QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

hii hapa ngoma saba usiku na dakika 12.....
alamsiki....hiyo mida ya wanga....ndio hii kabda ...labda viranja wao..!!!...
 
SEHEMU YA 71



Nimetangaza vita lakini naamini
nitashinda kwani ninafanya jambo sahihi
kwa nchi na watu wake.Siko tayari tena
kuona taifa likiangamia kwa kupitia
mikono yangu.I must stand up and fight
.I’m doing this for Monica.Sitaki watoto wa
mtoto wangu waje kuishi katika taifa
ambalo nimeshiriki katika kuliharibu.It’s
time to make things right.Bado
sijachelewa ninayo nafasi ya kufanya
mabadiliko “ akawaza Ernest halafu
akaanza kuandika hotuba yake.
Aliandika
machache
atakayoyazungumza ,akaipitia tena
hotuba yake na alipohakikisha
imekamilika akatoka mle katika chumba
cha kusomea akaenda chumba cha
kulala.Mke wake hakuwepo chumbani.Juu
ya meza kulikuwa na karatasi yenye
ujumbe
“ Stop what you are trying to do.You
are going to turn the country upside
down.Usithubutu kuhutubia taifa usiku wa
leo”
Ulikuwa ni ujumbe toka kwa
Agatha.Ernest akaichana chana karatasi
ile na mara taratibu akasikia mlango
ukifunguliwa.Akageuka
akajikuta
akaitazamana na watu wawili waliovalia
suti nyeusi na kila mmoja alikuwa na
bastora mkononi iliyofungwa kiwambo
cha kuzuia sauti.Ernest hakuwafahamu
watu wale na hakuwahi kuwaona hata
mara moja.Anawafahamu walinzi wake
wote lakini jamaa hawa waliosimama
mbele yake ilikuwa ni mara ya kwanza
kuwaona.Alihisi kutetemeka mwili
akajikaza asionyeshe woga wa aina yoyote
“ Hey ! who are you?? Akauliza
Ernest kwa ukali
“ Huna haja ya kutufahamu
mheshimiwa rais.Tumesimama hapa
mbele yako kwa heshima kubwa
kukutaarifu kwamba usithubutu
kulihutubia taifa usiku wa leo.Hii ni amri
na hakuna kuipuuza.Endapo ukipuuzia
basi unajua nini kitatokea.Hatuna maneno
mengi kwa leo kwani tayari ujumbe
umefika na sisi tuaondoka” akasema
mmoja wao na wote wakaingiza bastora
zao katika makoti wakafungua mlango na
kuondoka wakimuacha Ernest akiwa bado
amesimama akitetemeka .Alihisi miguu
kuishiwa nguvu akakaa kitandani
“ Vita imeanza.Nilitegemea mambo
kama haya lazima yajitokeze na kweli
yameanza.Alberto’s tayari wamekwisha
weka mizizi yao kila sehemu na wanaweza
wakafanya jambo lolote muda wowote
wautakao na ndiyo maana watu wale
wameweza kuuvuka ulinzi wote wa ikulu
hadi wamefanikiwa kuingia katika
chumba cha rais.Huu ni udhaifu mkubwa
sana wa idara ya usalama .Sintomueleza
mtu juu ya hiki kilichotokea lakini lazima
nichukue hatua za haraka.Watu wale
wangeweza hata kuniua bila ya walinzi
wangu kuwa na habari.Nitamueleza Austin
jambo hili ili kwa pamoja tujue namna ya
kufanya.” Akawaza na kujifuta jasho
jembamba la uoga lililomtoka
“ Wamenitetemesha kweli wale
jamaa lakini pamoja na hayo usiku wa leo
lazima nilihutubie taifa.Najua hawawezi
kuniua kwa sasa kwani bado wanajiuliza
sababu ya mimi kuchukua maamuzi yale”
Akawaza Ernest na kuwaita mkurugenzi
wa idara ya mawasiliano ikulu na mlinzi
wake mkuu akawapa maelekezo ya
kuhakiki usalama katika ukumbi wa
habari ikulu.
 
SEHEMU YA 72



ufuatia agizo la rais waandishi wote
wa habari wakatolewa nje ,ukumbi
ukakaguliwa na wakaruhusiwa kuingia
mmoja mmoja huku wakikaguliwa .Baada
ya kuhakikisha ukumbi uko salama ,rais
akataarifiwa kuwa sasa anaweza
kulihutubia
taifa.Ernest
mkasa
akajitazama katika kioo akarekebisha tai
yake na kuvuta pumzi ndefu
“ I must do this.Litakalotokea na
litokee tu.” Akawaza Ernest akatoka mle
chumbani na kabla ya kuingia katika
chumba habari akaandaliwa muonekano
wake na alipokuwa tayari akaruhusiwa
kuingia katika chumba cha habari
“ Please help me God ! Help me do
the right thing for this country” akaomba
kimya kimya huku akitembea kuingia
katika chumba cha habari.karibu vituo
vyote vikubwa vya redio na televisheni
vilisimamisha matangazo yao kupisha
hotuba hii ya rais iliyokuwa inasubiriwa
sana na wananchi
Milango ya chumba cha habari
kilichokuwa na ulinzi mkali sana
ikafunguliwa na rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania akajitokea
akaenda
kuketi
katika
kiti
alichoandaliwa.Tofauti na ilivyozoeleka
kuwa hotuba ya rais huwa imeandaliwa
safari hii aliitoa karatasi mfukoni
aliyoiandaa yeye mwenyewe na kuanza
kuisoma
“ habari za usiku huu ndugu
watanzania wenzangu”
“ Awali ya yote ninapenda nichukue
nafasi hii kumshukuru mwenyezi Mungu
mwingi wa rehema kwa kuniwezesha kuja
mbele yenu na kuongea nanyi kuhusiana
na masuala kadhaa muhimu kwa taifa
letu.Kuna mambo kadhaa makubwa kwa
taifa letu ambayo yamenilazimu nije mbele
yenu leo”
akanyamaza halafu akaendelea
“ Kwa muda wa zaidi ya mwaka
mmoja sasa tumekuwa katika mchakato
wa kuandaa muswada wa haki za
binadamu .Uandaaji wa muswada huo
umekuwa na changamoto nyingi na kubwa
ni kupingwa kutoka kila kona na makundi
mbali mbali ya wananchi,viongozi wa dini
n.k.Ndani ya muswada huo kuna vipengele
kadhaa vinavyopigiwa kelele sana na
wananchi ambavyo vinatambua haki za
makundi ya watu wanaojihusisha na
mapenzi na ndoa za jinsia moja.Vile vile
kuna haki ya kutoa mimba pamoja na
mambo mengine kadhaa ambayo
yanakwenda kinyume kabisa na tamaduni
zetu na hata mafundisho ya dini zetu.”
Akanyamaza tena halafu akaendelea.
“ Kumekuwa na shinikizo kubwa
toka kwa nchi tajiri , zikizitaka nchi zote
za afrika kuhakikisha kwamba zinapitisha
sheria za kutambua haki kadhaa za
binadamu na hapa wanalenga makundi
hayo niliyokwisha yaeleza.Nchi nyingi za
Afrika tayari zimekwisha pitisha sheria
hiyo na chache ikiwemo Tanzania bado
hatujafanya hivyo japokuwa sisi tulikuwa
katika mchakato wa kuupeleka bungeni
muswada wa sheria hiyo ili kutimiza
matakwa hayo ya nchi tajiri.Mchakato wa
kuandaa muswada huo umekamilika na
unategemewa kuwasilishwa katika kikao
kijacho cha bunge lakini kumekuwa na
shinikizo kubwa toka kwa wanachi,wazee
kwa vijana,wake kwa waume wakipinga
muswada huo kupelekwa bungeni.Katika
kila mkoa kumeanzishwa kampeni kubwa
za kupinga muswada huu na tayari
makundi ya watu wameanza kujiandikisha
 
SEHEMU YA 73



kwa ajili ya kuelekea bungeni Dodoma
kuupinga muswada huo” akanyamaza
kidogo na kuendelea
“ Binafsi kama rais wenu nimekuwa
kimya nikijaribu kulitafakari suala hili
kwa kina na kusikiliza maoni ya watu
mbali mbali ,viongozi wa dini n.k na leo hii
nimefanya maamuzi yafuatayo
1.
Nimeona muswada huo hauna tija
kwa taifa letu bali lengo lake ni
kuibomoa jamii yetu kwa kutimiza
matakwa ya mataifa makuwa
ambayo yametutaka tufanye hivyo
kwa kisingizio cha misaada.Taifa
letu limejengwa katika misingi na
tamaduni zake.Waasisi wetu
wametuachia taifa lenye harufu
nzuri linalopendwa na
kuheshimika lakini tunataka
kulifanya linuke uvundo kwa
mambo haya ya hovyo tunayotaka
kuyabariki.Mimi kama rais wenu
siko tayari kuwa sehemu ya laana
hiyo kwa hiyo natangaza kuwa
nimeufuta muswaada huo na
kuufunga kabisa mjadala
wake.Sitaki kusikia kuanzia sasa
mtu au kikundi cha watu
wakiendeleza mjadala huu.Badala
yake serikali itapeleka bungeni
muswada wa kutambua vitendo
vya mapenzi ya jinsia moja au
utoaji mimba au utumiaji wa
madawa ya kulevya ni kosa la jinai
na yeyote atakayekutwa akifanya
mambo hayo afungwe
gerezani.Kwa hiyo ndugu zangu
hakuna tena haja ya maandamano
kwani sauti zenu tayari
zimesikika.”
Akanyamaza na
kuendelea
2.
Kulipa uzito suala la
nililolizungumza hapo
juu,nimeamua kutengua uteuzi wa
waziri mkuu na kulivunja baraza
la mawaziri .Sababu kubwa
iliyonifaya nivunje baraza la
mawaziri ni utendaji kazi
usioridhisha.Katika kikao kijacho
cha bunge nitawasilisha jina la
waziri mkuu mpya na wabunge
watalipigia kura na baada ya
kuidhinishwa na bunge mimi na
huyo waziri mkuu mpya tutaunda
baraza jipya la
mawaziri.Ninawaomba ndugu
zangu watanzania tuendelee kuwa
watulivu katika kipindi hiki
ambacho taifa linapitia katika
majaribu makubwa.Tushikamane
na tuliombee taifa letu lizidi kuwa
imara na salama
Mungu ibariki Afrika
Mungu ibariki Tanzania
Ahsanteni kwa kunisikiliza
Ernest Mkasa rais wa jamhuri ya
Muungano wa tanzania akamaliza hotuba
yake akakunja karatasi zake akaziweka
katika mfuko wa koti akainuka na
kuzungukwa na walinzi wake
akaondoka.Alipotoka ndani ya chumba
kile cha habari akamuelekeza mlinzi wake
mkuu Evansi aweke vijana tayari kwani
 
SEHEMU YA 74


anaondoka muda si mrefu kuelekea
hotelini kwake
Ernest akaingia chumbani kwake
akakaa kitandani,akavuta pumzi ndefu
“ Oh thank you lord.”
“ I did it.Nimefanikiwa kulihutubia
taifa na ninaamini hotuba hii itafanikiwa
kuleta utulivu nchini.Hotuba hii
naichukulia kama tamko la vita .Kuvunjwa
kwa baraza la mawaziri ni pigo lingine
kubwa kwa Alberto’s kwani karibu
mawaziri wote ni watu wao.Nitaendelea
kuwaondoa katika kile sehemu
walikootesha mzizi wao.Hii ni vita ngumu
na ya hatari na ninapaswa kujilinda sana
pamoja na kumlinda Monica.Kama kweli
ni mwanangu nitamlinda kwa nguvu
zote.”akawaza wakati akibadili mavazi
kwa ajili ya kuelekea hotelini kwake.
Alipobadili mavazi akaondoka
kuelekea hotelini.Kichwa chake kilijaa
mawazo mengio mno.Alipofika hoteini
akaelekea katika chumba chake na
kumuita Mukasha
“ Mheshimiwa hotuba yako imekuwa
gumzo kila mahali.Nimekuwa nafuatilia
mtandaoni watu wote hawaamini
kilichotokea.Unastahili
pongezi
mheshimiwa kwa maamuzi haya ya
kishujaa uliyoyafanya.Unapongezwa na
kila mwananchi.Kwa hiki ulichokifanya
mheshimiwa rais kinakusafishia njia ya
kupita kirahisi katika uchaguzi
ujao.Hautakuwa na haja ya kufanya
kampenzi
kubwa”
akasema
Mukasha.Ernest akatabasamu kwa mbali
na kusema
“ Mukasha sifikirii tena kuwania
urais kwa kipindi kingine.”
“ Mheshimiwa rais ni mapema mno
kutoa tamko kama hilo.Wewe bado ni rais
mwenye nguvu na wanachi wanakupena
na kukukubali sana” akasema Mukasha
“ Mukasha tayari nimekwisha fanya
maamuzi kwamba sintogombea tena
katika kipindi kingine.Nitakapomaliza
kipindi changu sitaki tena”
“ Kwa nini umechukua maamuzi
hayo mheshismiwa rais? Bado una nguvu
sana kisiasa .Tafadhali nakushauri
mheshimiwa rais usiwaze jambo kama
hilo.Unategemewa sana kukivusha chama
katika uchaguzi ujao.Wewe ni ng........”
“ Naomba nikukatishe Mukasha
mimi si mwanasiasa na wala si chama
kilichoniweka madarakani kwa hiyo
chama hakipaswi kunitegemea mimi
nikivushe katika uchaguzi ujao” akasema
“ Mheshimiwa rais najaribu sana
kutaka kukuelewa lakini nashindwa”
akasema MUkasha

Huwezi
kunielewa
Mukasha.Tuachane na hayo nimekuita
hapa kukueleza jambo moja muhimu
kuwa hotuba ile niliyoitoa leo ni tamko la
vita “
“ Vita na nani mheshimiwa rais?
Akauliza Mukasha
“ Siwezi kukueleza sasa hivi lakini
nataka ufahamu kuwa kwa hivi sasa wewe
ni mtu pekee kati ya watu
wanaonizunguka ninayekuamini.Please
don’t evey betray me.I need you so much
in this.Hata ikitokea kwa gharama ya uhai
wako usimueleze mtu yeyote kuhusu
Austin.Mukasha kuna mambo makubwa
yanaendelea hivi sasa na nitakufahamisha
wakati mwingine”
“ Mheshimiwa unaniogopesha”
akasema Mukasha
hapana Mukasha,sikuogopeshi ila
huo ndio ukweli.waandae vijana tunaenda
kuonana na Austin” akasema Ernest
 
SEHEMU YA 75


KINSHASA – DRC
Wahudumu
waliokuwa
wanamremba Monica walimaliza kazi yao
na kuondoka.Monica akasimama mbele ya
kioo akajitazama namna alivyopendeza
akataasamu
“ I hope I’m doing the right
thing.Nimeshindwa kabisa kulishinda
jaribu hili na kumpa David mwili
wangu.Sikuwa nimepanga kufanya
mapenzi kabla ya ndoa lakini kwa David
nimeshindwa kujizuia.Nahisi labda David
kuna nguvu anatumia kunilainisha kwani
I’m not the same Monica anymore.Kila
anachokisema
David
ninajikuta
nakubali.Ninajishangaa kwa namna
nilivyobadlika.” Akawaza Monica
“ Kingne ni kwamba baada ya
kufanya mapenzi jana leo nahisi hamu
kubwa ya kufanya tena.Naona kama vile
David anaanza taratibu kuniingia
akilini.Ngoja tu niolewe naye kwani
anaonekana ni zaidi ya mwanaume yule
niliyekuwa namuhitaji katika maisha
yangu.Siw.....”
Monica
akatolewa
mawazoni na mlango uliofuguliwa
akaingia David Zumo ambaye uso wake
ulikuwa na tabasamu kubwa baada ya
kumuona Monica,akamfuata akamshika
mkono akaubusu.
“ Monica uzuri wako siwezi
kuuelezea.Ninajiona ni mwanaume
mwenye bahati kubwa sana kukupata
malaika kama wewe.Ninakupena sana
Monica na sipati maneno mazuri ya
kukueleza namna ninavyokupenda”
akasema David na kumshika Monica
mkono akamketisha na kumbusu akaanza
kumpapasa maungoni
“ David una haraka sana.Huna
sababu ya kuwa na haraka .Mimi tayari ni
wako ” Akasema Monica
“ Nitashindwaje kuwa na haraka
Monica mbele ya mwanamke mrembo
kuliko wote duniani” Akasema David
“ Monica narudia kusema kuwa
inawezekana sina hata kigezo kimoja cha
mwanaume Yule umtakaye katika maisha
yako lakini nakuahidi kuwa nitajitahidi
kuwa mwanaume bora kabisa kwako.Mimi
si mkamilifu ni mdhaifu kama wengine
lakini naomba unichukulie hivyo hivyo
nilivyo pamoja na madhaifu yangu.Mimi ni
mtawala wa nchi hii lakini wewe ni
mtawala
wangu.Nataka
unitawale.Niamuru chochote nitakutii.”
Akasema David kwa sauti ya taratibu na
kwa hisia kubwa.Monica akabaki
anamtazama bila kusema chochote
“ Ama kweli huyu jamaa
amebarikiwa sauti nzuri
ya
kushawishi.Haya maneno aliyoyaongea
yameniingia hadi moyoni na kunisisimua
mno.Hapa nilipo nahisi kama vile
ninavutwa na sumaku.Halafu mhh...”
Monica akastuka kidogo na kuyaelekea
macho yake katika maeneo nyeti ya David
ambayo yalionekana kukasirika .Ngozi ile
aliyoivaa David haikuweza kuzuia
kuonyesha
namna
ikulu
kulivyochachamaa
 
LEGE asante sana, nimenywea chai, lakini sijashiba. Ongeza nyingine za kutosha, weekend ndio hii.
 
Back
Top Bottom