QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

SEHEMU YA 4



ayari ni usiku mwingi na
hakukuwa na magari barabarani hii
ilimpa Amarachi nafasi ya kuendesha
gari kwa mwendo mkali mno
.Ilimchukua dakika kumi na mbili
kuwasili hospitali waliyoelekezwa na
rais.Tayari taarifa za ujio wa Austin
zilikwisha fika na madaktari na wauguzi
tayari walikwisha jiandaa
kumpokea.Haraka haraka akashushwa
garini na kukimbizwa katika chumba
cha upasuaji.
Akiwa nje ya chumba cha
upasuaji,Amarachi akampigia simu Job
“Hallo Job” akasema Amarachi na
kukawa kimya
“Job !! akaita Amarachi
“Amarachi mikono inanitetemeka
ninaogopa hata kupokea simu yako
nikihofia pengine kuna taarifa isiyo
nzuri.Tayari umefika hospitali?
“Usihofu Job.Tayari nimefika
hospitali na tayari Austin amekimbizwa
katika chumba cha
upasuaji.Kinachohitajika hivi sasa ni
maombi.Austin amepoteza damu nyingi
lakini anao nafasi ya
kupona.Anaonekana ni mpambanaji.Hii
ni hospitali kubwa,rais na viongozi wote
wakubwa waserikali hutibiwa hapa kwa
hiyo uhakika wa kupona ni
mkubwa.Tusimame katika maombi na
tumuachie Mungu suala hili
ikimpendeza asimchukue Austin kwa
sasa.Kwa hali aliyokuwa nayo Austin
wakati namfikisha hapa hospitali lolote
linaweza kutokea.Mimi si muoga kabisa
lakini kwa mara ya kwanza nahisi
kuingiwa na woga” akasema
Amarachi.Job akasikika akivuta pumzi
ndefu na kusema
“Austin is strong and he can fight
this.Austin hapaswi kufa.Operesheni hii
yote inamtegemea yeye.Kama
ulivyoshauri tuungane katika maombi
kumuombea.Naamini Mungu ana
makusudi yake kwa jambo kama hili
kutokea .Kama angekuwa hana mipango
mizuri na Austin basi usingetokea kwa
wakati ule” akasema Job
“Hata mimi naamini ni mpango wa
Mungu kwani uliponipigia simu usiku
na kunieleza kwamba tuonane kuna
jambo zito sikutaka kusubiri hadi
kesho.Tayari nilikuwa nimelala lakini
niliamka na kuelekea kwako bila ya
kukutaarifu kuwa ninakuja.Nilipofika
nilifungua geti na kuingia ndani
,nikaelekea katika mlango na nilipotaka
kuufungua nilistuka baada ya kuona
kupitia katika kioo cha mlango jamaa
mmoja anamfungua mwanamke
aliyekuwa ameketi sofani amefungwa
mikono.Baada ya tu ya kumfungua Yule
mwanamke akaongea kitu na Yule
jamaa na mara tu alipogeuka akampiga
pigo moja zito jamaa akaanguka na
kupoteza fahamu.Yule mwanamke
akachukua bastora iliyokuwa mezani
akaelekea mlangoni akashika kitasa cha
mlango ili aufungue atoke mara
akatokea Austin toka ghorofani na
kumuamuru aweke chini silaha
yake,Yule mwanamke akatii na
kubonyea ili kutii amri aliyopewa lakini
ghafla aligeuka kama upepo na kumpiga
risasi Austin akaanguka.Akamfuata pale
chini alipoanguka na kutaka kummaliza
kabisa kwa risasi ndipo nilipomuwahi
risasi ya kiganjani akaanguka chini.Ni
nani yule mwanamke? Anaonekana ni
mtu hatari sana kwa namna alivyo kuwa
mwepesi katika kucheza na silaha.Huyu
Austin ni nani? Akauliza Amarachi.
“Nakubaliana nawe Amarachi
mwanamke huyu ni hatari mno zaidi ya
tunavyodhani.Austin,ni rafiki
yangu,amewahi kufanya kazi katika
idara ya ujasusi ya taifa lakini kwa sasa
anaishi nchini Afrika ya kusini na
amekuja nchini Tanzania kwa mwito wa
rais kuna kazi anamfanyia.Austin na
Yule mwanamke ni wapenzi.”
“Wapenzi?!! Amarachi akashangaa
“Ndiyo ni wapenzi.Suala hili
linaonekana kuwa pana na ndiyo maana
inatubidi tumuombee Aus.
 
SEHEMU YA 5


ob !!..Akaita Amarachi na
kumkatisha Job
“Nitakupigia baada ya muda
kidogo” akasema Amarachi na kukata
simu
“Amarachi kuna nini? Akauliza Job
lakini tayari simu ilikwisha katwa
Amarachi aliyaelekeza macho yake
katika varanda ambako rais wa jamhuri
ya muungano wa Tanzania akiwa
ameongozana na madaktari wawili
wakielekea kule katika chumba cha
upasuaji.Amarachi akaingiwa na hofu
baada ya mmoja wa madaktari
kumnyooshea kidole.Akajikaza na
kusimama imara.Rais akiwa
ameongozana na walinzi wake
akamfuata
“ Shikamoo mzee” Amarachi
akamsalimu rais kwa adabu
“ Marahaba mama.habari yako?
“ Nzuri kabisa mzee”
“ waitwa nani?
“ naitwa Amarachi.”
“ Nafurahi kukufahamu
Amarachi.Mimi unanifahamu?
“ Ndiyo nakufahamu mheshimiwa
rais” akajibu Amarachi
“ Vizuri.Nimeambiwa wewe ndiye
uliyemleta Austin hapa hospitali.Nini
hasa kimetokea? Unaweza kunieleza
chochote unachokifahamu?
“ Mheshimiwa rais ,huyu Austin
nimemfahamu usiku huu lakini yupo
mtu ambaye anaweza akakueleza kila
kitu kilichotokea.Anaitwa Job ndiye
aliyekupigia simu kukupa taarifa
hizi.Anaweza kufika hapa ndani ya
muda mfupi kwani hakuna magari
mengi barabarani usiku huu”
“ Good.Mpigie simu mwambie rais
anahitaji kuonana naye mara moja”
akasema Ernest kisha akaongozana na
madaktari wakaelekea sehemu ya
kupumzika kusubiri upasuaji
umalizike.Bila kupoteza wakati
Amarachi akachukua simu na kumpigia
Job
“Job nilikata simu ghafla baada ya
rais kutokea.”akasema Amarachi
“Rais amefika hapo hospitali? Job
akashangaa
“Ndiyo rais yuko hapa anasubiri
upasuaji umalizike.Anahitaji kukuona
mara moja hapa hospitali anataka
kufahamu namna tukio lilivyotokea kwa
hiyo Job naomba uje mara moja hapa
hospitali kuonana naye”
Job akafikiri kidogo na kusema
“Sawa nitafika hapo muda si
mrefu”
Job akamfuata Marcelo na
kumtaka amsikilize kwa makini
“Sikia Marcelo,ninakwenda
hospitali kujua maendeleo ya
Austin,nitakuacha hapa nyumbani.Pana
usalama wa kutosha.Mwanamke Yule
aliyeleta kizaa zaa nimemfungia katika
moja wapo ya chumba humu ndani na
hawezi kutoka.Ninakuachia bastora hii
utaitumia endapo kutatokea tatizo
lolote lakini kila kinachoendelea hapa
mimi nitakiona kupitia kifaa
changu.Tafadhali usijaribu kugusa kitu
chochote usichokifahamu .Nitarejea
baada ya muda mfupi”akasema Job
akapanda chumbani kwake akachukua
kopo dogo akaenda katika chumba
alimofungiwa Maria akafungua mlango
akatoa mfuniko wa kopo lile na
kuufunga mlango.Kupitia kioo kikubwa
kilichokuwa nje ya chumba kile
akaushuhudia moshi ukitoka ndani ya
lile kopo uliokijaza chumba
chote,taratibu Maria akaanza kusinzia
“Itamchukua zaidi ya saa mbili
kuzinduka na wakati huo tayari
nitakuwa nimekwisha rejea.Siwezi
kumuacha akiwa macho ni mtu hatari
sana huyu.Sasa niwahi hospitali
kuonana na rais” akawaza Job na kutoka
akaingia garini kuwahi hospitali
***********************
 
SEHEMU YA 6



tu wa kwanza Job kuonana naye
mara tu alipowasili hospitali alikuwa
Amarachi
“Hakuna taarifa zozote toka kwa
madaktari hadi sasa hivi? Akauliza Job
“Mpaka sasa hakuna taarifa
zozote.Bado upasuaji unaendelea.Job
huyu Austin ni nani hadi rais amekata
usingizi wake na kufika hapa usiku huu
wote kujua maendeleo yake? Amarachi
akauliza
“Austin ni mtu muhimu sana kwa
rais na endapo ikatokea bahati mbaya
akafariki dunia mambo mengi ya rais
yataharibika.Rais anamtegemea katika
mambo mengi na ndiye aliyemleta
kutoka Afrika ya kusini.Austin
anatakiwa apone.” akasema
Job.Wakatazama kwa sekunde kadhaa
akauliza
“Rais yuko wapi?
Amarachi na Job wakazunguka
upande wa pili na kumkuta rais akiwa
ameketi na walinzi wake
.Wakasimamishwa na walinzi
“It’s ok guys.Waacheni wapite ni
wageni wangu” akasema rais. Job na
Amarachi wakamsogelea akasimama na
kuwasalimu kisha akawataka walinzi
wake wasogee mbali kidogo wamuache
nafasi ya kuwa huru na wageni wake.
“Mheshimiwa rais huyu anaitwa
Job Israel.Ni rafiki wa Austin na ndiye
anayeweza kukueleza kwa ufasaha
mkasa mzima uliompata
Austin”akasema Amarachi
“Job karibu sana.Nimefurahi
umefika kwa haraka baada tu ya
kupokea wito.Nini hasa kimetokea?
nani aliyefanya jambo hili kwa Austin?
Nahitaji maelezo tafadhali”akasema rais
“Mheshimiwa rais ,kama Amarachi
alivyokutambulisha naitwa
Job.Nimewahi kufanya kazi katika idara
ya ujasusi ya taifa na Austin ni mmoja
wa watu ambao nimewahi kufanya nao
kazi kwa ukaribu sana.Hatukuwa
tumeonana kwa muda mrefu na hivi
majuzi aliporejea alinitafuta .Kwa kuwa
mimi na yeye ni watu wa karibu
alinifahamisha kilichomleta hapa
Tanzania na akanitaka niungane
naye.Usiku huu amekuja nyumbani
kwangu akiwa ameongozana na watu
waiwli mmoja anaitwa Dr Marcelo na
mwingine ni mpenzi wake Maria.Huyu
Maria mpenzi wake alikuwa amefungwa
mikono .Tuliwaacha Maria na Marcelo
sebuleni tukaenda ghorofani kwa
maongezi kidogo huku nyuma Maria
akamlaghai Marcelo amfungue mikono
akajisaidie na mara tu alipofanya hivyo
basi akapiga pigo kubwa kichwani
Marcelo akapoteza fahamu.Akainyakua
bastora ya Marcelo na kutaka kukimbia
lakini Austin akawahi kutokea na
akapigwa risasi nne .Hivyo ndivyo
ilivyokuwa mheshimiwa rais”
Rais akavua miwani akafikicha
macho na kumtazama Job.
“Nashukuru kukufahamuni Job na
Amarachi.Nawashukuru vile vile kwa
jitihada zenu mlizofanya kuokoa maisha
ya Austin.Kama amekuamini akakueleza
kila kitu basi hata mimi napaswa
kukuamini na kama alikuomba
ushirikiane naye basi fahamu kuwa
unashirikiana pia na rais wa jamhuri ya
muungamno wa Tanzania.Austin ni mtu
muhimu mno kwangu na kwa taifa pia
kwa hiyo nimewaelekeza madaktari
wafanye kila linalowezekana kuokoa
maisha yake.Nimeelekeza ndege
iwekwe tayari endapo kutakuwa na
ulazima wa kupelekwa nje ya nchi kwa
matibabu zaidi.Nitafanya kila
linalowezekana kuhakikisha Austin
anapata matibabu anayostahili”
akasema rais akanyamaza kidogo na
baada ya muda akasema
“Huyo mwanamke aliyefanya tukio
hili yuko wapi? Tayari amedhibitiwa?
“Ndiyo mzee.Amedhibitiwa na
yuko sehemu salama.Tunamfanyia
uchunguzi kumbaini ni nani ila kwa
haraka haraka anaonekana ni mtu
hatari .Ana uwezo mkubwa wa kucheza
na silaha.Austin hakumfahamu vyema
mpenzi wake .Tumuombee apone ili
mambo haya yote yakamilike” akasema
Job
“ Sifahamu nini nitafanya ikitokea
Austin akapoteza maisha”akasema rais
kwa sauti ndogo .Ukapita ukimya mfupi
Job akasema
“Mheshimiwa rais kama
nilivyokueleza kuwa Austin alinieleza
kila kitu na alinitaka kushirikiana
naye.Kazi zote alizokuwa anazifanya
ninazifahamu kwa hiyo usihofu,kila kitu
kitaendelea hata kama itatokea Austin
 
SEHEMU YA 7



akatutoka ingawa hatuombi iwe
hivyo.Kama ikitokea sisi wawili mimi na
Amarachi tutavaa viatu vyake na
tutaimaliza kazi aliyoianza”akasema Job
kwa kujiamini
Rais akamtazama Job kwa makini
halafu akamtazana na Amarachi kisha
akasema
“Ahsanteni sana kwa moyo huo wa
kujitolea lakini mtanisamehe vijana
wangu si kwamba siwaamini lakini
hadi sasa bado Austin ndiye mtu pekee
ninayemuamini mno” akasema rais
“Tumekuelewa mzee,na sisi
tunakuahidi ushirikiano mkubwa kila
pale itakapotokea ukatuhitaji lakini
mheshimiwa rais kuna jambo nataka
nikueleze”
“ Go ahead tell me” akasema rais
“Ulipaswa kulisikia jambo hili
moja kwa moja toka kwa Austin lakini
kwa vile hatuna uhakika na hali yake
itaboreka wakati gani ,inanilazimu
kukueleza kwani linahitaji utekelezaji
wa haraka” akanyamaza kidogo na
kuendelea
“Austin alinidokeza kwamba tayari
umekwishampata mtu unayedhani
anafaa kuwa waziri mkuu mpya wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania
ambaye ni ndugu Wilson Mukasha”
“Ndiyo.Ninatarajia kuwasilisha
jina lake katika kikao cha bunge
kinachoanza wiki hii.Wilson Mukasha
ndiye ambaye ninamuona ananifaa kwa
nafasi ya waziri mkuu katika serikali
ninayotarajia kuiunda hivi
karibuni.Nitateua wabunge wapya kumi
kwa mujibu wa mamlaka yangu ya
kikatiba na miongoni mwa wabunge
hao nitakaowateua atatoka waziri mkuu
ambaye ni Mukasha” akasema rais
“Tayari umekwisha mtaarifu
Mukasha juu ya suala hilo? Akauliza Job
“ Ndiyo nimekwisha zungumza
naye na amekubali kuwa waziri
mkuu.Mukasha ni mtu safi,mchapakazi,
muaminifu na mzalendo wa kweli”
akasema rais.Job akavuta pumzi ndefu
na kusema
“Mheshimiwa rais tungeomba
uvute subira kidogo katika suala hili la
kumteua Mukasha kushika nafasi ya
waziri mkuu au hata kumteua kuwa
mbunge.Mimi na Austin kuna uchunguzi
tunaufanya kuhusiana na Mukasha na
tulipanga kuja kwako mara tu
uchunguzi wetu utakapokuwa
umekamilika”
Ernest Mkasa akastushwa kidogo
na maneno yale ya Job
“Sijakuelewa Job unamaanisha nini
unaposema kwamba nisimteue
Mukasha kuwa waziri mkuu?Uchunguzi
upi mnaoufanya ? nani kawatuma
mumchunguze? Akauliza rais
“Mzee tuliamini jambo hili
litakustusa sana hasa kwa namna
unavyomfahamu na kumuamini Wilson
Mukasha.Kwa upande wangu nilimtaka
Austin akueleze suala hili mapema
lakini alikataa hadi pale tutakapokuwa
na ushahidi wa kutosha kuhusu kile
tunachokichunguza.Bado hatujapiga
hatua katika uchunguzi wetu na hatuna
bado ushahidi ndio maana nakuomba
mheshimiwa rais utupe muda kidogo
tulikamilishe hili jambo na
tutawasilisha kwako matokeo ya
uchunguzi wetu” akasema Job
“Bado sijakuelewa
Job.Mnachunguza nini kwa
Mukasha?Yule mbona ni mtu
safi?Ninamuamini sana na ndiyo maana
sina hata chembe moja ya wasiwasi
kumteua kuwa waziri
mkuu.Ninamfahamu vizuri kuliko ninyi
nyote .Yule si mtu wa kutiliwa shaka
hata kidogo.Mnachunguza nini kwa
Mukasha? Akauliza rais
“I’m sorry Mr President but Wilson
Mukasha he’s not who you think he
is.You don’t know him yet” akasema Job
kwa kujiamini.Rais akamuangalia kwa
macho makali na kusema
“Do you know him than I do? Mimi
ndiye ninayeshinda naye muda wote na
ninamfahamu vizuri sana.Kumchunguza
yeye ni sawa na kunikosoa mimi
niliyeamua kumteua awe waziri
mkuu.Mpaka nimeamua kumteua awe
waziri mkuu tayari nimekwisha
jiridhisha vya kutosha kuwa Mukasha ni
mtu safi na hana kasoro zozote za
kiutendaji.”akasema rais.Job
 
SEHEMU YA 8


akamtazama Amarachi halafu
akamtazama rais na kusema
“Kwa zaidi ya miaka mitatu
nimeishi maisha ya kuigiza kama
mgonjwa wa akili” akanyamaza baada
ya rais kuonyesha kustuka kwa kauli ile
ya Job
“Watu wote wanaamimi mimi ni
kichaa.Mimi huyu ninayeongea nawe
sasa hivi nikiwa katika mavazi haya
nadhifu nimekuwa nikishinda
majalalani na kuokota vyakula,maisha
ambayo sikuwahi kuyaota hata mara
moja.Ninaamimi hapo ulipo unajiandaa
kuniuliza ni kwa nini nikaishi hivyo?
Akanyamaza na baada ya muda
akendelea
“ Nimefanya kazi katika idara ya
ujasusi ya Taifa na kama utahitaji taarifa
zangu unaweza kuomba faili ukalipitia
na kunifahamu zaidi.Nikiwa katika kozi
fupi nchini Korea kusini nilipata tetesi
kuwa mke wangu ana mahusiano na
mwanaume mwingine.Niliporejea
nyumani nikafanya uchunguzi wangu
nikagundua kuwa ni kweli mke wangu
alikuwa na mahusiano na mwanaume
mmoja anaitwa dogo Bill.Nilimchunguza
huyo dogo Bill nikagundua ni
mfanyabiashara bilionea na
anajishughulisha na biashara ya dawa
za kulevya.Ana mtandao wake mkubwa
uliosambaa sehemu mbali mbali na
kuwahusisha watu wengi hata waliopo
serikalini.Mmoja wa watu waliopo
katika mtandao huo ni Wilson Mukasha”
“ No ! that’s not true .Mukasha
hajihusishi kabisa na mambo
hayo.Namfahamu Mukasha ni mtu safi
.Sina shaka naye hata chembe na ndiyo
maana nataka awe waziri mkuu wa
Tanzania.” Akasema rais
“Mheshimiwa rais,tunafahamu
imani yako kubwa kwa Mukasha na
hiyo ndiyo sababu Austin alikataa
kukueleza jambo hili hadi hapo
tutakapokuwa na ushahidi wa
kutosha.Ninakuhakikishia mzee endapo
utanipa muda kidogo nilishughulikie
suala hili nitawasilisha kwako ushahidi
usio na shaka kuwa Wilson Mukasha
anajihusisha na mtandao wa dawa za
kulevya kwa siri sana.Ni muda kidogo
tunaomba mzee na endapo tutashindwa
kuthibitisha tutakuruhusu uendelee na
mipango yako ya kumteua Mukasha
kuwa waziri mkuu” akasema Job.Ernest
Mkasa akakuna kichwa
“Ninyi vijana mmenichanganya
sana lakini kwa kuwa ninamuamini
Austin yawezekana jambo hili lina
ukweli ndani yake.Endeleeni na
uchunguzi na nitahitaji huo uthibitisho
usio na shaka .Mnahitaji muda gani ili
muukamilishe huo uchunguzi?
“Naomba siku saba mzee” akasema
Job
“Hapana nakupa siku
tano.Hakikisha ndani ya siku hizo tano
unapata ushahidi huo unaoutaka
kuhusu Mukasha.Fanya kila lililo ndani
ya uwezo wako kulikamilisha suala hili
na endapo nitaridhika na ushahidi
utakaoniletea basi nitabadili mawazo
yangu na sintomteua tena Mukasha
kuwa waziri mkuu na nitamshughulikia
kama ninavyotaka kuwashughulikia
wengine.Nitakupa namba yangu ya
simu utawasiliana nami moja kwa moja
na chochote utakachokihitaji
nitakupatia”akasema rais na kumpa Job
namba zake za simu.
“Mheshimiwa rais ninashukuru
sana kwa kuniamini.Ninakuahidi katika
kipindi hicho cha siku tano nitakuwa
nimefanikiwa kupata ushahidi kuhusu
Wilson Mukasha “akasema Job halafu
ukimya ukapita rais akasema
“Job ,tunamuombea Austin aweze
kupona lakini hatujui nini mipango ya
Mungu .Lolote linaweza kutokea hivyo
tunapaswa kujiandaa.Endapo Austin
hatapona nitakukabidhi wewe
majukumu yote niliyokuwa
nimemkabidhi.Ni majukumu mazito na
inahitaji kujitoa sadaka .Austin alijitoa
kuifanya kazi hii kwa nguvu na uwezo
wake wote na ndiyo maana hapa nilipo
nahisi kichwa kinataka kupasuka kwa
mawazo.Hata hivyo endapo itatokea
bahati mbaya Mungu akamchukua
Austin,kile ambacho mimi na yeye
tulikianzisha lazima kiendelee.Hawa
panya wanaojiita Alberto’s lazima
nihakikishe nimewafagia wote na nchi
 
SEHEMU YA 9


inabaki safi.Hapa ni kufa ama kupona na
lazima tupambane tushinde.Kwa hiyo
Job nifanye nikuamini kuwa unaweza
kuchukua nafasi ya Austin ikitokea
akatutoka”akasema Ernest
“Mheshimiwa rais,nashukuru kwa
kuonyesha imani kwangu kwa muda
huu mfupi ulionifahamu.Ninakuahidi
kuyabeba vyema majukumu yote
utakayonipatia” akasema Job
“Job nimekuamini japo kidogo kwa
sababu ya Austin.That young man
fighting his life in that room,I trust him
with my life.You have to work hard for
me to trust you like I trust him.”
“Mzee usiwe na shaka kuhusu
mimi.Austin ananifahamu vyema na
ndiyo maana akaamua kunishirikisha
katika mambo yake.Siwezi
kukuangusha mzee”akasema Job
“ Good” akajjibu rais ns kuikunja
mikono yake kifuani
“mzee kuna jambo lingine ninataka
kukushauri”akasema Job
“Endelea nakusikia” akasema rais
“lengo kuu la Austin kunishirikisha
katika operesheni hii ambayo yeye
anaiita fagio ilikuwa ni kuwepo katika
kikosi cha kumlinda rais anachotarajia
kukiunda baada ya usalama wako
kuwepo shakani hivi sasa” akasema Job
“ Ndiyo.Tulizungumza jambo hilo
na nilimpa kazi ya kuunda kikosi hicho”
akasema rais
“Kwa hali ilivyo hivi sasa jambo
hili linaweza likachelewa kwani
sifahamu bado ni akina nani ambao
Austin alikuwa amekusudia kuwateua
katika kikosi hicho kwa hiyo ninashauri
kwamba kikosi cha sasa cha walinzi wa
rais kiwekwe pembeni na badala yake
rais alindwe na kikosi cha makomando
kutoka jeshi la wananchi .Nina uhakika
mkubwa kwamba utakuwa salama zaidi
endapo utakuwa chini ya ulinzi wa
kikosi cha makomando.”
Kwa mara ya kwanza Job akaliona
tabasamu la rais Ernest Mkasa
“That’s a good Idea Job.Ahsante
sana kwa wazo hilo zuri.Nilikuwa
naumiza kichwa sana kuhusu usalama
wangu.Ni wazo zuri
kuwat................”Ernest akanyamaza
baada ya daktari kutokea.Akasimama
kwa wasi wasi
“ Karibu daktari.Kuna habari gani?
Akauliza rais
“Mzee upasuaji umemalizika
Umekuwa na mafanikio .Madaktari
wamefanikiwa kutoa risasi zote mwilini
mwa Austin .Hakuna madhara
makubwa yaliyotokea ila risasi iliyotaka
kuleta madhara ni ile iliyopigwa kifuani
kwani ilipita karibu sana na moyo.Kwa
ujumla madaktari wamefanikiwa
kuyaokoa maisha ya Austin na hayuko
tena katika hatari”
“Oh ahsante Mungu” Ernest
akashukuru akampa daktari mkono wa
pongezi.Job na Amarachi wakatazamana
nao pia wakapongezana.Rais
akaongozana na daktari katika chumba
alimolazwa Austin baada ya kutolewa
katika chumba cha upasuaji.Bado
hakuwa na fahamu .Rais akaagiza ulinzi
uimarishwe kuzunguka chumba kile
alimo Austin
“Job na Amarachi ninawashukuru
sana kwa kuokoa uhai wa Austin.Bila
jitihada zenu angeweza kupoteza
maisha.Mimi naondoka na ninyi pia
mnapaswa kwenda kupumzika
sasa.Muda si mrefu kutapambazuka”
“Ahsante sana mzee.Tunashukuru
kwa kuacha usingizi wako na kuja
kuungana nasi.Hii ni heshima kubwa
kwa Austin na kwetu pia.Sisi
tutaendelea kuwepo hapa tukisubiri
Austin aamke” akasema Job
“ Sawa Job.Kumbuka kuyazingatia
yale yote niliyokuagiza”
“Nitayatekeleza yote mzee”
akasema Job wakaagana na rais
akaondoka
“Job kwa sasa baada ya kuwa na
uhakika kuwa Austin hayuko katika
hatari ,wewe rudi nyumbani
ukaimarishe ulinzi pale kwani tunaye
mtu hatari mle ndani.Mimi nitabaki
hapa nikimsubiri Austin
aamke.Nitakujulisha kila kitu
kinachoendelea hapa”akasema
Amarachi
 
SEHEMU YA 10


ilo ni wazo zuri Amarachi.
Endapo kutatokea tatizo lolote naomba
unitaarifu mara moja.Kabla sijasahau
simu ya Austin hii hapa akizinduka
anaweza akaihitaji”akasema Job,akapiga
hatua tatu akageuka na kuita
“Amarachi”
Amarachi akageuka
“ You did a great job .You saved all
of us” akasema job.Amarachi hakujibu
kitu akatasamu,Job naye akatabasamu
na kuondoka
Baada ya Job kuondoka Amarachi
akaingia katika chumba alimolazwa
Austin akamtazama kwa zaidi ya dakika
tatu
“Ana sura nzuri sana huyu
kaka.Hata akiwa usingizini bado sura
inatabasamu.kwa nini mpenzi wake
afikie hatua ya kutaka kumuua?Halafu
kijana mzuri kama huyu kwa nini
aliamua kujiingiza katika kazi kama hizi
za hatari? Hata hivyo anaonekana ni
mtu muhimu sana hadi rais aamue
kuacha usingizi wake kuja kujua
maendeleo yake.Ni wazi kuna jambo
kubwa na la muhimu ambalo Austin
analifanya ambalo amemshirikisha pia
Job.Nadhani ni jambo hilo ndilo ambalo
Job alikuwa ananiitia
kunifahamisha.Mambo yakitulia nina
hakika atanieleza kila kitu” akawaza
Amarachi
********************
Kumepambazuka Tanzania,tayari
ni saa kumi na mbili na dakika nane za
asubuhi,Boaz alipoamka
“Maria anapaswa kuanza
kujiandaa kwa safari ya kurejea afriaka
ya kusini leo .Austin aliomba
nimuondoe hapa Dar es salaam kwani si
sehemu salama kwa yeye kuwepo kwa
sasa.Nakubaliana na Austin ,Maria
lazima aondoke leo kurejea Afrika ya
kusini”
Boaz akatoka chumbani kwake na
kwenda katika chumba cha Maria
akabonyeza kengele ya mlangoni na
kusubiri kwa muda bila
majibu.Akabonyeza tena na kusubiri
lakini hakujibiwa.Akarejea chumbani
kwake akapiga simu ya chumbani kwa
Maria lakini simu ikaita tu bila
kupokelewa.Akapiga tena na hali ikawa
ile ile.Akaingiwa na wasi wasi
akawapigia simu mapokezi akawaomba
kama wanaweza kumsaidia kufungua
mlango wa chumba cha Maria kwani
milango yote ya hoteli hii hufunguliwa
kwa kadi maalum.Kadi ya kufungulia
mlango wa chumba cha Maria haikuwa
imerejeshwa mapokezi na hii iliashiria
kwamba bado alikuwa nayo.Wahudumu
pia walijaribu kugonga mlango lakini
hawakujibiwa.Kwa kutumia kadi ya
akiba wakaufungua mlango na wote
wakapigwa na butwaa.Chumba kilikuwa
kitupu na hakukuwa na dalili zozote za
mtu kulala mle ndani.Kila kitu cha maria
kilikuwa mle chumbani
“ Inaonekana hajalala humu
chumbani leo.Where is she? Akauliza
Boaz na ndipo muhudumu mmoja
aliyekuwa mapokezi zamu ya usiku
akakumbuka kitu
“ Nimekumbuka.Msichana mmoja
ambaye naamini atakuwa ni wa chumba
hiki aliomba huduma ya gari jana usiku
akidai kwamba ameboreka sana na
anataka kwenda kwenye klabu ya
usiku.Hapa hotelini tunatoa huduma ya
usafiri kwa wateja wetu kwa saa ishirini
na nne hivyo tulimuhudumia mteja
wetu kama alivyokuwa
ametaka.Yawezekana aliamua kulala
huko huko” akasema Yule
muhudumu.Boaz akazidi kuwa na wasi
wasi
“Naweza kumpata huyo dereva
aliyemuendesha Monica usiku? Akauliza
Boaz na dereva akaitwa akaulizwa
alikompeleka Monica .Dereva
akaelekeza mahala alikompeleka
Monica na Boaz akastuka
“Naomba unipeleke haraka sana
huko ulikompeleka .Yule ni binti yangu
na anatakiwa kuondoka na ndege ya saa
nne asubuhi ya leo kuelekea Afrika
kusini.”akasema Boaz na kukimbia hadi
chumbani kwake akabadili mavazi na
kuongozana na dereva wakaondoka
 
SEHEMU YA 11


Kwa maelezo ya huyu dereva
,mahali alikompeleka Monica
kunafanana sana na nyumbani kwa
Austin.Kuna uwezekano mkubwa Maria
alirejea kwa Austin jana usiku” akawaza
Boaz
“ Kijana uliweza kumuona mtu
yeyote mahala ulikompeleka Maria?
Kuna mtu alitoka kumpokea? Unaweza
kuikumbuka sura yake? Boaz akauliza
“ Sikumuona mtu yeyote
pale.Nilipomfikisha katika ile nyumba
alinitaka niondoke kwani hatarudi
hotelini usiku ule.Nilimuacha pale
nikaondoka”akasema dereva .Safari
ikaendelea kimya kimya huku Boaz
akiwa na mawazo mengi
Waliwasili katika nyumba ambayo
Maria aliletwa usiku .
“ Hii ni nyumba anayoishi
Austin.Nilikuwa sahihi ,Maria aliamua
kurudi kwa Austin usiku .Sikatai
mapenzi yao lakini kwa wakati huu
mapenzi tunayaweka kwanza pembeni
.Huu ni wakati mbaya.Tukivuka tufani
hii mapenzi yataendelea kama
kawaida.Kwa sasa anatakiwa amuache
Austin afanye kazi niliyompa” akawaza
Boaz huku akishuka na kuelekea getini
akabonyeza kengele zaidi ya mara tatu
hakuna aliyejitokeza kufungua
geti.Alitamani apande juu ya ukuta
achungulie ndani lakini juu ya ukuta
kulikuwa na nyaya za umeme .Akapata
wazo.Akachukua zimu yake na
kumpigia rais
“ hallow Boaz,habari za asubuhi”
“ habari nzuri mheshimiwa
rais.Samahani sana kwa usumbufu
asubuhi hii”
“ Bila samahani Boaz,nikusaidie
nini? Akauliza Rais
“ Niko hapa nje ya nyumba ya
Austin.Binti yangu Maria amelala hapa
na Austin .Nadhani unafahamu kama
binti yangu na Austin ni wapenzi”
“ Ndiyo nafahamu Boaz”
“ Good.Maria anatakiwa kuondoka
asubuhi hii kwenda Afrika kusini kuna
mambo ya muhimu sana ya kwenda
kushughulikia.Nimekuja hapa kwa
Austin ili kumchukua akajiandae lakini
nimegonga sana na hakuna mtu yeyote
anayekuja kufungua mlango.Naomba
umpigie simu Austin mjulishe kuwa
niko hapa nje” akasema Boaz.Ukapita
ukimya mfupi rais akasema
“ Boaz nadhani bado haujapata
taarifa.Kuna tatizo limetokea jana
usiku.Austin alipatwa na tatizo”
“ tatizo gani? Akauliza Boaz kwa
wasiwasi
“ Austin alipigwa risasi”
Boaz alipatwa na mstuko mkubwa
.Baada ya dakika moja akaulia kwa sauti
yenye hofu
“ is he ok?
“ yes he’s ok.Alipigwa risasi nne na
madaktari walimfanyia upasuaji jana
hiyo hiyo usiku wakatoa risasi
hizo.Nimetaarifiwa asubuhi hii na
madaktari kwamba anaendelea vizuri.”
Boaz akashusha pumzi
“ Nani aliyefanya kitendo hicho?
Tayari amekwisha kamatwa? Akauliza
Boaz.rais akachelewa kujibu
“ Mheshimiwa rais aliyempiga
risasi Austin amekamatwa? Akauliza
tena Boaz
“ Hapana bado hajafahamika mtu
aliyempiga Austin risasi ila nimeagiza
vyombo vya dola kuwasaka kokote
waliko watu hawa waliofanya hivi na
kuwatia nguvuni.”
“ Mheshimiwa rais nakuomba
fanya kila lililo ndani ya uwezo wako ili
watu hawa waliofanya tukio hili kwa
Austin wakamatwe.Yuko hospitali gani
kwa sasa? Akauliza Boaz na rais
akamuelekeza mahala alikolazwa Austin
“Ahsante mheshimiwa rais lakini
bado nina swali.Binti yangu Maria
aliondoka jana usiku katika hoteli
tuliyofikia na na akaletwa hapa kwa
Austin.Wakati Austin anashambuliwa
walikuwa wote? Kama walikuwa wote
yuko wapi? Kama hawakuwa wote yuko
wapi? Naomba msaada wako katika hili
mheshimiwa rais Nahitaji kufahamu
alipo Maria” akasema Boaz
“Usihofu Boaz nitavielekeza
vyombo vinavyolichunguza suala hili
vilifanyie kazi pia suala hilo na
kufahamu alipo Maria.Nitakupa taarifa
kila pale nitakapokuwa ninazipata.”
 
SEHEMU YA 12


“ Anaitwa Maria”
“ Yuko wapi sasa hivi?
“ Yuko hapa nyumbani
kwangu.Nimemuhifadhi sehemu salama
kwa ajili ya mahojiano.”
“ Good.Kuna jambo lingine kuhusu
huyo binti.Baba yake anaitwa Boaz
.Huyo Boaz ndiye aliyemkomboa Austin
katika mikono ya Alshabaab akamsaidia
kuanza maisha mapya Afrika ya
kusini.Boaz ndiye aliyemsaidia Austin
kufika hapa alipofika.Hata mimi
nimelazimika kupitia kwa Boaz ndipo
nikafanikiwa kumpata Austin.Boaz
amenipgia simu muda mfupi uliopita
akanijulisha kwamba Maria ameondoka
hotelini usiku wa jana akaelekea kwa
Austin .Nilimueleza kwamba Austin
amepigwa risasi akastuka sana na
ameanza kuhoji alipo
mwanae.Nimemuhakikishia kwamba
vyombo vya uchunguzi vitampata
mwanae hivyo asijali.Hivi tuongeavyo
ameanza safari ya kuelekea hospitali
kumtazama Austin.Nimeona nikujulishe
ili Austin apewe taarifa haraka kwamba
asimueleze Boaz chochote kuwa
mwanae ndiye aliyempiga risasi jana
usiku.Umenielewa Job? Akauliza rais
“ Nimekuelewa mzee lakini kuna
jambo nataka niombe msaada wako”
“ nakusikiliza Job” akasema rais
“ jana nilikueleza kwamba mimi na
Austin tayari tumeanza uchunguzi
kuhusu Mukasha na mmoja wa watu
ambao tunawahitaji kutupatia taarifa za
Mukasha ni huyo Boaz.Tunamuhitaji
sana na ninadhani huu ni wakati
muafaka wa kumpata”
“ That’s a good idea.Hata mimi
ninakubaliana nanyi.Ni kweli Mukasha
ndiye aliyeniunganisha na Boaz kwa
kudai kwamba ni marafiki kwa hiyo
ninakubaliana kabisa na mpango wenu
wa kumtumia Boaz kumfahamu zaidi
Mukasha.Nitawaelekeza vijana wangu
pale hospitali ili Boaz atakapojitokeza tu
basi achukuliwe mara moja na
wamkabidhi kwenu ili mumfanyie
mahojiano”
“Ahsante mheshimiwa rais
nitakupa taarifa za kila tutakachokuwa
tunakifanya.” Akasema Job na rais
akakata simu.Job akampigia Amarachi
“Hallow Job” akasema Amarachi
baada ya kupokea simu .
“Amarachi kuna habari yoyote
mpya hapo hospitali?
“Hakuna habari mpya.Austin
anaendelea vizuri .Nimetoka kuongea
naye muda si mrefu amesema anahitaji
supu.Nimeagiza hotelini waniletee supu
haraka.He’s so strong”
“ That’s a good news.Nashukuru
kwa maendeleo hayo ya haraka.Huku
nyumbani kuko salama.Mtu wetu naye
anaendelea vizuri.”
“ Good.” Akajibu Amarachi
“ Amarachi rais amenipigia simu
muda mfupi uliopita tumezungumza na
kuna jambo amenieleza.Baba yake
Maria ameanza kumtafuta
mwanae.Huyu ni mtu muhimu sana
kwetu ambaye alikuwa tayari katika
orodha ya watu tunaowatafuta.Hivi
tuongeavyo yuko njiani anaelekea
hospitali kuja kumuona
Austin.Tunatakiwa kuitumia fursa hiyo
kumpata.Rais amekwisha toa Baraka
zake na kuturuhusu tumchukue Boaz”
akasema Job na kumpa Amarachi
maelekezo
“Usijali Job nitafanya kama
ulivyoelekeza” akasema Amarachi
 
SEHEMU YA 13



**********************
Boaz akiwa ndani ya gari akielekea
hospitali alihisi kama kichwa chake
kinataka kupasuka kwa mawazo.
“Najaribu kufikiri lakini sipati jibu
huyu Maria amekwenda wapi? Swali
ambalo linanitoa jasho ni je alikuwa na
Austin wakati shambulio linafanyika?
Kama alikuwa na Austin yuko wapi sasa
hivi? Shambulio hilo limetokea wapi?
Imekuaje Austin akapigwa risasi? Mtu
au watu waliofanya kitendo hicho
lazima watakuwa ni watu hatari sana na
wenye ujuzi wa kutosha kwani Austin ni
mtu hatari mno .Ngoja niwasiliane na
Mukasha yawezekana anaweza
kulifahamu tukio hili kwa kina.”
Akawaza Boaz na kuchukua simu
akampigia Mukasha
“Boaz” akasema Mukasha
“Mukasha samahani kwa
kukusumbua asubuhi asubuhi “
“ Usijali Boaz.Habari za asubuhi?
“ habari naweza sema si nzuri
sana.Kuna tukio limetokea usiku wa leo
limenistua sana”
“ Tukio gani Boaz? Akauliza
Mukasha
“ Austin amepigwa risasi”
“ Austin?!! Mukasha akashangaa
“ ndiyo .Huna taarifa?
“ Hapana sina taarifa zozote
kuhusiana na tukio hilo.Wewe ni wa
kwanza kuniambia.Nani kafanya
shambulio hilo?
“ Bado haijafahamika ila rais
amenihakikishia kwamba vyombo vya
usalama viko kazini kulichunguza tukio
hilo na kumpata aliyemshambulia
Austin
“ Rais anafahamu tayari? Akauliza
Mukasha
“ Ndiyo rais anazo
taarifa.Nashangaa kwanini
hajakutaarifu”
“ Vipi hali ya Austin? Akauliza
Mukasha
“ Kwa mujibu wa rais anaendelea
vizuri.Ila Mukasha hapa nilipo
nimechanganyikwa.Binti yangu alikuwa
na Austin jana usiku lakini mpaka sasa
sifahamu yuko wapi.Nyumbani kwa
Austin hayupo.Nina wasi wasi mkubwa
na maisha ya mwanangu.Kama
walikuwa wote wakati wa shambulio
hilo atakuwa wapi? Ni mzima au
amekufa? amekimbilia wapi? Au
ametekwa na washambuliaji? Wilson
naomba unisaidie kupata taarifa za
kuhusu mwanangu Maria.Wewe uko
ngazi za juu na ni rahisi sana kupata
taarifa za uchunguzi
unavyokwenda.Hivi sasa naelekea
hospitali kumtazama Austin na kama
tayari anaweza kuzungumza basi
anaweza akanieleza ukweli mwanangu
yuko wapi.Nakuomba Mukasha fuatilia
suala hili na unijulishe kila hatua
inayofikiwa” akasema Boaz
“Pole sana Boaz .Hiki kilichotokea
kinazidi kuichafua hali ya hewa.Nahisi
Alberto’s ndio waliofanya tukio hili.Au
inawezekana ni kazi aliyopewa na rais
ndiyo ilipelekea Austin akapigwa
risasi.Nitachunguza suala hili na
nitakupa taarifa baadae.” Akasema
Mukasha
“ Ahsante Mukasha.Nitakujulisha
nitakachokipata toka kwa Austin lakini
nakusisitiza ujitahidi kuwa makini sana
upepo mbaya unavuma hivi sasa.”
Akasema Boaz na kukata simu
“ Nani kampiga risasi Austin na
kwa nini? Hisia zangu zinanituma
lazima tukio hili linahusiana na kazi
anayomfanyia rais.Ni kazi gani hiyo? I
must find out” akawaza Mukasha.
“There is only one way to find out
what Austin is doing for president”
akawaza Mukasha na kuzitafuta namba
za simu za Janet Mwamsole akampigia
Toka ilipotimu saa kumi na moja
za asubuhi,mzee Benedict mwamsole
alikuwa macho.Mke wake Janet
alionekana kuwa na usingizi mzito.Simu
ya Janet iliita lakini kutokana na kuwa
katika usingizi Janet hakuweza
kustuka.Ben akaichukua simu ile na
kutazama mpigaji alikuwa ni Mukasha
“ Mukasha anataka nini asubuhi
hii? Akawaza na kumuamsha Janet
 
SEHEMU YA 14



ambaye alipoona jina Mukasha
akaipokea simu haraka haraka na
kutoka mle chumbani
“Mukasha kulikoni asubuhi
asubuhi namna hii? Akauliza Janet
akiongea kwa sauti ndogo
“ Samahani kwa kukusumbua
asubuhi namna hii.Nimekupigia nahitaji
tuonane leo.Kuna jambo la msingi sana
nataka tuzungumze”
“ Tukutane wapi na muda gani?
“ Tuonane leo saa saba mchana
pale kwa Sakina”
“ Sawa nitafika bila kukosa”
akasema Janet na kukata simu akareja
chumbani
“ Mukasha anataka nini asubuhi
hii? Akauliza Ben
“ Kuna kitu alikuwa anauliza”
akajibu Janet na kugeuka upande wa pili
akaendelea kulala.Ben akamtazama
akatikisa kichwa na kugeukia upande
mwingine
“Mwanamke mlaghai sana
huyu.Bado anakutana na rais na
Mukasha ndiye mshenga wake.Yeye
ndiye hutumwa kwa Jane.Siku inakuja
ambapo hakuna jiwe litasalia juu ya
jiwe,wote waliohusika katika usaliti
watakuputishwa kama makapi.”
Akawaza Ben
“Naanza kuwa na wasiwasi kama
Jane bado hajamuekleza Ernest kuwa
Monica ni mwanae.Monica hatakiwi
kabisa kujua kuwa mimi si baba yake
mzazi.Sitaki kumpoteza mtoto
niliyemlea kwa mapenzi makubwa
mno.Niko tayari hata kutoa uhai wa mtu
ili kuilinda siri hii.Kwa sasa ngoja
niendelee kuipigania ndoa yake na rais
David ifanikiwe na baada ya hapo
nitakuwa nimeingia katika jumuiya ya
watu wenye nguvu kwani David
aliniahidi hivyo.Nikifankiwa kufikia
ngazi hiyo hapo ndipo kisasi changu
kitaanza.I’ll make them pay ” Akawaza
Ben halafu akachukua simu yake
akatoka mle chumbani akampigia kijana
wake akamtaka amfuatilie Jane kwa
siku ile halafu akampigia simu Monica
“Shikamoo baba” akasema Monica
baada ya kupokea simu
“Marahaba Monica.Umeamkaje?
“Nimeamka vizuri baba sijui ninyi
huko .Mbona leo umenitafuta asubuhi
namna hii,kwema huko? Akauliza
Monica
“ Nimekukumbuka nikaona
nikusalimie na kujua maendeleo yako”
“ Ninaendelea vizuri baba sina
tatizo lolote”
“ Good to hear that.Uhm ! Monica
jioni ya leo utakuwa na nafasi? Nataka
tukutane kwa chakula cha usiku ,tukae
tuzungumze.Unakaribia kuolewa na
David na pengine itachukua muda
mrefu tena kukutana na kukaa pamoja
kwa chakula “ akasema Ben
“ Baba kuolewa na David
hakutakuwa sababu ya mimi kushindwa
kupata nafasi ya kukaa nanyi wazazi
wangu tukala na kunywa kama
zamani.I’ll never change.Hata hivyo kwa
usiku wa leo sintoweza kupata nafasi
kuna mtu nina miadi ya kuonana
naye.Nitatafuta wakati mwingine na
tutakutana kwa chakula “
“ Sawa ahsante sana Monica.By the
way ,How’s David?
“ Anaendelea vizuri”
“ Ahsante Monica nikutakie siku
njema tafadhali unitaarifu siku
utakapokuwa na nafasi”
“Nitakujulisha baba usijali”
akasema Monica na kukata simu
“Kwa namna nilivyomlea Monica
kwa mapenzi makubwa ninaamini hata
kama akijua kuwa mimi si baba yake
mzazi hataliamiani hilo na siku zote
ataendelea kunipenda na kunijali
.Ninampenda sana Yule mtoto naye
ananipenda .” akawaza Ben
Baada yakuongea na baba yake
simuni,Monica alionekana kuwa na
mawazo
“Baba amenifanya nimkumbuke
Austin.Jana nilimfahamisha kuwa niko
tayari kukutana naye kwa chakula cha
usiku leo.Lengo lilikuwa ni kujenga
ukaribu ili nimtumie pale ninaposhikwa
na tamaa ya kukutana kimwili na
mwanaume hasa kwa wakati huu
ambao David yuko mbali nami.I think
that’s a mistake.Ninachotaka kukifanya
 
SEHEMU YA 15




si kitu kizuri hata kidogo.Natakiwa
kuutawala mwili wangu na kuzitawala
hisia zangu .Kumtafuta mwanaume kwa
ajili tu ya kunistarehesha si suluhisho
.Ni vipi endapo nitajaribu kufanya hivyo
halafu nikanikuta nimezama mapenzini
na Austin? Ni vipi endapo David
akafahamu kuwa nina mahusiano ya siri
na Austin? Hataniamini tena.I have to
call Austin and cancell that dinner.I’m
about to make a huge mistake of my
life” akawaza Monica na kuchukua simu
akazitafuta namba za simu za Austin
akampigia.
“ Hallow” ikasema sauti ya kike
iliyopokea simu ya Austin na kumstua
Monica
“ Halow who is this? Akauliza
Monica kwa wasi wasi
“ Naitwa Amarachi.You are Monica
right?
“ Yes I am.I need to talk to Austin
please” akasema Monica
“ I’m sorry Monica you cant talk to
him right now”
“ Why ? akauliza Monica kwa sauti
ya ukali kidogo
“ He’s in hospital”
“ Hospital ??! Monica akashangaa
“ Ndiyo.Alipata matatizo alipigwa
risasi jana usiku”
“ Oh my God !!! akasema Monica
kwa mstuko mkubwa na kukaa kimya
“ Halo Monica “ akaita Amarachi
“How’s he? akauliza Monica kwa
sauti ya chini iliyojaa woga
“ Kwa sasa anaendelea
vizuri.Alipigwa risasi nne lakini
maendeleo yake si mabaya”
“ Oh ! Thank you Lord!!..” akasema
Monica na kusikika akishusha pumzi
“ Nielekeze hospitali alikolazwa
nahitaji kuja kumuona sasa hivi”
akasema Monica na Amarachi
akamuelekea
Monica akaitupa simu pembeni,
alihisi mwili wote hauna nguvu
“ Ninajiona nina bahati
mbaya.Nimefahamiana na Marcelo na
muda mfupi toka nimefahamiana naye
akapigwa risasi.Austin naye
nimefahamiana naye na ndani ya muda
mfupi amepigwa risasi,whats going
on?Am I cursed? Akajiuliza
Monica.Akavaa haraka haraka na
kuondoka kuelekea hospitali
Baada ya kumaliza kuongea na
Monica simuni Amarachi akaingia
chumbani alimo Austin .Tayari
madaktari walikuwa wametoka.
“Hey Amarachi nahitaji
kuzungumza na Job” akasema Austin
kwa sauti ya chini
“Austin kabla hujazungumza na
Job kuna jambo nataka
nikufahamishe.Monica amepiga simu
muda mfupi uliopita”
“ Monica?? Austin akauliza
“Ndiyo”
“Anasemaje?
“Alihitaji kuzungumza nawe
ikanilazimu nimueleze hali halisi”
“ Amesemaje ulipomueleza?
“ Alistuka sana.She’s on her way
here “ akasema Amarachi.Austin
akamtaka Amarachi asogee karibu zaidi
“ Amarachi I need you to do
something for me its very important”
akasema Austin
“ Ndiyo nakusikiliza Austin”
akasema Amarachi
“ Monica akifika hapa ,fanya kila
uwezavyo upate nywele yake.Ninaihitaji
sana” akasema Austin.Amarachi
akatabasamu na kusema
“ Usijali Austin hesabu tayari
unywele umeupata.”
“ Ahsante .Sasa mpigie Job nahitaji
kuzungumza naye.” Akasema Austin
“ Austin nadhani kwa sasa
ungeendelea kupumzika Job atakuja
baadae mtazungumza ana kwa ana na
kwa muda mrefu”
********************
 
SEHEMU YA 16


az aliwasli hospitali alikolazwa
Austin.Akashuka garini na kumfuata
muuguzi mmoja akamuuliza sehemu
anakoweza kupata maelekezo ya
wagonjwa waliofikishwa
pale.Akaelekezwa na kuwaendea
wauguzi watatu akawasalimu na
kuwauliza kuhusu Austin.Mmoja wa
wauguzi wale akatazama katika
kompyuta yake na kusema
“ Samahani mzee,huyu mtu
unayehitaji kumuona kwa sasa
haitawezekana”
Boaz akabadilika sura
“ Kwa nini? Akauliza
“Kuna zuio limewekwa.Kuna watu
maalum tu walioruhusiwa kuingia
kumuona”
“Nani kaweka hilo zuio? Mimi ni
baba yake.I need to go see my son now
!! akasema Boaz kwa ukali
“ Samahani mzee hatukujua kaa
wewe ndiye baba yake.Hata hivyo
itakubidi uongee kwanza na walinzi
wanaomlinda mwanao na endapo
watakuruhusu basi utaenda kumuona
mwanao.” akasema Yule muuguzi wa
mapokezi.Boaz akaelekezwa kilipo
chumba alimolazwa Austin akaelekea
huko.Nje ya chumba alimolazwa Austin
kulikuwa na walinzi wanne waliovaa
suti nadhifu .Hawa ni walinzi
waliowekwa na rais kuhakikisha Austin
anakuwa salama.Boaz akawasalimu na
kujieleza.
“Tunashukuru kukufahamu
mzee.Sisi tumewekwa hapa kuhakikisha
kijana wako anakuwa salama.Hakuna
anayeruhusiwa kuingia humo chumbani
zaidi ya madaktari lakini kwa kuwa
wewe ndiye baba mzazi tutakuruhusu
uingie uonane naye ila kabla
hatujakuruhusu tunao utaratibu wetu
wa kuwapima watu wote na
kuhakikisha kuwa wako salama na
hawana hatari yoyote”
Kauli ile ikaonekana kuzidi
kumchafua Boaz
“Ninawaheshimu sana vijana na
ninapaswa kuwashukuru kwa kazi
kubwa ya kumlinda kijana wangu,hata
hivyo sioni sababu ya mimi kupima
wakati ndiye baba yake na hata rais
ananifahamu sana na ndiye aliyenipa
taarifa hizi za mwanangu kupigwa
risasi”
“Utatusamehe mzee hatutaweza
kukuruhusu hadi ufuate taratibu za
hapa.Tafadhali naomba unifuate”
akasema mmoja wa walinzi wale .Kwa
shingo upande Boaz akakubali
kuongozana na wale walinzi hadi nje
katika maegesho wakaingia katika gari
la Amarachi .Boaz akaanza kuwa na
wasiwasi
“Mnafanya uchunguzi gani ndani
ya gar......” kabla hajamaliza sentesi
yake akapigwa pigo zito na kupoteza
fahamu.
“Amarachi,he’s now yours”
akasema mmoja wa wale walinzi
“Thanks.Kuna jambo lingine
nataka kuwaomba.Muda si mrefu kuna
mwanamke mmoja atakuja hapa
anaitwa Monica.Tafadhali mpeni ruhusa
aingie aonane na Austin.Ni mtu muhimu
sana kwake.Mimi ninampeleka huyu
mzee mapumzikoni na nitarejea baada
ya muda mfupi.Monica asiondoke kabla
sijarejea nahitaji sana kuonana naye”
akasema Amarachi na kuondoka
“Natamanai sana kujua
kinachoendelea kwani ninashiriki
katika mapambano ambayo sifahamu
mzizi wake.lakini ngoja niwe mvumilivu
naamimi mambo yakitulia nitaelezwa
kila kitu” akawaza Amarachi akiwa
garini akielekea nyumbani kwa Job
 
SEHEMU YA 17


*****************
Job aliingia katika chumba
alimofungiwa Maria akiwa
ameongozana na Dr
Marcelo.Walikutana na harufu kali .Job
akamsogelea Maria akamtazama kwa
hasira akamfuata na kumnasa kibao
kikali,damu ikaanza kumtoka mdomoni
“ Job usimpige tafadhali” akasema
Marcelo baada ya kumuona Maria
akigugumia kwa maumivu
“kwa nini umejisaidia humu?
Huwezi kujizuia? Akauliza Job kwa ukali
na bila kutazamia akatemewa mate
usoni.Hasira zikazidi kumpanda
akainua mkono kwa lengo la kumpa
kipigo Maria lakini Marcelo aliyekuwa
karibu akawahi kuudaka
“ Imetosha Job.Usimpige tena”
akasema Marcelo kwa upole.Job
akamtazama kwa hasira
“ Unamuonea huruma? Jana alitaka
kukuua .Huyu si mwanamke wa
kuonewa huruma hata kidogo.Halafu
naomba ufahamu Marcelo kama
unataka kufanya kazi na sisi lazima uwe
kama sisi.Kuwa na moyo mgumu.Usiwe
na huruma .We’re dangerous than
devils when we’re working.kaa kikazi.I
don’t care if you are sick or not,hapa ni
kazi tu.Huyu mwananke unayemuonea
huruma leo jana alitaka kumuua
Austin.I hate her so much.You
understand me Marcelo?!!! Akauliza Job
kwa ukali.Alikuwa na hasira kali
zisizomithilika
“ Yes I do “ akajibu Marcelo kwa
woga
“ Good” akasema Job na kutoa
bastora yake akaenda ukutani
akabonyeza namba kadhaa na kile kiti
kikajifungua
“Mvue nguo zote !!! Job
akamuamuru Marcelo huku akiwa
ameielekeza bastora kwa Maria.Bila
ubishi Marcelo akamvua Maria nguo
zote na kumuacha mtupu.Job
akamuamuru atoke mle chumbani
akaelekea bafuni kwa kuwa mkono
mmoja alikuwa na jeraha akamuamuru
Marcelo amuogeshe.Marcelo
akatekeleza amri ile halafu akamrejesha
chumbani
“ Marcelo mtibu jeraha lake”
akasema Job.Marcelo akamtibu Maria
jeraha la mkono na alipomaliza Job
akamuamuru arejee katika kiti na
kukifunga .Job akamtazama kwa hasira
“I’m hungry !!! akasema Maria kwa
sauti ya chini
“You will starve to death you devil”
akasema Job na kumuamuru Marcelo
watoke mle chumbani akakifunga kile
chumba
“Job hii si sawa” akasema Marcelo
mara tu walipotoka ndani ya kile
chumba na wakimtazama Maria katika
kioo kikubwa kilichokuwa nje ya kile
chumba.
“kwa nini si sawa? akauliza Job
“Jaribu kuwa na ubinadamu hata
kidogo.Sikatai kwamba anastahili
adhabu lakini tusimdhalilishe utu wake
kwa kumuacha mtupu namna ile.Halafu
anaonekana dhaifu ana njaa anahitaji
chakula.Kingine ni kwamba usiku
mzima amefungwa pale kwenye kiti
unategemea angejisaidia wapi? Kwa
kuwa yuko mle ndani ya chumba
ambacho si rahisi kutoka sioni sababu
ya kuendelea kumfungia kwenye
kiti.Mpe uhuru akiwa chumbani”
Job akamtazama Marcelo kwa
hasira
“ You don’t know anything Marcelo
so do what I tell you to do.No questions”
akasema Job .Dr Marcelo akaonekana
kukereka akasema kwa hasira
“Unadhani Austin atafurahi
akigundua kwamba umekuwa
unamtenda hivi Maria?
“She shot Austin four times.Risasi
moja ilikaribia sana moyo wake.Ni wazi
kwamba alitaka kumuua .Kwa hiki
alichokifanya anastahili adhabu kali
mno.She need to suffer !!!! akasema Job
“ Wote tumeumizwa na hiki
alichokifanya na wote tunamjali Austin
lakini hatupaswi kumtenda hivi huyu
mwanamke.Tumtendee
 
SEHEMU YA 17


ubinadamu.Binafsi sijapendezwa kabisa
na hiki unachokifanya Job” akasema
Marcelo
“ Sikiliza Marcelo usiwe na akili
ndofgo kama panya”
“ Unasema nini Job? Marcelo
akahamaki
“ Nimekwambia usiwe na akili
ndogo kama panya.”
Ghafla Marcelo akakurupuka na
kumvaa Job akamgandamiza ukutani
“Iwe ni mara ya kwanza na
mwisho kunitusi” akasema Marcelo na
Job akamsukuma kwa nguvu Marcelo
akaanguka chini na kugugumia kwa
maumivu
“You want tofighty me? Siwezi
kupigana na kiumbe dhaifu kama
wewe” akasema Job na kumuinua
Marcelo akamtaka aelekeze macho
katika kioo kikubwa ukutani
“Mtazame vizuri Yule mwanamke
ambaye unamtetea.She’s not who you
think she is.She’s very dangerous than
we all know.Austin amekaa naye kama
mpenzi kwa muda wa miaka kadhaa
lakini nini kimetokea? Alitaka kumuua
bila huruma.Mwanamke kama huyu sio
wa kufanyia mchezo hata kidogo.Nafasi
ndogo tu akipata anaweza kuleta maafa
makubwa.Kwa hiyo unapoona
ninamuadhibu ni halali yake.We have to
make her weak.” Akasema Job na mara
simu yake ikaita alikuwa ni Amarachi
“Hallow Amarachi” akasema Job
“ Shuka chini njoo uchukue mzigo
wako” akasema Amarachi na haraka
haraka Job akashuka chini na kumkuta
Amarachi amesimama nje ya gari
lake.Bila kupoteza muda akaufungua
mlango na Job akatabasamu
“Thank you Amarachi ,good job”
akasema Job huku akimtoa Boaz toka
ndani ya gari akambeba kueleka
ndani.Bado hakuwa na fahamu
.Alimfungia katika mojawapo ya
chumba.Miguu na mikono vyote
vilivungwa kwa pingu zilizounganishwa
na kitanda
“Amarachi umefanya kazi nzuri
sana”
“Ahsante” akajibu Amarachi.
“Vipi maendeleo ya Austin?
“Austin anaendelea vizuri
sana.Alitaka kuzungumza nawe
nikamzuia.Anatakiwa atulize akili yake
kwa sasa.Anataka aruhusiwe kutoka
hospitali leo” akasema Amarachi
“Austin he’s very sturbon.Akiwa na
kazi ndivyo alivyo.Hata hivyo anapaswa
kupumzika kama kuna kazi yoyote sisi
tupo tutazifanya”
“ Hata mimi nimemueleza hivyo”
“ Good.Unatakiwa sasa
ukapumzike Amarachi.Umefanya kazi
kubwa usiku na bado unaendelea na
kazi” akasema Job na Amarachi
akatabasamu
“ Nilimueleza Austin apumzike
akanijibu kwa utani kwamba hatuna
muda wa kupumzika.Ninarejea tena
hospitali .Natakiwa kuonana na
Monica.Austin amenipa kazi ya
kuchukua unywele toka kichwani
kwake”
“Monica tayari anafahamu kuhusu
Austin? Job akauliza
“ Ndiyo.Alipiga simu asubuhi
nikamjulisha kila kitu.Hivi tuongeavyo
nina hakika tayari atakuwa amefika
hospitali.Job wewe shughulikia mambo
ya hapa nyumbani mimi nitashughulika
na hospitali.Nitakujulisha kila kitu
kinachoendelea huko” akasema
Amarachi.
“Amarachi hiyo kazi aliyokuomba
Austin uifanye ya kuchukua nywele ya
Monica naomba uifanye kwa umakini
mkubwa kwani ni kazi ya muhimu
mno.Hakikisha umeupata unywele
halisi na si wa bandia.” Akasema Job na
Amarachi akaondoka kuelekea hospitali
“Mchezo unazidi kunoga.Boaz
tunaye tayari.Who is next? Akajiuliza
Job
“ Mukasha.Si mbali sana nitamfikia
pia dogo Bill.Huyu ndiye hasa ninayelala
nikimuota.Nitahakikisha anapatikana
siku si nyingi.Nitampa mateso makali
kuzidi yote anayoyafahamu katika hii
dunia” akawaza Job akaenda katika
chumba chake akachagua suruali moja
na fulana akamfuata Marcelo wakaenda
katika chumba alimo Maria akaufungua
 
SEHEMU YA 18


mlango na kumtaka Marcelo amvishe
Maria yale mavazi halafu wakatoka
“ Are you happy now? Job
akamuuliza Marcelo ambaye hakujibu
kitu .Job akayachukua yale mavazi
waliyomvua Maria akayakagua lakini
hakukuta kitu chochote.Akaufungua
mkoba wa Maria na ndani yake akakuta
kuna nguo mbili za ndani na vitu vidogo
vidogo kama mkufu,hereni na rangi za
mdomo,vile vile aliikuta kadi ya
kufungulia mlango wa chumba
akaichukua na kwenda katika chumba
alimomfungia Boaz akamsachi pia na
kumkuta na simu na kadi ya kufungulia
mlango
“ kadi hii ya Boaz na hii ya Maria
zinafanana.Hii inanipa picha kuwa hawa
wote wawili wanaishi katika hoteli
moja.Kadi hizi zina namba za vyumba
na hii itanipa urahisi katika kazi
ninayotaka kuifanya.Natakiwa kwenda
katika hoteli hiyo na kufanya uchunguzi
katika vyumba vyao.Kuna mambo
naweza kuyapata” Akawaza Job na
kumfuata Marcelo
“ Marcelo I’m sorry for what
happened earlier.Nilikutamkia maneno
yaliyokuudhi .I’m so sorry for that.Sisi
tunapokuwa kazini huwa tunabadilika
sana na ndiyo maana watu kama sisi
hatuna maisha ya kawaida.Nisamehe
sana” akasema Job kwa upole
“Ni kweli nilikwazika mno leo
lakini wakati mwingine hamtakiwi
kutoka kabisa katika ubinadamu hata
kama mko kazini.Hali hiyo nimeiona
hata kwa Austin.Tayari nimewazoea na
hamnipi taabu tena.Nitajitahidi kuwa
mkimya na sintaingilia mambo yenu ila
pale mnapoona mnahitaji msaada
wangu msisite kunieleza.Msiniache
nikakaa bure .Japo sina ujuzi wa hizi
kazi zenu lakini ninaweza kuwa na
msaada kwenu hata mdogo tu.Mimi ni
daktari ninaweza kuwatibu mkipata
matatizo,ni mpishi mzuri pia ninaweza
kuwapikia chakula humu wakati
mkiendelea na kazi zenu kwa hiyo
naomba mnichukulie kama mwenzenu
na si kama mzigo” akasema Marcelo
“Nimekuelea Marcelo na
ninakuahidi sintorudia tena kukutamkia
maneno kama yale niliyokutamkia
asubuhi.Tafadhali jisikie nyumbani.You
are one of us.Austin anaendelea vizuri
na nina imani hata kama akija hapa
nyumbani leo basi hakuna tatizo kwa
kuwa tayari tunaye daktari wa
kumuhudumia.Karibu sana
Marcelo.Tufungue ukurasa mpya .Hapa
ni nyumbani kwangu,ni kwako pia ,ni
kwetu sote wazalendo wa nchi
hii.Tutaikomboa nchi yetu tukitokea
hapa” akasema Job na Marcelo
akatabasamu.
“Mimi sina tatizo lolote
Job.Nimekwisha sahau yote
yaliyotokea.Tufanye kazi.” Akajibu
Marcelo
“ Nashukuru .Nimekuja
kukutaarifu kuwa ninatoka kidogo
ninakwenda kufanya manunuzi .Humu
ndani hakuna kitu chochote kwa sababu
hakuna mtu aliyekuwa akiishi.Kwa sasa
kuna watu wanaishi kwa hiyo
tunapaswa kuwa na mahitaji ya msingi
kama chakula na vitu
vingine.Ninakwenda kununua kila kitu
kwa hiyo ninakukabidhi kila kitu hapa
.Humu ndani tunao watu wawili
muhimu na hatari pia.Yupo Maria na
baba yake Boaz ambaye anakutafuta
kwa udi na uvumba.Hakuna kati yao
anayeweza kutoka ndani ya chumba
alimofungwa lakini lazima tujihadhari
kwani yawezekana wakawa na watu
wao wanaowatafuta hivi sasa.Usiruhusu
mtu yeyote akaingia humu
ndani,usifungue chumba chochote kati
ya vile nilivyowafunga hawa wageni
wetu.Nitakuachia bastora utaitumia
endapo kutatoeka hatari yoyote.I think
you know how to use a gun”
“Ndiyo nafahamu .Nimewahi
kupitia mafunzo ya jeshi la kujenga taifa
kwa hiyo nafahamu vyema kutumia
silaha.Nitakuwa makini sana kwani
tayari nimejifunza kupitia kosa
nililolifanya jana.Siwezi tena kurudia
ujinga kama ule”akasema Marcelo
“Good” akasema Job na kumpa
Marcelo bastora akamuelekeza mambo
kadhaa pale ndani kisha akaondoka
 
Back
Top Bottom