani aliokuwa
anatokwa na jasho akanywa glasi ya
maji na kusema
“Nyote mmefuatilia
mazungumzo yangu na Yasmin.Kuna
jambo hapa linaendelea kati ya rais na
Alshabaab kiasi cha kufanya
makubaliano ya kumuachia huru
Yasmin.Kitu gani kinaendelea kati ya
rais na Alshabaab? Hiki ni kikundi cha
kigaidi rais anawezaje kufanya
makubaliano na kikundi hiki? Kuna
siri kubwa imejificha hapa.Lazima iko
sababu iliyomplekea rais akafanya
makubaliano na hawa jamaa huku
akifahamu ni watu hatari” Akasema
Job
“Niliwaeleza jana kwamba
mwenendo wa rais si mzuri kwa hiyo
inatupasa kuwa na jicho la tatu ili
tuweze kuona zaidi mambo
anayoyafanya.Alikana kumfahamu
Yasmin lakini anamfahamu na
amefanya makubalianao na Alshabaab
ya kumuachia mtu huyu hatari kabisa
.Kwa nini akaamua kukubaliana na
Alshabaab kumuachia mtu huyu
hatari ndilo swali tunalopaswa
kujiuliza.Nadhani itatulazimu kuweka
pembeni mambo mengine yote na
kuanza kushughulika na rais kwanza
ili tumfahamu vyema kutokana na
mambo yake anayoyafanya.Huyu ni
mtu ambaye bado hatumfahamu
vizuri. Vita na Alberto’s inamtegemea
sana yeye lakini hatuwezi kufanikiwa
endapo mtu tunayemtegemea
anakuwa na ndimi mbili.Kama
ameweza kutudanganya kuhusu
Yasmin tutamuaminije mtu kama
huyu? Tunachopaswa kufanya ni
kuweka pembeni mipango yote ili
kwanza tujiridhishe na mtu ambaye
tunashirikiana naye kama tunapaswa
kuendelea naye au vipi.Kitendo cha
kuwa na mawasiliano na Alshabaab
kinatosha kabisa kutufanya tuwe na
mashaka kwamba huyu sio mtu
mwema hata kidogo.Wakati
tukiendelea kumsubiri Yasmin apige
simu na kutupatia hicho kitu cha
muhimu na chenye thamani
anachokisema ,Amarachi utakwenda
kufuatilia majibu ya kile kipimo cha
vinasaba kwani waliahidi leo majibu
yatakuwa tayari.Job tutaendelea
kumuhoji Maria ili kumfahamu kwa
undani zaidi.” Akasema Austin

SEHEMU YA 17: SEASON 5

Inakaribia saa tano za
asubuhi,Ernest Mkasa rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania tayari
alikuwa katika nyumba walimolala
Tariq na Yasmin.Kikubwa
kilichomleta hapa ni kumkabidhi
Yasmin hati ya muungano wa
Tanganyika na Zanzibar kama
walivyokubaliana na Habib mkuu wa
kikundi cha Alshabaab.
Akaufungua mkoba wake na
kutoa bahasha ya khaki ambayo ndani
yake akatoa hati ya muungano
akaitazama na kisha akamkabidhi
Yasmin.
“Hii ndiyo hati halisi ya
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar.Ninakukabidhi kama
tulivyokubaliana na wakuu wako”
akasema Ernest.Yasmin hakujibu kitu
akaifungua akaitazama kurasa
mojamoja halafu akampatia Tariq
naye akaipitia na kumrudishia.
“Nadhani nyote mmeiona na
kuridhika nayo” akasema Ernest
“Tumeiona lakini bado
wataalamu wetu wataipitia tena ili
kuhakiki kama kweli ni halisi ingawa
kwa macho ya kawaida inaonekaan ni
halisi” akasema Yasmin.Rais
akachukua simu yake na kumpigia
Habib
“ Habari za asubuhi mheshimiwa
rais.Nadhani utakuwa na taarifa
njema za kunipatia ” akasema Habib
“Ndiyo habib ninazo taarifa
nzuri kwako.Ni kwamba tayari
nimempatia Yasmin ile hati halisi ya
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar kama tulivyokubaliana.”
“Nafurahi kusikia hivyo.Naomba
nizungumze na Yasmin” akasema
Habib na rais akampa simu Yasmin
wakaanza kuzungumza kwa lugha ya
kiarabu.Walizungumza kwa zaidi ya
dakika kumi halafu Yasmin akampa
simu rais azungumze na Habib
“Mheshimiwa rais ahsante kwa
kutekeleza ahadi yako ,kinachofuata
sasa ili makubaliano yetu yatimie
nataka Yasmin na Tariq waondoke
hapo nchini Tanzania haraka
iwezekanavyo.Nataka kablaya saa
kumi na moja jioni ya leo wawe tayari
wamefika Mogadishu.” Akasema
Habib
“Kila kitu kimekwisha andaliwa
Habib na ndege watakayoondoka
nayo iko tayari .Kitu ninachokuomba
ni kuyaheshimu makubaliano yetu”
“ Usijali kuhusu hilo.Kila kitu
kitafanyika kama tulivyokubaliana”
akasema Habib na kukata simu.Rais
akafuta jasho usoni na kusema
“ Kila kitu kimekwenda vizuri na
tayari ndege inawasubiri kwa ajili ya
kuwapeleka Mogadishu.Vijana wangu
watawapeleka uwanja wa ndege
tayari kwa kuondoka hapa
nchini.Ndege ni salama na haina
tatizo lolote.” Akasema rais.
“Tunashukuru rais kwa kukubali
kutuachia huru na kwa huduma nzuri
tulizopata kuanzia jana.Lakini kabla
hatujaondoka kuna vitu ningeomba
umtume mmoja wa vijana wako
akaninunulie.Sina mavazi ,sina
vipodozi naonekana kama mzimu”
akasema Yasmin na rais akainuka kwa
ajili ya kuondoka.Yasmin akampa
Tariq ile hati ya muungano aendelee
kuipitia wakati akimsindikiza rais.
“Mheshimiwa rais,jana ulitaka
kufanya makubaliano na mimi
kuhusu kurejeshewa mwanangu
.Nitafanya kama unavyotaka kwa ajili
ya mwanangu lakini kuna kitu
nitakiomba.” Akasema Yasmin
wakiwa nje .Ernest akatabasamu kwa
mbali an kuuliza
“ Unahitaji nini?
“ Nahitaji kijana utakayemtuma
aniletee mavazi na vipodozi aniletee
pia bastora mbili ,simu na fedha
taslimu shilingi milioni
kumi.Ukinipatia hivyo viwili basi
ukae ukisubiri simu yangu ili unipatie
mwanangu na mimi nikupatie hati
yako ya muungano.Uko tayari kwa
hilo?
“Sina tatizo na hilo hata
kidogo.Nitaongozana na kijana mmoja
nitampatia vitu hivyo atakuletea ila
tafadhali naomba uwe mkweli.”
“Namuhitaji sana mwanangu
kuliko kitu chochote kwa hiyo niko
tayari kufanya jambo lolote
kumpata.Huyo kijana utakayemtuma
aniletee vitu hivyo aweke vitu hivyo
katika begi sitaki Tariq afahamu
chochote ” akasema Yasmin na kurejea
ndani ,rais na walinzi wake
wakaondoka.Wakiwa garini rais
akajaribu tena kupiga simu ya
Austin.Simu ikaita bila
kupokelewa,akapiga tena simu ya Job
nayo ikaita bila kupokelewa
“ Hawa vijana wana tatizo gani
leo? Namuhitaji sana Maria ili pindi tu
Yasmin atakapopiga simu basi niwe
tayari kwa mabadilishano .Ngoja
kwanza nimalize suala kubwa la leo
halafu nitawatafuta” akawaza rais.
Alirejea ikulu na moja kwa moja
akaenda chumbani kwake na
kuwasiliana na Jenerali Lameck
Msuba akamtaarifu kuwa tayari
amekwisha ikabidhi hati ya
muungano kwa Yasmin kwa hiyo
maandalizi ya tukio la jioni yaendelee.
“Zimebaki saa chache sana kwa
Tanzania kutikisika.Kuna wakati hofu
inaniingia lakini sina namna nyingine
lazima nifanye hivi.Lazima niisafishe
nchi.Lazima Alberto’s wote niwafagie
,na mwisho wao ni leo.” Akaendelea
kuwaza huku akinywa mvinyo mkali
 
SEHEMU YA 18: SEASON 5

Baada ya Amarachi kuondoka
kwenda kufuatilia majibu ya kipimo
cha vinasaba ,Austin na Job
wakaelekea chumbani kwa Maria.
“hallo Maria’ akasema Austin
huku akivuta kiti na kuketi,Maria
akamtazama na kusema
“ Nitafungwa katika kiti hiki
mpala lini? Hamuwezi kuniachia huru
walau kwa saa mbili? Tafadhali
Austin nimechoka na mateso haya
,nifungueni japo kwa saa moja niweze
kupumzika na mateso haya
mnayonipa.” Akasema Maria huku
machozi yakimtoka
“ Maria hata mimi sipendi
kukuona ukiwa katika hali hiyo na
sikutegema kabisa kama siku moja
naweza kushuhudia ukifanyiwa hivi
lakini siwezi kurudia kosa la
kukuacha huru hata kwa dakika
kumi.Tuacheni na hayo ,nimerudi tena
kuja kuzungumza nawe.Ulisikia
mazungumzo yangu na mama yako
na endapo atatekeleza kile
anachokisema basi itakuwa ni salama
yako.I swear I’ll let you and your
mother go.lakini endapo hatatekeleza
mambo aliyoyasema utakuwa ndio
mwisho wako.”akanyamaza
akamtazama Maria kisha akasema
“ Wakati tunasubiri mama yako
apige simu kama alivyoahidi nataka
kufahamu vitu vichace toka
kwako.Nimeishi nawe kwa miaka
kadhaa na hata siku moja sikuwahi
kudhani umewahi kuigusa silaha
yoyote .Wapi umejifunza matumizi ya
silaha? Akauliza Austin na kumtaka
Job amfungue maria mikono
“Austin mimi na wewe tumeishi
kama wapenzi kwa miaka kadhaa
lakini hiki kilichotokea kilikuwa ni
bahati mbaya.Sikutegemea kabisa
jambo kama hili
lingekutokea.Sikutegemea kama
ningeweza kuzamisha risasi nne
katika mwili wako.Ninaumia sana kila
nikilifikiria hili suala ,lakini tayari
limekwisha tokea na kuharibu kila
kitu ambacho tulikijenga kama
wapenzi.Kitu kimoja tu ambacho
naomba ufahamu ni kwamba pamoja
na yote yaliyotokea lakini toka ndani
ya moyo wangu nilikupenda kwa
dhati na nitaendelea
kukupenda.Sijawahi kukutana na
mwanaume niliyempenda kama
wewe.” Akatulia akamtazama Austin
usoni na kuendelea.
“Kwa sababu ninakupenda
sikutaka uufahamu upande wangu wa
pili lakini kwa sasa hakuna sababu ya
kuendelea kukuficha tena kwani
tayari kila kitu unakifahamu .Mama
alipogundua kwamba anatafutwa
akamatwe alinisafirisha kwenda kwa
mjomba wangu anaitwa Abdulshafir
anayeishi nchini Syria.Wakati mama
anakamatwa tayari alikuwa
ameachana na baba .Niliishi Syria kwa
miaka mitano na hapo ndipo
nilipoanza mafunzo katika kikundi
cha dola ya kiislamu au IS kwa lengo
la kuja kumkomboa mama
yangu.Baadae nilimtafuta baba
ambaye kwa wakati huo alikuwa
anaishi Afrika kusini nikaanza kuishi
naye hadi sasa.Kwa muda wote
nilioishi na baba hakuwahi kugundua
kama mimi ni mfuasi wa
IS.Nimekuwa mfuasi wa IS kwa siri
kwa muda mrefu na lengo kubwa la
kuja Dar es salaam lilikuwa ni
kumtafuta mama yangu ambaye
alikamatwa akiwa katika harakati za
kueneza kikundi hiki afrika
mashariki.Sifurahii matendo maovu
yanayofanywa na kikundi hiki kwa
kuua watu hovyo na kusababisha
mamilioni ya watu wasio na hatia
kuteseka lakini lengo kuu la kujiunga
nao ni ili kumpata mama yangu.Kwa
kuwa tayari mama yangu yuko huru
tafadhali Austin fanya kila uwezalo ili
mimi na mama tuweze kutoweka na
kwenda kuishi mbali kabisa na IS
kama mama alivyoomba. Nataka
kuanza maisha mapya na mama na
hata ikiwezekana baba pia unaweza
ukamuachia huru tukaambatana naye.
Mama ameteseka kwa miaka zaidi ya
kumi gerezani lakini hawajafanya
juhudi zozote za kumtoa hadi
nilipoamua kuja mwenyewe na ndiyo
maana yuko tayari kufanya lolote kwa
ajili ya kuanza maisha mapya” Maria
akanyamaza baadaya simu ya Austin
kuita.Alikuwa ni Amarachi
“ Hallo Amarachi”
“ Austin tayari nimepata majibu
na niko njiani ninarejea”
“ Good.Umesoma kilichomo
ndani ya hayo majibu?
“ Hapana bado sijasoma
chochote”
“ Safi sana.Tunakusubiri ili
tuweze kujua nini kimetokea”
akasema Austin na kumgeukia Job
“ Amarachi tayari ana majibu ya
kipimo cha vinasaba,yuko njiani
anakuja” akasema Austin na
hawakuendelea kumuhoji tena Maria
wakatoka
 
SEHEMU YA 19: SEASON 5

Inakaribia saa tisa za alasiri lakini
bado Monica alikuwa amejilaza
kitandani.Hakwenda kokote siku
hii.Hakujisikia kufanya kazi yoyote
katika bali alishinda amejifungia
chumbani kwake.Kichwa chake kilijaa
mawazo mengi.Kwanza ni kuhusu
msiba wa Pauline,pili ni majadiliano
kati ya ujumbe wa David na wazazi
wake yaliyokwenda vizuri na
kuashiria mwanzo mzuri wa kuelekea
katika kile wanachokitarajia yaani
kufunga ndoa.Aliwaza mengi
kuhusiana na maisha yake mapya
anayotarajia kuyaishi akiwa na David
zumo tajiri namba moja
afrika.Ukiacha hayo kikubwa
kilichokaribia kumpasua kichwa ni
kitendo cha kutokuziona siku
zake.Kutwa nzima alikuwa na
kompyuta yake akijaribu kusoma na
kuelewa zaidi kuhusiana na masuala
ya hedhi.Kikubwa alichokuwa
anakitafuta ni sababu za kukosa
hedhi.Alisoma mambo mengi na
akazidi kuchanganyikiwa
“Nimesoma sababu kadhaa za
mwanamke kushindwa kuziona siku
zake lakini naona kama hizi zote
haziendani na mimi.Mpangilio wa
siku zangu haujawahi kubadilika na
kwa mujibu wa mpangilio nilitakiwa
tayari niwe nimeziona lakini mpaka
leo hii bado sijaona kitu.Kuna jambo
moja linanipa wasi wasi mno na
ambalo sitaki hata
kuliwaza.Yawezekana nimeshika
ujauzito.Imenilazimu kuanza kufikiri
hivi kwani sioni sababu yoyote ya
kushindwa kuziona siku zangu na
sijawahi kutokewa na hali hii hata
mara moja hii ni mara ya
kwanza.Nakumbuka hatukutumia
kinga yoyote nilipofanya mapenzi na
David na hili ni kosa kubwa
nililifanya.kwa nini sikuwaza jambo
kama hili linaweza kunitokea?
Akawaza Monica na kuinuka akakaa
na kushika kichwa.
“ Baada ya wiki moja nitapima ili
nijue kama ni kweli nitakuwa na
mimba au kuna sababu nyingine
iliyosababisha nisizione siku
zangu.Kama nitakuwa mjamzito oh
my gosh ! itakuwa ni aibu kubwa
kwangu na kwa wazazi.Nimejitunza
kwa muda huu wote lakini
nimenaswa katika tundu bovu.Najua
David atafurahi sana kusikia habari
hizi kama kweli nitakuwa na mimba
lakini haikuwa katika mipango yangu
kushika mimba kabla ya ndoa.Ni aibu
kubwa kwangu” akawaza Monica
“ Hata hivyo naamini David
hataweza kuwa na wasi wasi na mimi
endapo kweli nitakuwa mjamzito
kwani yeye ndiye aliyenitoa usichana
wangu”
Monica aliwaza mno kuhusu
jambo hili na mwisho akaamua
kumshirikisha mama yake.Akampigia
simu akamueleza kila kitu na mama
yake akamshauri asiogope bali asubiri
baada ya wiki moja akapime ili
kuthibitisha kama kweli ni
mjamzito.Baada ya kuzungumza na
mama yake, Monica akawa na ahueni
japokuwa bado kichwa kiliendelea
kugonga kwa mawazo mengi
aliyokuwa nayo.
Taarifa aliyopewa na mwanae
Monica ilimstua sana Janet.
“Kwa maelezo niliyopewa na
Monica ni lazima atakuwa
mjamzito.Nimekuwa nikisifiwa jiji
zima kwa kumlea vyema Monica kwa
maadili mazuri na kumfanya licha ya
umaarufu wake asiwe na kashfa
zozote wala kusemwa au kuandikwa
vibaya.Hiki kilichotokea kitaharibu
kabisa ile taswira yote nzuri ya
Monica.Nini kifanyike? Tuiharibu
mimba hiyo angali bado changa?lakini
huu utakuwa ni uuaji na sina hakika
kama hata Monica mwenyewe
atakubaliana na hilo ,nini basi
kifanyike? Akajiuliza bi janet akiwa
ofisini kwake
“ hapa hakuna ujanja lazima
kuharakisha mipango ya ndoa yao na
David Zumo.Potelea mbali kama mke
wake amefariki hivi karibuni lakini
lazima ndani ya muda mfupi awe
amemuoa Monica .Hapo mwanzo
nilikuwa mpinzani mkubwa wa ndoa
kati ya David Zumo na Monica lakini
kwa sasa sina ujanja tena lazima
nikubali na lazima nisukume mambo
yaende haraka haraka ili Monica
asigundulike ana mimba akiwa bado
nyumbani.Nadhani kuna umuhimu
wa kumshirikisha pia baba yake ili
afahamu kinachoendelea kwani hata
yeye mwenyewe hakuwa tayari
Monica aolewe na David Zumo ili
kama kuna tofauti zozote na David
Zumo wazimalize kwani hakuna
namna ya kufanya lazima Monica
aolewe na David ” akawaza Janet na
kuchukua simu akampigia Ernest
Mkasa
“ Hallow Janet habari yako?
“ Habari nzuri Ernest.”
“Nafurahi kusikia hivyo.Kuna
habari gani?
“ Tunaweza kuonana leo ? Kuna
jambo la muhimu nataka
tuzungumze”
“ Kwa sasa kuonana nawe
itakuwa vigumu sana nimekuwa na
ratiba ngumu mno kutokana na
mambo yanayoendelea hivi sasa.kama
una jambo lolote unalotaka kunieleza
niambie sasa hivi katika simu.”
Akasema Ernest
“ Sawa Ernest kwa kuwa ni
jambo ambalo haliwezi kusubiri ,ngoja
tu nikueleze.Ni kwamba nimetoka
kuzungumza na Monica simuni muda
mfupi uliopita na kuna jambo
amenieleza ambalo nimeona
nikushirikishe na wewe pia.Ni kuhusu
yeye na David Zumo.” Akasema Janet
na Ernest akanonekana kustuka
kidogo
“ Kuna nini kimetokea kati yake
na David ? akauliza
“ Hivi majuzi alikwenda
kumtembelea David Zumo huko
Kinshasa kama unavyofahamu kuwa
wawili hawa tayari wana
mahusiano.Akiwa huko kwa mujibu
wa maelezo yake walifanya mapenzi
bila kutumia kinga na ana wasi wasi
anaweza kuwa mjamzito.Kwa
maelezo aliyonipa kuna kila sababu ya
kuamini lazima Monica atakuwa
mjamzito.Kwa hiyo kuna kila sababu
ya kuhakikisha ndoa yake na David
inafanyika tena haraka iwezekanavyo
kabla mimba hiyo haijawa kubwa na
kujulikana.Itakuwa ni aibu kwetu na
kwa Monica pia.Nimeona nikujulishe
suala hili mapema kwani awali
haukupendezwa kusikia Monica na
David wana mahusiano kwa hiyo
nataka mzimalize tofauti zenu ili
David amuoe Monica.Ni hilo tu
nililotaka kukushirikisha ili hata kama
ikitokea ukasikia kwa watu wakisema
usistuke.” Akasema Janet
“ Dah ! nimekosa neno la kusema
Janet.Nashukuru kwa taarifa hizi
.Naomba nilitafakari hili suala halafu
nitakujulisha nini mawazo yangu”
akasema rais na kukata simu
Ernest Mkasa akagonga meza
kwa hasira baada ya kumaliza
kuzungumza na Janet
simuni.Akainamisha kichwa akafikiri
kwa muda na kujikuta akitamka kwa
sauti
“No ! that wont happen.Siwezi
kuruhusu David na Monica
wakaoana.Ngoja kwanza nisubiri
majibu ya kipimo na endapo kipimo
kitathibitisha Monica ni mwanangu
basi hakutakuwa na ndoa kati yake na
David.”akawaza Ernest akachukua
simu na kumpigia mmoja wa vijana
wake waliowapeleka akina Yasmin
uwanja wa ndege ambako
kuliandaliwa ndege maalum ya
kuwapeleka Mogadishu akauliza
endapo tayari wameondoka.
“ Tayari wameondoka mzee
kama saa moja iliyopita.Kila kitu
kimekweda vizuri .”
“ Nafurahi kusikia hivyo.Sasa
waandae vijana kwa ajili ya kazi
nyingine nitakayowapeni” akasema
rais na kukata simu kisha akatazama
saa yake.
“Muda unakwenda kwa kasi
kubwa.bado saa chache sana moshi
mweusi utande” akawaza
 
SEHEMU YA 20: SEASON 5

Yasmi na Tariq walifika uwanja
wa ndege wakisindikizwa na vijana
maalum waliotumwa na rais.Baada ya
kuingia ndegeni kila mmoja akaketi
katika kiti chake na haikuchukua
muda mrefu ndege ile maalum ya
kifahari ikapaa na ilipokaa sawa
angani Yasmin akafungua begi lake
dogo lililokuwa na mavazi na kutoa
bastora mbili.Akamuelekezea Tariq
ambaye alihisi ni utani.
“Yasmin umepata wapi bastora
hizo? Kwa nini hukunieleza kama una
silaha? Akauliza Tariq
“ Usipige ukelele wala usifanye
fujo zozote.Utafuata kile
nitakachokuamuru” akasema Yasmin
“ Yasmin !! akasema Tariq kwa
mshangao.Yasmin akakata mmoja wa
mkanda wa kiti na kumfunga Tariq
miguu na mikono kisha akamjaza
kitambaa mdomoni.Akaelelekea
katika chumba cha marubani
akagonga mlango.Mlango
ukafunguliwa na marubani wakastuka
walipojikuta wakitazamana na
bastora mbili
“hello gentlemen.There is a
change of plan.Tutatua Unguja badala
ya Mogadishu.Mtaomba kutua kwa
dharura baada ya ndege kuwa na
hitilafu” akasema Yasmin.wale
marubani walionekana kutaka kuleta
ubishi
“ tafadhali nawaonya msilete
ubishi.Sina tatizo na ninyi
.Ninachotaka mtue unguja na
mtakuwa salama .Msitoe taarifa
sehemu yoyote kama mmelazimishwa
mtue Unguja.Mkitii maelekezo yangu
mtabaki salama lakini mkiniletea
ubishi nitawafumua vichwa vyenu
kwa risasi na nitaendesha mimi
mwenyewe.Fuateni hayo
niliyowaelekeza” akasema Yasmin na
ndege ikabadili uelekeo ikaelekea
Zanzibar.
 
SEHEMU YA 21: SEASON 5

Mishale ya saa ilionyesha ni saa
kumi na moja za jioni Jenerali lameck
Msuba alipowasili katika makazi ya
rais na wakaelekea katika chumba cha
maongezi ya faragha.
“Mheshimiwa rais muda
unakaribia sana.Vijana wako tayari na
nimetoka kuwasiliana nao muda si
mrefu wanasubiri kauli yako tu.Uko
tayari? Akauliza Lameck.Ernest
Mkasa akafikiri kwa muda na kusema
“Tumekula ng’ombe mzima
hatuwezi kushindwa kumaliza hapa
tulipofika.Tell them to go ahead with
the plan” akasema rais na Lameck
akawasiliana na makamanda wake
akawapa ruhusa ya kuendelea.Bila
kupoteza muda wakaondoka ikulu
kuelekea mahala ambako rais
amepanga kukutana na
Alberto’s.Ilionyesha kwamba rais
anakwenda kwa maongezi binafsi na
wageni wake..
Mkuu wa majeshio ambaye naye
alikuwepo katika msafara ule alikuwa
anawasiliaan na makamanda wake
kujua kila kilichokuwa
kinaendelea.Akiwa garini rais alikuwa
anafuta jasho mara kwa mara na
alikuwa kimya kabisa.
Mita kadhaa kabla ya msafara wa
rais kufika pale hotelini,kikasikika
kishindo kikubwa sana na eneo lote
likatikisika kama vile kumetokea
tetemeko la ardhi.Mara tu kishindo
kile kilipotokea, kwa wepesi wa aina
yake makomando wanaomlinda rais
waliruka toka katika gari lao
wakavunja vioo katika gari la rais na
kumtoa rais wakamuingiza katika gari
lao lakini kabla hawajaondoka
kikasikika kishindo kingine cha pili na
hiki kikawa kikubwa zaidi.Gari la
makomando walinzi wa rais
likaondoka kwa kasi kubwa
likifuatiwa na magari mengine
yaliyokuwapo katika msafara
ule.Moshi mzito mweusi ulitanda
katika eneo lile.Hoteli ilikuwa
imesambaratishwa..

RAIS ERNEST AMEKUBALI
KUITOA HATI YA MUUNGANO
WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR
KWA ALSHABAAB JE MIPANGO
YAKE ITAFANIKIWA?
TAA NYEKUNDU
INAMUWAKIA AUSTIN KUHUSU
MWENENDO WA RAIS NA
WAKATI HUO RAIS ANA
MIPANGO YA KUWAMALIZA
AKINA AUSTIN NINI KITATOKEA ?
MIPANGO YA NDOA YA
DAVID ZUMO NA MONICA
INAENDELEA WATAFIKIA LENGO
LAO?
USIKOSE SEASON 6
ITAKAYOKUWA NA MAJIBU YA
MASWALI MENGI…
 
Halafu kuna raia wanachonga sana humu, ili hali nilshaweka bandiko kama Lege hatatupia mi nitatupia siku ya leo {Jumatatu}.
Season 6, ikitoka tutaweka namba ya mwandishi tumchangie kwa sh.3,000...ili wale wachongao sana na wao wapate kumchangia yule aumizaye kichwa ili kutupatia burudani.
 
Halafu kuna raia wanachonga sana humu, ili hali nilshaweka bandiko kama Lege hatatupia mi nitatupia siku ya leo {Jumatatu}.
Season 6, ikitoka tutaweka namba ya mwandishi tumchangie kwa sh.3,000...ili wale wachongao sana na wao wapate kumchangia yule aumizaye kichwa ili kutupatia burudani.
Mkuu kama nimekuelewa season ya 6 utauzwa kwa sh 3000 au itawekwa hapa? Fafanua mkuu..

Asante kwa kuiweka kama ulivyo ahidi....
 
Halafu kuna raia wanachonga sana humu, ili hali nilshaweka bandiko kama Lege hatatupia mi nitatupia siku ya leo {Jumatatu}.
Season 6, ikitoka tutaweka namba ya mwandishi tumchangie kwa sh.3,000...ili wale wachongao sana na wao wapate kumchangia yule aumizaye kichwa ili kutupatia burudani.
Asante mbududa ubarikiwe jamaan
 
Asante sana Mbududa, asante mkuu, majibu bado, kumbe kuna season 6, huenda ni series hii. Ni tamu sana.

Nimeanza kuichukia kazi ya usalama, wema, bidii, weledi, uaminifu, ujasiri na ushujaa wa Austin, unakaribia kumwangamiza. Mzee Pantileo lazima atauawa.

Austin for president, maana ndiye atakaeirudisha hati ya muungano.
 
Back
Top Bottom